Waziri Simba aonja joto ya jiwe kwa Babu

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
234




Waziri Simba aonja joto ya jiwe kwa Babu


na David Frank, Loliondo


WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii Wanawake na Watoto Sophia Simba, ameonja joto ya jiwe baada ya kuzuiwa na wananchi kumfikia Mchungaji Ambilikile Maisapila, kwa madai kuwa ‘alichakachua’ foleni kumfikia.

Waziri Simba alifika katika kijiji cha Samunge majira ya alasiri (Alhamisi iliyopita), akiwa katika msafara wa magari manne na kutaka kwenda moja kwa moja kumwona Babu eneo alilokuwa akitolea tiba hiyo.

Ghafla waziri huyo alivamiwa na kundi la watu wenye hasira ambao wengi wao walikuwa wamekaa kijijini hapo kwa zaidi ya siku saba, wakisota kumwona Babu.

Mashuhuda wa tukio hilo la aina yake, waliliambia Tanzania Daima Jumatano kuwa Waziri Simba alizuiliwa kwani alitaka kumwona Babu muda mfupi tu baada ya kuwasili kijijini hapo bila kufuata foleni.

“Watu hawakujali uwaziri wake, walimzonga na kumhoji imekuwaje amefika na kukimbilia kikombe bila kupanga foleni kama wanavyofanya wao. Uliibuka mzozo mkubwa kati yake na wananchi hao ambao baadhi walikuwa wakisema hovyo kwa hasira,” alisema shuhuda wetu.

Wakati tafrani hiyo ikitokea, wasaidizi wa Babu pamoja na baadhi ya viongozi wa serikali ya kijiji cha Samunge, walikimbia kwa hofu ya kupewa maneno makali na wananchi, hali iliyomlazimu Babu kusitisha tiba yake kwa muda kutuliza hali hiyo.

Wakati akituliza hali hiyo, Babu akiwatahadharisha wananchi waliofurika kijijini kwake kwamba wanapaswa kuwaheshimu viongozi wanaofika hapo kwani mbali ya kupata kikombe, pia wanaratibu shughuli zinazohusiana na tiba hiyo ya ajabu.

“Nawaomba muwaheshimu viongozi wanaokuja hapa kwani mbali ya kuja kupata tiba wanafika kuona namna ya kuboresha hali ya mazingira ili tiba hii iweze kuwa endelevu,” alikaririwa Babu akisema.

Babu alimwongoza Waziri Simba kwenda kumpa kikombe pamoja na ujumbe wake na baada ya kupata tiba hiyo, waliondoka kurudi Arusha.

Katika hatua nyingine siku chache tu baada ya Babu kusitisha huduma kwa watu na wagonjwa wanaotoka ndani na nje ya nchi, kumeibuka staili mpya ya magari kusafiri na kupeleka watu kwenda kijijiini Samunge kupitia njia za panya.

Uchunguzi uliofanywa umebaini kuwa mbali na barabara zilizowekewa vizuzi, yapo magari yanayotumia barabara ya Longido kupitia Ziwa Natron na kuingia moja kwa moja kijijini Samunge.

“Pamoja na kuwepo vizuizi maalumu kama vile vya Arusha, Mto wa Mbu, Babati mkoani Manyara, Mugumu na Musoma mjini mkoani Mara, bado madereva watukutu wanafanya hila na kusafirisha watu na wagonjwa hao kupitia Longido na kuchepukia Ziwa Natron na kuunganisha moja kwa moja kwa Babu,” alisema mmoja wa viongozi wa wilaya ya Ngorongoro.

Wakati hayo yakiendelea, magari zaidi ya 300 yamezuiliwa katika kizuizi cha Mto wa Mbu, huku zaidi ya magari 100 yakiwa yamekwama eneo la Melerani wilayani Monduli, yakiwa njiani kwenda Loliondo.

Kuzuiliwa kwa magari hayo ni sehemu ya utekelezaji wa mapendekezo ya mchungaji huyo ambapo aliomba wagonjwa wapya kusitisha kuingia Loliondo katika kipindi cha wiki moja.

Chanzo: Tanzania Daima.


My Take:

Wadau -- hii anavyofanya Babu ni sahihi -- kuwatetemekea wakuu wa siasa na serikali kwa visingizio ya kuboresha mazingira? ya sehemu hiyo

Sasa kila kiongozi wa serikali ataruka foleni kwa kisingizio hicho -- hiyo dawa itawaponyesha?

 




Waziri Simba aonja joto ya jiwe kwa Babu


na David Frank, Loliondo


WAZIRI wa Maendeleo ya Jamii Wanawake na Watoto Sophia Simba, ameonja joto ya jiwe baada ya kuzuiwa na wananchi kumfikia Mchungaji Ambilikile Maisapila, kwa madai kuwa ‘alichakachua' foleni kumfikia.

Waziri Simba alifika katika kijiji cha Samunge majira ya alasiri (Alhamisi iliyopita), akiwa katika msafara wa magari manne na kutaka kwenda moja kwa moja kumwona Babu eneo alilokuwa akitolea tiba hiyo.

Ghafla waziri huyo alivamiwa na kundi la watu wenye hasira ambao wengi wao walikuwa wamekaa kijijini hapo kwa zaidi ya siku saba, wakisota kumwona Babu.

Mashuhuda wa tukio hilo la aina yake, waliliambia Tanzania Daima Jumatano kuwa Waziri Simba alizuiliwa kwani alitaka kumwona Babu muda mfupi tu baada ya kuwasili kijijini hapo bila kufuata foleni.

"Watu hawakujali uwaziri wake, walimzonga na kumhoji imekuwaje amefika na kukimbilia kikombe bila kupanga foleni kama wanavyofanya wao. Uliibuka mzozo mkubwa kati yake na wananchi hao ambao baadhi walikuwa wakisema hovyo kwa hasira," alisema shuhuda wetu.

Wakati tafrani hiyo ikitokea, wasaidizi wa Babu pamoja na baadhi ya viongozi wa serikali ya kijiji cha Samunge, walikimbia kwa hofu ya kupewa maneno makali na wananchi, hali iliyomlazimu Babu kusitisha tiba yake kwa muda kutuliza hali hiyo.

Wakati akituliza hali hiyo, Babu akiwatahadharisha wananchi waliofurika kijijini kwake kwamba wanapaswa kuwaheshimu viongozi wanaofika hapo kwani mbali ya kupata kikombe, pia wanaratibu shughuli zinazohusiana na tiba hiyo ya ajabu.

"Nawaomba muwaheshimu viongozi wanaokuja hapa kwani mbali ya kuja kupata tiba wanafika kuona namna ya kuboresha hali ya mazingira ili tiba hii iweze kuwa endelevu," alikaririwa Babu akisema.

Babu alimwongoza Waziri Simba kwenda kumpa kikombe pamoja na ujumbe wake na baada ya kupata tiba hiyo, waliondoka kurudi Arusha.

Katika hatua nyingine siku chache tu baada ya Babu kusitisha huduma kwa watu na wagonjwa wanaotoka ndani na nje ya nchi, kumeibuka staili mpya ya magari kusafiri na kupeleka watu kwenda kijijiini Samunge kupitia njia za panya.

Uchunguzi uliofanywa umebaini kuwa mbali na barabara zilizowekewa vizuzi, yapo magari yanayotumia barabara ya Longido kupitia Ziwa Natron na kuingia moja kwa moja kijijini Samunge.

"Pamoja na kuwepo vizuizi maalumu kama vile vya Arusha, Mto wa Mbu, Babati mkoani Manyara, Mugumu na Musoma mjini mkoani Mara, bado madereva watukutu wanafanya hila na kusafirisha watu na wagonjwa hao kupitia Longido na kuchepukia Ziwa Natron na kuunganisha moja kwa moja kwa Babu," alisema mmoja wa viongozi wa wilaya ya Ngorongoro.

Wakati hayo yakiendelea, magari zaidi ya 300 yamezuiliwa katika kizuizi cha Mto wa Mbu, huku zaidi ya magari 100 yakiwa yamekwama eneo la Melerani wilayani Monduli, yakiwa njiani kwenda Loliondo.

Kuzuiliwa kwa magari hayo ni sehemu ya utekelezaji wa mapendekezo ya mchungaji huyo ambapo aliomba wagonjwa wapya kusitisha kuingia Loliondo katika kipindi cha wiki moja.

Chanzo: Tanzania Daima.


My Take:

Wadau -- hii anavyofanya Babu ni sahihi -- kuwatetemekea wakuu wa siasa na serikali kwa visingizio ya kuboresha mazingira? ya sehemu hiyo

Sasa kila kiongozi wa serikali ataruka foleni kwa kisingizio hicho -- hiyo dawa itawaponyesha?



Babu ameanza kuvunja masharti yake kuhusu kuruka foleni?
 
Kwa sharti la babu, Ukiruka foleni tu dawa haifanyi kazi, ni sawa na kunywa juice tu hivyo na wasi wasi viongozi wetu wengi haitawasaidia.

wanapenda kutumia vyeo vyao kujinufaisha wao kwanza km ilivyo kwa mafisadi.

Ufisadi hadi kwa babu hii imezidi.

ingekuwa vyema wakapanga foleni na kuona adha na machungu wanyayopata wananchi wengine wangeshughulikia suala la miundombinu kwa haraka.

Ila sasa kwa kuwa wanajipa kipaumbele wakibwia kikombe tu wanasahau wananchi wanyonge ambao wamekaa ktk foleni siku kibao.

hawa ndio viongozi wetu, kila pahala utaona wao wanataka wawe mbele mbele.

Nakumbuka Mwalimu Nyerere alikuwa akienda kupiga kura anapanga foleni na wananchi, lakini hawa wetu maphoto genic, waonekane ktk magazeti na vyombo vya habari.

Kwa wale wanaochakachua foleni dawa haitawasaidia kamwe babu alishasema hilo.
 
Kiutu uzima, babu anaona aibu pale wadau wa serikalini wanapozomewa!...nadhani akichekelea kitu kama hicho ataonekana chizi...Uso umeumbwa na haya jamani!!
NDIYO MAANA ANAPOONA kiongozi amekiuka taratibu na anataka ahudumiwe mapema kuliko wengine, basi anaamua kumpa dawa ili aondoke na hali irudi kawaida!
SASA suala la mtu huyo kupona au kutopaona hatuwezi kujua zaidi!
 
Kiutu uzima, babu anaona aibu pale wadau wa serikalini wanapozomewa!...nadhani akichekelea kitu kama hicho ataonekana chizi...Uso umeumbwa na haya jamani!!
NDIYO MAANA ANAPOONA kiongozi amekiuka taratibu na anataka ahudumiwe mapema kuliko wengine, basi anaamua kumpa dawa ili aondoke na hali irudi kawaida!
SASA suala la mtu huyo kupona au kutopaona hatuwezi kujua zaidi!

Lakini alitamka hakuna kuruka foleni, ama sivyo dawa haitafanya kazi!
 
Kiutu uzima, babu anaona aibu pale wadau wa serikalini wanapozomewa!...nadhani akichekelea kitu kama hicho ataonekana chizi...Uso umeumbwa na haya jamani!!
NDIYO MAANA ANAPOONA kiongozi amekiuka taratibu na anataka ahudumiwe mapema kuliko wengine, basi anaamua kumpa dawa ili aondoke na hali irudi kawaida!
SASA suala la mtu huyo kupona au kutopaona hatuwezi kujua zaidi!
Mkuu binafsi mimi nilitamani sana kuona Babu anasimamia kauli zake hii ingemuongezea heshima na umakini wake.
Hii yakubadilibadili kauli kama nikweli itazidi kumpunguzia imani kwa jamii husika (ikumbukwe kwa Mungu hakuna aliye zaidi ya mwingine).

Na maswali kidogo bado najiuliza:_
Alisema ukichakachua foleni dawa haitibu je ni kweli haitatibu?Kama haitawatibu heshima yake kwao iko wapi sasa?na kama itawatibu kwanini alisema uwongo?je anapanda nini vichwani mwetu?
Vp na ile aliyosema kua haruhusiwi kuhama hapo alipo linaukweli ?
Vp serikali ikimtingishia kiberiti kua kama hawezi kuhamia sehemu ambayo itafanya huduma yake iwe nyepesi kufikiwa na salama kijamii asitoe dawa kabisa ataweza kusimamia alichokisema awali?

Maoni yangu ...Kama Babu anaouwezo wa kuvunja masharti aliyopewa na hakutakua na madhara kimatibabu basi asiwe na upendeleo au kama vp aongee na kina Mengi au Bakresa waijaze kwenye makopo ya maji ya ya Uhai, Dasani au Kilimanjaro yaingizwe kitaa!!
 
Wakati akituliza hali hiyo, Babu akiwatahadharisha wananchi waliofurika kijijini kwake kwamba wanapaswa kuwaheshimu viongozi wanaofika hapo kwani mbali ya kupata kikombe, pia wanaratibu shughuli zinazohusiana na tiba hiyo ya ajabu.

"Nawaomba muwaheshimu viongozi wanaokuja hapa kwani mbali ya kuja kupata tiba wanafika kuona namna ya kuboresha hali ya mazingira ili tiba hii iweze kuwa endelevu," alikaririwa Babu akisema.


Babu alimwongoza Waziri Simba kwenda kumpa kikombe pamoja na ujumbe wake na baada ya kupata tiba hiyo, waliondoka kurudi Arusha.

Sasa mbona hakufanya hivyo babu?
 
Hilo ni swala la kiimani ndio maana ni vigum sana kwa walio wengi kuelewa,kwakua aliruhusiwa na babu mwenyewe hakuna tabu.maana yeye ndie aliyepewa mamlaka na MUNGU wake.
 
Waziri huyo na msafara wake wamekunywa juice na si tiba kwa mjibu wa babu
 
Back
Top Bottom