Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,813
- 11,991
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako amesema Wanafunzi wote wa Darasa la Saba 907,802 waliofaulu Watafanikiwa kujiunga kidato cha kwanza Mwaka 2022 kutokana ongezeko la Madarasa. Amesema Serikali imewezesha ujenzi wa Madarasa mapya elfu 15 Nchi nzima kwa mkupuo huku Madarasa elfu 12 yakiwa ya Shule za Sekondari.
Ameyasema hayo leo tarehe 03 januari 2022, kwenye Uzinduzi wa bodi ya wakurugenzi wa bodi ya huduma za maktaba tanzania maktaba kuu ya taifa,
Dar es salaam.
Prof. Ndalichako ameitaka Bodi ambayo Prof. Rwekaza Mukandala ndiye Mwenyekiti wa Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania, kupitia Sheria ya Bodi Na. 6 ya mwaka 1975 kuangalia kama inaendana na Teknolojia ya wakati huu kisha wamshauri, kwani matarajio ni kuwa na Maktaba mtandao ambayo itawafikia watu wote.
"Kuna usemi maarufu kwamba eti “ukitaka kumficha jambo Mtanzania, liweke katika maandishi’’! Tukatae usemi huu kwa vitendo kwa kuanza sasa kutumia maktaba zetu kujinufaisha" amesema Prof! Ndalichako.
Ameshauri kwenye Maktaba viwekwe Vitabu vya ufugaji bora wa kuku, ng'ombe nk, ili kuweza kuwahudumia watu wote na
kuhakikisha Elimu inayotolewa inalenga ujuzi na umahili katika kuleta tija.
Prof Ndalichako amesema katika miezi 9 ya rais Samia, amewezesha mambo mengi kwenye Wizara ya Elimu ikiwemo ujenzi wa shule 26 za wasichana kila Mkoa, Shule 10 Ujenzi umeshaanza. Sasa hivi kazi za Ujenzi wa Vyuo vya Ufundi Stadi vya VETA 28 inaendelea nia ikiwa kuhakikisha katika kila Halmashauri inakuwa na Chuo cha VETA kwa ajili ya kutoa ujuzi.
Ameyasema hayo leo tarehe 03 januari 2022, kwenye Uzinduzi wa bodi ya wakurugenzi wa bodi ya huduma za maktaba tanzania maktaba kuu ya taifa,
Dar es salaam.
Prof. Ndalichako ameitaka Bodi ambayo Prof. Rwekaza Mukandala ndiye Mwenyekiti wa Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania, kupitia Sheria ya Bodi Na. 6 ya mwaka 1975 kuangalia kama inaendana na Teknolojia ya wakati huu kisha wamshauri, kwani matarajio ni kuwa na Maktaba mtandao ambayo itawafikia watu wote.
"Kuna usemi maarufu kwamba eti “ukitaka kumficha jambo Mtanzania, liweke katika maandishi’’! Tukatae usemi huu kwa vitendo kwa kuanza sasa kutumia maktaba zetu kujinufaisha" amesema Prof! Ndalichako.
Ameshauri kwenye Maktaba viwekwe Vitabu vya ufugaji bora wa kuku, ng'ombe nk, ili kuweza kuwahudumia watu wote na
kuhakikisha Elimu inayotolewa inalenga ujuzi na umahili katika kuleta tija.
Prof Ndalichako amesema katika miezi 9 ya rais Samia, amewezesha mambo mengi kwenye Wizara ya Elimu ikiwemo ujenzi wa shule 26 za wasichana kila Mkoa, Shule 10 Ujenzi umeshaanza. Sasa hivi kazi za Ujenzi wa Vyuo vya Ufundi Stadi vya VETA 28 inaendelea nia ikiwa kuhakikisha katika kila Halmashauri inakuwa na Chuo cha VETA kwa ajili ya kutoa ujuzi.