Waziri Nchimbi hakuvamia kwa bahati mbaya maandamano ya waandishi wa habari leo Jangwani

bushman

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
2,411
743
Moderator usiiunganishe hii thread na ille ya maandamano ya waandishi wa habari

Nawapongeza sana waandishi wa habari kwa kumtimua waziri wa mambo ya ndani Emmanuel Nchimbi nawapongeza sana kwa kuonyesha hisia zenu kwa kitendo kiovu kabisa ambacho kila mpenda demokrasia na haki katika ulimwengu huu ambacho amefanyiwa mbali ya kuwa mwandishi wa habari ni Mtanzania mwenzetu huyu marehemu Daudi Mwangosi.

Haina ubishi polisi ndio wameua kinachopiganiwa hapa wahusika wote ambao wako nyuma ya mauji haya washughulikiwe zaidi wale ambao wanatoa amri dhalimu kwa polisi,lakini nataka niwaambie waandishi wa habari Emanuel Nchimbi waziri wa mambo ya ndani, kuvamia maandamano yenu ya wanahabari na kutaka kuhutubia bila kualikwa sio bahati mbaya anajua mtaandika zaidi kuhusu yeye kutimuliwa kwake kwenye maandamano na kuacha kuandika maaovu na ujumbe mliokusudia kuupeleka kwa serikali na polisi wao,haingii akilini kwa mtu mwenye ngazi ya waziri kuvamia kwa mfano sherehe ambayo hana kadi ya mwaliko??

Kwa hiyo rai yangu kwa wanahabari ni kuandika kile ambacho mlikusudia kukiwakilisha leo kwa watanzania na dunia nzima !!Hawa ndio mawaziri wa tanzania huwezi kujua wakati gani yuko serious!!

Je mnakumbuka mjadala wa dowans ulivyopamba moto wakatuletea kikombe cha babu loliondo?? Na viongozi wote waserikali wakawa wa kwanza kupata kikombe na kusifia kikombe?? Kwa hiyo nchimbi asiwatoe kwenye lengo lenu. Kama hamfahamu vizuri Nchimbi ni zao la wanamtandao waliomweka Kikwete madarakani na ndio mwenyekiti aliyevuruga uvccm, na kama mnataka ukweli zaidi nendeni mkamhoji Sumaye Fredrick waziri mkuu mstaafu alikua anamaanisha nini alivyosema "anayefagia njia ya kwenda ikulu kwa karatasi basi akifika huko atatumia risasi ili aweze kutawala"mwaka 2005 kwenye kinyang'anyilo cha urais alipokuwa amechafuliwa sana na wanamtandao kwenye kampeni za kuwania urais kwa tiketi ya CCM.

kwa hiyo waandishi mshikamane mno kipindi hiki kwani serikali inajaribu kutumia kila aina ya hila kuwagawa na kuwatoa kwenye mjadala wa msingi kuwa waliomuua Daudi Mwangosi wachukuliwe hatua na wengine wawajibishwe kutokana na nyadhfa zao.
 
Mkuu bushman tumekupata kwa mchanganuo na uchambuzi wa huyu mwanamtandao. Akina Nchimbi na wanamtandao mwenzie ndio walioifikisha serikali ya JK hapa ilipo na kumfanya rais kunyamazia mambo ya msingi kana kwamba hayuko nchini. Mungu atawalaani wote mnaoharibu nchi kwa masalahi yenu binafsi
 
Bushman,

Well noted, Nchimbi hana uwezo wa kuongoza wizara...kwanza aliiba kura na kupata ubunge...

Hivi CCM wanajipenda kweli?? Madaktari...Waalimu...Waandishi wa habari....Wananchi maisha magumu...kazi wanayo 2015
 
Anaweza baadaye akajitetea kuwa hakuja kama Waziri wa mambo ya ndani, bali alikuja kama mjumbe wa KAMATI fulani tu.
 
mimi sina hofu kabisa najua bila hata nguvu yoyote ccm haitawali tena
 
Likiletwa fungu la mpunga waandishi mtakataaa zile bahasha zetu zileeeeeeeeeeeeeeeeee!!!!!!!!!!!!!!!
 
Mie mwenyewe nilidhani mabadiliko ya kanunu CCM yalikuwa na lengo la kukiboresha chama...kumbe ilikuwa na janja ya wanamtandao ili wawapitishe nndugu na wanamtandao kirahisi bila challenge ili waingie CCM-NEC.

Kivuli kilikua eti wanataka kuwabana mafisadi, usanii mtupu uchaguzi unaoendelewa shv CCM ndio nimegundua ilikuwa danganya toto ni njia ya kujaza mtandao kwenye vyombo vya maamuzi CCm ili watawale wanamtandao tuu...kazi ipo sijui niende chama gani CDM kuna kanafiki kakijana kamoja kananifanya nisiende lbd wakatimue...nikifikiria ADC ndio chama kipya na kizuri lkn nasikia kuna libaba nafiki moja lipo nyuma ya pazia la ADc sijui niende TLP ...mh lkn napo kula yule jemedari anayefanya siasa kisanii na mie wasanii mbalimbali lbd mnisaidie niende wapi
 
Naam huyu jamaa anaishi kwa fitina na mungu wa ajabu sana kumbuka ripoti ya awali polisi walisema bomu lilirushwa na waandishi wa habari,lakini hawakujua kama kunawatu walikuwa wanapiga picha tukio zima picha zilipokuja kutoka wakarudi nyuma na kujifungia ndani mpaka leo!!!!!!!Nchimbi hwezi sema kwamba akijiuzulu Tanzania haitapata waziri kama yeye bora wangesema kina magufuli na mwakyembe...................
 
bushman Wapendwa hiki alichosema mwenzetu ni bastola tosha kabisa, hajapiga kona, zingatieni. Ni kweli 2005 Nchimbi alifanya kazi kubwa sana ya ufagizi katika kundi la SSM linaloongoza nchi kwa sasa. Na ndiyo maana hata kama alishindwa ile Thesis ya PhD at first hadi alipojua alichofanya hadi akapata PhD basi hawataweza kumwondoa katika uwaziri. Atakuwa waziri awamu hii yote hata kama ataboronga kiasi gani. Mambo ya kubebana bwana!
 
Last edited by a moderator:
"I can not teach you violence, as I do not myself believe in it. I can only teach you not to bow your heads before any one even at the cost of your life" Gandhi
 
Huyu hapa akisepa

427870_413390608723016_1858638376_n.jpg
 
hii style ya kuleta matukio ya kuteka vichwa vya habari ya magazeti ilishashtukiwa siku nyingi na wananchi hawadanganyiki tena mimi naona hata wakiandika nchimbi kafukuzwa kwenye maandamano ya wanahabari ndio vizuri kabisa kufikisha ujumbe ila mimi napendekeza kichwa kisomeke;

WANAHABARI WAANDAMANA KUPINGA MAUWAJI YA MWANGOSI, WAZIRI WA WIZARA HUSIKA AFUKUZWA KWA AIBU, AZOMEWA KWA KUVAMIA MKUTANO BILA KIBALI
 
Back
Top Bottom