Waziri na Katibu Mkuu Wizara ya Afya mna maslahi gani NTLP

Nyakarungu

JF-Expert Member
May 1, 2011
472
375
Dr Hamis Kigwangala na Katibu Mkuu Wizara ya Afya mna maslahi gani na jipu la NTLP lina usaha limeichafua Nchi na nyie mjiandae kuumeza usaha wake au kuutapika.

Nianze maandiko haya kwa kutoa tahadhari, jipu linaloonyesha dalili za kupasuka na likakosa kitu chenye ncha kali kulipasua, ipo siku litakuadhiri mbele za watu, kwani hata nguo yako tu uliyovaa ikiligusa litatumbuka na kukuchafua hadharani.

Leo naleta kwenu jipu hili lililolimbikiza bacteria (Abscessical Bacteria) kwa muda mrefu na kwa kuwa alikosekana mtumbuaji mwenye tahadhari leo linatumbuka hadharani kwa kuguswa na mate yake mwenyewe kwa sababu liko kwenye ulimi kabisa, hivyo usaha utamwagika na sijui kama mwenye jipu ataumeza ili kuficha aibu ili ahuharishe baadae kimyakimya au atautapika hadharani tumshangae.

Kwa ufupi mimi ni mpelelezi wa kujitolea naifanya kazi hii katika idara yeyote bila kujali lolote zaidi ya kutaka usafi katika idara za huduma kwa jamii, naitwa ‘NYUNDO YA CHUMA’

Mradi wa kifua kikuu na ukoma wenye tawi tanzu la kifua kikuu na ukimwi umekuwa ukifadhiliwa na watu wa marekani CDC kwa miaka kadhaa, CDC wamekuwa wakitoa pesa kwa ajili ya utafiti, mafunzo, tiba na vitendea kazi vingine, ili kuimarisha afya ya jamii, hasa kwenye upande wa kutokomeza kifua kikuu na ukoma, zoezi ambalo limefanikiwa sana ukanda wa kusini mwa jangwa la sahara.

CDC ndio mzazi na mlezi wa watu walioathirika kwa kifua kikuu na ukimwi, bila CDC huduma kwa watu hawa zingekuwa duni na zaidi sana tungewapoteza watu wengi sana kwa kukosa pesa za kuendeshea mafunzo na kupata vitendea kazi vya kutolea huduma na dawa.

CDC hutoa pesa kwa taasisi na nchi ambayo inatekeleza sawa na malengo, ikiwa tutakeleza ipasavyo ufadhili wao utaendelea kwa kiwango cha juu zaidi, na endapo tutaonekana kuyumba na matumizi yasiyoeleweka ufadhili utayumba pia.

Mpaka sasa Tanzania ikiwa na Mradi huu wa National Tb and Leprosy Program (NTLP) unaosimamiwa na wizara ya afya tumeshafeli na kushusha thamani ya umahili na elimu za watendaji wetu na taifa kwa ujumla, lakini pia uaminifu kwa wafadhili tumeupoteza kwa sababu mwaka jana NTLP ilipewa dola za kimarekani million 2, lakini tumeporomoka mpaka kupewa dolla za kimarekani 750,000/- na pengine hili jipu tunatakiwa tulitumbue likiwa mdomoni mwa aliyelilea na kumlazimisha ameze usaha wake ili akaharishe kimya kimya chooni kwake kuepusha kipindupindu mitaani.

Chanzo cha kuporomoka kwa kiasi hicho ni mtu mmoja tu anaitwa Beatrice Mtayoba ambaye ndiye mratibu wa mradi huu kitaifa, huyu mama ndiye chanzo cha matatizo yote katika mradi huu, anaitumia ofsi kwa manufaa yake binafsi kwa mfano;-

Amefanikiwa kuwakatisha tamaa watumishi wengine tamaa kwa kubuni njia mbalimbali za namna ya kuiba fedha za wafadhili kwa kuibua vimiradi vya hovyohovyo ambavyo anakuwa anashindwa kuvitolea maelezo

Kwa hali hiyo baadhi ya watumishi walianza kugomea mipango yake, lakini mwenzao kwa ufundi wake wa kiasili aliweza kuwahujumu mpaka wengine wakaacha kazi wenyewe na kutafuta maeneo mengine

Uwezo wake kiutendaji ni mbovu sana lakini alifanikiwa kumshika mwanasheria wa wizara ya afya Patricia Maganga akawa ndiye mshauri wake mkuu na kumzunguka katibu mkuu wa wizara,

Alifanikiwa kuwahujumu baadhi ya viongozi wenzake waliokuwa wakifanya mambo yaende kama yalivyopangwa, mfano alimhujumu Dr Nyamkala aliyekuwa mratibu wa kifua kikuu na ukimwi kwa kuzuia miradi iliyokuwa imeelekezwa na wafadhili kwa mwaka mzima akiwa anaikwamisha, huku akishirikiana na mwanasheria wa wizara ya afya Ndugu Patricia Maganga ambae amekuwa akishirikiana nae kwa kila mbinu chafu dhidi ya watumishi wenzake kwa sababu wana mahusiano yao ya siri kwa maana ya kunufaika na pesa hizi za miradi kwa sababu ili katibu mkuu wa wizara atie saini pesa za miradi zikachukuliwe ni lazima mwanasheria wa wizara ahusike, hivyo Bi. Betrice amekuwa akimtumia vilivyo na mambo yao yamenyooka huku wakiumiza wananchi waliotegemea kupata huduma safi na zenye weledi, hivi sasa takwimu za watu wanaoumia kwa kifua kikuu ni wengi kulinganisha na kipindi cha nyuma.

Lakini Bi. Beatrice ili afanikiwe kuwa salama na acheze michezo yake vizuri alimuondoa mwajiriwa wa mradi ambaye alikuwa Mratibu wa mradi wa kifua kikuu na ukimwi na kumzunguka kwa mgongo wa nyuma kupitia mwanasheria mkuu wa wizara wakafanikiwa kumwajiri kwenye nafasi hiyo mdogo wake wa kinasaba Dr. Wenzekoyi ambaye mpaka sasa cv yake ina utata hana uwezo kabisa wa kusimamia mradi huu, nay eye ni sababu namba mbili ya kupunguziwa ufadhili kwa sababu takwimu za mradi zimeshuka kabisa hana ubunifu, hafanyi kazi za maana zaidi ya kufanya kazi ya kutafuta wataalamu wa kuandika proposal ya namna ya kuchota pesa za mradi, ameanza kazi miezi kadhaa iliyopita lakini sasa ana gari V.8 hata kwa akili ya kawaida tu haingii akilini.

Hata mshahara anaolipwa ni aibu tupu na ni usaha tele, kwa mfano ukilinganisha na Nyamkala aliyefanya kazi miaka 9 alianza na mshahara wa 2mil kwa mwezi akafikia kiwango cha kulipwa 4.8mil kwa mwezi (hii ni performance based), lakini kwa huyu kibaraka wa Bi.Beatrice inashangaza kumuona ameanza tu na kiwango cha 4.8mil akiwa na miezi 2 tu kwenye mradi bila hata kuona performance.

Ilipoulizwa Bi. Beatrice aligeuka mbongo kiasi kwamba huyu kibaraka wake analipwa na allowance ya ziada 2mil ukijumlisha na mshahara wake 4.8+2=6.8mil ni aibu sana hii. Hili lilisimamiwa na mwanasheria mkuu wa wizara ya afya Maganga.

Bi. Beatrice ni fundi wa fitina alianikiwa kuwapa stress watumishi kadhaa akiwemo aliyekuwa Ass. Accountant Bwana Kidawa na aliyekuwa mtaalamu wa physiotherapy Doris waliamua kuacha kazi kwa hiari zao kwa kuona uozo huu uliokuwa unadhalilisha taaluma zao.

Lakini pia Bi. Beatrice ana akiba ya mtu anayeitwa Basila Dolla mwenye asili ya Somalia habari nyepesi zinasema kuwa huyu msomali ni Serengeti boy wake, huyu ni mkuu wa kitengo cha maabara na vipimo, huyu ndiye mtaalamu wa kuchonga dili za njia za panya kwa sababu anajua mbinu za kukwepa mitego kwa sababu ana mkono huko juu, na Bi. Bite amekuwa akimtumia kama mkono wake wa kazi.

Mungu apewe shukrani kwa sababu penye uozo bado pana kona yenye unafuu kidogo, ndani ya NTLP bado wapo watumishi wanaoishi kwa uvumilivu sana kiasi kwamba wanatamani mradi huu upinduliwe utawala ubadilike na mateso wanyoyapata waishe,

Bwana Msuya ambaye ni mwasibu mkuu wa mradi amekuwa mwiba kwa Bi. Beatrice na amekuwa akizuia ujinga mwingi ambao huyu mama amekuwa akitaka kuufanya, lakini sasa Bwana Msuya anaelekea kustaafu mwezi wa tano mwaka huu (05/2016) ambapo NTLP inahitaji mwasibu mpya

Bi. Beatrice ameshapanga majeshi yake sawasawa kwa ajili ya kumwajiri ndugu Lutashobya Lucas ambaye kwa sasa anafanya kazi katika taasisi binafsi ili iwe njia yake kukomba mboga zote.

Maswali

Ni usingizi gani katibu wa wizara umelala mpaka uchezewe na mwanasheria wako kiasi hicho?

Ni dharau kiasi gani tunayodharauliwa ikiwa pesa za mradi essential huu wa kifua kikuu na ukimwi tunapata zinaishia midomoni mwa walafi na hatimaye tunawekwa kwenye orodha ya walafi tunaochezea pesa za wangonjwa?

Waziri kesho utajitambulisha mbele ya mataifa kuwa wewe ni waziri wa afya wa Tanzania?

JE, utashangaa ukizomewa, kumbe kosa ni kutoona mambo ya kipumbavu kama haya?

Kwa sasa watu wenye maambukizi ya ukimwi wanaugua kifua kikuu wengi sana kwa sababu huduma kwao imeporomoka kisa ulafi wa Bi. Beatrice na watu wake

Kwa sababu mtu mwenye maambukizi ya ukimwi kinga zake hushuka na tahadhari ya magonjwa nyemelezi isopochukuliwa kifua kikuu huibuka na kumuua mtu.

USHAURI

Waziri Hamisi na katibu mkuu wa wizara ambao wote ni Technical leader (Madaktari) wasimame kidete kutumbua jipu hili na wahakikishe mwasibu mpya anapatikana kwa njia sahihi na vigezo na sio huyu mama kumwajiri mkono mwingine wa kukombea mboga.

Naitwa NYUNDO YA CHUMA NITAENDELEA KUFUNUA KILA IDARA, JIANDAENI WIZARA YA Mifugo mjiandae.
 
  • Thanks
Reactions: MZK
Kumbe palepale wizarani kuna jipu halafu utawaona Mawaziri wanazungukia vijipu upele kwenye hospitali za mkoa.
 
Moods these are not lumour mills, but investigative reports, so let them be alive open here
Dr Hamis Kigwangala na Katibu Mkuu Wizara ya Afya mna maslahi gani na jipu la NTLP lina usaha limeichafua Nchi na nyie mjiandae kuumeza usaha wake au kuutapika.

Nianze maandiko haya kwa kutoa tahadhari, jipu linaloonyesha dalili za kupasuka na likakosa kitu chenye ncha kali kulipasua, ipo siku litakuadhiri mbele za watu, kwani hata nguo yako tu uliyovaa ikiligusa litatumbuka na kukuchafua hadharani.

Leo naleta kwenu jipu hili lililolimbikiza bacteria (Abscessical Bacteria) kwa muda mrefu na kwa kuwa alikosekana mtumbuaji mwenye tahadhari leo linatumbuka hadharani kwa kuguswa na mate yake mwenyewe kwa sababu liko kwenye ulimi kabisa, hivyo usaha utamwagika na sijui kama mwenye jipu ataumeza ili kuficha aibu ili ahuharishe baadae kimyakimya au atautapika hadharani tumshangae.

Kwa ufupi mimi ni mpelelezi wa kujitolea naifanya kazi hii katika idara yeyote bila kujali lolote zaidi ya kutaka usafi katika idara za huduma kwa jamii, naitwa ‘NYUNDO YA CHUMA’

Mradi wa kifua kikuu na ukoma wenye tawi tanzu la kifua kikuu na ukimwi umekuwa ukifadhiliwa na watu wa marekani CDC kwa miaka kadhaa, CDC wamekuwa wakitoa pesa kwa ajili ya utafiti, mafunzo, tiba na vitendea kazi vingine, ili kuimarisha afya ya jamii, hasa kwenye upande wa kutokomeza kifua kikuu na ukoma, zoezi ambalo limefanikiwa sana ukanda wa kusini mwa jangwa la sahara.

CDC ndio mzazi na mlezi wa watu walioathirika kwa kifua kikuu na ukimwi, bila CDC huduma kwa watu hawa zingekuwa duni na zaidi sana tungewapoteza watu wengi sana kwa kukosa pesa za kuendeshea mafunzo na kupata vitendea kazi vya kutolea huduma na dawa.

CDC hutoa pesa kwa taasisi na nchi ambayo inatekeleza sawa na malengo, ikiwa tutakeleza ipasavyo ufadhili wao utaendelea kwa kiwango cha juu zaidi, na endapo tutaonekana kuyumba na matumizi yasiyoeleweka ufadhili utayumba pia.

Mpaka sasa Tanzania ikiwa na Mradi huu wa National Tb and Leprosy Program (NTLP) unaosimamiwa na wizara ya afya tumeshafeli na kushusha thamani ya umahili na elimu za watendaji wetu na taifa kwa ujumla, lakini pia uaminifu kwa wafadhili tumeupoteza kwa sababu mwaka jana NTLP ilipewa dola za kimarekani million 2, lakini tumeporomoka mpaka kupewa dolla za kimarekani 750,000/- na pengine hili jipu tunatakiwa tulitumbue likiwa mdomoni mwa aliyelilea na kumlazimisha ameze usaha wake ili akaharishe kimya kimya chooni kwake kuepusha kipindupindu mitaani.

Chanzo cha kuporomoka kwa kiasi hicho ni mtu mmoja tu anaitwa Beatrice Mtayoba ambaye ndiye mratibu wa mradi huu kitaifa, huyu mama ndiye chanzo cha matatizo yote katika mradi huu, anaitumia ofsi kwa manufaa yake binafsi kwa mfano;-

Amefanikiwa kuwakatisha tamaa watumishi wengine tamaa kwa kubuni njia mbalimbali za namna ya kuiba fedha za wafadhili kwa kuibua vimiradi vya hovyohovyo ambavyo anakuwa anashindwa kuvitolea maelezo

Kwa hali hiyo baadhi ya watumishi walianza kugomea mipango yake, lakini mwenzao kwa ufundi wake wa kiasili aliweza kuwahujumu mpaka wengine wakaacha kazi wenyewe na kutafuta maeneo mengine

Uwezo wake kiutendaji ni mbovu sana lakini alifanikiwa kumshika mwanasheria wa wizara ya afya Patricia Maganga akawa ndiye mshauri wake mkuu na kumzunguka katibu mkuu wa wizara,

Alifanikiwa kuwahujumu baadhi ya viongozi wenzake waliokuwa wakifanya mambo yaende kama yalivyopangwa, mfano alimhujumu Dr Nyamkala aliyekuwa mratibu wa kifua kikuu na ukimwi kwa kuzuia miradi iliyokuwa imeelekezwa na wafadhili kwa mwaka mzima akiwa anaikwamisha, huku akishirikiana na mwanasheria wa wizara ya afya Ndugu Patricia Maganga ambae amekuwa akishirikiana nae kwa kila mbinu chafu dhidi ya watumishi wenzake kwa sababu wana mahusiano yao ya siri kwa maana ya kunufaika na pesa hizi za miradi kwa sababu ili katibu mkuu wa wizara atie saini pesa za miradi zikachukuliwe ni lazima mwanasheria wa wizara ahusike, hivyo Bi. Betrice amekuwa akimtumia vilivyo na mambo yao yamenyooka huku wakiumiza wananchi waliotegemea kupata huduma safi na zenye weledi, hivi sasa takwimu za watu wanaoumia kwa kifua kikuu ni wengi kulinganisha na kipindi cha nyuma.

Lakini Bi. Beatrice ili afanikiwe kuwa salama na acheze michezo yake vizuri alimuondoa mwajiriwa wa mradi ambaye alikuwa Mratibu wa mradi wa kifua kikuu na ukimwi na kumzunguka kwa mgongo wa nyuma kupitia mwanasheria mkuu wa wizara wakafanikiwa kumwajiri kwenye nafasi hiyo mdogo wake wa kinasaba Dr. Wenzekoyi ambaye mpaka sasa cv yake ina utata hana uwezo kabisa wa kusimamia mradi huu, nay eye ni sababu namba mbili ya kupunguziwa ufadhili kwa sababu takwimu za mradi zimeshuka kabisa hana ubunifu, hafanyi kazi za maana zaidi ya kufanya kazi ya kutafuta wataalamu wa kuandika proposal ya namna ya kuchota pesa za mradi, ameanza kazi miezi kadhaa iliyopita lakini sasa ana gari V.8 hata kwa akili ya kawaida tu haingii akilini.

Hata mshahara anaolipwa ni aibu tupu na ni usaha tele, kwa mfano ukilinganisha na Nyamkala aliyefanya kazi miaka 9 alianza na mshahara wa 2mil kwa mwezi akafikia kiwango cha kulipwa 4.8mil kwa mwezi (hii ni performance based), lakini kwa huyu kibaraka wa Bi.Beatrice inashangaza kumuona ameanza tu na kiwango cha 4.8mil akiwa na miezi 2 tu kwenye mradi bila hata kuona performance.

Ilipoulizwa Bi. Beatrice aligeuka mbongo kiasi kwamba huyu kibaraka wake analipwa na allowance ya ziada 2mil ukijumlisha na mshahara wake 4.8+2=6.8mil ni aibu sana hii. Hili lilisimamiwa na mwanasheria mkuu wa wizara ya afya Maganga.

Bi. Beatrice ni fundi wa fitina alianikiwa kuwapa stress watumishi kadhaa akiwemo aliyekuwa Ass. Accountant Bwana Kidawa na aliyekuwa mtaalamu wa physiotherapy Doris waliamua kuacha kazi kwa hiari zao kwa kuona uozo huu uliokuwa unadhalilisha taaluma zao.

Lakini pia Bi. Beatrice ana akiba ya mtu anayeitwa Basila Dolla mwenye asili ya Somalia habari nyepesi zinasema kuwa huyu msomali ni Serengeti boy wake, huyu ni mkuu wa kitengo cha maabara na vipimo, huyu ndiye mtaalamu wa kuchonga dili za njia za panya kwa sababu anajua mbinu za kukwepa mitego kwa sababu ana mkono huko juu, na Bi. Bite amekuwa akimtumia kama mkono wake wa kazi.

Mungu apewe shukrani kwa sababu penye uozo bado pana kona yenye unafuu kidogo, ndani ya NTLP bado wapo watumishi wanaoishi kwa uvumilivu sana kiasi kwamba wanatamani mradi huu upinduliwe utawala ubadilike na mateso wanyoyapata waishe,

Bwana Msuya ambaye ni mwasibu mkuu wa mradi amekuwa mwiba kwa Bi. Beatrice na amekuwa akizuia ujinga mwingi ambao huyu mama amekuwa akitaka kuufanya, lakini sasa Bwana Msuya anaelekea kustaafu mwezi wa tano mwaka huu (05/2016) ambapo NTLP inahitaji mwasibu mpya

Bi. Beatrice ameshapanga majeshi yake sawasawa kwa ajili ya kumwajiri ndugu Lutashobya Lucas ambaye kwa sasa anafanya kazi katika taasisi binafsi ili iwe njia yake kukomba mboga zote.

Maswali

Ni usingizi gani katibu wa wizara umelala mpaka uchezewe na mwanasheria wako kiasi hicho?

Ni dharau kiasi gani tunayodharauliwa ikiwa pesa za mradi essential huu wa kifua kikuu na ukimwi tunapata zinaishia midomoni mwa walafi na hatimaye tunawekwa kwenye orodha ya walafi tunaochezea pesa za wangonjwa?

Waziri kesho utajitambulisha mbele ya mataifa kuwa wewe ni waziri wa afya wa Tanzania?

JE, utashangaa ukizomewa, kumbe kosa ni kutoona mambo ya kipumbavu kama haya?

Kwa sasa watu wenye maambukizi ya ukimwi wanaugua kifua kikuu wengi sana kwa sababu huduma kwao imeporomoka kisa ulafi wa Bi. Beatrice na watu wake

Kwa sababu mtu mwenye maambukizi ya ukimwi kinga zake hushuka na tahadhari ya magonjwa nyemelezi isopochukuliwa kifua kikuu huibuka na kumuua mtu.

USHAURI

Waziri Hamisi na katibu mkuu wa wizara ambao wote ni Technical leader (Madaktari) wasimame kidete kutumbua jipu hili na wahakikishe mwasibu mpya anapatikana kwa njia sahihi na vigezo na sio huyu mama kumwajiri mkono mwingine wa kukombea mboga.

Naitwa NYUNDO YA CHUMA NITAENDELEA KUFUNUA KILA IDARA, JIANDAENI WIZARA YA Mifugo mjiandae.
Inatia uvivu kuisoma
NB:kaiandikie makala kwenye gazeti la Jamhuri
 
image.jpeg
 
Dah! Utumishi wa Umma umbea ni mtaji! Ila nilichoona Mwandishi ni mjinga sana maanatuhuma zake zinajichanganya! Au Ana wivu wa kike!

Ninachoona mti wenye matunda ndiyo unaorushiwa mame, inaonekana huyu dada ni jembe! Uzuri Awamu hii haiangalii uzushi bali facts, rejea Hotuba ya Mhe. JPJM kwanini aliwateua Prof. Mhongo na Makonda, mtu anaweza dhani anachafua watu, kumbe anawapa promo...Dada chapa kazi ya kujenga taifa
 
Dah! Utumishi wa Umma umbea ni mtaji! Ila nilichoona Mwandishi ni mjinga sana maanatuhuma zake zinajichanganya! Au Ana wivu wa kike!

Ninachoona mti wenye matunda ndiyo unaorushiwa mame, inaonekana huyu dada ni jembe! Uzuri Awamu hii haiangalii uzushi bali facts, rejea Hotuba ya Mhe. JPJM kwanini aliwateua Prof. Mhongo na Makonda, mtu anaweza dhani anachafua watu, kumbe anawapa promo...Dada chapa kazi ya kujenga taifa
Ila wapo waliotuhumiwa na uchunguzi ukafanyika ukweli ukajulikana wakatumbuliwa, km hizi tuhuma ni za kweli AJIPANGE awahi hii haangaliwi mtu usoni.
 
Dah! Utumishi wa Umma umbea ni mtaji! Ila nilichoona Mwandishi ni mjinga sana maanatuhuma zake zinajichanganya! Au Ana wivu wa kike!

Ninachoona mti wenye matunda ndiyo unaorushiwa mame, inaonekana huyu dada ni jembe! Uzuri Awamu hii haiangalii uzushi bali facts, rejea Hotuba ya Mhe. JPJM kwanini aliwateua Prof. Mhongo na Makonda, mtu anaweza dhani anachafua watu, kumbe anawapa promo...Dada chapa kazi ya kujenga taifa
Inaelekea kuna unaloliua lakini tayari umechemka!!Mpelelezi gani ambaye hata insia ya Basra huijui?Inakuwae Basra awe serengeti boy wa Beatrice?
Jipange upya inawezekana una hoja lakini kwa sasa retreat and compose yourself.
 
Inaelekea kuna unaloliua lakini tayari umechemka!!Mpelelezi gani ambaye hata insia ya Basra huijui?Inakuwae Basra awe serengeti boy wa Beatrice?
Jipange upya inawezekana una hoja lakini kwa sasa retreat and compose yourself.

Soma comment yangu, tuko pamoja, ninamshangaa huyo na habari ambayo ukiiangalia una ona ni jungu lisilo na ukweli, habari imejichanganya sana
 
Nimeis
Dr Hamis Kigwangala na Katibu Mkuu Wizara ya Afya mna maslahi gani na jipu la NTLP lina usaha limeichafua Nchi na nyie mjiandae kuumeza usaha wake au kuutapika.

Nianze maandiko haya kwa kutoa tahadhari, jipu linaloonyesha dalili za kupasuka na likakosa kitu chenye ncha kali kulipasua, ipo siku litakuadhiri mbele za watu, kwani hata nguo yako tu uliyovaa ikiligusa litatumbuka na kukuchafua hadharani.

Leo naleta kwenu jipu hili lililolimbikiza bacteria (Abscessical Bacteria) kwa muda mrefu na kwa kuwa alikosekana mtumbuaji mwenye tahadhari leo linatumbuka hadharani kwa kuguswa na mate yake mwenyewe kwa sababu liko kwenye ulimi kabisa, hivyo usaha utamwagika na sijui kama mwenye jipu ataumeza ili kuficha aibu ili ahuharishe baadae kimyakimya au atautapika hadharani tumshangae.

Kwa ufupi mimi ni mpelelezi wa kujitolea naifanya kazi hii katika idara yeyote bila kujali lolote zaidi ya kutaka usafi katika idara za huduma kwa jamii, naitwa ‘NYUNDO YA CHUMA’

Mradi wa kifua kikuu na ukoma wenye tawi tanzu la kifua kikuu na ukimwi umekuwa ukifadhiliwa na watu wa marekani CDC kwa miaka kadhaa, CDC wamekuwa wakitoa pesa kwa ajili ya utafiti, mafunzo, tiba na vitendea kazi vingine, ili kuimarisha afya ya jamii, hasa kwenye upande wa kutokomeza kifua kikuu na ukoma, zoezi ambalo limefanikiwa sana ukanda wa kusini mwa jangwa la sahara.

CDC ndio mzazi na mlezi wa watu walioathirika kwa kifua kikuu na ukimwi, bila CDC huduma kwa watu hawa zingekuwa duni na zaidi sana tungewapoteza watu wengi sana kwa kukosa pesa za kuendeshea mafunzo na kupata vitendea kazi vya kutolea huduma na dawa.

CDC hutoa pesa kwa taasisi na nchi ambayo inatekeleza sawa na malengo, ikiwa tutakeleza ipasavyo ufadhili wao utaendelea kwa kiwango cha juu zaidi, na endapo tutaonekana kuyumba na matumizi yasiyoeleweka ufadhili utayumba pia.

Mpaka sasa Tanzania ikiwa na Mradi huu wa National Tb and Leprosy Program (NTLP) unaosimamiwa na wizara ya afya tumeshafeli na kushusha thamani ya umahili na elimu za watendaji wetu na taifa kwa ujumla, lakini pia uaminifu kwa wafadhili tumeupoteza kwa sababu mwaka jana NTLP ilipewa dola za kimarekani million 2, lakini tumeporomoka mpaka kupewa dolla za kimarekani 750,000/- na pengine hili jipu tunatakiwa tulitumbue likiwa mdomoni mwa aliyelilea na kumlazimisha ameze usaha wake ili akaharishe kimya kimya chooni kwake kuepusha kipindupindu mitaani.

Chanzo cha kuporomoka kwa kiasi hicho ni mtu mmoja tu anaitwa Beatrice Mtayoba ambaye ndiye mratibu wa mradi huu kitaifa, huyu mama ndiye chanzo cha matatizo yote katika mradi huu, anaitumia ofsi kwa manufaa yake binafsi kwa mfano;-

Amefanikiwa kuwakatisha tamaa watumishi wengine tamaa kwa kubuni njia mbalimbali za namna ya kuiba fedha za wafadhili kwa kuibua vimiradi vya hovyohovyo ambavyo anakuwa anashindwa kuvitolea maelezo

Kwa hali hiyo baadhi ya watumishi walianza kugomea mipango yake, lakini mwenzao kwa ufundi wake wa kiasili aliweza kuwahujumu mpaka wengine wakaacha kazi wenyewe na kutafuta maeneo mengine

Uwezo wake kiutendaji ni mbovu sana lakini alifanikiwa kumshika mwanasheria wa wizara ya afya Patricia Maganga akawa ndiye mshauri wake mkuu na kumzunguka katibu mkuu wa wizara,

Alifanikiwa kuwahujumu baadhi ya viongozi wenzake waliokuwa wakifanya mambo yaende kama yalivyopangwa, mfano alimhujumu Dr Nyamkala aliyekuwa mratibu wa kifua kikuu na ukimwi kwa kuzuia miradi iliyokuwa imeelekezwa na wafadhili kwa mwaka mzima akiwa anaikwamisha, huku akishirikiana na mwanasheria wa wizara ya afya Ndugu Patricia Maganga ambae amekuwa akishirikiana nae kwa kila mbinu chafu dhidi ya watumishi wenzake kwa sababu wana mahusiano yao ya siri kwa maana ya kunufaika na pesa hizi za miradi kwa sababu ili katibu mkuu wa wizara atie saini pesa za miradi zikachukuliwe ni lazima mwanasheria wa wizara ahusike, hivyo Bi. Betrice amekuwa akimtumia vilivyo na mambo yao yamenyooka huku wakiumiza wananchi waliotegemea kupata huduma safi na zenye weledi, hivi sasa takwimu za watu wanaoumia kwa kifua kikuu ni wengi kulinganisha na kipindi cha nyuma.

Lakini Bi. Beatrice ili afanikiwe kuwa salama na acheze michezo yake vizuri alimuondoa mwajiriwa wa mradi ambaye alikuwa Mratibu wa mradi wa kifua kikuu na ukimwi na kumzunguka kwa mgongo wa nyuma kupitia mwanasheria mkuu wa wizara wakafanikiwa kumwajiri kwenye nafasi hiyo mdogo wake wa kinasaba Dr. Wenzekoyi ambaye mpaka sasa cv yake ina utata hana uwezo kabisa wa kusimamia mradi huu, nay eye ni sababu namba mbili ya kupunguziwa ufadhili kwa sababu takwimu za mradi zimeshuka kabisa hana ubunifu, hafanyi kazi za maana zaidi ya kufanya kazi ya kutafuta wataalamu wa kuandika proposal ya namna ya kuchota pesa za mradi, ameanza kazi miezi kadhaa iliyopita lakini sasa ana gari V.8 hata kwa akili ya kawaida tu haingii akilini.

Hata mshahara anaolipwa ni aibu tupu na ni usaha tele, kwa mfano ukilinganisha na Nyamkala aliyefanya kazi miaka 9 alianza na mshahara wa 2mil kwa mwezi akafikia kiwango cha kulipwa 4.8mil kwa mwezi (hii ni performance based), lakini kwa huyu kibaraka wa Bi.Beatrice inashangaza kumuona ameanza tu na kiwango cha 4.8mil akiwa na miezi 2 tu kwenye mradi bila hata kuona performance.

Ilipoulizwa Bi. Beatrice aligeuka mbongo kiasi kwamba huyu kibaraka wake analipwa na allowance ya ziada 2mil ukijumlisha na mshahara wake 4.8+2=6.8mil ni aibu sana hii. Hili lilisimamiwa na mwanasheria mkuu wa wizara ya afya Maganga.

Bi. Beatrice ni fundi wa fitina alianikiwa kuwapa stress watumishi kadhaa akiwemo aliyekuwa Ass. Accountant Bwana Kidawa na aliyekuwa mtaalamu wa physiotherapy Doris waliamua kuacha kazi kwa hiari zao kwa kuona uozo huu uliokuwa unadhalilisha taaluma zao.

Lakini pia Bi. Beatrice ana akiba ya mtu anayeitwa Basila Dolla mwenye asili ya Somalia habari nyepesi zinasema kuwa huyu msomali ni Serengeti boy wake, huyu ni mkuu wa kitengo cha maabara na vipimo, huyu ndiye mtaalamu wa kuchonga dili za njia za panya kwa sababu anajua mbinu za kukwepa mitego kwa sababu ana mkono huko juu, na Bi. Bite amekuwa akimtumia kama mkono wake wa kazi.

Mungu apewe shukrani kwa sababu penye uozo bado pana kona yenye unafuu kidogo, ndani ya NTLP bado wapo watumishi wanaoishi kwa uvumilivu sana kiasi kwamba wanatamani mradi huu upinduliwe utawala ubadilike na mateso wanyoyapata waishe,

Bwana Msuya ambaye ni mwasibu mkuu wa mradi amekuwa mwiba kwa Bi. Beatrice na amekuwa akizuia ujinga mwingi ambao huyu mama amekuwa akitaka kuufanya, lakini sasa Bwana Msuya anaelekea kustaafu mwezi wa tano mwaka huu (05/2016) ambapo NTLP inahitaji mwasibu mpya

Bi. Beatrice ameshapanga majeshi yake sawasawa kwa ajili ya kumwajiri ndugu Lutashobya Lucas ambaye kwa sasa anafanya kazi katika taasisi binafsi ili iwe njia yake kukomba mboga zote.

Maswali

Ni usingizi gani katibu wa wizara umelala mpaka uchezewe na mwanasheria wako kiasi hicho?

Ni dharau kiasi gani tunayodharauliwa ikiwa pesa za mradi essential huu wa kifua kikuu na ukimwi tunapata zinaishia midomoni mwa walafi na hatimaye tunawekwa kwenye orodha ya walafi tunaochezea pesa za wangonjwa?

Waziri kesho utajitambulisha mbele ya mataifa kuwa wewe ni waziri wa afya wa Tanzania?

JE, utashangaa ukizomewa, kumbe kosa ni kutoona mambo ya kipumbavu kama haya?

Kwa sasa watu wenye maambukizi ya ukimwi wanaugua kifua kikuu wengi sana kwa sababu huduma kwao imeporomoka kisa ulafi wa Bi. Beatrice na watu wake

Kwa sababu mtu mwenye maambukizi ya ukimwi kinga zake hushuka na tahadhari ya magonjwa nyemelezi isopochukuliwa kifua kikuu huibuka na kumuua mtu.

USHAURI

Waziri Hamisi na katibu mkuu wa wizara ambao wote ni Technical leader (Madaktari) wasimame kidete kutumbua jipu hili na wahakikishe mwasibu mpya anapatikana kwa njia sahihi na vigezo na sio huyu mama kumwajiri mkono mwingine wa kukombea mboga.

Naitwa NYUNDO YA CHUMA NITAENDELEA KUFUNUA KILA IDARA, JIANDAENI WIZARA YA Mifugo mjiandae.

Nimeisoma vizuri article hii...... ukiachilia yooote kwa ufupi hoja ya msingi hapa inayojengwa ni kwamba utendaji mbovu wa Kiongozi wa taasisi hiyo umepelekea misaada kupungua kutoka usd 2M hadi dola 750,000 na matokeo yake huduma za TB zinazotolewa bure na serikali zimeathirika na wagonjwa wengi wameumia.

Kwa taarifa zilizopo kwenye public domain....programu ya Serikali ya kutoa matibu ya TB kwa wananchi bure bado inaendelea na inatolewa kwenye hospitali na vituo vya afya vya serikali na sekta binafsi. Hivyo athari zinazoongelewa hapa sio kweli

Pili, ninachojua Wizara ya Afya imekuwa na changamoto ya kibajeti iliyoathiri idara mbalimbali ikiwemo hospitali ya taifa ya muhimbili ambayo ilibidi ifanyike intervention ya Bwana Mkubwa ili mambo yaende sawa....hivyo programu ya TB kukosa fedha za kutosha sio jambo la kushangaza......

Tatu, wafadhili waliokuwa wanasaidia programu mbalimbali za afya wamepunguza misaada yao kwa taasisi za kimataifa zinazofadhili programu ya TB na ukimwi ya Global Fund for HIV,Tuberculosis na malaria....ndio maana misaada iliyokuwa inakuja kwenye programu ya TB ya Tanzania imepungua kama alivyosema mtoa taarifa japo hapa anadai imepungua sababu ya uongozi....ukitaka taarifa sahihi juuu ya fedha za ufadhili zilivyopungua angalia link hiihttp://www.healthmap.org/site/diseasedaily/article/gfatm-cuts-hiv-funding-sub-saharan-africa-carries-greatest-burden-113011

Reference alizotoa mtoa mada juu ya wafanyakazi kuondoka....taarifa zilizopo si kweli kwamba watumishi wengi wameondoka. Wapo wachache walioondoka kwasababu wamepata greener pasture elsewhere kwenye NGOs na research programmes zilozopo nchini....siwashangai wala kuwalaumu...mtu hawezi kuacha fursa ya kuhamia mahala pengine kwa mshahara wa usd 4000 kwa mwezi sawa na Shs milioni 8, kisa anabakia kwenye TB programme inayomlipa sh milioni 3.

Nimeshangazwa...mtoa mada anajenga hoja kwa kireeeefu alafu mwisho wake ushauri anaoutoa eti apatikane mhasibu mpya....Mhasibu ndio anayeleta pesa? Hivi mwandishi hajui pesa zinaletwa na wataalam wanaoandika miradi?
 
Hizi ni tuhuma, tusubiri wahusika wazifanyie kazi ili ukweli ujulikane. Asionewe au kupendelewa mtu hapa.
 
By 2020 Tz itakuwa na passo na ist nyingi sana kuliko nchi yeyote afrika...maana wapiga deal waendesha ma v8 hawatakuwepo
 
Well kama kigezo cha fedha za msaada ni effective program na donors wamepunguza funding maana yake ni moja tu huyo mama ni jipu kweli.

But then Tanzania ni nchi ambayo serikari mwezi huu tu imetoa karibu t/sh80 billions kwenye moja ya taasisi zake na kwa mwaka wanaichangia karibu t/sh500 billioni halafu raisi wa nchi anaenda kuomba wakurugenzi wa hiyo taasisi maji ya mabwawa ya kuzalisha umeme yasifunguliwe, shirika lenyewe lina hasara miaka nenda miaka rudi, waziri anazungukuka akibembeleza uzalendo kwenye utendaji and no one cares about end results. Sidhani kama uchakachuaji wa $2m dollars ni swala ambalo linawanyima usingizi na wala usishangae kuitwa mpika majungu ata kama ushahidi huko wazi.

People just dont care how things are done in Tanzania wao wanachojali ni kwenye kukamua wale wanaotakiwa kuwapa hela za kupeleka kwenye taasisi zao zinazo ongozwa na useless people; huko sasa ndio awana mzaha mpaka na wauza maandazi mtaani.
 
Nimeis


Nimeisoma vizuri article hii...... ukiachilia yooote kwa ufupi hoja ya msingi hapa inayojengwa ni kwamba utendaji mbovu wa Kiongozi wa taasisi hiyo umepelekea misaada kupungua kutoka usd 2M hadi dola 750,000 na matokeo yake huduma za TB zinazotolewa bure na serikali zimeathirika na wagonjwa wengi wameumia.

Kwa taarifa zilizopo kwenye public domain....programu ya Serikali ya kutoa matibu ya TB kwa wananchi bure bado inaendelea na inatolewa kwenye hospitali na vituo vya afya vya serikali na sekta binafsi. Hivyo athari zinazoongelewa hapa sio kweli

Pili, ninachojua Wizara ya Afya imekuwa na changamoto ya kibajeti iliyoathiri idara mbalimbali ikiwemo hospitali ya taifa ya muhimbili ambayo ilibidi ifanyike intervention ya Bwana Mkubwa ili mambo yaende sawa....hivyo programu ya TB kukosa fedha za kutosha sio jambo la kushangaza......

Tatu, wafadhili waliokuwa wanasaidia programu mbalimbali za afya wamepunguza misaada yao kwa taasisi za kimataifa zinazofadhili programu ya TB na ukimwi ya Global Fund for HIV,Tuberculosis na malaria....ndio maana misaada iliyokuwa inakuja kwenye programu ya TB ya Tanzania imepungua kama alivyosema mtoa taarifa japo hapa anadai imepungua sababu ya uongozi....ukitaka taarifa sahihi juuu ya fedha za ufadhili zilivyopungua angalia link hiihttp://www.healthmap.org/site/diseasedaily/article/gfatm-cuts-hiv-funding-sub-saharan-africa-carries-greatest-burden-113011

Reference alizotoa mtoa mada juu ya wafanyakazi kuondoka....taarifa zilizopo si kweli kwamba watumishi wengi wameondoka. Wapo wachache walioondoka kwasababu wamepata greener pasture elsewhere kwenye NGOs na research programmes zilozopo nchini....siwashangai wala kuwalaumu...mtu hawezi kuacha fursa ya kuhamia mahala pengine kwa mshahara wa usd 4000 kwa mwezi sawa na Shs milioni 8, kisa anabakia kwenye TB programme inayomlipa sh milioni 3.

Nimeshangazwa...mtoa mada anajenga hoja kwa kireeeefu alafu mwisho wake ushauri anaoutoa eti apatikane mhasibu mpya....Mhasibu ndio anayeleta pesa? Hivi mwandishi hajui pesa zinaletwa na wataalam wanaoandika miradi?

Salaama hoja zako zina mashiko....nimesoma alichosema mtoa mada na ulichosema wewe kuna mambo ya msingi hayajakaa sawa.
Mtoa mada amejichanganya anaposema Mkuu wa mradi anabuni njia mbalimbali za namna ya kuiba fedha za wafadhili kwa " kuibua vimiradi vya hovyohovyo ambavyo anashindwa kuvitolea maelezo, na hivyo watumishi kugomea mipango yake" kama ulivyomalizia Salaama nijuavyo mimi upatikanaji wa fedha kwa miradi ya wafadhili huandikwa na kundi la wataalamu wengi ndani ya miradi husika wakisaidiwa na wafadhili wenyewe. Inashangaza kuona mtoa mada hana hata facts ya jinsi miradi inavyopatikana.

Pili mtoa mada hajawa mkweli au ana ufahamu mdogo juu ya transaction za fedha Serikalini zinavyofanyika aliposema kuwa pesa za Wizara hazitoki mpaka mwanasheria wa Wizara ahusike. Kwa mtu anayefahamu taratibu za kiuhasibu ndani ya Wizara iko wazo kuwa mwanasheria hana nafasi yeyote katika kuidhinisha malipo ya Wizara au programu.

Inavyoonekana huyu mtoa mada ni mtu wa ndani tena wa ngazi ya chini mwenye issue na Bosi wake akaamua kuja kucheulia humu kwenye jukwaa la great thinkers. Ajipange vizuri tu kama anazo hoja na sio kuleta half-cooked allegations
 
Salaama hoja zako zina mashiko....nimesoma alichosema mtoa mada na ulichosema wewe kuna mambo ya msingi hayajakaa sawa.
Mtoa mada amejichanganya anaposema Mkuu wa mradi anabuni njia mbalimbali za namna ya kuiba fedha za wafadhili kwa " kuibua vimiradi vya hovyohovyo ambavyo anashindwa kuvitolea maelezo, na hivyo watumishi kugomea mipango yake" kama ulivyomalizia Salaama nijuavyo mimi upatikanaji wa fedha kwa miradi ya wafadhili huandikwa na kundi la wataalamu wengi ndani ya miradi husika wakisaidiwa na wafadhili wenyewe. Inashangaza kuona mtoa mada hana hata facts ya jinsi miradi inavyopatikana.

Pili mtoa mada hajawa mkweli au ana ufahamu mdogo juu ya transaction za fedha Serikalini zinavyofanyika aliposema kuwa pesa za Wizara hazitoki mpaka mwanasheria wa Wizara ahusike. Kwa mtu anayefahamu taratibu za kiuhasibu ndani ya Wizara iko wazo kuwa mwanasheria hana nafasi yeyote katika kuidhinisha malipo ya Wizara au programu.

Inavyoonekana huyu mtoa mada ni mtu wa ndani tena wa ngazi ya chini mwenye issue na Bosi wake akaamua kuja kucheulia humu kwenye jukwaa la great thinkers. Ajipange vizuri tu kama anazo hoja na sio kuleta half-cooked allegations

Tatizo tanzania Ina wajinga wengi, Kama huyu mtoa mada Eti Nndiyo mtaalam huyo! Watu wa aina hii kwenye UTUMISHI mara nyingi ni wajinga, wavivu, wazembe waliozoea kubebwa, ili aweze kubaki ofisini Ndiyo kuibua tuhuma za uongo
 
Back
Top Bottom