:A S embarassed:
KAHAMA, 05 Jan 2012
MBUNGE wa jimbo la msalala wilayani kahama, mkoani Shinyanga, Ezekiel Maige ametoa shilingi milioni 500, zilizozutumika katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo.
Mbunge huyo ambaye pia ni Waziri wa Maliasili na Utalii amesema fedha hizo zimetumika kuboresha elimu katika shule za sekondari za kata, barabara na ujenzi wa zahanati za vijiji.
Akizungumza katika kata ya Busangi, Waziri Maige amesema fedha hizo zimetumika kujenga Mabweni kwenye shule ya sekondari ya kata ya Isaka, Lunguya na Segese na madawati300 yaliyogawiwa kwenye shule tisa za sekondari katika jimbo la msalala.
Amesema katika fedha hizo, pia zimesaidia ununuzi wa mifuko 1200 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa zahanati za vijiji pamoja na ufungaji umeme wa Sora kwenye shule ya sekondari ya kata ya Ntobo na Ngaya pamoja na utafiti wa majiya visima virefu kwenye vijiji 32.
Kutokana na idadi ya ufaulu kuongezeka wilayani kahama, Waziri Maige amewataka wananachi kuhakikisha wanafanikisha ujenzi wa madarasa mapya ya shule za sekondari.
Maswali ya Kujiuliza
1. Kapata wapi fedha hizo Milioni 500TZS ?
2. Je, hayo siyo majukumu ya serikali ?
3. Vipi sehemu ambazo hazina watu matajiri kama Maige ?
4. Je, hili haliwezi kujenga hali ya serikali kuachia wabunge majukumu yake ?
5. Je, hili haliwezi kupelekea wabunge wengine wenye nafasi kushindana kuiba ili nao wapeleke majimboni kwao?
NB: Tukumbuke moja ya kazi za Mbunge ni kuongoza shughuli za maendeleo kutokana na fedha zinazotolewa na Serikali, na sio kugharamia shughuli za maendeleo.
...
KAHAMA, 05 Jan 2012
MBUNGE wa jimbo la msalala wilayani kahama, mkoani Shinyanga, Ezekiel Maige ametoa shilingi milioni 500, zilizozutumika katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo.
Mbunge huyo ambaye pia ni Waziri wa Maliasili na Utalii amesema fedha hizo zimetumika kuboresha elimu katika shule za sekondari za kata, barabara na ujenzi wa zahanati za vijiji.
Akizungumza katika kata ya Busangi, Waziri Maige amesema fedha hizo zimetumika kujenga Mabweni kwenye shule ya sekondari ya kata ya Isaka, Lunguya na Segese na madawati300 yaliyogawiwa kwenye shule tisa za sekondari katika jimbo la msalala.
Amesema katika fedha hizo, pia zimesaidia ununuzi wa mifuko 1200 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa zahanati za vijiji pamoja na ufungaji umeme wa Sora kwenye shule ya sekondari ya kata ya Ntobo na Ngaya pamoja na utafiti wa majiya visima virefu kwenye vijiji 32.
Kutokana na idadi ya ufaulu kuongezeka wilayani kahama, Waziri Maige amewataka wananachi kuhakikisha wanafanikisha ujenzi wa madarasa mapya ya shule za sekondari.
Maswali ya Kujiuliza
1. Kapata wapi fedha hizo Milioni 500TZS ?
2. Je, hayo siyo majukumu ya serikali ?
3. Vipi sehemu ambazo hazina watu matajiri kama Maige ?
4. Je, hili haliwezi kujenga hali ya serikali kuachia wabunge majukumu yake ?
5. Je, hili haliwezi kupelekea wabunge wengine wenye nafasi kushindana kuiba ili nao wapeleke majimboni kwao?
NB: Tukumbuke moja ya kazi za Mbunge ni kuongoza shughuli za maendeleo kutokana na fedha zinazotolewa na Serikali, na sio kugharamia shughuli za maendeleo.
...