A
Anonymous
Guest
Habari Wakuu?
Nimepita Mitaa ya Mikocheni leo na kukuta Kituo cha Mafuta cha Barrel kilichopo Mikocheni kinaendelea kufanya kazi ikiwa ni takriban mwezi mmoja tangu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa kusimamisha matumizi ya Kituo cha Mafuta cha Barrel Petrol Energy cha Mikocheni jijini Dar es salaam.
Soma: Waziri Silaa apiga marufuku ujenzi holela wa Vituo vya Mafuta na kusimamisha matumizi ya Kituo cha mafuta cha Barrel cha Mikocheni
Napata wakati mgumu sana na kusema Serikali inadharau sana Wananchi wake. Waziri Jerry Silaa alipotembela alisema kabisa yeye si mtoto wa masikini na hawezi kuchukua rushwa japo alitafutwa na wenye Kituo ili waweze kumpatia Milioni 300 na akataa. Lakini leo Kituo hiki kinafanya kazi na tangu baada ya tamko la Waziri hatujawahi kuambiwa nini kilitokea lakini sasa tunaona Kituo kinafanya kazi.
Soma: Waziri Jerry Slaa: Mimi siyo Mtoto wa Maskini, baba yangu alikuwa Rubani. Nimekataa Rushwa ya Milioni 300 | JamiiForums
Nikukumbushe Waziri Silaa, ulipokuwa kwenye Kituo hiki ulisema Mchakato wa kujenga Kituo hicho haujafuata taratibu na pia nikukumbushe kuwa Wananchi tunacholilia ni ujenzi wa vituo vya mafuta karibu na Mkazi ya Watu. Kituo hiki iwapo kutatokea shida hapa ama mlipuko madhara yake hayatakuwa ya kawaida.
Je, nikuulize Waziri ulikuwa unafanya maigizo kama wenzako wengine? Nini kimetokea hadi Kituo hiki kikaendelea kufanya Kazi hatua gani zilichukuliwa? Hukuona haja ya kuufahaamisha Umma kama ambavyo uliufahamisha ulipokwenda pale kusitisha matumizi?
Nimepita Mitaa ya Mikocheni leo na kukuta Kituo cha Mafuta cha Barrel kilichopo Mikocheni kinaendelea kufanya kazi ikiwa ni takriban mwezi mmoja tangu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa kusimamisha matumizi ya Kituo cha Mafuta cha Barrel Petrol Energy cha Mikocheni jijini Dar es salaam.
Soma: Waziri Silaa apiga marufuku ujenzi holela wa Vituo vya Mafuta na kusimamisha matumizi ya Kituo cha mafuta cha Barrel cha Mikocheni
Napata wakati mgumu sana na kusema Serikali inadharau sana Wananchi wake. Waziri Jerry Silaa alipotembela alisema kabisa yeye si mtoto wa masikini na hawezi kuchukua rushwa japo alitafutwa na wenye Kituo ili waweze kumpatia Milioni 300 na akataa. Lakini leo Kituo hiki kinafanya kazi na tangu baada ya tamko la Waziri hatujawahi kuambiwa nini kilitokea lakini sasa tunaona Kituo kinafanya kazi.
Soma: Waziri Jerry Slaa: Mimi siyo Mtoto wa Maskini, baba yangu alikuwa Rubani. Nimekataa Rushwa ya Milioni 300 | JamiiForums
Nikukumbushe Waziri Silaa, ulipokuwa kwenye Kituo hiki ulisema Mchakato wa kujenga Kituo hicho haujafuata taratibu na pia nikukumbushe kuwa Wananchi tunacholilia ni ujenzi wa vituo vya mafuta karibu na Mkazi ya Watu. Kituo hiki iwapo kutatokea shida hapa ama mlipuko madhara yake hayatakuwa ya kawaida.
Je, nikuulize Waziri ulikuwa unafanya maigizo kama wenzako wengine? Nini kimetokea hadi Kituo hiki kikaendelea kufanya Kazi hatua gani zilichukuliwa? Hukuona haja ya kuufahaamisha Umma kama ambavyo uliufahamisha ulipokwenda pale kusitisha matumizi?