EasyFit
JF-Expert Member
- Jul 4, 2011
- 1,269
- 1,082
Watu sita wamekamatwa na polisi wilayani Arumeru, watatu kati yao kwa tuhuma za mauaji ya aliyekuwa mwenyekiti wa Chadema, Kata ya Usa River, Msafiri Mmbwambo, na wengine kwa tuhuma za uvamizi wa mashamba ya wawekezaji.
Habari zilizopatikana jijini hapa jana na kuthibitishwa na Naibu Kamishna wa Polisi, (DCP), Isaya Mngulu, zilisema jana kuwa waliokamatwa ni wenyeviti wa vitongoji vitatu, lakini hawakubainisha kama ni viongozi wa chama gani.
DCP Mngulu hakutaka kutaja majina wala kuthibitisha kwamba waliokamatwa ni wenyeviti na wa vitongoji gani. Marehemu Mbwambo aliuawa kinyama wiki iliyopita kwa kuchinjwa na mwili wake uliokotwa kando ya makaburi wilayani humo.
CHANZO: NIPASHE
Habari zilizopatikana jijini hapa jana na kuthibitishwa na Naibu Kamishna wa Polisi, (DCP), Isaya Mngulu, zilisema jana kuwa waliokamatwa ni wenyeviti wa vitongoji vitatu, lakini hawakubainisha kama ni viongozi wa chama gani.
DCP Mngulu hakutaka kutaja majina wala kuthibitisha kwamba waliokamatwa ni wenyeviti na wa vitongoji gani. Marehemu Mbwambo aliuawa kinyama wiki iliyopita kwa kuchinjwa na mwili wake uliokotwa kando ya makaburi wilayani humo.
CHANZO: NIPASHE