Mauaji ya kutisha yafanyika Wilayani Mwanga. Rais tafadhali ingilia kati uisaidie hii familia

Ntu

JF-Expert Member
Sep 9, 2011
951
552
Wakuu nawasalimu kwa jina la JMT.

Jana nilifanikiwa kufika Wilayani Mwanga katika Kijiji cha Mangyo, kitongoji cha Vongo B. Kuna Mama mwenye umri wa zaidi ya miaka 80, ambaye tarehe 01/11 majira ya saa 1:45 Usiku, wakati akipika chakula chake cha usiku, alivamiwa na kuchinjwa shingo yake kama kuku! Haijaishia hapo, watu hao walimpiga mume wa marehemu kichwani na kumkata mkono, na baada ya mauaji hayo watuumiwa walitokomea kusikojulikana!

Cha kushangaza baada ya polisi kupewa taarifa, walifika 2/11 na kiuchukua mwili na kuupeleka mochwari ya Kijiji inayoitwa Kifula, na 3/11 ndugu wa marehemu waliofuatilia hilo suala wakaambiwa na CID wa wilaya kwamba wanaweza wakauzika huo mwili!

Msaada hii familia inayohitaji ni ifuatayo:

1. Kwanini police iruhusu mwili uzikwe angali upelelezi/majibu ya mauaji hayajakamilika/hayajatolewa kwa familia?

2. Mauaji haya siyo ya kwanza kwani Kuna watu wengine walishauliwa katika mazingira kama haya na hakukuwa na ufuatiliaji wa polisi, hivyo inaonekana mauaji haya Yana baraka ya polisi/Mkuu wa wilaya!

3. Diwani wa eneo hilo (Maradona), wiki mbili kabla ya mauaji haya, aliitaka familia hii imrudishe marehemu nyumbani kwake kwani aliwahakikishia usalama wake, na baada ya marehemu kurudi tu, ndipo mauaji haya yakafanyika! Je bwana Maradona hajahusika katika mauaji haya? Pia izingatiwe kuwa Maradona ana undugu na watuhumiwa (mfano ni urafiki/ukaribu wake na bwana Mashauri ambaye ni kati ya watuhumiwa wa mauaji haya), hivyo anatumia cheo chake cha udiwani kuiangamiza hii familia.

4. Je, usalama wa hiyo familia itakuwa mikononi mwa nani? Ikizingatiwa hii familia inaendelea kupokea vitisho kutoka katika familia ya Mashauri? Ikumbukwe, mume wa marehemu ni mgonjwa Sana baada yakukatwa kichwani na kuvunjwa mkono, pia mtoto mkuwa wa marehemu (Judika Yohana Mfinanga) anaendelea kupokea vitisho toka Kwa bwana Mashauri.

Maziko yanatakiwa kufanyika kesho juma tatu, ila chondochonde Mheshiwa Rais, naomba uingilie kati mauaji haya na ikiwezekana marehemu asizikwe kesho mpaka uchunguzi wakina ufanyike.

CC:
1. Mkuu wa wilaya ya mwanga
2. CID mwanga
3.Mkuu wa mkoa wa Kilimajaro
4. @PaulMakonda
5. Waziri Mkuu Kasim Majaliwa
6. Mh. Rais
7.Vyombo vya habari mkoa wa Kilimanjaro

NB: Samahani kwa uandishi mbaya.
 
Wakuu nawasalimu kwa jina la JMT.

Jana nilifanikiwa kufika Wilayani Mwanga katika Kijiji cha Mangyo, kitongoji cha Vongo B. Kuna Mama mwenye umri wa zaidi ya miaka 80, ambaye tarehe 01/11 majira ya saa 1:45 Usiku, wakati akipika chakula chake cha usiku, alivamiwa na kuchinjwa shingo yake kama kuku! Haijaishia hapo, watu hao walimpiga mume wa marehemu kichwani na kumkata mkono, na baadae ya mauaji hayo watuumia walitokomea kusiko julikana! Chakushangaza baada ya polisi kupewa taarifa, walifika 2/11 na kiuchukua mwili na kuupeleka mochwari ya Kijiji inayoitwa Kifula, na 3/11 ndugu wa marehemu waliofuatilia hilo swala wakaambiwa na CID wa wilaya kwamba wanaweza wakauzika huo mwili! Msaada hii familia inayohitaji ni ifuatayo:
1. Kwa nini police iruhusu mwili uzikwe angali upelelezi/majibu ya mauaji hayajakamilika/hayajatolewa kwa familia?
2. Mauaji haya siyo ya kwanza kwani Kuna watu wengine walisha uliwa Kwa mazingira kama haya na hakukuwa na ufwatiliaji wa polisi, hvyo inaonekana mauaji haya Yana baraka ya polisi/Mkuu wa wilaya!
3. Diwani wa eneo hilo (Maradona), wiki mbili kabla ya mauaji haya, aliitaka familia hii imrudishe marehe nyumbani kwake kwani aliwahakikishia usalama wake, na baada ya marehemu kurudi tu, ndipo mauaji haya yakafanyika! Je bwana Maradona hajahusika katika mauaji hay? Pia izingatiwe kuwa Maradona anaundugu na watuhumiwa (mfano ni urafiki/ukaribu wake na bwana Mashauri ambaye ni kati ya watuhumiwa wa mauaji haya), hvyo anatumia cheo chake cha udiwani kuiangamiza hii familia.
4. Je usalama wa hiyo familia itakuwa mikononi mwa nani? Ikizingatiwa hii familia inaendelea kupokea vitisho kutoka katika familia ya Mashauri? Ikumbukwe, mume wa marehemu ni mgonjwa Sana baada yakukatwa kichwani na kuvunjwa mkono, pia mtoto mkuwa wa marehemu (Judika Yohana Mfinanga) anaendelea kupokea vitisho toka Kwa bwana Mashauri.

Maziko yanatakiwa kufanyika kesho juma tatu, ila chondochonde Mheshiwa Raisi, naomba uingilie kati mauaji haya na ikiwezekana marehemu asizikwe kesho mpaka uchunguzi wakina ufanyike.

CC:
1. Mkuu wa wilaya ya mwanga
2. CID mwanga
3.Mkuu wa mkoa wa Kilimajaro
4. @PaulMakonda
5. Waziri Mkuu Kasim Majaliwa
6. Mh. Raisi
7.Vyombo vya habari mkoa wa Kilimanjaro

NB: Samahani kwa uandishi mbaya.
Mshirikishe mwanasheria akusaidie. Pole sana, very sad!
 
Sijaelewa,huyo Bwana Maradona aliitaka hiyo Familia imrudishe Marehemu nyumbani kutoka wapi??alikuwa mafichoni au??

Sent from my Infinix X6511B using JamiiForums mobile app
Mkuu dadamlamayao , huyo bibi baada yakupata vitisho, wanae walimchukua na kuishi nae Arusha, sasa 2 wks ago, Maradona aliwapigia simu watoto wa huyo mama akawaambia wamrudishe nyumbani kwani yeye kama diwani anamuhakishia usalama huyo mama, sasa baa ya huyo mama kurudishwa nyumbani, haijapita wk akauliwa....
 
Na pia rekebisha kichwa cha habari,hayo si mauaji ya kutisha,mauaji ya Kanyanabo kama sikosei yalitokea Shinyanga ndio yalikuwa hatari maana mpaka vitoto vidogo vilipigwa mapanga kama sehemu ya kulipiza kisasi,tafuta kuna Uzi humu unaoelezea yale mauaji
Sent from my Infinix X6511B using JamiiForums mobile app
 
Poleni kwa Msiba uliotokana na Mauaji hayo ya Kinyama.

Ushauri wangu pamoja na hizo taratibu za mazishi yaliyofanyika, kuna haja Huyo Mhe. Diwani awekwe mahabusu kwaajili ya kusaidia Upelelezi.

Lakini kuna haja nanyi Wananchi mzizonge zonge Mamlaka kuwataka wawasaidie kupunguza hayo Mauaji, maana kupitia maelezo yako ni kuwa Vifo vya namna hiyo vimekuwa vingi hapo Mwanga.
 
Marehemu alipelekwa wapi alikotakiwa arudishwe, diwani anasema atahakikisha usalama wake, maana yake aliondoka sababu hakuna usalama, nani alietishia usalama wake, mtoto wake unadai anatishwa, kafanya nini hadi atishiwe, kwa nini unadhani polisi wako kinyume na marehemu?

Mtoa mada umeficha vitu vingi kuhusu familia ya maeehemu ambavyo vingetuongezea uelewa wa tukio
 
Mkuu chanzo cha ugomvi ni story ndefu, ninachoweza kusaidia ni kutoa namba za wahanga hapa alafu serikali iwaaidie. Narusha hizi namba hapa muda sio mrefu Mkuu...
Weka namba hapa mkuu
 
Poleni kwa Msiba uliotokana na Mauaji hayo ya Kinyama.

Ushauri wangu pamoja na hizo taratibu za mazishi yaliyofanyika, kuna haja Huyo Mhe. Diwani awekwe mahabusu kwaajili ya kusaidia Upelelezi.

Lakini kuna haja nanyi Wananchi mzizonge zonge Mamlaka kuwataka wawasaidie kupunguza hayo Mauaji, maana kupitia maelezo yako ni kuwa Vifo vya namna hiyo vimekuwa vingi hapo Mwanga.
Ni kweli Mkuu. Nitaweka namba za watoto wa Wahanga hapa muda sio mrefu ili serikali iwasaidie Mkuu...
 
Marehemu alipelekwa wapi alikotakiwa arudishwe, diwani anasema atahakikisha usalama wake, maana yake aliondoka sababu hakuna usalama, nani alietishia usalama wake, mtoto wake unadai anatishwa, kafanya nini hadi atishiwe, kwa nini unadhani polisi wako kinyume na marehemu?

Mtoa mada umeficha vitu vingi kuhusu familia ya maeehemu ambavyo vingetuongezea uelewa wa tukio
Please waulize wahusika, mie nilisaidia kutoa taarifa ili wasidike: Namba za wahanga ni: 0766430284 0689512555 & 0672740412
 
Marehemu alipelekwa wapi alikotakiwa arudishwe, diwani anasema atahakikisha usalama wake, maana yake aliondoka sababu hakuna usalama, nani alietishia usalama wake, mtoto wake unadai anatishwa, kafanya nini hadi atishiwe, kwa nini unadhani polisi wako kinyume na marehemu?

Mtoa mada umeficha vitu vingi kuhusu familia ya maeehemu ambavyo vingetuongezea uelewa wa tukio
Namba za wahanga ni: 0766430284 0689512555 & 0672740412
 
Back
Top Bottom