Watoto wa Mjini Dar

Mkuu, unayejiita mtoto wa mjini, mbona unajiumbua? Hakuna kitu kama SINSEI. Karibu na daraja la salenda palikuwa na Italian Club. Mbele kidogo palikuwa na San Sui. San Sui ilikuwa kwenye hoteli ya Sea View ambayo siku hizi imebadilishwa kuwa Courtyard Hotel. Hata sisi wakuja tulikuwa tunajimwaga humo. Commodores ( Easy n.k.), Santana, Millie Jackson, Brass Construction n.k. mtindo mmoja. Hamna bolingo wakati ule.


Fundi Mchundo inaonekana mwenyeji sana mitaa ya Upanga mashariki, sea view na vitongoji hivyo, ile Etiennes mbele ya Seaview iliishia wapi? palikuwa panachomwa kuku safi sana pale.

Salender Bridge Club baada ya Disco Sansui, nadhani walifuatia Disco Biribi la Joseph Kusaga, au Jetset Dj Ratchie Cutty (Raph Chambo)

Sehemu nyingine za kujiburudisha katikati ya wiki ilikuwa Railways Club Gerezani, mwisho wa wiki Gymkhana Club, enzi hizo Movie za James Bond ndio zinatamba, au nyama choma na utumbo BOT club, Jumapili mchana kule mtoni.
Mind you, sehemu nyingi zilikuwa Members Only :(
 
Hii thread nimeifurahia. ...ila niulize tu; hawa wakuu waliokuwa wanaongoza huu mjadala bado wako hai ukiachana na NN ambae huwa namuona mara kwa mara?? Manake 2008 hadi 2014 ni parefu.
 
Hii thread nimeifurahia. ...ila niulize tu; hawa wakuu waliokuwa wanaongoza huu mjadala bado wako hai ukiachana na NN ambae huwa namuona mara kwa mara?? Manake 2008 hadi 2014 ni parefu.
wapo, sana tu sema wanatumia new ID kama ambavyo NasDaz aliamua kutumia new ID kwa sababu fulani fulani!
 
Basi tumekubali

hivi unajua SAIDI MOLEL yuko wapi?

Hivi ni kweli Ray alikamatwa Umangani?

halafu unakumbuka kile kijiwe cha lile block la kule kama unaelekea kwa WANYALUKOLO? kijiwe kile kilikuwa cha machizi wanaotaka kwenda SAUZI tuuuu

Hahahahahaha aisee nmekumbuka mbali sana
 
Hao jamaa wapo sana tembelea kule siasa utawakuta though wengine walichange IDs zao.

Hii thread nimeifurahia. ...ila niulize tu; hawa wakuu waliokuwa wanaongoza huu mjadala bado wako hai ukiachana na NN ambae huwa namuona mara kwa mara?? Manake 2008 hadi 2014 ni parefu.
 
Kile kishule cha vidudu? Mie nilikataa kusoma hapo miaka hiyo kwani nilijua nikirudi kijijini, kaka zangu watanicheka sana kuwa nilisoma shule ya VIDUDU na mie pia ni kidudu.
SIdhani kama utakuwa unanifahamu kwani sikuwa mwenyeji sana zaidi ya jamaa wa Block 4 kama akina Rashidi, Mohamed, Deo na kaka zake, Ray, nk. Kwa mbali bwana Nguvu, kijana Paul na miwani yake, dada yake na wadogo zake. Mhh, zile chips za Mangi na soda zake tamu si kawaida. Ila baadaye mama wa kiarabu(mama Halidi-Marehemu) akaweka Kiosk chake chini ya dirisha letu la jikoni.... Block IV hiloooo baba, miaka hiyo wanaliita ghorofa la watu wanaoshindana. Ukiweka AC, wanajibu, ukiweka antena ya TV, wanakujibu, ukanunua gari, wanakujibu. Kiboko yao ni yule Msomali, ila mkewe alikuwa anatumia sijui mi LADYGAY?? Akipita basi unafeel Oxygen imekwisha. Sijui alikuwa anawezaje kupumua na hiyo harufu?
Nilikuwa pale mwezi wa tatu, nilipotea. Pamebadilika sana. Ikabidi nianze kutafuta nyumba yetu. Mungu bariki nikamuona mama Sembuli (dada ya Marehemu Sembuli wa Yanga)........, heee,kamaliza Chuo kikuu na degree yake ukutani. I was too proud of her. Wamepanda miti na nyuma ya Block IV, nasikia mama Mkapa kanunua lile eneo na ghorofa la Posta na wako busy kuweka jengo hapo. Too sad maana jamaa walikuwa wakicheza mpira hapo jioni (wazee) huku watoto wakichezea huku kwenye shule ya vidudu. Ilikuwa saa nne usiku na sikuonana na watu zaidi ya majirani wa karibu. Sikurudi tena pale. Miaka 10 sasa tangu niwe pale mara ya mwisho na karibu miaka 17 tangu niondoke........... Kumbe yule Mzaramo karibu na Wasabato walimuhamisha na wakajenga kanisa jipya ..... too much change.....

Unajua Ray kafungwa South Africa? Nilikuwa nakuja sana ghorofa la posta kucheza mpira pale! Dah unanikumbusha machizi wangu wengi sana kweli maisha safari ndefu.
 
Hao jamaa wapo sana tembelea kule siasa utawakuta though wengine walichange IDs zao.

Basi waje upande huu washushe nondo. Hivi Jah Kimbute ni wa tanga? Kuna mzee wa tanga wa long time kweli niliskia watoto wake ni marasta alafu yuko mwanamziki..
 
Hapana, hajafungwa kokote. Yupo Tanzania na ni mfanyakazi muhimu sana kwenye kitengo chake.

Alimaliza SUA na sasa kaajiriwa Serikalini. Kwa harakaharaka ni kuwa sidhani hata kama alishawahi kusafiri nje ya nchi ya Tanzania, sana sana kama ni kusema tunaishi Tanganyika, basi alishasafiri kwenda Zanzibar.

Huyo atakuwa Ray mwingine.
Unajua Ray kafungwa South Africa? Nilikuwa nakuja sana ghorofa la posta kucheza mpira pale! Dah unanikumbusha machizi wangu wengi sana kweli maisha safari ndefu.
 
Fundi unapajua Mission Quarters mwanangu, wewe hata mchuzi kwa chapati wa SAIGON haukufai maana unaenda wayy baaack. Mambo ya Uhuru Mchanganyiko kabla ya Benjamin Mkapa na ukuta ule.

Nani kashaenda mechi ya Bomu FC? Au tizi la Super Star?

Karakata Fc kiboko ya Bomu Fc,unakumbuka?
 
Hapana, hajafungwa kokote. Yupo Tanzania na ni mfanyakazi muhimu sana kwenye kitengo chake.

Alimaliza SUA na sasa kaajiriwa Serikalini. Kwa harakaharaka ni kuwa sidhani hata kama alishawahi kusafiri nje ya nchi ya Tanzania, sana sana kama ni kusema tunaishi Tanganyika, basi alishasafiri kwenda Zanzibar.

Huyo atakuwa Ray mwingine.

Inawezekana Mimi namzungumzia Raymond matoke sijui Kama unamfahau? Vp Deo kanyau unamfahamu? Amefariki kitambo kidogo.
 
Mshaanza kuharibu thread

hii ni thread ya sehemu za maakuli sasa haya mambo yenu ya na Ikarus hayahusiani after all akina ES walishaiongelea sana tuu

that said

hii mnajua kama Pilau tamu kuliko yote linauzwa pale oteli ya BUTIAMA pale magomeni?

basi unachukua ndizi zako kwa jamaa pale mlangoni kisha waingia ndani kuagizia mindi weee


kama ndio ukitaka WALI MCHUZI basi pale juu kuna sinia zimejaa samaki walokaushwa basi oooooh

Ukitoka pale huyooooo unaingia kwa bitebo kushevu huku wapiga soga na kama juma mosi basi si haba kwenda kwa babu mtama mchungu kupiga simu za nje maana kule muhimbili noma

now top that

Alikuwa anakajibu kale katoto, yeye anajiona mtoto wa mjini kumbe kuna wazee wa mjini.
 
ba chala mbona tuliambiwa kuwa alipotoka shamba kubwa aliwatapeli jamaa pesa zao na aliposhuka minazi mirefu akatamba sana kuwa ana kama dola laki na nusu na ilala pamoja na vitongoji vyake ililijua hilo...na kama kawaida wazee wa msimbazi wakamfanya dili ikifika ijumaa tuu hao. Lakini wazee wa kule kilwa rd hawakuambulia kitu maana chala boy alikuwa na pesa tuuu mpaka alipoenda chimbo hukooo sinza kwa ma brazameni


pesa zilipoisha inasemekana alikuwa ana funga sana kwa mama ntilie nazaidi ya yote kule buruda nako alishakuwa wanted na ubatani nako alikuwa anakuona kama kituo cha polisi

mara ya mwisho nilisikia bachala alionekana kwenye maskani ya watoto wa kibongo -pahar ganj,pale green guest house,-delhi india na sijui kama alipona maana nako nasikia noma tupu


jamani nimeuliza baharia/zungu marvig gay hakuna mwenye habari zake? Hivi mnajua huyu ndio kati ya wajanja wachache walioanza kupeleka ma truck bongo toka buruda...jamaa aliingiza fleet ya ma fiat kama 50! Na haijulikani yaliishia wapi


ama kweli mdude noma

yupo holland huko ana mke na watoto, kajilipua anasubiri makaratasi….
 
gt,

wlikuwa wanakurushia vidudu vya mtoni nini? Straight from "kishtobe"?

Unamjua zungu vale alikuwa anazungusha batani na buruda?

Halafu kulikuwa na baharia mmoja muandishi wa habari anapiga sana gita freddy macha jamaa mara ya mwisho nilimsikia alikuwa mitaa ya copa cabana. Jamaa alizibukia safari mpaka akaandika short story "twen'zetu ulaya" miaka ya mwanzo ya 1980s.

Unawapata hawa?

huko uk huko naye, juzijuzi alipokwenda kikwete alikuwa anapigapiga ngoma kumkaribisha naona gitaa kaacha kupiga mcheki youtube utamuona
 
Dahh, nafikiri utakuwa unaongelea vijana sana hawa. Anyway, kuna kundi la Facebook linaitwa Ilala Flats.....
Inawezekana Mimi namzungumzia Raymond matoke sijui Kama unamfahau? Vp Deo kanyau unamfahamu? Amefariki kitambo kidogo.
 
Ohh ... kumbe sasa thread ni kwa ajili ya mabaharia tu?

Na BTW... kwani mabaharia ni watoto wa kiume peke yake? Au ndio mambo ya Saudi Arabia hapa ya gender dhaifu?

Mtoto wa kiume anayedhani kuwa kazi fulani ni kwa ajili ya gender fulani... hiyo dhana says alot about him/her


Bwana na wewe mbona unarusha stim tu hapa,watu tunawasikiliza watoto wa mjini na story zao ww unabwabwaja tu kama Ms.e.nge mzee kama vipi pita kimya bwana kwani kila kitu lazima ucomment…..
 
Back
Top Bottom