Watanzania Wengi ni Wavivu? The Moment of Truth!

Hoja hii ni potofu, Uvivu ni hulka ya kibinaadamu wala haijengeki kwa misingi ya Kitaifa, rangi, kabila wala Jinsia. hata walioandika THEORY X AND THEORY Y nawadhungu na walifanya utafiti kwenye Jamii zao za kidhungu, maana yake ni kwamba wavivu wamejaa na kuenea dunia nzima.

Pili unapofanya analysis kwa kuangalia wakenya 2 au mganda mmoja katikati ya watanzania 300 unakuwa unafanya kosa kubwa sana la sampling, matokeo ya utafiti wa namna hii yanakuwa yameharika kuanzia hapo. Sisi tuliofanya kazi huko huko Majumbani kwao tunajua namna na wao walivyokuwa wavivu na wajinga.

Mkuu Sangarara,

Nimefurahi sana kwa kuona mchango wako, wachangiaji wengi ni wavivu wa kufikiri lakini kwa bahati mbaya hawajui kwamba wanafikiria kivivu.
Wavivu wapo kila mahali duniani na wachapakazi wapo pia na mara nyingi uvivu unaanzia kwenye akili ya mtu mwenyewe.
Ni muhimu kuchukua tahadhari ya mawazo kama haya ya kusema watz ni wavivu generally, kwani yanaweza kuwa yamebuniwa kwa makusudi ya kuendeleza ukoloni mamboleo.
Yaweza kuwa mbinu ya kuwadumaza kiakili na pia kuhalalisha ubaguzi na dhuluma kwani ili uweze kumtumikisha mtu lazima uteke kwanza fikra zake kwa kumuaminisha kwamba yeye yu duni.
Hata hivyo yawapasa watz popote pale walipo kujua kwamba ili waendelee ni lazima kufanya kazi kwa bidii, kwa kutumia akili zao kwa faida.
 
kwanza nakushangaaaaaa. Kisha najiuliza hivi wewe ni mtanzania kweli? Hivi tupo wote hapa nchini kweli? Wewe fanya utafiti wa kina kisha ndio uje hapa kuongea na watu wenye fikra zao, huwezi kuchomoza kama uyoga na kudai unujua mbuyu wenye matunda kauotesha nani, wacha kupotosha. Katika kusoma kwangu nilipata kusoma somo linaitwa management, humo kuna usemi uliofanyiwa utafiti unadai kuwa binadamu hapendi kazi na kama angepata nafasi ange epuka kabisa kufanya kazi.. Unajua ni kwanini? Hiyo sio asilaya yetu, tulipewa adhabu baada ya makosa yetu kwa mwenyez Mungu. Ila hilo sio hoja sana kwa maana unaporojo zako zimenikera. Nianze hivi
1. Swala la ubunifu. We nimwongo sana, watanzania ni wabunifu na ubunifu upokila mahali isipo kua haupewi kipaumbele na serikali. Nianzie secta rasmi, hapo UDSM kitengo cha uhandisi ni hv juz tu mhadhiri wa hapo alikua akilaan utaratibu wa nchi hii kutotoa kipaumbele kwa mainjinia wake. Ataivyo pia aliongelea mchango wa maguful uliyo wezesha kutengenezwa mtreka pale, akasema pia yapo magar yameshabuniwa huku akionesha michoro ktk tv jins ya livyo na kusema kilichokua kimebakia ni uwezeshwaji tu.
B>Huku SIDO.
Jiulize mwenyewe sido inakipaumbele gan ktk serikal kwa sasa, sido ni kama imekufaa. Ukija huku mtaani kila siku wapo watu wanaibuka na ubunifu wao lakini wanapotezwa, wapo wagunduz wa kufua umeme, kutengeneza radio station na wanarusha matangazo yao na huyu mmoja nilikutana nae pale dodoma ktk maonesho ya nane nane anaitwa lamek yupo singida yeye kagundua mtambo wa kutengeneza mafuta ya biodizel kwa kutumia matunda ya miti fulani najua hadi anatoka pale ktk maonyesho lazma alishapewa onyo. Niseme serikal haina muda na wabunifu wetu.
2. Mwamko wa watu kufanya kazi. Tuanze na hawa watu wasio na elimu kubwa kama ulivyoonyesha wewe, hapa naona ni wazi hauna ushirikiano sana na maisha ya kijamii katika hali ya chini maana siku hizi hakuna kaz za jinsia, kama ni mafundi seremala, ujenz, machenical na umeme wote wapo unajua ni kwa ni nini, mwamko uko juu.
Kwa upande wetu wasomi ndio machozi yananilenga lenga, hivi unajua kama haujuan na mtu hata hiyo kaz ya kujitolea bure haupati. Hivi unajua vituko vinavyoendelea hapa nchini juu ya swala la ajira. Mwaka jana niliitwa ktk usaili pale UDOM lakin kabla ya kumaliza usaili tuligundua na ilikua kweli kwamba zile nafasi zilikua na watu tena walifanya usaili kabla yetu lakin tulituma maombi pamoja. Na usaili uliyofanyika chuon muccobs umesikia yaliyojiri pale, uongo ktk tarehe ya usaili ktk gazeti, kupewa vigezo vya usaili gafla kabla ya kuingia ktk vyumba vya usaili na kutokua na muda halisi wa kufanyika usaili.
Naomba tuje kuongelea jambo hili baada ya ukomboz wa hii nchi na ndio maana tunao mwamko zaidi katika siasa, we ajira inatangazwa ni vigezo vya uzoefu miaka sio chini ya mitatu hadi kumi na tano, graduet tukapate wapi huo uzoefu? Mama kabaka nae katangaza eti kazi za nje zipo uarabun lakin za ndani ya u house boy/girl, ndio wasomi wakazifanye?.

hapo kwenye kazi za kujitolea umeniwahi mkuu, huyu jamaa anaongea kivivu sana na sidhani kama amefanya utafiti.
 
Mvivu wa kwanza ni yule anayesema "asilimia kubwa ya watanzania ni wavivu" bila kuelezea hiyo asilimia kubwa ni ngapi? 51 au 99? Kaipataje? Anaongelea Watanzania wa aina gani maana Watanzania si monolithic kwamba wote tumetoka katika mkato mmoja.

Na hajatueleza uvivu huu umekuwaje kwa Watanzania tu, ni wa ki genetic au mazingira au vipi?

Kwa hiyo, hata bila ya kubisha au kukubali kwamba Watanzania asilimia kubwa ni wavivu, nashindwa pa kuanzia kwa sababu mleta mada kaileta kivivu vivu, haina research, detail wala contextual justification.

Labda anaongezea ushahidi kwamba Watanzania wengi ni wavivu, kwa kuupinga uvivu kivivuvivu.

Ukitaka kutumia mifano unaweza kusema Watanzania asilimia nyingi wana mahekalu kama ya Mbezi Beach, kwa sababu kuna mifano ipo. Tuonyeshe kwa nini unafikiri hiyo mifano yako ni representative sample space, umetumia methodology gani, control gani, conclusion yake ina validity kiasi gani na kiasi gani inaweza kuwa haina uhusiano na data, margin of error unayopata ni asilimia ngapi.

Then utaonekana unaongelea uvivu bila uvivu.
 
Mvivu wa kwanza ni yule anayesema "asilimia kubwa ya watanzania ni wavivu" bila kuelezea hiyo asilimia kubwa ni ngapi? 51 au 99? Kaipataje? Anaongelea Watanzania wa aina gani maana Watanzania si monolithic kwamba wote tumetoka katika mkato mmoja.

Na hajatueleza uvivu huu umekuwaje kwa Watanzania tu, ni wa ki genetic au mazingira au vipi?

Kwa hiyo, hata bila ya kubisha au kukubali kwamba Watanzania asilimia kubwa ni wavivu, nashindwa pa kuanzia kwa sababu mleta mada kaileta kivivu vivu, haina research, detail wala contextual justification.

Labda anaongezea ushahidi kwamba Watanzania wengi ni wavivu, kwa kuupinga uvivu kivivuvivu.

Ukitaka kutumia mifano unaweza kusema Watanzania asilimia nyingi wana mahekalu kama ya Mbezi Beach, kwa sababu kuna mifano ipo. Tuonyeshe kwa nini unafikiri hiyo mifano yako ni representative sample space, umetumia methodology gani, control gani, conclusion yake ina validity kiasi gani na kiasi gani inaweza kuwa haina uhusiano na data, margin of error unayopata ni asilimia ngapi.

Then utaonekana unaongelea uvivu bila uvivu.

heshima kwako Kiranga
 
Ukiwa una compare Tanzania na nchi jirani kama kenya ama Uganda ama Rwanda utangundua kua watanzania ni wavivu kwa asilimia kubwa sana tofauti na mataifa mengine.
mfano mwingine una kuta mtu kaajiriwa ofisini lakini kufanya kwake kazi mapaka asukumwe mara kwamara . Napenda sana wakenya wanavyo fanya kazi wko so smart na hakuna mchezomchezo mara viruhusa vya hapanapale mara hayupo offisini. kusema kweli East Africa community ita tufanya tuwe watumwa wakenya kama tusipo angalia nafasi zote nyeti zitashikwa na wakenya na sisi tutabaki tunapiga kelele za umbeya na ushabiki.

KUNA FACTORS NYINGI AMBAZO ZIMECHANGIA HAYA, ELIMU DUNI, MIANYA YA KUPATA FEDHA BILA KUFANYA KAZI KWA NJIA ZISIZO HALALI , RUSHWA, UNDUGUNAIZESHENI KTK MFUMO WA UTAWALA NA SERIKALI, NA KTK AJIRA.
 
acha upumbavu dogo...hicho chakula unachokula kimeagizwa kutoka Kenya au Rwanda?

we unahukumu watz m 35 b'se of watoto wamama wachache wenye hizo shahada za vyuo? dogo, be carefull!
 
....Kauli hii haina ukweli wowote....Watanzania si wavivu ila hawa walio madarakani ndio wanasababisha Watanzania waonekane wavivu kwa sababu asilimia kubwa wamekata tamaa ya kuwa na maisha bora.
 
kwanza nakushangaaaaaa. Kisha najiuliza hivi wewe ni mtanzania kweli? Hivi tupo wote hapa nchini kweli? Wewe fanya utafiti wa kina kisha ndio uje hapa kuongea na watu wenye fikra zao, huwezi kuchomoza kama uyoga na kudai unujua mbuyu wenye matunda kauotesha nani, wacha kupotosha. Katika kusoma kwangu nilipata kusoma somo linaitwa management, humo kuna usemi uliofanyiwa utafiti unadai kuwa binadamu hapendi kazi na kama angepata nafasi ange epuka kabisa kufanya kazi.. Unajua ni kwanini? Hiyo sio asilaya yetu, tulipewa adhabu baada ya makosa yetu kwa mwenyez Mungu. Ila hilo sio hoja sana kwa maana unaporojo zako zimenikera. Nianze hivi
1. Swala la ubunifu. We nimwongo sana, watanzania ni wabunifu na ubunifu upokila mahali isipo kua haupewi kipaumbele na serikali. Nianzie secta rasmi, hapo UDSM kitengo cha uhandisi ni hv juz tu mhadhiri wa hapo alikua akilaan utaratibu wa nchi hii kutotoa kipaumbele kwa mainjinia wake. Ataivyo pia aliongelea mchango wa maguful uliyo wezesha kutengenezwa mtreka pale, akasema pia yapo magar yameshabuniwa huku akionesha michoro ktk tv jins ya livyo na kusema kilichokua kimebakia ni uwezeshwaji tu.
B>Huku SIDO.
Jiulize mwenyewe sido inakipaumbele gan ktk serikal kwa sasa, sido ni kama imekufaa. Ukija huku mtaani kila siku wapo watu wanaibuka na ubunifu wao lakini wanapotezwa, wapo wagunduz wa kufua umeme, kutengeneza radio station na wanarusha matangazo yao na huyu mmoja nilikutana nae pale dodoma ktk maonesho ya nane nane anaitwa lamek yupo singida yeye kagundua mtambo wa kutengeneza mafuta ya biodizel kwa kutumia matunda ya miti fulani najua hadi anatoka pale ktk maonyesho lazma alishapewa onyo. Niseme serikal haina muda na wabunifu wetu.
2. Mwamko wa watu kufanya kazi. Tuanze na hawa watu wasio na elimu kubwa kama ulivyoonyesha wewe, hapa naona ni wazi hauna ushirikiano sana na maisha ya kijamii katika hali ya chini maana siku hizi hakuna kaz za jinsia, kama ni mafundi seremala, ujenz, machenical na umeme wote wapo unajua ni kwa ni nini, mwamko uko juu.
Kwa upande wetu wasomi ndio machozi yananilenga lenga, hivi unajua kama haujuan na mtu hata hiyo kaz ya kujitolea bure haupati. Hivi unajua vituko vinavyoendelea hapa nchini juu ya swala la ajira. Mwaka jana niliitwa ktk usaili pale UDOM lakin kabla ya kumaliza usaili tuligundua na ilikua kweli kwamba zile nafasi zilikua na watu tena walifanya usaili kabla yetu lakin tulituma maombi pamoja. Na usaili uliyofanyika chuon muccobs umesikia yaliyojiri pale, uongo ktk tarehe ya usaili ktk gazeti, kupewa vigezo vya usaili gafla kabla ya kuingia ktk vyumba vya usaili na kutokua na muda halisi wa kufanyika usaili.
Naomba tuje kuongelea jambo hili baada ya ukomboz wa hii nchi na ndio maana tunao mwamko zaidi katika siasa, we ajira inatangazwa ni vigezo vya uzoefu miaka sio chini ya mitatu hadi kumi na tano, graduet tukapate wapi huo uzoefu? Mama kabaka nae katangaza eti kazi za nje zipo uarabun lakin za ndani ya u house boy/girl, ndio wasomi wakazifanye?.

Kunishangaa siotatizo tena nilitegemea mimi nimesema asilimia kubwa na sijasema watanzania wote niwavivu wapowachapakazi sana lakini tuseme ukweli unauma asilimiakubwa ni wavivu.
We unataja ugunduzi wamagufuli na nyingine za chuo zimeishia wapi

Ndo hapo swala lauvivu linakuja kua baadayakugundua tunasubiri seriki amamsaada. Hapo ndopanauvivu hatufikirii jitihada nyingine.

Minimebahatilka kufanyakazi kenya na sasa nimerudi nakwasasa nimerudi nyumbani baada ya kumaliza nilichoendakufanya.
Hapa nyumbani watunikuzima moto ukimpakazi hafanyi mpakasiku ya mwisho na anaileta. Haipo complite

Kubalikataa ndo hali alisi
Ukiwa na wewe ni mvivu lazima itakuuma
 
....Kauli hii haina ukweli wowote....Watanzania si wavivu ila hawa walio madarakani ndio wanasababisha Watanzania waonekane wavivu kwa sababu asilimia kubwa wamekata tamaa ya kuwa na maisha bora.

Ulishawahifanya kazina watu wanje?

Jamani ukweli unauma na kwavile wewe umefungiwahapo ulipo nahaujawahiona watuwanapigakazi basi unafikirindowatu wanafanyakazi. Kwataarifayako tembea uone. Nahii nikwasababu wewe nimvivu wakufikiri so uantosheka naunachoona nakufikiri

Angalia na majiranizako pia
 
Ila it's true na ubaya wa watanzania ni kwamba hawapendi kuambiwa ukweli kwa sababu inawagusa. I would say 98% yetu tuko incompetent.
 
kuna ukweli asilimia nyingi kwakweli
watu wako maofisini huduma zinaenda slow
mfano unaweza kwenda hata hospital
yaani huduma utaipata kimagumashgumash
mtu anakaa anapiga story tuu
mda wa kuondoka ufike asepe bila kujali
wewe una mambo gani ya kufanya

ni wavivu ,wambea,wazembe,tusiojali muda
na ndo maana sisi bado maskini tuu
 
kiongozi ni yuke anaejiongoza mwenyewe na asiyengoja kuongozwa, anaengoja kuongozwa ni kondoo aliyepotea.

mkuu kwa hiyo hujui uhusiano wa kiongozi na anayeongozwa???
Sasa ninyi ccm mnataka nini kama haina haja ya kuwa na kiongozi??
Hujui watunga sera ni viongozi??
Ndo maana nchi hii ni masikini bcs ya watu kama ninyi,
kunamfanyabiashara alijinyonga mbeya kwa sababu ya kudaiwa kodi zaidi ya kipato chake, haya yanasababishwa na systerm mbovu ya ccm, ulitaka watu wajiongozaje??
Wakamtoe jk ikulu/, hujui kuna sheria??
Duu sikusoma jina kumbe nakujibu wewe taahila!
 
Watanzania wengi pamoja na kwenda shuleni,vyuoni bado wana matatizo lukuki kutokana na kuadhirika kisaikolojia,
asilimia kubwa wanaenda kupata vyeti na sio elimu na hili ni tatizo kubwa sana na ndio maana kila leo unasikia fulani alifoji cheti na hii yote ni ili apate cheo mahala fulani.

Utendaji wa mtu anayemiliki degree,master,bachelor hauendani na ufanisi wake na hapo ndipo unapojiuliza huo uprofesa,udokta kaupataje,

Tubadilike, ni heri kukosa cheti kuliko kukusa ujuzi kwani ujuzi ni bora zaidi ya hicho cheti,Je cheti ndicho kinachofanya kazi?

mf. Leo hii ofisi nyingi za serikali na binafsi customer service/care ni mbovu je , wahusika hawakupitia mafunzo? La walipitia isipokuwa walienda kuchukua vyeti.

Yatupasa kutumia elimu/ujuzi wetu sehemu tulipo na hii ndiyo changamoto tuliyonayo la sivyo tutazidi kulalamika kuwa wageni wanaajiriwa nchini mwetu na wazawa wanaachwa.
Penda kazi yako,furahia kazi yako,heshimu kazi yako boresha mazingira ya kazi yako kwa maendeleo yako mwenyewe,wafanyakazi wenzako,jamii yako n.k
je utaweza kujiajiri kama utendaji wako ni mbovu
 
jamani wana jf naomba mnisaidie kimawazo hivi ni kweli asilimia kubwa ya watanzania ni wavivu wa kufanya kazi hasa za mikono na hawapendi kufikiri sana?.
 
ndiyo, hasa wale wanaofanya kazi za kuajiriwa serikalini ni wavivu sana......ila wanapeda sana kuomba omba....fuatilia ni wavivu mno!
 
Back
Top Bottom