Warioba afichua siri nzito

Nilianza kuwa na wasiwasi na huyu jamaa pale alipoanza kutetea baadhi ya mafisadi na kuharakisha wengine waende korokoroni. Alikuwa anapendelea zaidi "tufisadi tudogo tudogo" ndiyo visakamwe, sasa watu wameanzia juu jasho linamtoka.
 
Waberoya,
Hata mie nimeanza kusoma nilikuwa sijui lolote. Ila nilianzia ukurasa wa kwanza na hadi kufika mwisho, nimeshaelewa kila kitu. NA WEWE NENDA UKAFANYE HIVYO. Vinginevyo, basi unaona kile tu unataka wewe ukione. Mzee kweli maji ya shingo. Mwanzo nilifikiri akina Mtanzania wanadanganya juu ya huyu Mzee. Ila sasa nimeelewa na kwa kweli siasa kitu kibaya. Mkapa kalisha watu wengi sumu na ukichunguza sana, utagundua kuwa kuanzia juu hadi wabunge wetu, walikula ASALI hiyo ya mti wa kati.
Mtanzania nakubali sasa maneno yako. USIMWAMINI MWANASIASA.

Kaka, unafikiri nina pinga? la kama siamini amini vile!, ikitokea mzee huyu akafika kwa pilato, loh! salale basi msururu utakuwa mrefu mno, maana hata wale tuliodhani wasafi kumbe wachafu!

You know what once we reach that stage, ndiyo tutakuwa tunaijenga Tanzania mpya, yenye watu wapya, wenye mawazo safi yasiyokua na chembechembe zozote za kujilimbikizia mali.

kama mna hakika na hili, basi taratiiiiibu naanza kushangilia goli sililoonekana, likifungwa nitakuwa nakamilisha furaha yangu!

waberoya
 
1. “Uamuzi wa kuanzishwa kwa Kampuni ya Mwananchi Gold ulitokana na nia njema ya serikali,

2. serikali iliamuru BoT na Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) na Kampuni ya MA-CE ya Italia kuunda kampuni hiyo.

3. Baada ya uamuzi huo, serikali ilikuja kwenye ofisi yetu ya uwakili ya Nyalali, Warioba & Mahalu Law Associates ili tuisaidie kuipatia huduma ya kisheria kabla na baada ya kuundwa kwa kampuni hiyo.

Now look at this:-

- Serikali ilimuamuru Warioba kuisaidia namna ya kuanzisha Wananchi Gold, huku ikiwa na nia njema, na kwa nia njema kabisa serikali ikaamuru kampuni ya MA-CE ya Italy, ambako balozi wetu alikuwa Mahalu, mshiriki wa Warioba kwenye shirika la sheria, ambalo serikali ililiomba kuisaidia namna ya kuanzisha Mwananchi Gold,

- Hivi wananchi wa Tanzania tunatakiwa kuwa tumelala kwa kiasi gani jamani?
 
Mzee Warioba alichokifanya yeye ni kuandika chini kimya kimya.Halafu anamalizia kwa kuuliza aliye msafi aanze kumrushia huyu jiwe.Ile sasa anaanza kuinuka anashangaa HAONI HATA MMOJA ALOBAKI ili arushe ilo jiwe.
Hakuna kitu hapa.Go Mzee Warioba.

Nasema kamwe hatothubutu mtu kujaribu kufikiria kwenda kisutu kumshitaki.I bet now na nasubiri mwanakijiji ambae nae ka-bet tuone itakuwaje.

Jamani tusishangae serikali kuomba ushauri kutoka kwa law firm binafsi ya kina warioba.Nasakumbusha kuwa tusimuone jaji warioba kama jaji tuu msitaafu bali tukumbuke kuwa ni Waziri mkuu Mstaafu wa Tanzania hadi sasa.

Sijawahi kumpenda Warioba ila sasa mimi naanza kuwa big fan wake.Mzee hakurupuki huyu,halopoki,na kibaya yuko makini sana.sasa nyie CCM jifanye kuikana CCM Trust muone "mlima wa madocuments" hapo ndo mtajiju.
 
hatimaye kaongea.Nilisema Warioba Fisadi. maji yanaanza kuzidi unga.
hakuna msafi hata mmoja kwenye uongozi wa CCM kwani hata wale walioonekana ni watakatifu ndio wezi wakubwa. Read btn the line. He is the big one.

Alikuwa wapi siku zote tukipiga kelele alivyoona sasa anakwenda chini anatafuta huruma ya wananchi, nail him down till death.
 
This is my hypothesis:

Jaji Joseph Sinde Warioba anadhamiria kuzima tuhuma za ufisadi dhidi yake kwa kuigeuzia kibao serikali (kuituhumu kuipiga vita Kampuni ya Mwananchi Gold Mining Ltd).

Sasa wenye dataz,please nisaidieni.Zinazo muunga mkono Warioba ziwekwe hapa.Halikadhalika mwenye dataz zinazothibitisha ufisadi wa Jaji Warioba pia waweke hapa.
This is a very very important 'experiment' to our beloved nation.
 
hatimaye kaongea.Nilisema Warioba Fisadi. maji yanaanza kuzidi unga.
hakuna msafi hata mmoja kwenye uongozi wa CCM kwani hata wale walioonekana ni watakatifu ndio wezi wakubwa. Read btn the line. He is the big one.

Alikuwa wapi siku zote tukipiga kelele alivyoona sasa anakwenda chini anatafuta huruma ya wananchi, nail him down till death.


kwani mzee Warioba nae aligoma kuongea???mbona alikuwa anaongea tu??Sema yeye huwa haongei kwa kukurupuka au ili kumfurahisha fulani.Yeye anaongea panapotakiwa kuongea tu.FULL STOP.
 
- Warioba amepiga kelele sana kuhusu serikali na rushwa na kutowajibika, never before amewahi kuzungumzia yanayomuhusu na Wananchi Gold, mpaka Magazeti ya Mengi yalipomchomoa, akatishia kuyashitaki na hasa Mengi mwenyewe, mpaka leo hajafanya hivyo WHY?, sasa leo anakuja na hizi za kuilaumu serikali,

- Kwa nini hakusema mapema mpaka sasa ameshikwa pabaya ndio anailamu serikali na haya ya Mwananchi Gold? Kabla ya magazeti ya Mengi kumsema mbona hakusema ukweli mapema kuwa anahusika na Mwananchi Gold? Na kwa nini hakuwahi kuitaja hata siku moja kwenye malalamiko yake yote na CCM na serikali yake?

- Hakuna anayemchukia Warioba, ila ukweli kama wanavyosema viongozi wengi anajichukia mwenyewe, kwa sababu kwa nini ujifanye kimbele mbele na kupigia makelele ufisadi wakati wewe mwenyewe sio msafi? Sasa this is the best showdown ever, maana ninaamini within serikali ya sasa kuna mafisadi wanaotaka kumkata ngebe ngebe na yeye anadai anayajua yao na atajibu, saafi sana sasa waanikane ili wananchi tujue ukweli na tuweze kuwachambua vizuri nani ni nani wa kutinga Kisutu.

Hakuna muungano permanent wa wachawi, saaa imefika sasa ya kusambaratika mimi ninawaonea huruma viongozi mafisadi wasioelewa kinachoendelea, I mean Muungwana anawaacha na kuwatosa pole pole hawa wanaodai wanajua siri zake na kundi lake, kama kweli wanazo hizo siri za ufisadi wake sijui wanasubiri nini kusema maana time is running out, kwa sababu habari za uhakika na Warioba mwenyewe anazo ni kuwa serikali wanamalizia uchunguzi unaomuhusu na soon atatinga Kisutu, he knows that kwa sababu hao viongozi wawili waliompooza hawana anything to do na kwenda Kisutu.

Serikali haiwezi kulumbana na Warioba kwenye media utakua ni upuuzi usio mfano, nasikia huu mchezo wa Kisutu ni wa Pinda, aliyesema wazi kua serikali haimuogopi Mkapa, kuna kiongozi mmoja aliwahi kuniambia kua kijana angalia sana maneno ya Pinda ninaanza kuamini, maana Warioba hawezi kukurupuka namna hii, lazima kuna la mgambo na anajua something we do not! Sasa yeye na serikali waburuzane lakini in the end watuambie ukweli wote wanaoujua.

Wakuu Halisi na Invisible, hebu chekini huko who is next kuelekea Kisutu maana huu mchezo ndio kwanza umeanza, kuna mkulu mmoja aliniambia utaendelezwa mpaka 2010, saafi sana maana haya yote aliyoyasema sasa Warioba tusingeyajua, au?
 
Kumbe wengi sasa hawalali....Keko, Segerea, Maweni, Butimba walidhani wanaenda wale wasingiziwao kuiba Kuku tu, sasa wajue kuongoza ni dhamana, na dhamana ina wenyewe...
 
...hivi kwani bado hatuna health insurance ambazo ndio kazi yake kulipia matibabu ya wateja wake,matatizo mengine ni ya kujitakia tuu

Kaka Tanzania kuna mfumo wa bima ya afya ambao bado mchanga. Wengi wa wanufaika wa sasa ni wafanyakazi wa serikali kupitia mfuko wa bima ya afya. Kuna wakati waingereza kupitia shirika lao la maendeleo walitaka kusaidia kuanzisha mfuko utakaojumuisha watanzania wote.

Wazo hilo likapigwa vita na wenye nchi wakiongozwa na Mama Anna Abdalah wakati huo akiwa waziri wa afya akiungana mkono na wenye nchi wenzake kwa madai kuwa "kufanya hivyo kutaendeleza tabia mbaya ya utegemezi miongoni mwa watanzania". Kwao wao kuanzisha bima ya afya kwa wote ni kuendeleza ujamaa ambao wanaona kuwa ndio kikwazo kikubwa cha kujenga Tanzania yao ya "kifisadi" kwa jina la Ubepari...ama soko huria.....

Hawa ndio tunaowaita "waheshimiwa" na kuwapa kila aina ya heshima wapitapo mbele yetu.....

Tanzanianjema
 
Warioba ni mhanga wa mkakati "chafua sote" ambao uliokuwa ukiratibiwa na APSON MANG'ONDA kwa kumtumia Balali..Lengo, pamoja na mengine likiwa ni kuhakikisha kuwa endapo watu wa enzi za Mkapa wakikosa URAIS basi watakaokuja wote wawe wachafu kiasi cha kushindwa kunyoshea kidole wengine.....

Mzee Warioba aliingia mkenge akiamini anaisaidia CCM kujitegemea hivyo kuondokana na kuwategemea kina ROSTAM kujiendesha. Tatizo hakujua kuwa kwenye YUSUF MUSHI ambaye alikuwa "strategist" wa SUMAYE hapakosi UFISADI. Vilevile hadi wakati huo alikuwa bado hajaweza kujing'amua kutoka katika fikira mgando kuwa Tanzania ni CCM na CCM ni Tanzania. Tatizo ambalo wengi bado tunalo.

Tanzanianjema
 
Kuna methali isemayo "jambo usilolijua ni kama usiku wa giza" Inaonekana wengi tumekuwa na chuki kubwa na ufisadi ambao tunaamini unafanywa na wakubwa waliokuwa serikalini, nasi kwa vile hatukupata hata kidunchu cha keki hiyo tunakasirika zaidi.

Lakini nadhani kupitia Intelligence unit ya JF hebu tupate utafiti makini, utakaoweka mambo katika mstari sahihi, isije ikawa " we thought we have seen a ray of light in a tunnel...... just to realise it was a train" kwani kwa kupata mtu kama JSW mengi yanaweza wekwa wazi na kusaidia uharaka wa kesi nyingi za ufisadi ambazo waswasi wangu zinaweza chukua miaka na nchi isipate chochote zaidi ya goodwill ya kuwa tunashughulikia mafisadi, lakini hata mmoja asifungwe.

Hatuna uhakika kama hizi kesi zote zinaweza kuwa "proven beyond reasonable doubts" ili mtu ahukumiwe kuwa mkosaji na afungwe.

Yawezekana ni danganya toto kama ya akina Marehemu Dito (Mungu amurehemu) akatolewa kimya kimya wakati tuliposahau baada ya mengine kuletwa kwenye sahani ya habari sijui, my fingers crossed
 
Duh, Mbona siwaelewi?

Jamani Warioba aliwaita waandishi wa Habari ili awaeleze ufahamu wake kuhusu tuhuma zinazosemwasemwa mitaani na katika baadhi ya vyombo vya habari. Sasa alichokisema ndicho alichokuwa tayari kukisema. Ndio maana anasema, kama kuna kushitakiwa yuko tayari kujibu mashitaka hayo wakati wowote.
Ndugu zangu, Jaji Warioba ni mtu makini sana. NI mtu anaefikiri kabla ya kusema. Na anasema kinachojitosheleza. Anapotaja Makampuni yenye uwekezaji katika hiyo MWANANCHI Gold anajua anachokisema. Kama unavyojua, Kampuni ina wamiliki wake, na wamiliki wanaweza kuwepo leo, kesho wakauza share zao. Hawezi kutaja tu moja kwa moja wamiliki wa hizo kampuni bila kuwa makini. Yeye kama Jaji anajua umuhimu wa kuhifadhi taarifa za watu (Kama Waziri Mkuu mstaafu, anaijua Katiba). Haikuwa nia yake kwenye kikao kile kisema majina ya watu wowote.

Pili ushiriki wake na Kampuni yake ameusema bayana. Kama unavyojua, Memorandum and Articles of Association za Kampuni yoyote huandaliwa na wana sheria. Kampuni yake ilipewa kazi ya kufanya hivyo, pamoja na ushauri mwingine wa kisheria endapo utahitajika wakati wowote kabla na baada ya kuanzishwa kwa Kampuni hiyo (hii ameisema vizuri katika taarifa hapo juu Sijaona mahali anaposema alikuwa mwendeshaji wa Kapuni hiyo (labda kama kuna mtu anaweza kunisaidia hilo).
Wakuu, nadhani mnajua pia kuwa Serikali imepewa mamlaka na Katiba kupitia Bunge kuanzisha Taasisi, na taratibu zimewekwa za kufanya hivyo. Serikali pia inaweza kuwa na wabia wengine (binafsi au Taasisi za serikali) katika kufikia matarajio ya uanzishwaji wa Taasisi hizo.
[COLOR="Orange[B]"][
B]Nilidhani mngeshitushwa zaidi na taarifa ya kudidimizwa kwa MWANCHI GOLD ambayo inaelekea ilikuwa na nia ya kuhakikisha rasilimali (madini) yetu yanasafishwa hapa hapa nchini na kutuhakikishia kuwa hatuporwi mali hizo. Mimi kwangu ni jambo la kushtua sana kusikia serikali inakusudia kwa nguvu zote kuua shirika/Kampuni muhimu kama hiyo.
[/B][/COLOR][/B]

JF mmeishiwa, kutwa kucha mnataka kudiscuss WATU BADALA YA HOJA shame on YOU/US
 
Duh, Mbona siwaelewi?

Ndugu zangu, Jaji Warioba ni mtu makini sana. NI mtu anaefikiri kabla ya kusema. Na anasema kinachojitosheleza. Anapotaja Makampuni yenye uwekezaji katika hiyo MWANANCHI Gold anajua anachokisema.

Ndugu yangu, sasa Ukiwa makini na ukasema mambo ya kweli tupu lakini at the wrong place and at the wrong time inasaidia nini sasa?

Kama jaji anahisi atashitakiwa, sehemu nzuri ya kuzungumza hayo yote ni kuanzia pale pale Kisutu. Cha msingi wakati huu ni kutayarisha dhamana, ili asiende mitaa ya akina Zombe.
 
Naona mna-enjoy CINEMA ya kisiasa. Anyway tusubiri tuone. Kila jambo kuu huja kwa kishindo.

Kuna Mkuu mmoja aliwahi kuniambi kuwa "Viongozi wameanza kunyoosheana vidole, kuna aibu kubwa sana itakayolikumba Taifa letu, siku za karibuni". Ukweli ni kwamba, kesi nyingi zinazofunguliwa zitawahusu zaidi watendaji wadogo wadogo. Nao watasema mengi sana yatayowaumbuwa Wakubwa wao (wa sasa na wazamani). Sijui tutayaona kweli ama lah.
 
Mkulu Nyani Ngabu
Naona umeamua kutofuata utawala wa sheria.Sasa umeamua kuchukua sheria mikononi mwako....teh..teh..
 
Now look at this:-

- Serikali ilimuamuru Warioba kuisaidia namna ya kuanzisha Wananchi Gold, huku ikiwa na nia njema, na kwa nia njema kabisa serikali ikaamuru kampuni ya MA-CE ya Italy, ambako balozi wetu alikuwa Mahalu, mshiriki wa Warioba kwenye shirika la sheria, ambalo serikali ililiomba kuisaidia namna ya kuanzisha Mwananchi Gold,

- Hivi wananchi wa Tanzania tunatakiwa kuwa tumelala kwa kiasi gani jamani?

Hizi tri-partite/triangular " business" relatioships zenye utata mbona ziko nyingi sana tu.Ikitokea mtu achunguze ubia wa watu mbalimbali ukiachilia mbali "silent partnerships" tutagundua kwamba kuna walakini mwingi sana katika mambo mengi.

Yote hii hupelekea kuvuja kwa rasilimali za walala hoi wa nchi hii.
-Lakini je tunaweza kufanya nini?
-Hivi sheria ya Public Procurement Act infanya kazi katika kila nyanja au ni kwa maeneo fulani fulani tu?
-Kama inafanya kazi iweje basi serikali "iamuru" law firm hii kuisaidia kuanzisha mradi kama huu?
-It is so obvious kuwa mradi huu haukuwa kwa manufaa ya watanzania wote bali kasehemu tu ka watanzania!
-Warioba akiwa kinara wa kupambana na rushwa alipaswa kuona zaidi ya hapo alipoona - kwamba isingeweza kueleweka vingine!
 
Back
Top Bottom