Wapenda amani nchini kumtetea mahakamani Waziri Mkuu, Mizengo Kayanza Pinda

[FONT=century
gothic]KAMATI ya Vijana Wapenda Amani Tanzania (VIWATA) keshokutwa
itawasilisha maombi kwa Mwanasheria Mkuu, ya kupinga kesi aliyofunguliwa
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu
(LHRC) na Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS).[/FONT]


Akizungumza na waandishi wa habari Dar es
Salaam jana, Katibu wa kamati hiyo, Said Mwaipopo, alisema wamechukua
uamuzi huo baada ya kujiridhisha kuwa kesi hiyo imefunguliwa na
wanaharakati hao kwa utashi wa kisiasa zaidi na haitowaletea Watanzania
mapinduzi wanayoyataka.


“Sisi vijana wapenda amani na haki, tumeona
kesi hii ni uzushi wa wazi au ajenda za kisiasa za kupanda mbegu za
chuki kwa Waziri Mkuu na Mwanasheria wa Serikali,” alisema
Mwaipopo.


Alisema kauli aliyoitoa Waziri Mkuu
bungeni, kwamba watakaokaidi amri ya vyombo vya dola wapigwe, haikuwa na
maana mbaya kama ambavyo imechukuliwa na watu wengi, kwani kabla ya
hatua ya kupiga, vyombo hivyo vya dola hufuata kwanza utaratibu na
kanuni zao walizojiwekea.


“Hii si kwa polisi nchini, vyombo vyote vya
dola duniani, haviwezi kukuangalia pale unapotishia usalama wa
mwananchi mwingine, lazima uchukuliwe hatua na ikibidi upigwe kwa ajili
ya kutuliza amani na kuhakikisha usalama wa eneo husika,”
alisisitiza.


Kamati hiyo pia imeelezea kusikitishwa na
namna wanaharakati hao, walivyoichukulia vibaya kauli hiyo ya Pinda na
kukimbilia mahakamani, wakati siku za nyuma kulitokea matamshi yenye
dalili za kuvunja amani na hakuna hatua yoyote
iliyochukuliwa.


Alitaja matukio hao kuwa ni pamoja na
baadhi ya wanasiasa kutamka wazi kuwa “nchi haitatawalika, mauaji ya
Mwembechai, mauaji ya vikongwe Shinyanga, mauaji ya watu wenye ulemavu
wa ngozi, vurugu za Mtwara, vurugu za kisiasa na mabomu Arusha na
Morogoro na wananchi kumwagiwa tindikali.


“Hivi karibuni kauawa hadi Kamanda wa
Polisi Mkoa wa Mwanza na vurugu za sasa za kidini na tukirejea nyuma
kuna wanasiasa walikaririwa wakisema nchi haitotawalika, mbona watu hawa
wa haki za binadamu hatuwaoni wakilalamika au kuchukua hatua kama hii…”
alihoji.


Mjumbe wa Kamati hiyo, Andrew Mwila alisema
kitendo cha wanaharakati hao kumshitaki Pinda, ni kinyume cha Katiba
kwa kuwa inabainisha wazi kuwa mbunge yeyote ana kinga na yuko huru
kuzungumza bungeni bila kushitakiwa.


“Kule (bungeni) wana taratibu zao, kama
kweli mbunge kazungumza mambo mazito, kuna Kamati ya Maadili,
anafikishwa huko lakini ana kinga ya kushitakiwa huku nje, na hilo
tumeshuhudia kwani wapo wabunge wamezungumza mambo hatari na
hawajashitakiwa, hii kesi ni danganya toto kuna mambo mengine nyuma
yake,” alisema.


Kwa upande wake, Wakili kutoka kampuni ya
Uwakili ya Austin Wilson, Sweetbert Nkubi, alisema kampuni yake
inakamilisha utafiti wake juu ya suala hilo, na inatarajiwa kuwasilisha
maombi ya kupinga kesi hiyo dhidi ya Pinda, keshokutwa.


“Tunachotaka ni kumuomba Mwanasheria Mkuu
awaingize wateja wetu kwenye kesi hii ili watumie fursa hiyo kupinga
mashitaka hayo dhidi ya Waziri Mkuu ambayo yamelenga kutaka ufafanuzi wa
Katiba juu ya tamko hilo alilolitoa bungeni,” alisema.

Kwa hisani ya Habarileo.

Toa kichefuchefu chako na uma------ wako.
 
waacheni vijana waonyeshe uzalendo wao na si hawa vibibi vizee akina kijo bisimba ambao wanakabiliwa na njaa kali

Wewe ni -------- kati ya wapumbavu waliopo. Kila mara post zako huwa ----- mtupu. Unapenda kushambulia watu binafsi badala ya hoja. Sisi tunajadili hoja iliyoko mahakamani wewe pimbi unamjadili mtu binafsi - kijo Bi simba. Eti wewe nawe great thinker.
 
Ni nani yupo nyuma ya hawa wahuni, wapiga dili wanaojiita vijana wapenda amani tz?...
 
KAMATI ya Vijana Wapenda Amani Tanzania (VIWATA) keshokutwa itawasilisha maombi kwa Mwanasheria Mkuu, ya kupinga kesi aliyofunguliwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) na Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS).

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Katibu wa kamati hiyo, Said Mwaipopo, alisema wamechukua uamuzi huo baada ya kujiridhisha kuwa kesi hiyo imefunguliwa na wanaharakati hao kwa utashi wa kisiasa zaidi na haitowaletea Watanzania mapinduzi wanayoyataka.

“Sisi vijana wapenda amani na haki, tumeona kesi hii ni uzushi wa wazi au ajenda za kisiasa za kupanda mbegu za chuki kwa Waziri Mkuu na Mwanasheria wa Serikali,” alisema Mwaipopo.

Alisema kauli aliyoitoa Waziri Mkuu bungeni, kwamba watakaokaidi amri ya vyombo vya dola wapigwe, haikuwa na maana mbaya kama ambavyo imechukuliwa na watu wengi, kwani kabla ya hatua ya kupiga, vyombo hivyo vya dola hufuata kwanza utaratibu na kanuni zao walizojiwekea.

“Hii si kwa polisi nchini, vyombo vyote vya dola duniani, haviwezi kukuangalia pale unapotishia usalama wa mwananchi mwingine, lazima uchukuliwe hatua na ikibidi upigwe kwa ajili ya kutuliza amani na kuhakikisha usalama wa eneo husika,” alisisitiza.

Kamati hiyo pia imeelezea kusikitishwa na namna wanaharakati hao, walivyoichukulia vibaya kauli hiyo ya Pinda na kukimbilia mahakamani, wakati siku za nyuma kulitokea matamshi yenye dalili za kuvunja amani na hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa.

Alitaja matukio hao kuwa ni pamoja na baadhi ya wanasiasa kutamka wazi kuwa “nchi haitatawalika, mauaji ya Mwembechai, mauaji ya vikongwe Shinyanga, mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi, vurugu za Mtwara, vurugu za kisiasa na mabomu Arusha na Morogoro na wananchi kumwagiwa tindikali.

“Hivi karibuni kauawa hadi Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza na vurugu za sasa za kidini na tukirejea nyuma kuna wanasiasa walikaririwa wakisema nchi haitotawalika, mbona watu hawa wa haki za binadamu hatuwaoni wakilalamika au kuchukua hatua kama hii…” alihoji.

Mjumbe wa Kamati hiyo, Andrew Mwila alisema kitendo cha wanaharakati hao kumshitaki Pinda, ni kinyume cha Katiba kwa kuwa inabainisha wazi kuwa mbunge yeyote ana kinga na yuko huru kuzungumza bungeni bila kushitakiwa.

“Kule (bungeni) wana taratibu zao, kama kweli mbunge kazungumza mambo mazito, kuna Kamati ya Maadili, anafikishwa huko lakini ana kinga ya kushitakiwa huku nje, na hilo tumeshuhudia kwani wapo wabunge wamezungumza mambo hatari na hawajashitakiwa, hii kesi ni danganya toto kuna mambo mengine nyuma yake,” alisema.

Kwa upande wake, Wakili kutoka kampuni ya Uwakili ya Austin Wilson, Sweetbert Nkubi, alisema kampuni yake inakamilisha utafiti wake juu ya suala hilo, na inatarajiwa kuwasilisha maombi ya kupinga kesi hiyo dhidi ya Pinda, keshokutwa.

“Tunachotaka ni kumuomba Mwanasheria Mkuu awaingize wateja wetu kwenye kesi hii ili watumie fursa hiyo kupinga mashitaka hayo dhidi ya Waziri Mkuu ambayo yamelenga kutaka ufafanuzi wa Katiba juu ya tamko hilo alilolitoa bungeni,” alisema.

Kwa hisani ya Habarileo.

Kama kweli ni wapenda amani si waiachie mahakama iamue?
 
wanajisumbua tu
hawana locus stand, sio parties to the case
sheria haziwatambui kama watetezi wake kwenye hii kesi.
 
Hawa ni wachumia tumbo tu, wanastahili kupuuzwa.
Kwanza hata sheria hawajui, wanaongea pumba tu.
 
hawa vijana ndiyo kiboko ya hawa watetezi fake wa haki za binadamu waliovaa magwanda ndani huku wamenyoosha vidole viwili.
 
...kumtetea M.P.u.m.b.a.v.u ni kazi!,na hauwezi kumtetea M.P.m.b.a.v.u kama na wewe si m.m.p.a.m.b.a.v.u pia, kwahiyo ata hao vijana nao ni w.a.p.u.m.b.a.v.u kwa sababu wamejitolea kukutea upumbavu...
 
Hao sio wapenda amani, ni waua amani, do they know the rule of law? Vijana wa siku hizi kila kitu wanaweka maslahi yao mbele tuu, tunalipeleka taifa hili wapi? Wanatazamia kupata kitu!

The next day wakipigwa wao, wanaanza maandamano! Hebu vijana akili zenu zifanye kazi, nchi inaendeshwa ka sheria sio utashi wa kiongozi!

Neno VIJANA linatumika mno na wanasiasa siku hizi hata kama wazo ni la mwanasiasa mzee na wajanja siku hizi hukusanya vijana wanaambiwa tengeneza n-g-o halafu wanaambiwa cha kusema na mwishowe wanapigwa picha. Dhambi hiyo jamani tuache
 
Mtu akiuliza kwanini vijana wengi wa Dar ni wagumu kubadilika, atazame katika kikundi hiki hapa. Kwanza jina la kikundi chenyewe ni magumashi. Amani kwa asili yake ni kitu ambacho huwezi kusema kuwa kuna wanaoipenda kana kwamba kuna wengine wanaoichukia. Amani haigawi makundi kwamba kuna vijana au wazee wapenda amani, au kuna mwenyekiti na katibu wa kupenda amani. Amani inawahusu wote na kwa namna sawa. Vijana wengi wa Dar wanaishi kwa deals (Madili), kazi yao ni kutafuta tu wapi kuna tukio ili wakapige dili. Ukitazama hoja za hicho kikundi utagundua kwamba vijana hao wameona mwanya wa kupiga dili katika kesi hiyo. Na kwasababu hiyo hawawezi kujihusisha na mambo ambayo yanahusu mipango ya muda mrefu, kwasababu dili halitakiwi kuchelewachelewa. Wamekwisha ona kwamba kwa njia hiyo kuna uwezekano wa kuonekana na kuvushwa mpaka ng'ambo. Hapa ndipo tulipokwama.
 
Mjumbe wa Kamati hiyo, Andrew Mwila alisema
kitendo cha wanaharakati hao kumshitaki Pinda, ni kinyume cha Katiba
kwa kuwa inabainisha wazi kuwa mbunge yeyote ana kinga na yuko huru
kuzungumza bungeni bila kushitakiwa
.


Hii ndiyo taabu ya kuwa na vijana wanaoishi mujini kwa kwa kupewa Buku saba za pale Lumumba.Hawajui kipi chenye nguvu kisheria -Katiba ya Nchi VS Kanuni ya Bunge.
 
Neno VIJANA linatumika mno na wanasiasa siku hizi hata kama wazo ni la mwanasiasa mzee na wajanja siku hizi hukusanya vijana wanaambiwa tengeneza n-g-o halafu wanaambiwa cha kusema na mwishowe wanapigwa picha. Dhambi hiyo jamani tuache
Mkuu umenikumbusha inawezekana ndiyo maana hata Jaji Warioba na timu yake ameacha kuelezea mtu/binadamu atakaye someka Kijana ni mtu/binadamu wa Umri gani

Rasimu ya Katiba Mpya-2013
43. Kila kijana ana haki na wajibu wa kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo ya Jamhuri ya Muungano pamoja na jamii kwa ujumla, na kwa mantiki hiyo, Serikali ya Jamhuri ya Muungano, Serikali za Washirika wa Muungano na jamii zitahakikisha kuwa vijana anawekewa mazingira mazuri ya kuwa raia wema na kupatiwa fursa za kushiriki kikamilifu katika nyanja za kisiasa, kiuchumi,kijamii na kiutamaduni.



Kwa maoni yangu lazima kuwe na mipaka ya Umri Mtu kuitwa kijana.

[h=1]Hapana kwa baadhi ya mambo ndani rasimu ya katiba mpya-2103[/h]
43.- (1)Kila kijana ana haki na wajibu wa kushiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo ya Jamhuri ya Muungano pamoja na jamii kwa ujumla, na kwa mantiki hiyo, Serikali ya Jamhuri ya Muungano, Serikali za Washirika wa Muungano na jamii zitahakikisha kuwa vijana

wanawekewa mazingira mazuri ya kuwa raia wema na kupatiwa fursa za kushiriki kikamilifu katika nyanja za kisiasa, kiuchumi,kijamii na kiutamaduni.
(2)Kijana kwa mujibu wa Ibara ya Katiba hii atakuwa mtu wa Umri wa miaka kati ya 15-29.
 
Hawa ni wapenda vurugu. Wapenda amani hawawezi kumtetea anayeamrisha wenzake wapigwe. Hawa nao ni pinda!
 
Back
Top Bottom