Wapemba Waanza Kukamatwa

Haki ya kujitenga (right of secession) ni miongoni mwa haki za msingi za binadamu, mradi iwe imedaiwa kwa msingi wa amani na uamuzi kufikiwa kwa njia za kidemokrasia (mfano referrendum). Hawa wapemba mpaka hapo walipodai haki hiyo hawajakosea chochote, hakuna hata chembe ya uhaini. Ingekuwa uhaini kama wangechukua silaha na kujitangazia jamhuri yao kwa nguvu, au wangeeleza nia ya kutwaa serikali kwa nguvu. Lakini hawa wameandika tu barua na kupeleka katika mamlaka ambayo jambo kama hilo linaweza kujadiliwa, na ambako haki hiyo imetamkwa, ambako ni Umoja wa Mataifa. Kuwaita hawa wahaini na kuanza kuwatisha kwa kuwasomba kwenye madege ya kijeshi kwenda kuwahoji Unguja ni udikteta wa hali ya juu, ni kuwazuia kueleza mawazo yao, jambo ambalo ni kinyume kabisa cha haki za binadamu. Serikali ya CCM inapaswa kuacha kutenda udikteta wakati inahubiri demokrasia.
Hakuna asiejua serikali ya CCM ni genge la Majambazi na Mafisadi ambao hawajui demokrasia ni nini na wala hawaheshimu haki za binadamu, kwa kifupi ni madikteta wakubwa. CCM wanachojua zaidi ni kujitajirisha binafsi, kuiba rasilimali za nchi, kupokea rushwa kubwa ambazo zinadhoofisha uchumi wa nchi na kufanya ufisadi kwa kasi mpya na ari ya kinyonyaji. GOD DAMN CCM.
 
Mimi maoni yangu kukamatwa hao wapemba ni sawa tu maana wao wanajiita ni waaraabu sasa kama ni waarabu sisi wa nini nimeona mama wa kipemba akiileza kuwa wanafanya mgomo wa kupeleka mazao unguja sasa wanamkobmoa nani maana hata wao wakwama kiuchumi kwani hayo mazao wanapeleka bure tatizo la wapemba ni wabaguzi sana
 
Mimi maoni yangu kukamatwa hao wapemba ni sawa tu maana wao wanajiita ni waaraabu sasa kama ni waarabu sisi wa nini nimeona mama wa kipemba akiileza kuwa wanafanya mgomo wa kupeleka mazao unguja sasa wanamkobmoa nani maana hata wao wakwama kiuchumi kwani hayo mazao wanapeleka bure tatizo la wapemba ni wabaguzi sana
Hebu tuondolee chuki zako za kibaguzi hapa, kwani mtu kujiita mwaarabu ni kuvunja sheria?? Kama huna cha kusema just shut the hell up.
 
Mimi maoni yangu kukamatwa hao wapemba ni sawa tu maana wao wanajiita ni waaraabu sasa kama ni waarabu sisi wa nini nimeona mama wa kipemba akiileza kuwa wanafanya mgomo wa kupeleka mazao unguja sasa wanamkobmoa nani maana hata wao wakwama kiuchumi kwani hayo mazao wanapeleka bure tatizo la wapemba ni wabaguzi sana

Mtu kujiita mwarabu ni kosa?
 
Serikali ya JK iko mstari wa mbele kuvamia COMOROS under pretext of SPREADING DEMOCRACY lakini huku nyumbani iko stari wa mbele kuignore democracy na misingi yake

WAPEMBA kama hawataki kuwa ndani ya Muungano nadhani wanazo kila sababu ya kujitenga na kama kweli wewe ni progressive member wa JAMBO FORUMS sidhani utakataa kisiwa hiki kisijitenge

Muungano haukuwepo kisha ukawepo na unaweza usiwepo tena. Its a fair fact in political life

WATAWALA wetu hawataki waliamua kuwa IGNORE wapemba for years na sasa hivi wanataka kutumia mijiguu kuresolve matatizo kule

they are bound to fail

 
Tunafahamu huko Pemba iko songombino pamoja na mambo ya muafaka n.k.

Mwiba tuwekee hapa yale yaliyotokea ili tuweze kujua pumba na mchele. Maana hii habari iko nusu nusu sana ama mwenye full details atuwekee hapa.
 
Mimi maoni yangu kukamatwa hao wapemba ni sawa tu maana wao wanajiita ni waaraabu sasa kama ni waarabu sisi wa nini nimeona mama wa kipemba akiileza kuwa wanafanya mgomo wa kupeleka mazao unguja sasa wanamkobmoa nani maana hata wao wakwama kiuchumi kwani hayo mazao wanapeleka bure tatizo la wapemba ni wabaguzi sana
Wacha kunyooshea vidole wengine ,sijasikia wapemba kujiita waarabu labda wameitwa waarabu au unajichanganya na msemo wa waarabu wa Pemba hata Tabora kuna waarabu ,mbeya wapo waarabu tena wengi kuliko Pemba na Unguja yake au huyajui hata Burundi na Ruanda wapo waarabu.
Hapa kuna watu wanataka kunyongwa au kupotea na kupelekwa kusiko julikana ila CCM wameumbuka ,ndipo waswahili tuna msemo usemao Usihadaike na usiku(kiza) ukanya njiani ,kama polisi wanasema hawana taarifa sawa wakae hivyo hivyo wasiwe na taarifa na kama Kikwete hana habari na akae hivyo hivyo asiwe na habari kwani ndivyo viongozi wa CCM wanapoulizwa husema hawajapata taarifa basi wakae hivyo hivyo taarifa wataipata.
Usalama wa taifa huu ni usalama wa Utawala wa Chama kimoja CCM,mabo yote ya kulipuliwa mabomu,kuunguza transformer kuweka kinyesi kwenye visima vya maji huko Pemba yamefanywa na CCM na waliofanya wanajulikana kwa majina polisi na usalama walipewa taarifa ya wahusika na hakuna alieitwa polisi wala kukamatwa usiku.
Mbinde hizi za kukamata watu usiku zimepitwa na wakati ,wako maraisi na wafalme kama akina Shah wa Irani,Mabutu na wengine wengi ambao walikuwa na nguvu kubwa tu na hakuna aliefikiria kuwa wangeliweza kuangushwa na kupinduliwa chali ,leo hii wako wapi na wao walikuwa hizo kamata kamata ndio zao ,je wamefikia wapi ,CCM na utawala wenu wa kidikteta unakaribia mwisho mambo mnayowafanyia WaPemba hakuna kwa sasa ulimwenguni kote zaidi ya hapa Tanzania ,Pemba inahisabika ni moja katika visiwa vidogo sana vinavyoishi binadamu sasa Taifa kubwa kama Tanzania kukibana kisiwa kidogo tu ambacho ni kasehemu kasichozidi hata kilomita 56 na upana usiozidi kilomita 21 ni uharamia wa hali ya chini kabisa ,serikali imeshindwa kukijenga kisiwa hiki ambacho ndicho kilichotowa fedha ya kununua vyombo vyote vya fahari vilivyoko Zanzibar ,si wa umeme wala maji tokea uhuru hadi Muungano,na lililo baya zaidi ni kila ufikapo uchaguzi mkuu hupigwa na kudhalilishwa kama si waTanzania ,hakuna katika Taifa hili la Tanzania sehemu ambayo wanapigwa kama wanyama na vyombo vya dola ,fisadi Mkapa aliwapandisha vyeo polisi waliosimamia zoezi la kuwapiga watu wa Pemba na hili la sasa Kikwete ajifanye kipofu maana watu hawa hawakwenda kwa siri kwenda kupeleka maoni yao ,walifanya hivyo Balozi wa Marekani alipokwenda Pemba na juzi pia hawakufanya siri kwenda kwenye ofisi za Umoja wa Mataifa.
Serikali kama ingekuwa na njia njema na watu wa Pemba ingewaita kwenye vyombo vya sheria kwa mwito wa dhahiri kabisa kuliko kuwafuatilia usiku wakidhani WaTanzania ni wale wale wa zamani wa kuchapa usingizi na wasijue lipitalo.
Huu ni udikteta ambao mjeshi Kikwete anaanza kuonyesha kucha zake baada ya kushindwa kuwashughulikia wanaoliteketeza taifa na kuliibia matrilion ya shilingi.
Baada ya kushindwa kwao na mafisadi wanarudi kule kule kwa wanyonge wao na kuanza kuwadhalilisha wakiwa wamelala,Usalama gani huu wa Taifa ,kwenda kuwakamata watu wa pemba ambao wameenda kushitaki katika Jumuia za Kimataifa ,kama kweli watu hawa CCM na Usalama wao wanaona nchi itaharibika mbona majambazi walioko kwenye njia kuu ambao ni juzi tu walimuua mtu wa wa Usalama na pia majambazi wanaoiba mchana hata baada ya kutangazwa vita dhidi yao wameanza kuchomoza tena ,huu ni mkakati wa kuwasulubisha watu wa Pemba kama walivyozoea hakuna cha Usalama wala kuhatarisha amani kwani Tanzania hakuna amani isipokuwa kwa mafisadi tu ndio wanaoishi katika amani na utulivu.
 
Wajitenge ndo fresh, unguja wenyewe ndo wanajiona watu, kwa nini wabaguliwe wapemba. Ikibidi waingie msituni ili haki ipatikane ikiwa kwa amani ccm watagoma.
 
Mwaka 1967 wakati Lieutenant Colonel Chukwuemeka Odumegwu Ojukwu alipoamua kutangaza "Jamhuri ya Biafra" na kujitenga na serikali ya Nigeria, Tanzania ilikuwa miongoni mwa nchi chache za Afrika zilizomuunga mkono na kuitambua jamhuri hiyo, kwa msingi huohuo wa haki yao ya kuishi wapendavyo mradi hawavunji sheria za haki za binadamu. Sababu za Biafra kujitenga zinakaribiana kufanana na hizi za Pemba, kwamba eneo lao lilikuwa na rasilimali nyingi zilizokuwa zinatumiwa na serikali ya Nigeria kufaidisha maeneo mengine huku wenyeji wa eneo hilo (kabila la Igbo) wakitengwa na kubakia watu duni, na hata hawakushirikishwa kwenye utawala wa nchi. Kilichofanya ya Kanali Ojukwu yawe uasi ni njia aliyotumia, vita. Vita hiyo ilisababisha serikali ya Nigeria kujibu kwa vita pia, na kuwawekea vikwazo zaidi vya kuzuia mahitaji (chakula, dawa nk) visiwafikie na baada ya miaka 3 ya mapambano makali Biafra ikatoweka kwenye ramani. Licha ya Nigeria kudai ilikuwa inapambana na "uasi", ilichofanya pale Biafra kinalaaniwa hadi leo, kwani watu(raia) zaidi ya milioni moja walikufa, si kwa risasi tu, bali zaidi kwa magonjwa na njaa iliyosababishwa na hujuma zilizofanywa na serikali ya Nigeria wakati huo chini ya Lt Col Yakub Gowon. Fikiria watu milioni moja waliuawa kati ya watu takribani milioni 13 wa Biafra wakati huo, hiyo ilikuwa mauaji ya kimbari kwa ngazi ileile ya Rwanda, lakini kwa kuwa aliyeua ndiye aliyeshinda vita ile na ndiye aliyebakia madarakani, basi ikaishia hivyohivyo (tunayaona Rwanda leo hii pia, historia hujirudia kwa wale walio wavivu wa kuifuatilia!)

Yako mambo kadhaa yaliyochangia kuvuruga na kuharibu kabisa mwelekeo wa malengo ya watu wa Biafra, mojawapo ni mapambano yale "kutekwa" na mataifa ya nje kwa malengo yao ya kisiasa. Mfano Israel iliyokuwa na "bifu" na nchi za kiarabu (kumbuka ni kipindi hichohicho ilikuwa imetoka kumchakaza kamanda Gamal Abdel Nasser na umoja wa nchi za kiarabu katika ile iliyoitwa "six day war") ilimuona Murtala Muhammad (aliyepindua nchi na kumkabidhi Gowon) kuwa ni tishio kutokana na uhusiano wake na nchi za kiarabu, na hasa kwa kuwa kina Gowon na kundi tawala la Nigeria wakati huo lilitoka kaskazini kwa waislamu wengi. Israel ikaona Biafra ni mahali pazuri pa kuweka nguvu za kumcheki vizuri Gowon na wenzie, kwa hiyo ikamuunga mkono Ojukwu na Biafra. Inasemekana silaha nyingi ambazo Kanali Ojukwu na majeshi yake walizitumia kumchachafya Gowon alipewa na Israel, ambayo iliziteka kutoka kwa waarabu mwaka huohuo kwenye ile vita yao. Ian Smith wa Rhodesia aliona kujitenga kwa Biafra kutakuwa alama nyingine ya kuhalalisha kujitenga kwa Rhodesia kutoka Uingereza, kwa hiyo alitaka wafanikiwe aendelee kujipatia marafiki na kuhalalisha nafasi yake, kwa hiyo Rhodesia nayo ikatuma msaada kwa Ojukwu. Wakati huohuo, Uingereza ambayo ndio mkoloni wa Nigeria alikuwa na "bifu" na Ian Smith kama alilowahi kuwa nalo dhidi ya George Washington miaka 300 kabla walipoamua kuwa huru, Uingereza kwa makusudi akaamua kumsapoti Gowon na Nigeria! Urusi ilikuwa na interest na mafuta yaliyokuwa yanapatikana Biafra, na ilihakikishiwa na Gowon kuwa ikisaidia kumng'oa Ojukwu itafaidika, na hiyo ni miongoni mwa mara chache ambazo Urusi (ya kisoshalisti) ilipigana upande mmoja na Uingereza (ya kibepari) tangu kuisha kwa vita kuu ya pili ya dunia! Kwa hiyo jeshi la serikali ya Nigeria ambalo tayari lilikuwa na nguvu nyingi dhidi ya Biafra liliongezewa tena msaada mkubwa sana wa waingereza na warusi, na walifanya mauaji ya kutisha sana. Mwalimu Nyerere, Felix Houphouet-Boigny (Cote d'Ivoire) na Kenneth Kaunda (Zambia) waliendelea na msimamo wao wa kuunga mkono Biafra, lakini masikini hawakuwa na hela, vita ikaisha walioshinda wakashinda!

Turudi Pemba. Kwa msingi huohuo wa mafunzo tuyapatayo kutokana na historia, jambo kama hili linapogeuzwa kuwa "uhaini", mgogoro unakuwa mkubwa zaidi. Kwa mfano tuliouona hapo juu, tusidhani kuwa "scavengers" hawapo! Wapo, wanasubiri tu wakati muafaka waje kuanza kuokota. Lakini anayegeuza hii genuine plight ya wapemba kuwa "uhaini" ni CCM. Hili ni jambo katika hatua ya kawaida tu ya wazo, ambalo hujadiliwa na kupata ufumbuzi. Kule Nigeria Gowon alijibu risasi kwa risasi, sie hapa tunapaswa kuiga kwa kujibu wazo kwa wazo, sio wazo kwa matisho na madege ya kijeshi! Hawa wameandika barua tu, kwa nini msisubiri UN ikawaletea hiyo barua, mkaona kilichomo na kuijibu? Yaani barua tu na saini za watu elfu 10 kwenye karatasi majibu yake ni kuwasomba watu kwa madege ya kijeshi na kuwapeleka kusikojulikana? Hivi wangesema wanapindua kama Biafra ingekuwaje? Labda kisiwa chote kingezamishwa au wangepuliziwa hewa ya sumu kisiwa kizima kama Saddam alivyowafanyia wakurdi? Hi reaction ya serikali imetisha sana, na si ajabu ikawachokoza watu kufanya ambayo hata hawakuwa wameyafikiria!
 
Mimi maoni yangu kukamatwa hao wapemba ni sawa tu maana wao wanajiita ni waaraabu sasa kama ni waarabu sisi wa nini nimeona mama wa kipemba akiileza kuwa wanafanya mgomo wa kupeleka mazao unguja sasa wanamkobmoa nani maana hata wao wakwama kiuchumi kwani hayo mazao wanapeleka bure tatizo la wapemba ni wabaguzi sana

Ipole this is too low kaka.Si kuandika pekee hata kuwaza .Mbona mna wahindi wanajiita Watanzania wa passport lakini hamuwezi hata kuoleana wala kukaa msikiti mmoja na wanatuibia na kuwatumikisha nduguzetu ? Ama kweli wewe ***** kweli siwezi kuamini kwamba unaweza kuandika haya maneno .
 
People should not be afraid of their governments. Governments should be afraid of their people.

This is a perfect idea..the logic that the Goverment should fear people comes from the fact that its been elected by the people and thereby granted the authority to lead and provide development to their people..But this contradicts to the African contextual view of this body..namely government.. for its there to impose fear among people by using excessive of the power vested and so be able dictate as they do...Poleni wapemba..tupo pamoja..
 
Mimi maoni yangu kukamatwa hao wapemba ni sawa tu maana wao wanajiita ni waaraabu sasa kama ni waarabu sisi wa nini nimeona mama wa kipemba akiileza kuwa wanafanya mgomo wa kupeleka mazao unguja sasa wanamkobmoa nani maana hata wao wakwama kiuchumi kwani hayo mazao wanapeleka bure tatizo la wapemba ni wabaguzi sana

wapemba wamejiita waarabu wapi na saa ngapi?
toa maandishi au hutuba inayothibitisha hilo, kama huna itabidi tukuweke kwenye wale watu wanaochochea ubaguzi, na wanaotafuta visingizio vya kuwanyanyasa watu wa aina fulani.
 
Waliokamatwa wengi ni wazee wakiongozwa na mzee Ahmed Marshed Khamis, ambaye anatajwa kuwa alikua Kiongozi wa watu waliokwenda katika Ofisi za Umoja wa Mataifa (UN) Jijini Dar es Salaam kuwasilisha waraka wa barua wakidai serikali shirikishi Kisiwani Pemba.

Wengine ni: Dk. Gharib Omar Gharib, Jirani Ali Hamad, Bi. Mariam Hamad Bakar, Bi. Hidaya Khamis Ally, Mzee Salim M. Abeid, na mzee Mohamed Mussa, na wote wamechukuliwa na kupelekwa Zanzibar kwa ndege ya jeshi na hatimaye Dar es Salaam. Polisi wamekanusha kufahamu lolote, na kazi hiyo inafanywa na maofisa Usalama na Maofisa wa JWTZ kutoka Bara wakishirikiana na wenzao wa Unguja
SWADATA HII HABARI NI MIA KWA MIA,WANA JF I MAY BE WRONG BUT I DONT HAVE DAUGHT WATU HAWA WATAKUWA KWENYE MATESO HILI WADHIBITISHE KAMA WAMETUMWA NA SEIF AU PROF LIPUMBA.
 
mie ninalotaka kujua juu ya hili ni, jee hiyo barua waliyoipeleka ofisi za Umoja wa Mataifa imefika pahala husika, au Umoja wa Mataifa tanzania pia kunanuka ufisadi, kiasi cha kuitia barua mfukoni na kuwaita usalama wa taifa?
 
hao walokamatwa wote vizee wa kukaribia miaka 70, mambo ya utandawazi naona kama si yao hivi.

mtu na atupatie nakala ya barua, tuibandike hapa ikiwezekana
 
Kazi kweli kweli, suluhisho la matatizo ya Pemba na Zanzibar ni mgawanyo sawia wa madaraka na rasilimali za Taifa, haiwezekani kundi moja lifaidi kipande kikubwa cha keki at the expense of others halafu utegemee hawa binadamu wenye akili timamu wavumilie upuuzi huu!
 
This is very very bad news to my ears.
Natumaini kuwa JK anao uwezo kidogo wa kusimamia hii issue kama kiongozi. Tunamtegemea, hatutaki aibu hii, utafikiri tuko Tibet? ina maana weakness za nyerere ndio wanarithi, strengths zake wanazichimbia!
Kweli tembea ujionee.
I hope latest today, tutapata taarifa ya kueleweka ya hao watu walipo, statement ya serikali na position yake, otherwise hii ni embarasment kwa nchi, na fadhaa zaidi kwa sisi wananchi, hivi, kama serikali haiwajali,
kwanini wasijitenge?
Lini Pemba iliunganishwa rasmi na Zanzibar?
 
Back
Top Bottom