Marufuku kuwaona
2008-05-15 09:14:57
Na Dunstan Bahai
Jeshi la Polisi nchini, limesema halitawaruhusu ndugu wa watuhumiwa wa `uhaini` waliokamatwa kisiwani Pemba kwenda kuwajulia hali mahala wanakohifadhiwa.
Aidha, jeshi hilo limesema ndugu hao wasiwe na wasiwasi kwani ndugu zao wako salama na wakiumwa wanapatiwa huduma za kimatibabu kama binadamu wengine.
Kauli hiyo ilitolewa na Kamishna wa Polisi wa Zanzibar, Bw. Khamis Mohammed Simba, wakati akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu.
Bw. Simba alikuwa ameombwa aeleze waliko watuhumiwa hao na kama ndugu wanaweza kwenda kuwajulia hali.
Alasiri!!!!!!
2008-05-15 09:14:57
Na Dunstan Bahai
Jeshi la Polisi nchini, limesema halitawaruhusu ndugu wa watuhumiwa wa `uhaini` waliokamatwa kisiwani Pemba kwenda kuwajulia hali mahala wanakohifadhiwa.
Aidha, jeshi hilo limesema ndugu hao wasiwe na wasiwasi kwani ndugu zao wako salama na wakiumwa wanapatiwa huduma za kimatibabu kama binadamu wengine.
Kauli hiyo ilitolewa na Kamishna wa Polisi wa Zanzibar, Bw. Khamis Mohammed Simba, wakati akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu.
Bw. Simba alikuwa ameombwa aeleze waliko watuhumiwa hao na kama ndugu wanaweza kwenda kuwajulia hali.
Alasiri!!!!!!