Wanawake wanaweza kuua,duuh!!!

mashizo

Member
Feb 24, 2009
43
32
heshima zenu wakubwa.
wiki iliyopita nilikutana na yule msichana niliyeomba ushauri kwenu kwenye post inayosema nimfanye nini huyu msichana. https://www.jamiiforums.com/mahusiano-mapenzi-urafiki/158191-nimfanye-nini-huyu-msichana.html.

basi tulivyokutana nilimuomba afungue message kwenye facebook yake,duuh nilichokiona moyo ulikufa ganzi, maana wanaandikiana karibia kila siku mambo ya mapenzi na yule ex boyfriend wake, jamaa kamualika kwenda uturuki kwa mshikaji likizo next month, jamaa lina pesa kweli.alafu demu kamdanganya jamaa hadi jina langu eti naitwa tomek(jina la kipolo) wakati jina langu john.

basi ikabidi nimwambie kuanzia siku ile mimi na yeye basi tena,demu hakulia sana kivile maana anajua sasa atakuwa yuko free na mshikaji,ila mimi kutokana na kutopenda uhongo na kumfunza adabu next time hasije akamfanyia mtu mwingine ujanja wake ule,basi nikamtumia message yule jamaa wake kumwambia kwamba mimi jina langu siyo tomek na nikamuelezea kila kitu na picha nikamtumia nikiwa na demu namla mate na mambo mengine.

sasa jamaa baada ya kujua demu kumbe chizi na muongo naye kamtosa sasa demu kachanganyikiwa eti anadai anajuta kwa nn hakunisiliza mimi na kuwa na mimi pekee.demu kurudi kwangu anataka ila milango ya moyo ishafungwa,jana kaniona na msichana mmoja nasoma nae hapa chuo demu kachanganyikiwa, akaja kwangu akanikumbatia huku analia mimi nikampotezea tu. basi mpaka leo sms haishi kunitumia kwenye simu mimi namjibu ila kama rafiki tu sio wapenzi tena.

sasa hivi ni kazi tu kwenda mbele na shule,pesa kwanza mapenzi baadae.asanteni kwa ushauri wenu waheshimiwa umeniokoa kwenye mdomo wa kifo.hehehhe
 
sasa endelea na wewe kujibishana hizo sms ''kama rafiki'' hadi pale ambapo zitavuka mstari kidogo wa urafiki na ww ukamatwe na ''demu'' wako wa sasa. halafu vicious cycle ijirudie kama kawa! yaani hata huweki pause kwenye mahusiano,walau harufu ya huyo unayemuita x-wako itoke kwenye mashati yako tayari usharukia branch ingine? sikuwezi,lol
 
heshima zenu wakubwa.
wiki iliyopita nilikutana na yule msichana niliyeomba ushauri kwenu kwenye post inayosema nimfanye nini huyu msichana. https://www.jamiiforums.com/mahusiano-mapenzi-urafiki/158191-nimfanye-nini-huyu-msichana.html.

basi tulivyokutana nilimuomba afungue message kwenye facebook yake,duuh nilichokiona moyo ulikufa ganzi, maana wanaandikiana karibia kila siku mambo ya mapenzi na yule ex boyfriend wake, jamaa kamualika kwenda uturuki kwa mshikaji likizo next month, jamaa lina pesa kweli.alafu demu kamdanganya jamaa hadi jina langu eti naitwa tomek(jina la kipolo) wakati jina langu john.

basi ikabidi nimwambie kuanzia siku ile mimi na yeye basi tena,demu hakulia sana kivile maana anajua sasa atakuwa yuko free na mshikaji,ila mimi kutokana na kutopenda uhongo na kumfunza adabu next time hasije akamfanyia mtu mwingine ujanja wake ule,basi nikamtumia message yule jamaa wake kumwambia kwamba mimi jina langu siyo tomek na nikamuelezea kila kitu na picha nikamtumia nikiwa na demu namla mate na mambo mengine.

sasa jamaa baada ya kujua demu kumbe chizi na muongo naye kamtosa sasa demu kachanganyikiwa eti anadai anajuta kwa nn hakunisiliza mimi na kuwa na mimi pekee.demu kurudi kwangu anataka ila milango ya moyo ishafungwa,jana kaniona na msichana mmoja nasoma nae hapa chuo demu kachanganyikiwa, akaja kwangu akanikumbatia huku analia mimi nikampotezea tu. basi mpaka leo sms haishi kunitumia kwenye simu mimi namjibu ila kama rafiki tu sio wapenzi tena.

sasa hivi ni kazi tu kwenda mbele na shule,pesa kwanza mapenzi baadae.asanteni kwa ushauri wenu waheshimiwa umeniokoa kwenye mdomo wa kifo.hehehhe

dahh hongera mwana...na pole sana...
ushautua mzigo...amka na ujipange upya usjie rudia the same mistakes
 
sasa hivi sihitaji msichana mwingine ndio maana sms zake nazijibu ila nikija kumpata hapo baadae basi huyu mawasiliano nae nasitisha kabisa
 
umefanya uamuzi sahihi mkuu...huyo bibie anakulilia baada ya kumkosa mshikaji...usikubali kufanywa sub.
 
mimi binafsi nilimpa huyu msichana kila anachotaka alinipotezea muda sometimes ila sikujali maana nilikuwa namuheshimu na nampenda ila sasa kwenye moyo nishamtoa kabisa.alafu juzi nimepigiwa simu naitajika kwenye interview nmepata kazi nzuri zaidi ya mwanzo sasa sijui huyu demu alikuwa na nuksi nini.daah
 
Hongera sana kwa kuchukua maamuzi mazito, lakini sijakuunga mkono pale ulipowasiliana na huyo aliyekuwa bwana wake. Hakuna haja ya kumkomoa demu kicheche kwa kumpigisha chini ktk uhusiano wake mpya, other wise bado unamuonea wivu.
 
hongera sana,ila nataka kukwambia kitu kimoja cha maana sana,achana na habari za kumtumia text wala kuwa karibu nae kwa sasa kwa sababu hujui ni nini anawaza kukufanyia baada ya wewe kuamua kumweleza ukweli huyo bwanaake wa ng'ambo
nakueleza hivi kwa sababu mi nimeshakutana na kisanga kinachofanana na chako then yule mwanamke akawa ananitumia text na mimi namjibu kama rafiki kumbe mwenzangu anayake kichwani,basi siku moja akanipigia simu kuwa yupo kwenye bar ya jirani na kwangu ananiomba niende basi nami nikaenda pale bar,tukawa tunaongea mambo ya kawaida then akaniambia kuna rafiki yake anamsubiri pale hivyo akaniomba simu yangu ili amtumie text mi nikampa simu,alichokifanya ni kujitumia text za matusi mazito kwenda kwenye namba yake bila mimi kugundua
kesho yake mimi nashangaa yule dada anakuja na police kunikamata kuwa nimemtumia text za matusi,basi ile kesi ilinisumbua sana na ukizingatia sikuwahi kupellekwa mahakamani ktk maisha yangu,nilisumbuliwa na ile kesi mwaka mzima na mahakama ikanikuta na hatia nikalipa faini 50,000/
hivyo kama umeamua kuachana nae basi muepuke kwa sasa
 
Kaka kumchukia mtu ni siri, ila wewe umeonyesha wazi kwa kuwasiliana na bwana wa huyo msichana aliyepo nje ya nchi, we unge muacha aendelee na maisha yake, may be ulifanya hivyo kwa hasira tu, but usirudie tena
 
We bado luza tu. Kama ungekuwa umeachana naye bila kumharibia kwa huyo bwana wake halafu akajirudisha kwako, ningekuona mshindi... Siku akipata bwana mwingine utajishangaa jinsi moyo utakavyokuuma! Mwanaume hajengi bifu kwa demu hata kama amemwaga...
 
Samahani kama ntakuudhi ila me naona kama umetumia sana akili na maarifa yako kuliko busara kidoooogo tu.
Hukuwa na sababu yoyote ya msingi kumwambia yule na picha sjui nn,wht if he will misuse the pic?
Anyway, sio swala la pesa kwanza pesa baadae, and u will learn to love someone very soon, any money u have to find too.
Also there is NO absolute NO a friendship btn u or anyone in JF with your X,THIS IS STRICTLY PROHIBITADE COZ ITS EASY FOR U GUYS TO BRING BACK WHT U HAD BEFORE.
Lastly, becareful in the coming relationship.
 
Unajua a real gentle man wala hana haja ya kuharibu huko anakotaka kwenda, ni umejua ukweli unaondoka zako kuanza maisha,na yule unamwacha aende zake dunia ikamfunze

Na cha pili kama ushaona hakufai huna haja ya kuendelea na msg,unajua udhaifu wa wanaume,kuna siku utaangukia mikononi mwake huku ukitoa ahadi kedekede,tushayaona kama haya mkuu,chunga sana
 
unajua mimi nimemuandikia yule jamaa wake si kwamba nina chuki nae hapana,ila huyu demu kutokuwa muwazi toka mwanzo na kudanganya hadi jina langu na kunibadilisha race yangu kutoka black kwenda white.angesema ukweli toka mwanzo kwamba ana mipango na ex wake na bado anampenda so wanaweza kuwa pamoja,mimi ningemuelewa na ningefanya mambo yangu mengine ya msingi.kama wanaume wote na wanawake tungekuwa wawazi kwenye mahusiano basi ingekuwa hakuna kuumizana kabisa kwenye mapenzi.
 
sasa umemtumia picha jamaa ili akutafune mgongo wewe amuache demu wako?
Utaliwa **** wewe mtoto wa kiume acha ungese tomak mkubwa
 
Ukiona mwanamume anamkomoa mwanamke basi ujue kuna tatizo kichwani, mara nyingi wanaume wa namna hiyo wapo tayari kuwanyang'anya kila kitu walicho gharamia wanawake ambao uhusiano ulifikia kikomo

Siku moja nikiwa kituo cha polisi jamaa mmoja akaja na kudai kaibiwa gari lakini kumbe alihonga nyumba ndogo, matokeo yake aliishia kuaibika baada ya iliyokuwa nyumba ndogo kuripoti polisi na kudai jamaa alijitoa mhanga kufadhili maisha na akamwambia kama anabisha atatoa uthibitisho mke wa jamaa akiwapo, ilibidi jamaa awe mpole na akate pochi zaidi kumaliza ishu
 
Back
Top Bottom