DASA
JF-Expert Member
- Jan 6, 2011
- 1,031
- 301
Wanawake wanapenda sana kuwa huru na hii inafanya baadhi ya wanaume wasijisikie vizuri. Kutokana na mabadiliko ya maisha ya ,wanawake wanafanya kila ambacho kipo kwenye akili zao kwa ajili ya kuendeleza na kuimarisha familia, wanafanya kazi, wanafanya business, wanasafiri na pia wanafanya miradi yenye lengo la kuimarisha uwezo wa familia kiuchumi.
Wapo wanaume huona haiwezekana mwanamke kufanya kazi za ofisini eti atakuwa huru mno kiasi kwamba atachukuliwa na wanaume wengine. Hayo ni mawazo ya kizamani na hayana nafasi kwa karne ya leo. Unamzuia mke hata kwenda shule eti atachukuliwa na wanaume wengine.
Mimi naamini ni vizuri kumtia moyo kwanza awe anajiamini na kwamba anaweza kufanya jambo lolote akitaka kwani uwezo anao. Asipotiwa moyo na mume ni nani ataweza kumtia moyo ili ajiamini na kufanya mambo makubwa kwa ajili ya familia. Maisha ya sasa hivi yanahitaji wana ndoa ambao wanachakarika kwelikweli hivyo ni suala la kumpa mke wako uhuru ili muweze kusaidiana kuendeleza familia na maisha kwa ujumla.
https://www.jamiiforums.com/newthread.php?do=newthread&f=62
Wapo wanaume huona haiwezekana mwanamke kufanya kazi za ofisini eti atakuwa huru mno kiasi kwamba atachukuliwa na wanaume wengine. Hayo ni mawazo ya kizamani na hayana nafasi kwa karne ya leo. Unamzuia mke hata kwenda shule eti atachukuliwa na wanaume wengine.
Mimi naamini ni vizuri kumtia moyo kwanza awe anajiamini na kwamba anaweza kufanya jambo lolote akitaka kwani uwezo anao. Asipotiwa moyo na mume ni nani ataweza kumtia moyo ili ajiamini na kufanya mambo makubwa kwa ajili ya familia. Maisha ya sasa hivi yanahitaji wana ndoa ambao wanachakarika kwelikweli hivyo ni suala la kumpa mke wako uhuru ili muweze kusaidiana kuendeleza familia na maisha kwa ujumla.
https://www.jamiiforums.com/newthread.php?do=newthread&f=62