Wanaume kupika na kupakua ni ushamba jamani??

Mie pia nina rafiki yangu ameolewa, mara kadhaa nikienda kwao kwa dinner unakuta mume yupo jikoni tena amepachika kwa juu na ile nguo special ya kupikia na msosi mtamu..of course wanasaidiana na majukumu mengine,raha sana maisha yale kama heshima haipotei!..mwingine hata kutoa chombo mezani hatoi acha kuosha,huh!.
Asante, tutazidi habarishana via sport page yetu kuhusu huo mpambano ujao!..Naona umekamia sana 0-0,na iwe ila mie nataka ushindi tuongeze magoli na points ha ha...bye 4 now!

BJ naona wanaume wasiotaka kuingia jikoni walikuwa wa mwaka 47 siku hizi wengi hawaoni kama it is a big deal kumsaidia mwenzao katika kazi mbali mbali za nyumbani ikiwemo kupika. Mchana nilikuwa naongea na jamaa basi akaniambia mama kachoka kalala mimi nakorofisha msosi na kufua pia (wanatumia mashine na wote ni Wabongo) na wala alikuwa haongei kwa kusikitika na mkewe huappreciate sana msaada huo. Sasa mwanamke ukiwa na Mume kama huyo uombe nini tena kwa Mungu!? Naomba sana iwe 0-0 maana nahisi bingwa mwaka huu anaweza kuwa ni kwa tofauti ya magoli, sasa nyinyi na Chelsea mmetuzidi kwa magoli hivyo mkitoa sare ya 0-0 nasi tukimpiga mtu bao nne au zaidi tutaweza kupunguza gap ya magoli iliyokuwepo.
 
hakuna kazi ya mwanamke wala mwanaume. biblia ilisema adamu atakula kwa jasho kuna wanawake wangapi leo ni bread winners? na wewe unayepika wakati wageni hawapo unaficha nini? ushamba tu na kutoendelea
 
Kusema mwanamme kusaidia ni ushamba ndio ushamba wenyewe.

Hawa wanawake wanaosema kusaidiana ni ushamba hawako mbali sana na wale wanaosema "mwanamme asipokupiga hakupendi"
 
BJ naona wanaume wasiotaka kuingia jikoni walikuwa wa mwaka 47 siku hizi wengi hawaoni kama it is a big deal kumsaidia mwenzao katika kazi mbali mbali za nyumbani ikiwemo kupika. Mchana nilikuwa naongea na jamaa basi akaniambia mama kachoka kalala mimi nakorofisha msosi na kufua pia (wanatumia mashine na wote ni Wabongo) na wala alikuwa haongei kwa kusikitika na mkewe huappreciate sana msaada huo. Sasa mwanamke ukiwa na Mume kama huyo uombe nini tena kwa Mungu!? Naomba sana iwe 0-0 maana nahisi bingwa mwaka huu anaweza kuwa ni kwa tofauti ya magoli, sasa nyinyi na Chelsea mmetuzidi kwa magoli hivyo mkitoa sare ya 0-0 nasi tukimpiga mtu bao nne au zaidi tutaweza kupunguza gap ya magoli iliyokuwepo.

Mambo ya kusaidiana kwenye ndoa ni muhimu, inapendeza na kufanya wapenzi waone kila mmoja anamjali mwenzie....BAK na hiyo wish yako ya 0-0, haya wee tusubiri wikend vinginevyo jiandae kunipongeza!..Alamsiki!!
 
hakuna tatizo kumsaidia mamaa mambo ya jikoni....tunachoogopa ni maneno yenu kina mama..hamkawii kutuona mume ***** kisa tu tumewasaidieni kupika...
Nakubaliana nawewe. Wengi tunapenda kuwasaidi ila yakianza maneno inakuwa shida kidogo. mara mchoyo, mara anakaba mpaka penati basi ni fulu matatizo. But inshort kuwasadia ni jambo jema tena sana.
 
Embu tuabarishane jamani

nimeenda kwa shoga yangu nikiwa na rafiki yangu mmoja
aakashangaa gafula binti yuko sebulen akasiki sauti
shemeji umekuja karibu yakhe...leo nimeingia mwenyewe
kwenye mtalimbo!!!watu wakacheka wenye kuhisi mtalimbo mwingine
gafra tukaingia tukakuta mwanaume anausukuma ugali kana ana akili nzuri jamani kuna watu wana bahati nyie..kurudi sebulen mwana ume yule akatenga chakula amemaliza tukaagana njian best anauliza hivi rafiki yako kalipata wapi lile shamba wallahi....
Nikasema kweli wengine tunawatafuta wengine wanaikimbia

nkasea jamani labda sijui kwangu nikaona normal...ila mwanaume kupika ushamba???

Mama mia,

Mwanamume kupika siyo ushamba. Ila kuna mambo mengi sana ya kuangalia. Kubwa kati ya hayo ni mazingira mnayoishi na matajario ya jamii. Kama mnaishi Tandika kwenye room 1, mnapikia mkaa kule uani ambapo mnachangia kama familia 10, basi siyo vizuri mwanamume kukimbia kimbia na misufuria ya ugali huko jikoni. Ila kwa kama mnaishi kwenye apartment yenu wenyewe, jiko lenu la kisasa na mambo yenu private hakuna shida.

Mimi ni mpenzi na mtetezi wa usawa katika ndoa ila sidhani kama ni busara kukimbia kimbia jikoni wakati kuna wageni ambao hamna uhakika na mitizamo yao. Sipendi na wala my wife wangu hataki niwe kichekesho mitaani. Kwa hiyo sitaenda jikoni kama kuna wageni.
 
hakuna kazi ya mwanamke wala mwanaume. biblia ilisema adamu atakula kwa jasho kuna wanawake wangapi leo ni bread winners? na wewe unayepika wakati wageni hawapo unaficha nini? ushamba tu na kutoendelea

Unaweza kuwa sahihi ila ukumbuke kuwa biology yenyewe ilishaleta ubaguzi mkubwa. Mmoja anasukumbwa na testosterone wakati mwingine anacheza na estrogen. Matokeo ya hivyo vitu ni makubwa sana. Ndo maana katika michezo kama riadha wanaume na wanawake hawachanganyiki. Kwa hiyo tofauti katika gender ni natural na zimebebwa hivyo hivyo katika tamaduni zetu. Na pale tunapotaka kufanya mabadiliko hatuna budi kwenda taratibu, vinginevyo tutaonekana vituko tu!
 
INATEGEMEA,mwanamme anaweza kupika kutokana na sababu zifuatazo;
1.Mkewe anaumwa
2.Kazi ni nyingi sana hivyo inabidi mme asaidie,
3.Mwanamke hana ujuzi sana wa mapishi,hivyo mwanamme atajifanya kumsaidia,lakini lengo
ni kumuelekeza anataka chakula kipikweje.
4.Wapo wanaume wanaopenda mambo ya kike,kike,kike,kike, kila shughuli waifanyao
akina mama nao wanatamani, si ajabu ukakuta kavaa khanga ya mkewe kutwa nzima
5. Wapo wanaume wenye huruma ya hali ya juu,hivyo wanasaidia tu
6. Upendo nao ukizidi sana sana sana ndio hivyo tena
7. Limbwata likikolea sawasawa atapika,atafua nguo,ataosha vyombo,hata gesti atakusindikiza
(naomba usiniulize limbwata ninini hata mimi huwa nalisikia tu)


Point ya tatu ni sahihi sana
 
m.ume kupika sio ushamba....wala ujinga....
hapo ndiyo mnapokosea nyie w.wake!!!!
waume zenu wakiacha hata kuwafulia kufuli zenu mnasema eti wanaboa, sasa mnataka wafanyeje?
 
wakuu suala la kupika kwa wanaume ni zaidi ya mapenzi au kuwa mume *****; wanaume naturally ni wapishi wazuri sana na ndio maana hoteli nyingi chefs wengi ni wanaume.

kupika ni art kama vile sanaa nyingine na kusema kweli kipaji kile hakiigiki,

wanaume wengi waliolelewa vizuri hujua kupika na huweza kupika, pia wanaume waliowahi kuishi mabachelor au colleges mara nyingi wamekua wanapika

Now back to family issues
Mwanaume anayepika mara nyingi huwa na kipaji au uwezo wa kuwa karibu pia hata na watoto na mamaa. zaidi ya hayo, mwanaume anayepika is naturally romantic, more helpful, loved by kids na pia inaonyesha ana muda wa kufanya mazuri kwa mke na watoto

Moreover, kupika tu ni fun kinoma

TO ANSWER THE QUESTION, MWANAUME KUPIKA SIO USHAMBA
Mkubwa, nakubaliana nawewe kabisa. Kupika inakuja naturally kwangu, najikuta ninataka kufanya mautundu flani, and it is funny.

BUT, mwanume hauwezi kuwa unaingia jikoni tuu kila wakati kupika "everyday food" mnaweza kukutaa hoja yangu. lakini, mwanaume unatakiwa kupika vitu ambavyo sio vyakula vya kila siku..............unaweza kukaa chini unakuna nazi ili upike wali nazi na nyama??
Mi naona inakuwa fresh kama unafanya mambo flani ya michemsho, mikaango ya maini hivi, misamaki flani.......week end flani watu wana-look foward kuona baba atafanya nini different na chakula cha kila siku.
 
Unaweza kuwa sahihi ila ukumbuke kuwa biology yenyewe ilishaleta ubaguzi mkubwa. Mmoja anasukumbwa na testosterone wakati mwingine anacheza na estrogen. Matokeo ya hivyo vitu ni makubwa sana. Ndo maana katika michezo kama riadha wanaume na wanawake hawachanganyiki. Kwa hiyo tofauti katika gender ni natural na zimebebwa hivyo hivyo katika tamaduni zetu. Na pale tunapotaka kufanya mabadiliko hatuna budi kwenda taratibu, vinginevyo tutaonekana vituko tu!
Mkubwa, umenena vizuri kabisa. Tukisema tunapenda kitu fulani, haimaanishi tufanye tuu hata kama mazingira hayaruhusu kulingana na tunapoishi.
 
Mkubwa, nakubaliana nawewe kabisa. Kupika inakuja naturally kwangu, najikuta ninataka kufanya mautundu flani, and it is funny.

BUT, mwanume hauwezi kuwa unaingia jikoni tuu kila wakati kupika "everyday food" mnaweza kukutaa hoja yangu. lakini, mwanaume unatakiwa kupika vitu ambavyo sio vyakula vya kila siku..............unaweza kukaa chini unakuna nazi ili upike wali nazi na nyama??
Mi naona inakuwa fresh kama unafanya mambo flani ya michemsho, mikaango ya maini hivi, misamaki flani.......week end flani watu wana-look foward kuona baba atafanya nini different na chakula cha kila siku.
ni kweli kabisa kamanda... sidhani mleta mada alitaka tupike kila siku... sasa na mengine tutafanya saa ngapi
 
Mkubwa, umenena vizuri kabisa. Tukisema tunapenda kitu fulani, haimaanishi tufanye tuu hata kama mazingira hayaruhusu kulingana na tunapoishi.
kweli bana yaani we ukae jikoni unapika wakati mkeo anapiga soga na mashostito wake dah hii kali...
 
Mmmmng there's nothing wrong with this....i love to have my bfast done by my swtty....and once in a while we cook together!!!
 
Iko haja ya kubadili ladha ya chakula nyumbani,Mwanaume kupika ni safi sana, nimekuwa napika mara nyingi nyumbani kwangu, Lakini Pia nimejifunza toka kwa baba yangu alikuwa mpishi mzuri sana, Siku alizokuwa akikaanga watoto tulikuwa tunainjoi sana.
Japo si wanaume wengi wanajua kupika kutokana na nature yetu ya waafrika kwamba mwanaume Jikoni si mahali pake familia nyingine ukionekana uko jikoni siku hiyo utasema nini kilikupeleka uko.
 
Iko haja ya kubadili ladha ya chakula nyumbani,Mwanaume kupika ni safi sana, nimekuwa napika mara nyingi nyumbani kwangu, Lakini Pia nimejifunza toka kwa baba yangu alikuwa mpishi mzuri sana, Siku alizokuwa akikaanga watoto TULIKUWA tunainjoi sana.
Japo si wanaume wengi wanajua kupika kutokana na nature yetu ya waafrika mwanaUME JIKONI SI MAHALI PAKE, NA FAMILIA NYINGI STRICTLY MWANAUME HARUHUWI JIKONI.

Ni kweli kabisa, hata mimi baba yangu mzazi alipokuwa hai (kwa sasa ni marehemu) siku moja moja alikuwa anaandaa bonge la msosi halafu tunakula pamoja katika familia. Kweli inapendeza sana. Pia hata mimi mwenyewe mtoto wa kiume kuna wakati wazazi wakitingwa sana na kazi na pengine wakati fulani wanakuwa wamechoka, basi hata mimi naingia jikoni naandaa msosi wa nguvu.

Ila si vema sana mwanamke kukaa sebuleni na mashosti zako halafu mwanaume akawa jikoni anapika. Kwa hapa italeta picha ambayo si nzuri kwa hao mashosti zako ambao mkishaagana tu wanabadilika kuwa Radio Umbea. Ila kama mwanamke ni mgonjwa sana na huna uwezo wa kukaa jikoni kwa wakati huo itakuwa sawa maana hata hao mashosti watakuwa wanaiona hali yako.

Halafu kwenye nyumba za kupanga ambako mara nyingi mnakaa uani kupika mfano familia 5 au zaidi, hata 2 si vema kwa mwanaume kukaa na wanawake kupika. Kwa hapo kama mwanamke hajiwezi ni mgonjwa sana, basi mwanaume afanye utaratibu wa kuiomba familia mojawapo za wapangaji hao kumsaidia kupika.
 
Ni kweli kabisa, hata mimi baba yangu mzazi alipokuwa hai (kwa sasa ni marehemu) siku moja moja alikuwa anaandaa bonge la msosi halafu tunakula pamoja katika familia. Kweli inapendeza sana. Pia hata mimi mwenyewe mtoto wa kiume kuna wakati wazazi wakitingwa sana na kazi na pengine wakati fulani wanakuwa wamechoka, basi hata mimi naingia jikoni naandaa msosi wa nguvu.


.

Aisee nimependa hiyo kumbe tuko wengi ambao baba zetu walikuwa wanatupikia, Manake kwa marafiki zangu nilikuwa sioni hiyo halafu nilikuwa naona aibu nikija na rafiki home afu tunakuta baba ndo anapika!!!!
 
endelea kuwa na upendo huo kaka wa kumsaidia mkeo,wewe ni mfano wa mwanaume bora.
avatar21903_3.gif

Avatar hii unaipendea nini? Aaaaaahh nilikuwa nakubipu tu, haya turudi kwenye mada.

Kuna jamaa yangu mmoja hata kupika ugali hajui. Hivyo ikitokea mke wake kapata safari ya ghafla analazimika kuwaomba majirani wampikie ugali/chakula. Duh haya sasa!
 
Back
Top Bottom