Wanaotaka Muungano Uvunjike watoke kwanza Bungeni na BLW

unaonaje ukaukataa uraia wa tanzania kwanza ili tukubaliane nawe kuwa mtanzania analazimika kukubali chochote eti yuko kwenye kiapo cha aina fulani katika kuitumikia tanzania? Umekuwa ukipinga maagizo sahihi yaliyopitishwa na vyombo halali wakati unafungwa na wajibu wako katika kukubali kila kitu kilichopitishwa "kisheria" ukiwa kama raia wa tanzania, jee uhuru huo wa kufanya hivyo haupo kwa mwengine?

Hivyo unataka wengine wasiwe na uhuru wa kutowa maoni yao eti wamefungwa na viapo? Naona mwenzetu unataka kutuburuza. Na hili kwa huu muungano tu au kwa mambo yote? Pengine wazo lako la kujenga lile daraja linakusumbua>

Ni kweli mkuu, ni lazima muungano ujadiliwe kwa uwazi maana kwa sasa unafanya baadhi ya watanzania wajisikie guilty. The solutuion iso kufunika funika ni kujadili kwa uwazi. Kuna baadhi ya mambo yanatuhusu moja kwa moja, na yanahitaji tuyajadili sisi wenyewe. Inawezekana kabisa kuwa yaliyomo kwenye articles of union yalikuwa ni mawazo ya Nyerere na Karume, na sio mawazo ya wazanzibari na watanganyika.

kipindi cha muungano kuwa fumbo la imani kimepita, ujinga wa kupostpone matatizo unatifanya tukumbane na makubwa zaidi katika siku za baadaye, mfano mzuri umeme. Tuliichekea IPTL sasa imekuja Richmond na Dowans. Muungano itakuja kuwa hivyo.
 
Companero, naomba uangalie kipengele cha tatu cha document hii ya CIA (natumaini si ngeni kwako). Bunge la Tanganyika na Baraza la Mapinduzi la Zanzibar viliridhia Muungano. Vyombo halali vya wakati huo vilivyokuwa na madaraka ya kufanya hivyo. Kama Baraza la Mapinduzi lililoongoza Mapinduzi Zanzibar (arguably) liliweza kushawishiwa basi ulikuwa Muungano halali. Kinyume na watu wengine wanavyosema suala la Kuunganisha Zanzibar na Bara halikuanza na Nyerere, Hanga na Kambona walishalizungumzia hili tangu siku zao masomoni Uingereza, na kumekuwa na mahusiano ya karibu kati ya viongozi wa Bara na Visiwani hata kabla ya Mapinduzi. As a matter of fact I'll propose to you that haijalishi nani angefanikiwa kwanza (kundi la Babu au Hanga au Karume) yote yaliikuwa yanaelekea kuungana na Bara.

Niende mbele zaidi, Baraza la Mapinduzi la Zanzibar ni chombo halali ambacho kipo hadi leo hii na uhalali wake haujawahi kuhojiwa. Wanaweza vipi kuhoji uhalali wa muungano bila kuhoji uhalali wa walioingia? Hoja ya kukosekana Uhalali haipo.

Mwanakijiji mimi nauaminia/naukubali zaidi uchambuzi huu wa Mwanasheria wa Katiba aliyebobea katika kutafiti Historia ya Muungano:

Chimbuko la Katiba ya Kudumu ni kuunganishwa kwa vyama vya TANU na ASP kuwa chama kimoja. Tukio hilo lilitanguliwa na mjadala miongoni mwa wanachama wa vyama hivyo. Kulikuwa na kamati ya watu 20 wakiwemo nusu kutoka Bara na nusu kutoka Zanzibar iliyoshughulikia muundo na katiba ya chama kipya ambacho kikaitwa CCM.
Kamati hiyo hiyo ikateuliwa na Rais wa Jamhuri kama Tume ya Katiba kutoa mapendekezo ya katiba mpya ya Jamhuri kama ilivyotakiwa afanye na Sheria za Muungano. Uteuzi huo ulifanyika Machi 25, 1977. Tarehe hiyo hiyo Rais pia akateua Bunge Maalumu la Katiba. Hii pia Rais alitakiwa afanye kwa mujibu wa Sheria za Muungano.
Lakini wajumbe wa Bunge Maalumu wakawa wale wale wabunge wa Bunge la muungano, jambo ambalo labda halikutarajiwa na Sheria za Muungano/Mkataba wa 1964. Kwa mantiki ya sheria inawezekana kujenga hoja kwamba Rais alitekeleza jukumu lake lakini nia, madhumuni na malengo ya vifungu hivyo vya Sheria za Muungano (na Mkataba wa 1964) vilivyoagiza uteuzi wa Tume na Bunge Maalumu yalipondwa.
Ni wazi kwamba madhumuni ya kuwa na Tume ikifuatiwa na Bunge Maalumu kutunga Katiba ya Muungano yalikuwa kuwapatia wananchi - umma wa Zanzibar na wa Tanzania Bara - nafasi na fursa ya kujadili katiba yao mpya. Lengo hilo halikutiliwa maanani hata chembe moja.
Katika hali hiyo, kwa maoni yangu, haukuwepo ushirikishwaji wowote wa wananchi katika kuunda Katiba ya Kudumu. Yaani Mkataba wa 1964 labda ulifuatwa kwa marembo tu yasiyo na maana. Hii inathibitika wazi wazi ukiitilia maanani muda mfupi wa chini ya mwezi moja Tume iliyafanyia kazi mapendekezo ya Katiba ya Kudumu.
Tume ikateuliwa Machi 25; ikatoa mapendekezo yake kwa Halmashauri (sio kwa Bunge Maalumu ilivyoagizwa na Mkataba wa 1964); Halmashauri ikajadili na kupitisha mapendekezo hayo katika mkutano wake wa faragha katika siku moja. Muswada wa katiba ukatangazwa siku saba tu kabla ya katiba yenyewe kupitishwa. Bunge Maalumu likapitisha katiba katika saa tatu.
Wajumbe waliochangia mawazo walikuwa saba tu na wote wakatoa hotuba za jazba kuunga mkono bila kufikiria kwa kina Muswada muhimu kama ule wakatiba ya kudumu. Hotuba ya Kiongozi wa shughuli za serikali katika Bunge, wakati ule Hayati Edward Sokoine, inadhihirisha wazi kwamba mjadala wa kina juu ya Katiba ya Kudumu na wajumbe wa Bunge Maalumu haukutarajiwa na yeyote yule bali Muswada huu ulipelekwa kwa Bunge Maalumu kwa kuhalalisha tu uamuzi ambao ulikuwa umekwishafanywa na chombo cha chama tawala.
Kwa kifupi basi, kwa maoni yangu, ushirikishwaji wa wananchi ama moja kwa moja au kupitia wawakilishi wao katika kutunga Katiba ya 1977 haukuwepo. Kwa hivyo, hata tukikubali kwamba taratibu za kisheria (ingawa hata hizi zina walakini kutokana na dosari nilizotaja hapa juu) zilifuatwa, ni vigumu kudai kwamba Katibaya 1977 ina uhalali wa kisiasa (political legitimacy) au inadhihirisha muafaka (consensus).

Chanzo: Katiba ya Muungano haina uhalali wa kisiasa wala kimuafaka-Profesa Shivji
 
Mwanakijiji kinachohitajika ni mapinduzi ya kikatiba (constitutional revolution) na sio mageuzi ya kikatiba (constitutional reform). Tutaanza na kufuta sheria zote za kikoloni na ukoloni-mamboleo zinazopelekea uporaji wa rasilimali za (wana)nchi. Kisha tutatunga Katiba mpya yenye uhalali/ ukubali wa wananchi. Hapo ndipo viongozi watatambua kuwa hawawezi kuchezea muafaka (consensus) ya wananchi tuliochoka kuchezewa kisiasa!

PS. Napenda kukumbusha kuwa leo ndio BASTILLE DAY, siku ambayo Wafaransa baada ya kuchoshwa waliivamia 'Ikulu' na kufanya Mapinduzi!
 

Kwa kifupi basi, kwa maoni yangu, ushirikishwaji wa wananchi ama moja kwa moja au kupitia wawakilishi wao katika kutunga Katiba ya 1977 haukuwepo. Kwa hivyo, hata tukikubali kwamba taratibu za kisheria (ingawa hata hizi zina walakini kutokana na dosari nilizotaja hapa juu) zilifuatwa, ni vigumu kudai kwamba Katibaya 1977 ina uhalali wa kisiasa (political legitimacy) au inadhihirisha muafaka (consensus).

Chanzo: Katiba ya Muungano haina uhalali wa kisiasa wala kimuafaka-Profesa Shivji

Ningeweza kutoboa matundu mengi kwenye hoja yenyewe ilivyo hapo; ila nimependa hitimisho lake kuwa kinachogomba ni "political legitimacy". Well political legitimacy is not an issue here. When you come to questions of "political legitimacy" kuna mambo mengi ambayo hata kwenye Katiba ambazo zimekubaliwa yanaweza kushukiwa. Hoja yenyewe ya Shivji imedhania (presume) mambo mengi kweli ambayo ukiyaangalia utaona yenyewe yana shida vile vile. Kwamba Katiba yetu ni halali kisheria halina shaka. Kwamba, yumkini kulikuwa na matatizo ya hapa na pale, well, Katiba gani haijawahi kuwa nayo?
 
Mwanakijiji kinachohitajika ni mapinduzi ya kikatiba (constitutional revolution) na sio mageuzi ya kikatiba (constitutional reform). Tutaanza na kufuta sheria zote za kikoloni na ukoloni-mamboleo zinazopelekea uporaji wa rasilimali za (wana)nchi. Kisha tutatunga Katiba mpya yenye uhalali/ ukubali wa wananchi. Hapo ndipo viongozi watatambua kuwa hawawezi kuchezea muafaka (consensus) ya wananchi tuliochoka kuchezewa kisiasa!

PS. Napenda kukumbusha kuwa leo ndio BASTILLE DAY, siku ambayo Wafaransa baada ya kuchoshwa waliivamia 'Ikulu' na kufanya Mapinduzi!

Mzee hoja ya constitutional revolution nakubali kabisa, lakini kukubali kwangu hakutokani na kusema kuwa Katiba ya sasa ni illegitimate. Kwangu, ni kwamba Katiba ya sasa haitoshi na kama ulivyoonesha imetokana na context ya kihistoria ya wakati wake na sasa kama Taifa tuna uwezo wa kuandika Katiba bora zaidi yenye kuangalia mbali zaidi.
 
Mkuu unaongea vizuri sana, ni lazima issues zijadiliwe kwa uwazi bila woga, kama watu hawataki hawataki tu wasilazimishwe. Hata bara kuna watu pia wanaonesha kuchoka kutokuwa na identity kwa expense ya muungano, siku hizi hakuna mtu anayeweza kujiita mtanganyika mbali na Mtikila. Sasa hivi sio suala la uhalali kisheria, undugu wa damu (hatuna undugu wa damu na waarabu) historia, ubara uvisiwani, upemba au uunguja. Tunatakiwa tuufumue muungano tuuangalie kama hautufai tuuache, kama wabara tunaonekana kuleta kile kilichokataliwa kwenye mapinduzi ni bora tuuvunje muungano. Wazanzibar waende kwa amani na waiendeshe Zanzizbar yao, hata wakileta waarabu masultani kama anavyotaka Seif sawa tu, ni mambo ya ndani. Tuongee kwa uwazi tu.

Katika mijadala mingi ya muungano(rekodi zipo) binafsi nimewahi kusema mambo ya muungano yaongelewe kwa uwazi. Kwa mtazamo wangu nimewahi sema kama kuna kutoridhika(kwa pande zote) ni vema wawakilishi au wabunge wapeleke hoja zijadiliwe kwa utaratibu.
Nadhani ndio kiini cha mjadala huu. Nimesoma baadhi yetu wakidhani mada hii imelenga kufunga midomo watu. Si kweli. Kinachoongelewa hapa ni kuwa watu wenye nafasi za kushiriki mjadala wakiwa na hifadhi ya kufikisha mawazo yao kwa utaratibu kama wabunge au wawakilishi ni vema wakafanya hivyo.

Inapotokea mtu aliye na immunity ya bunge na uwezo wa kuandaa hoja binafsi au kwa kikundi akasimama na kusema vunja muungano hapo kuna tatizo. Tatizo ni kuwa huyu alikula kiapo cha kulinda katiba. Kulinda katiba si kutokuongelea muungano bali kukubali taratibu alizokubali kama mbunge. Ni katika kuilinda katiba hiyo, mbunge ana nafasi ya kupeleka hoja ya muungano ijadiliwe.

Dhana nzima ni kuwa wale wanaoliona tatizo wafuate taratibu, lau kama hawawezi kufuata taratibu hawafai kuwemo ndani ya bunge. Maana yake ni kuwa wana haki ya kujadili muungano kulingana na taratibu za sera za vyama vyao, utaratibu wa bunge au BLW chini ya viapo vyao, na si kusimama na kutoa maneno tu.Hali hiyo ndio inayowafanya waonekane waasi. Waasi kwasababu waliapa kuilinda na kuitetea katiba ya JMT. Haina maana kuilinda isijadiliwe, la hasha, ni je utaratibu wa kuijadili umefuata katiba ile waliyoapa kuitetea?
Kwani kinaharibika nini watu wakiandaa hoja na ikajadiliwa?
 
Katika mijadala mingi ya muungano(rekodi zipo) binafsi nimewahi kusema mambo ya muungano yaongelewe kwa uwazi. Kwa mtazamo wangu nimewahi sema kama kuna kutoridhika(kwa pande zote) ni vema wawakilishi au wabunge wapeleke hoja zijadiliwe kwa utaratibu.
Nadhani ndio kiini cha mjadala huu. Nimesoma baadhi yetu wakidhani mada hii imelenga kufunga midomo watu. Si kweli. Kinachoongelewa hapa ni kuwa watu wenye nafasi za kushiriki mjadala wakiwa na hifadhi ya kufikisha mawazo yao kwa utaratibu kama wabunge au wawakilishi ni vema wakafanya hivyo.

Inapotokea mtu aliye na immunity ya bunge na uwezo wa kuandaa hoja binafsi au kwa kikundi akasimama na kusema vunja muungano hapo kuna tatizo. Tatizo ni kuwa huyu alikula kiapo cha kulinda katiba. Kulinda katiba si kutokuongelea muungano bali kukubali taratibu alizokubali kama mbunge. Ni katika kuilinda katiba hiyo, mbunge ana nafasi ya kupeleka hoja ya muungano ijadiliwe.

Dhana nzima ni kuwa wale wanaoliona tatizo wafuate taratibu, lau kama hawawezi kufuata taratibu hawafai kuwemo ndani ya bunge. Maana yake ni kuwa wana haki ya kujadili muungano kulingana na taratibu za sera za vyama vyao, utaratibu wa bunge au BLW chini ya viapo vyao, na si kusimama na kutoa maneno tu.Hali hiyo ndio inayowafanya waonekane waasi. Waasi kwasababu waliapa kuilinda na kuitetea katiba ya JMT. Haina maana kuilinda isijadiliwe, la hasha, ni je utaratibu wa kuijadili umefuata katiba ile waliyoapa kuitetea?
Kwani kinaharibika nini watu wakiandaa hoja na ikajadiliwa?

Mkuu nadhani ulichosema hapa ni kweli kabisa. Leadership inayotakiwa kutolewa na vyama nni kuwa suala hili liongelewe kwenye proper channels, lisiongelewe kwa jazba na kwa kejeli. Bungeni na BLW ndiko kwa kuongekea issue hizo haswa, regardless of policies of our political parties. Nyerere aliwahi kuizima G55 kimizengwe, lakini hakujua kuwa alikuwa anatega bomu la kutisha zaidi kuliko alivyodhani.

Ukiangalia hoja nyingi kuhusu kuvunja muungano ni ulevi tu, wa madaraka, kama leo Seif Sharif Hamad anayetakawazi kuitenga Zanzibar kutoka kwenye muungano na kuiunganisha na waarabu angekuwa rais wa jamhuri kusingekuwa na hoja hiyo. Au wanaoshikilia hoja hiyo wangekatiwa keki kubwa ya madaraka wasingesema wanayosema leo.

So ni better debate iwe free and open, ijulikane hasa ni nini wanachotaka, kusema chini chini kupitia radio mbao hakutavunja muungano wala hakutasaidia kuuimarisha. Na kusema watoke bungeni na kwenye BLW ni even worse. Let them talk the talk, and let us see whether we can walk the walk.
 
From DAILY NEWS reporter in Zanzibar

THE deputy minister of education and vocational training Ms Zahra Ali Hamad confirmed on Wednesday that despite recognizable achievement in the construction of schools, some villages still are without schools, prompting students to walk long distance.

Citing Ngomeni village in Pemba as an example of village with no school, where students walk for eight kilometres in search of education, the deputy minister said efforts to solve the problem had started by constructing a nursery school.

"We have successfully worked with the community in various areas to establish schools, but admit that few villages such as Ngomeni villages where students have to walk to Ngwachani, Mkoani district, South Pemba for school," she said.

She said that the ministry was ready to work with people in Ngomeni to construct a school, as the government promises to improve road and health centre in the villages.

Meanwhile Ultra sound room at Makunduchi cottage hospital in South Unguja is without automatic Air Conditioner (AC) machine, the deputy minister of health Dr Sira Ubwa Mamboya confirmed on Wednesday promising to solve the problem.

Responding to a question from Mr Jaku Hashim Ayoub (CCM- Muyuni) who wanted to know when AC would be fixed at the Ultra Sound room to improve working condition for the medical staffs.

My take: Huu ni mpango wa Nyerere kuhakikisha kuwa hakuna shule Zbar ili watu wahamie bara.
Mpango huu unahusisha kung'oa AC hospitali ili wagonjwa waletwe Bara. Mpango huu ni mahusisi ili kuidhoofisha Zbar kieleimu.
Hata kama amefariki lakini kuna mkono wake kama ule wa mapinduzi. Tumezinduka na muda si mrefu mtaona.

Zbar for Zbaris.
 
Kwanini wahusika hawatuletei referendum?
Wailete na waone sie wabara na wavisiwani tutachagua nini!
 
Hatuko kwenye utawala wa kisultani uliokua wa wakitumwa wala wakikristu, swala ni wabara na wavisiwani wote waamue kwa kura kama wanataka huu muungano, watupe nafasi tuchague sisi wenyewe, matokeo yake ndio serikali iyafuate.
 
Wanaweza kujadiliana kero za Muungano na wanaweza hata wakipenda kuzungumzia jinsi ya Kubadilisha Katiba; lakini hawawezi kuzungumzia "kuvunja Muungano". Hakuna mtu aliyetumwa kwenda kupelekea hoja ya kuvunja Muungano maana kama yupo alipoteza hilo pale aliposhika Katiba na kuapa kulinda. Na naweza kusema ni makosa makubwa kwa Maspika wetu kuwapa wawakilishi hao jukwaa la kuzungumzia kuvunja Muungano. Wanatakiwa kuwauliza kwanza:

a. Uliapa kuilinda Katiba Mheshimiwa fulani?
b. Ulimaanisha kiapo chako au uliapa tu ili uingie Bungeni?
c. Kama ulimaanisha iweje uzungumzie kuvunja Muungano?
d. Chama chako kina sera ya kuvunja Muungano?
e. Ulipofanya kampeni uliwaahidi wananchi kuwa utapigania kuvunja Muungano?

Haya ni maswali rahisi; wale wanaotaka kuvunja Muungano hawawezi kuwa wale wale walioapa kuulinda! Hili mbona si gumu sana kulielewa. Ni sawasawa na mtu asimame na kusema "mimi siupendi kabisa ukatoliki na laiti ungefutiliwa mbali" halafu mtu huyo huyo ameshika rozali na kumpanga mstari kwenda kupokea Komunyo baada ya kusali sala ya "Nasadiki kwa Kanisa Katoliki". Au mtu mwingine ajitokeza na kuseme "Siamini kabisa katika Uislamu na misikiti yote ivunjwe" halafu huyo huyo akasimama na kusema shahda na akawa wa kwanza kutoa fedha za kujenga na kusaidia misikiti. Haiwezekani.

Aidha unamaanisha unachosema au humaanishi. Kama unamaanisha huwezi kumaanisha halafu ukafanya jitihada ya kwenda kinyume cha kule kumaanisha kwako. Wanataka kuvunja Muungano watoke kwanza Bungeni na kwenye BLW ili wafanye yale ambayo wanaamini ni sawa.


Mifano yako mara nyingi ni mfu na ya kupotosha kwa maslahi ya kikundi fulani tu (sorry)

Mbunge kikatiba ana haki ya kujadili, kutoa mawazo ya wananchi na yake ikiwemo kuvunja, kubadili katiba, nk.

Usifikiri muungano ni kitu kikubwa kuliko katiba (mawazo mfu)

Bungeni hakujaliwi sera tu ya chama fulani (mawazo uchwara)

Bungeni mahali pa kujadili kila issue kwa maslahi ya wananchi...kama kuvunja muungano ni kwa maslahi ya mataifa yaliyoungana ni ruhusa kujadiliwa bungeni hatimaye kuvunjwa...

Tatizo lako unafikiri kinyerere na kikatoliki kwamba waweza kulazimisha mambo ya wananchi (dogmatism) kama mambo ya dini yako pole
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom