Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,413
- 31,402
TANGANYIKA ISIWE 'CASH COW'
Kwa hisani na shukrani kwa gazeti la The Citizen
Gazeti la la Tarehe 09/02/2024 linaripoti ufunguzi wa Mkutano wa maradhi yasiyoambukiza ikiwemo ugonjwa wa Moyo huko ' Zanzibar, mgeni ni Makamu wa Rais( VP) Dr P. Mpango.
VP Mpango akasema kuna uhitaji wa Taasisi ya moyo JKCI Muhimbili ili kurahisha upatikanaji wa huduma Tanzania na mbali. VP akaeleza utayari wa Serikali kuwekeza katika utafiti na matibabu ya maradhi ya Moyo
Akijibu hoja za VP, Waziri wa Afya wa Tanzania Bara au Tanganyika Bi Ummy Mwalimu alisema kuna eneo maalumu limetengwa Zanzibar kuanzisha huduma za JKCI .
Bi Mwalimu alisema tangu kuanzishwa JKCI, taasisi imekuwa kituo cha utafiti na mafunzo katika A.Mashariki.
Mkurugenzi wa JKCI Dr Kisenge alieleza ongezeko la uhitaji wa huduma hiyo Tanzania na nchi za Jirani
Dr akaeleza mpango wa kufungua JKCI Zanzibar ili kupunguza rufaa ikizingatiwa taasisi haina nafasi za kutosha
HOJA ZITOKANAZO.
1. VP wa Tanzania kufungua makongamano au shughuli nyingine zisizo za kiutendaji Zanzibar si si tatizo.
Majuzi , Makamu wa Zanzibar alifungua mkutano wa Vyama vya siasa, ni mambo ya kawaida.
2. Waziri wa Afya wa inayoitwa Tanzania Bara ni wa Tanganyika.
Jina Tanzania Bara si rasmi kwa nchi yoyote bali linatumiwa makusudi kufunika jina la Tanganyika.
Wizara ya Afya ya Tanganyika si jambo la Muungano, Waziri wa Tanganyika hana mamlaka ya mambo ya Afya Zanzibar. Waziri Ummy kuagiza ijengwe Taasisi ya JKCI Zanzibar si sahihi wala hana mamlaka, Zanzibar ina SMZ yenye Katiba, Wizara ikiwemo Afya, Taasisi n.k.
Kuingiza Wizara ya Afya kinyemelea katika Muungano kama alivyofanya Waziri si kuwatendea haki Wazanzibar.
Wazanzibar wamelalamika haya kwa muda mrefu, hawataki yasiyo ya Muungano kufanywa ya Muungano
Lakini pia Wazanzibar wanajukumu. Linapotokea la kero kama la Waziri wa Tanganyika kufanya maamuzi ya Wizara ya Afya Zanzibar, Wazanzbar waeleza kutoridhishwa na kuingiliwa.
Bila Wazanzibar kuzungumzia hili watathibitisha hoja ya UNAFIKI walionao katika Muungano.
Ni unafiki kwasababu unyemela wa kuongeza mambo ya muungano ni huu, wako wapi kukemea?
3. Mkurugenzi wa JKCI anasema wana mpango wa kujenga kituo Zanzibar.
Ukifuatia hotuba ya VP na Waziri Ummy, kuna ushirikiano wa kulisukuma jambo hili kwenda Zanzibar.
Si kazi ya Mkurugenzi kuingiza siasa katika tiba , pengine aliagizwa ayaseme ili kujenga hoja ya JKCI Zannzibar.
Mkurugenzi anaaminisha Umma kwamba rufaa za Wagonjwa 20 kutoka Zanzibar ni kubwa ukilinganisha na rufaa kutoka Mwanza, Kigoma, Mbeya au Ruvuma na nchi za jirani 8 ambazo ni kwa maelfu
Mkurugenzi wa JKCI akiacha siasa na kukumbatia tiba na huduma kwa mtazamo wa sayansi na uchumi, JKCI itakuwa taasisi bora duniani ikizingatiwa soko la Watu milioni 120 la nchi 8 tunazopakana nazo na si wagonjwa 30 au 200 kutoka Zanzibar. Kuna uwezekano mkurugenzi alipewa shinikizo tu na yeye kutamka tu !!!
4. Ikiwa lengo ni kupeleka huduma kwa Wananchi wengi wa Tanzania na nchi jirani kama ilivyoelezwa, JKCI haina manufaa yoyote kujengwa Zanzibar. Kwanza, Zanzibar ina idadi ndogo ya Wakazi kwa wakati mmoja ambao zi zaidi ya milioni moja.
Wazanzibar wengi wanaishi Tanganyika hivyo rufaa za Wagonjwa ni chache na ukweli ni kwamba hakuna.
Wazanzibar wanapanda boti na kutibiwa Muhimbili kama wanavyotibiwa watu wa Kigoma.
Zanzibar inapakana kwa ukaribu na Kenya kama jirani.
Tanganyika inapakana na nchi 8 na kati ya hizo yenye idadi ndogo ya Watu ni Burundi yenye Watu Milioni 12.
Kwa mantiki, kupata Wagonjwa wa nchi 8 zenye idadi ya watu zaidi ya milioni 120 ni muhimu kwa Taasisi ya JKCI kujiendesha kwa faidia ukilinganisha na Wagonjwa 30 au 200 kutoka Zanzibar.
Msukumo wa kujenga JKCI ni wa kisiasa badala ya kisayansi , kiuchumi na kisosholojia.
Ni msukumo unaolenga kufurahisha viongozi au unaosukumwa kisiasa bila kuzingatia uhalisia wa gharama za kuendesha kituo hicho Zanzibar na gharama za Wananchi. i! Hakuna mantiki ya kujenga Zanzibar
Badala ya kujenga Zanzibar, JKCI ijengwe maeneo ya kimkakatia kama Dodoma ambako Wananchi watafika kwa urahisi kutoka mikoani ikiwemo nchi jirani ikiwemo nchi ya Zanzibar.
Kituo kijengwe Kigoma ili kuhudumia Watanganyika wa Magharibi na nchi jirani ya DRC, Rwanda au Burundi ambazo pekee zina ujumla ya watu milioni 80. Hili ni soko linalohitaji JKCI si Zanzibar
Kijengwe Mbeya kuhudumia Wananchi wa kanda za kusini na nchi za Zambia , Malawi n.k. watu Milioni 40
Kudhani Wananchi watatoka Malawi, Songea, Kigoma, Musoma , DRC, Rwanda, Burundi n.k kwenda kutibiwa Zanzibar ni wazo lisilo na maana lililojengwa kwa misingi ya kisiasa isiyo na maana pia.
Haiingi akilini kwa anayefikiri sawa sawa kwamba ni rahisi Wagonjwa kusafiri kutoka Sumbawanga hadi Zbar
Hakuna mtu yoyote anayefikiria kimkakati, kiuchumi na kijimii anayeweza kuafiki wazo la kiwango duni kama hili
Ni wazo lenye taswira ya kisiasa lisilo na maana yoyote wala faida kwa jamii.
Kwa hisani na shukrani kwa gazeti la The Citizen
Vice President Mpango wants more cardiac institutes in Tanzania
Vice President Philip Mpango has directed Health Minister Ummy Mwalimu to liaise with health stakeholders over the possibility of establishing another cardiac institute in the country.
www.thecitizen.co.tz
Gazeti la la Tarehe 09/02/2024 linaripoti ufunguzi wa Mkutano wa maradhi yasiyoambukiza ikiwemo ugonjwa wa Moyo huko ' Zanzibar, mgeni ni Makamu wa Rais( VP) Dr P. Mpango.
VP Mpango akasema kuna uhitaji wa Taasisi ya moyo JKCI Muhimbili ili kurahisha upatikanaji wa huduma Tanzania na mbali. VP akaeleza utayari wa Serikali kuwekeza katika utafiti na matibabu ya maradhi ya Moyo
Akijibu hoja za VP, Waziri wa Afya wa Tanzania Bara au Tanganyika Bi Ummy Mwalimu alisema kuna eneo maalumu limetengwa Zanzibar kuanzisha huduma za JKCI .
Bi Mwalimu alisema tangu kuanzishwa JKCI, taasisi imekuwa kituo cha utafiti na mafunzo katika A.Mashariki.
Mkurugenzi wa JKCI Dr Kisenge alieleza ongezeko la uhitaji wa huduma hiyo Tanzania na nchi za Jirani
Dr akaeleza mpango wa kufungua JKCI Zanzibar ili kupunguza rufaa ikizingatiwa taasisi haina nafasi za kutosha
HOJA ZITOKANAZO.
1. VP wa Tanzania kufungua makongamano au shughuli nyingine zisizo za kiutendaji Zanzibar si si tatizo.
Majuzi , Makamu wa Zanzibar alifungua mkutano wa Vyama vya siasa, ni mambo ya kawaida.
2. Waziri wa Afya wa inayoitwa Tanzania Bara ni wa Tanganyika.
Jina Tanzania Bara si rasmi kwa nchi yoyote bali linatumiwa makusudi kufunika jina la Tanganyika.
Wizara ya Afya ya Tanganyika si jambo la Muungano, Waziri wa Tanganyika hana mamlaka ya mambo ya Afya Zanzibar. Waziri Ummy kuagiza ijengwe Taasisi ya JKCI Zanzibar si sahihi wala hana mamlaka, Zanzibar ina SMZ yenye Katiba, Wizara ikiwemo Afya, Taasisi n.k.
Kuingiza Wizara ya Afya kinyemelea katika Muungano kama alivyofanya Waziri si kuwatendea haki Wazanzibar.
Wazanzibar wamelalamika haya kwa muda mrefu, hawataki yasiyo ya Muungano kufanywa ya Muungano
Lakini pia Wazanzibar wanajukumu. Linapotokea la kero kama la Waziri wa Tanganyika kufanya maamuzi ya Wizara ya Afya Zanzibar, Wazanzbar waeleza kutoridhishwa na kuingiliwa.
Bila Wazanzibar kuzungumzia hili watathibitisha hoja ya UNAFIKI walionao katika Muungano.
Ni unafiki kwasababu unyemela wa kuongeza mambo ya muungano ni huu, wako wapi kukemea?
3. Mkurugenzi wa JKCI anasema wana mpango wa kujenga kituo Zanzibar.
Ukifuatia hotuba ya VP na Waziri Ummy, kuna ushirikiano wa kulisukuma jambo hili kwenda Zanzibar.
Si kazi ya Mkurugenzi kuingiza siasa katika tiba , pengine aliagizwa ayaseme ili kujenga hoja ya JKCI Zannzibar.
Mkurugenzi anaaminisha Umma kwamba rufaa za Wagonjwa 20 kutoka Zanzibar ni kubwa ukilinganisha na rufaa kutoka Mwanza, Kigoma, Mbeya au Ruvuma na nchi za jirani 8 ambazo ni kwa maelfu
Mkurugenzi wa JKCI akiacha siasa na kukumbatia tiba na huduma kwa mtazamo wa sayansi na uchumi, JKCI itakuwa taasisi bora duniani ikizingatiwa soko la Watu milioni 120 la nchi 8 tunazopakana nazo na si wagonjwa 30 au 200 kutoka Zanzibar. Kuna uwezekano mkurugenzi alipewa shinikizo tu na yeye kutamka tu !!!
4. Ikiwa lengo ni kupeleka huduma kwa Wananchi wengi wa Tanzania na nchi jirani kama ilivyoelezwa, JKCI haina manufaa yoyote kujengwa Zanzibar. Kwanza, Zanzibar ina idadi ndogo ya Wakazi kwa wakati mmoja ambao zi zaidi ya milioni moja.
Wazanzibar wengi wanaishi Tanganyika hivyo rufaa za Wagonjwa ni chache na ukweli ni kwamba hakuna.
Wazanzibar wanapanda boti na kutibiwa Muhimbili kama wanavyotibiwa watu wa Kigoma.
Zanzibar inapakana kwa ukaribu na Kenya kama jirani.
Tanganyika inapakana na nchi 8 na kati ya hizo yenye idadi ndogo ya Watu ni Burundi yenye Watu Milioni 12.
Kwa mantiki, kupata Wagonjwa wa nchi 8 zenye idadi ya watu zaidi ya milioni 120 ni muhimu kwa Taasisi ya JKCI kujiendesha kwa faidia ukilinganisha na Wagonjwa 30 au 200 kutoka Zanzibar.
Msukumo wa kujenga JKCI ni wa kisiasa badala ya kisayansi , kiuchumi na kisosholojia.
Ni msukumo unaolenga kufurahisha viongozi au unaosukumwa kisiasa bila kuzingatia uhalisia wa gharama za kuendesha kituo hicho Zanzibar na gharama za Wananchi. i! Hakuna mantiki ya kujenga Zanzibar
Badala ya kujenga Zanzibar, JKCI ijengwe maeneo ya kimkakatia kama Dodoma ambako Wananchi watafika kwa urahisi kutoka mikoani ikiwemo nchi jirani ikiwemo nchi ya Zanzibar.
Kituo kijengwe Kigoma ili kuhudumia Watanganyika wa Magharibi na nchi jirani ya DRC, Rwanda au Burundi ambazo pekee zina ujumla ya watu milioni 80. Hili ni soko linalohitaji JKCI si Zanzibar
Kijengwe Mbeya kuhudumia Wananchi wa kanda za kusini na nchi za Zambia , Malawi n.k. watu Milioni 40
Kudhani Wananchi watatoka Malawi, Songea, Kigoma, Musoma , DRC, Rwanda, Burundi n.k kwenda kutibiwa Zanzibar ni wazo lisilo na maana lililojengwa kwa misingi ya kisiasa isiyo na maana pia.
Haiingi akilini kwa anayefikiri sawa sawa kwamba ni rahisi Wagonjwa kusafiri kutoka Sumbawanga hadi Zbar
Hakuna mtu yoyote anayefikiria kimkakati, kiuchumi na kijimii anayeweza kuafiki wazo la kiwango duni kama hili
Ni wazo lenye taswira ya kisiasa lisilo na maana yoyote wala faida kwa jamii.