omarilyas
JF-Expert Member
- Jan 24, 2007
- 2,130
- 145
..mbona Mwinyi na Kinana waliuza Loliondo kini hawakufukuzwa?
No wonder propaganda ya kuwa wanaomkosoa Kikwete wanafanya hivyo kwa kuwa ni Muislamu inafanikiwa. Mbaya zaidi ni kuwa watanzania wengi wanaelekea kuingia katika mtego huo wa udini ambao mwisho wake ni kupelekea katika uchaguzi ujao watanzania walio wengi kupiga kura kuegemea DINI ZAO na hivyo KURASIMISHA TANZANIA INAYOAMINI KATIKA UDINI.
Hivi hadi leo hatujaweza kung'amua kuwa hakuna ardhi, pori wala mbuga ya wanyama iliyowahi kuuzwa? Hivi inakuaje kukodishwa kwa mbuga mmoja wakati wa mwivnyi ndio kuonekane hadi leo na huku tunajua wazi wakati wa enzi ya BENJAMINI maelefu ya ekari za mapori na mbuga zetu yamekodishwa kwa wageni wakiwemo haohao waarabu waliolaaniwa enzi hizo. Inakuwaje kuwa anapohusika MUARABU ambao kwa mantiki za kitanzania ni MUISLAMU iwe kashfa ya kudumu lakini anapokodishwa/kuuziwa MZUNGU ambae kwa mantinki ya kitanzania ni Mkristo iwe ni issue ya kupita?
Ndugu zangu tuwe makini na hiz sumu za chuki za kijamii ambao tunaendelea kuzipanda kwa kujua ama kutokujua....
Hali ya nchi ni mbaya kuliko tunavyotaka kujidanganya, na tukikosa umakini katika kushughulikia masuala yenye religious ama ethnic sensitivities, tutaifikisha nchi hii pale ambapo MAFISADI WAKUU wanasubiri tuifikishe, ili waweze kuhatamisha MFUMO FISADI wao kwa nguvu za giza walizojiandaa nazo
omarilyas