Kiboko ya Jiwe
JF-Expert Member
- Apr 7, 2020
- 12,712
- 36,167
Habari za asubuhi!
Katiba ya Tanzania sio kikwazo cha maendeleo, katiba ya Tanzania sio kikwazo cha haki za binadamu. Yet, mapungufu madogo madogo yapo lakini si makubwa. Nchi zote duniani katiba zao zina mapungufu kulingana na muda. Hivyo nashauri marekebisho kufanyika kidogo kidogo kadri siku zinavyokwenda kulingana na muda uliopo.
Mostly wanaoimba kupigania katiba mpya ni watu wa fursa, ulaji wao siasa, uvaaji wao siasa.
Haya nauliza swali:
Ni kipengele kipi cha katiba ya JMT kikiondolewa au kuongezwa kitaleta maendeleo? Hii katiba iliyopo wananchi ndio wanaongoza kuivunja.
HAKI YA KUISHI
Hii ndio haki kubwa zaidi kuliko haki zote za mwananchi, lakini wananchi wa Tanzania ndio wa kwanza kuivunja kila siku. Kijana ameiba elfu 5 anauwawa. Mtu kaiba kuku anauwawa. Kakata dirisha la mtu usiku anauwawa.
Rushwa kwa watumishi wa umma inachochewa na wananchi wenyewe. Anakwenda kwa mwalimu mkuu Ili amwamishie mtoto wake shule hiyo yeye mwenyewe anaanza kumshawishi mkuu wa shule kuwa pesa ya maji ipo. Hospital vivyo hivyo.
Kila sehemu za umma Mtanzania akienda anajiandaa kutoa rushwa. Nimeona mwenyewe mazingira kadhaa ambayo hayakuwa na ulazima wa kutoa rushwa lakini mtu anakuambia tuchange tutoe pesa tuhudumiwe haraka. Yaani mpaka nikashangaa.
Taratibu zote ziko wazi na free lakini mtu hamwamini anayemuhudumia anamshawishi ampe rushwa.
Hii katiba iko vizuri, tuifuate kwanza hii halafu tuwaze ijayo. Ijulikane kuwa Mimi si mwanachama wa chama chochote, na umri wangu huu wa miaka 36 sijawahi kupiga kura na sifikirii kupiga kura, musije kusema nimetumwa.
Ninajielewa na siwezi kutumika kama pedi, sina njaa, najiweza.
Katiba ya Tanzania sio kikwazo cha maendeleo, katiba ya Tanzania sio kikwazo cha haki za binadamu. Yet, mapungufu madogo madogo yapo lakini si makubwa. Nchi zote duniani katiba zao zina mapungufu kulingana na muda. Hivyo nashauri marekebisho kufanyika kidogo kidogo kadri siku zinavyokwenda kulingana na muda uliopo.
Mostly wanaoimba kupigania katiba mpya ni watu wa fursa, ulaji wao siasa, uvaaji wao siasa.
Haya nauliza swali:
Ni kipengele kipi cha katiba ya JMT kikiondolewa au kuongezwa kitaleta maendeleo? Hii katiba iliyopo wananchi ndio wanaongoza kuivunja.
HAKI YA KUISHI
Hii ndio haki kubwa zaidi kuliko haki zote za mwananchi, lakini wananchi wa Tanzania ndio wa kwanza kuivunja kila siku. Kijana ameiba elfu 5 anauwawa. Mtu kaiba kuku anauwawa. Kakata dirisha la mtu usiku anauwawa.
Rushwa kwa watumishi wa umma inachochewa na wananchi wenyewe. Anakwenda kwa mwalimu mkuu Ili amwamishie mtoto wake shule hiyo yeye mwenyewe anaanza kumshawishi mkuu wa shule kuwa pesa ya maji ipo. Hospital vivyo hivyo.
Kila sehemu za umma Mtanzania akienda anajiandaa kutoa rushwa. Nimeona mwenyewe mazingira kadhaa ambayo hayakuwa na ulazima wa kutoa rushwa lakini mtu anakuambia tuchange tutoe pesa tuhudumiwe haraka. Yaani mpaka nikashangaa.
Taratibu zote ziko wazi na free lakini mtu hamwamini anayemuhudumia anamshawishi ampe rushwa.
Hii katiba iko vizuri, tuifuate kwanza hii halafu tuwaze ijayo. Ijulikane kuwa Mimi si mwanachama wa chama chochote, na umri wangu huu wa miaka 36 sijawahi kupiga kura na sifikirii kupiga kura, musije kusema nimetumwa.
Ninajielewa na siwezi kutumika kama pedi, sina njaa, najiweza.