Maghayo
JF-Expert Member
- Oct 5, 2014
- 13,725
- 29,095
Ndo maana Lilith alimkacha Adamu. Kumbe tunawalaumu Taliban kumbe si wao pekee yao.Inasikitisha sana. Tumekuwa tukisikia walimu wakihusika kuwaua wanafunzi kwa vipigo na baadhi yao wameishafungwa gerezani na kuhukumiwa kunyongwa hadi kufa lakini huku mtaani nako hali si shwari.
Tazama mabaladhuli haya yanavyomuadhibu huyu binti bila huruma huku watu wazima wakishuhudia na kucheka wakichukua video wakatupie mtandaoni. Nchi hii kweli imefikia ufedhuli wa kiasi hiki? Mbona kuna baadhi ya watu wapo uraiani lakini wanaishi kama vile wapo jehanamu?
View attachment 2938392
Haya majitu yanamuonea binti mdogo asiyekuwa na hatia kwa kumfunga kamba na kumuadhibu kwa kiasi hiki kama vile nchi hii haina utawala wa sheria? Naomba vyombo vya sheria vichukue hatua kuwashughulikia wapuuzi hawa. Yaani wanamchapa binti kiasi hiki hadi wanammaliza nguvu za kike? Na utashangaa akiolewa asipate watoto yatakuwa yanakesha kwa Mwamposa kumuombea apate watoto wakati yenyewe ndiyo yamempa adhabu kali hadi yameua mayai yanayozalisha watoto.
Halafu tazama hilo shabiki la Utopolo jinsi linavyomchapa utadhani linaua nyoka! Majitu ya Yanga yana roho mbaya zaidi ya shetami. Hizi zote ni hasira za kufungwa na Azam. Yaani kufungwa yafungwe kiwanjani halafu hasira yanaenda kumalizia kwa binti wa watu asiyekuwa na hatia?
Tafadhali sana Dkt. Gwajima D naomba uchukue hatua haya mashenzi yakamaatwe yatiwe adabu. Hayawezi kuifanya nchi hii kama shamba la wanyama lisilokuwa na utawala wa sheria. Mambo ya kishenzi kama haya hayakubaliki duniani wala mbinguni. Haya majitu yakikamatwa yaadhibiwe zaidi ya yalivyomuadhibu huyu binti asiyekuwa na hatia. Naomba wanaoifahamu lugha hii inayoongewa na hawa wanaizaya watusaidie kutambua ni lugha ya kabila gani ili kuisaidia polisi kufanya upelelezi na kuwatia nguvuni wahalifu hawa wasiokuwa na chembe ya huruma.