Wanafunzi wa Vyuo/Sekondari waruhusiwe kufanya kazi kuchangia elimu yao?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Kuna kundi kubwa la watu ambao wanasubiri serikali iwapatie fedha za masomo n.k na wazazi wao wakati wana uwezo wa kufanya kazi. Kwa muda mrefu mfumo ulioundwa na serikali ya CCM unazuia na kufanya iwe ngumu sana kwa wanafunzi kufanya kazi. Matokeo yake, walinzi kwenye vyuo wanaajiriwa nje, wasafisha madarasa na vyoo ni watu wa nje, wakata majani ni watu wa nje wakati kuna nguvu kazi ambayo ipo tu.

Tumetengeneza mfumo wa kundi tegemezi ambalo linachukua tu kutoka kwenye jamii lakini halirudishi. Wengi wa hawa wanapata nafasi ya kufanya kazi kidogo kama sehemu ya kutimizwa matakwa ya elimu yao (research, internships n.k). Je, umefika wakati wa kutengeneza mfumo wa wanafunzi kuchangia elimu kwa kuwapatia nafasi za kazi humo humo mashuleni na kuweka kiwango cha chini cha mishahara ya wanafunzi (iwe tofauti na kima cha chini cha mtu wa kawaida).

Kwa mfano, badala ya kuwapatia posho bila kufanyia kazi kwanini posho za wanafunzi nchini zisiingizwe kama sehemu ya mapato yao wanayofanyia kazi?

je wanafunzi watakuwa tayari kusafisha vyoo, kufagia, kukata majani, kulisha wanyama, kufanya kazi za uwaiter/bartender n.k ili wajipatie kipato cha matumizi?

Je, tunaweza kuweka utaratibu hata wanafunzi wa sekondari nao waruhusiwe kufanya kazi na kujipatia kipato badala ya kutegemea fedha za posho toka kwa familia, wadau na wapambe?
 
Mkuu Mwanakijiji naunga hoja yako hapo juu tena kwa nguvu zote. System ya kuruhusiwa wafanye kazi itaondoa idadi ya mategemezi nchini pia itainua kipato kwa wanafunzi/itapunguza ukali wa maisha kwa wanafunzi hawa. Hapa Tanzania ni Chuo kimoja tu ndio kifuatacho hiyo system. St.John's kimewaajiri wanafunzi wake ktk idara zake kutoa usaidizi, mfano 85% ya wafanyakazi wa maktaba ya St.John's University ni wanafunzi wafanyao kazi under part-time bases! Hii system tukiifata itakuwa poa sana!
 
Inafikirisha ,
inawezekana wakafanya kazi japo itachukua muda vijana kuelewa mantiki ya swala kama hilo hasa ktk kizazi kinachovuka toka ktk fikra za kua ni wajibu wa serikali kubeba mzigo wa elimu. . .
 
Kuna kundi kubwa la watu ambao wanasubiri serikali iwapatie fedha za masomo n.k na wazazi wao wakati wana uwezo wa kufanya kazi. Kwa muda mrefu mfumo ulioundwa na serikali ya CCM unazuia na kufanya iwe ngumu sana kwa wanafunzi kufanya kazi. Matokeo yake, walinzi kwenye vyuo wanaajiriwa nje, wasafisha madarasa na vyoo ni watu wa nje, wakata majani ni watu wa nje wakati kuna nguvu kazi ambayo ipo tu.

Tumetengeneza mfumo wa kundi tegemezi ambalo linachukua tu kutoka kwenye jamii lakini halirudishi. Wengi wa hawa wanapata nafasi ya kufanya kazi kidogo kama sehemu ya kutimizwa matakwa ya elimu yao (research, internships n.k). Je, umefika wakati wa kutengeneza mfumo wa wanafunzi kuchangia elimu kwa kuwapatia nafasi za kazi humo humo mashuleni na kuweka kiwango cha chini cha mishahara ya wanafunzi (iwe tofauti na kima cha chini cha mtu wa kawaida).

Kwa mfano, badala ya kuwapatia posho bila kufanyia kazi kwanini posho za wanafunzi nchini zisiingizwe kama sehemu ya mapato yao wanayofanyia kazi?

je wanafunzi watakuwa tayari kusafisha vyoo, kufagia, kukata majani, kulisha wanyama, kufanya kazi za uwaiter/bartender n.k ili wajipatie kipato cha matumizi?

Je, tunaweza kuweka utaratibu hata wanafunzi wa sekondari nao waruhusiwe kufanya kazi na kujipatia kipato badala ya kutegemea fedha za posho toka kwa familia, wadau na wapambe?

Mkuu mwanakijiji hoja yako ni nzuri ila ni impractical kwa Tanzania. Zamani miaka ya 80 kurudi nyuma wanafunzi wengi wa chuo kikuu, nikiongelea chuo kikuu kwa wakati huo unanielewa (yaani UDSM) walikuwa wana muda wa kufanya kazi za ziada na baadhi yao walikuwa wanafanya kazi. Kilichokuja kuharibu ni baada ya migomo na watawala kutukanwa. Ikaonekana kuwa wanafunzi wa chuo kikuu wana muda mwingi wa ziada ndiyo unaowafanya kufanya mambo ya kipuuzi kama migomo, n.k. Mkakati ukawa dawa ni kuwa keep busy na shule, wataalam wa mitaala wakaanzisha kitu kinachomuweza busy mwanafunzi kuanzia saa moja asubuhi mpaka saa mbili usiku. Anachofikiria ni chakula na darasani tu kama yupo serious na elimu.

wakaanzisha mfumo wa semester kutoka term system, wakaongeza idadi ya kozi, unakuta mtu ana kozi mpaka nane kwa semester na zote hizo anatakiwa kuhudhuria, lecture, seminar/tutorials, katika course assessment anakuwa na homework plus tests. Hii inamfanya mwanafunzi 24hrs a day kufikiria jinsi ya kupangua issue moja ya elimu baada ya ingine, je saa ngapi atapata muda wa kufanya part time job?.

Kingine ni suala la uchumi, kutokana na hali kuwa ngumu waajiri hawaajiri tena, maana kama kuna mtu kamaliza masomo miaka miwili iliyopita na bado hajapata kazi unatarajia aliyeko shuleni atafanikiwa?. Nakumbuka mimi enzi zetu unakuta mtu bado hajamaliza hata mitihani tayari ana offer tatu au nne za kazi mpaka anachanganyikiwa lakini si sikuhizi, tena kibaya zaidi waajiri wameanzisha mchezo wa kuangalia GPA (Grand Points Average) ili mtu awe shortlisted for an interviews, the higher the GPA the higher the chance of being called for the interviews, sasa mtu akiangalia kufocus katika part time kutampunguzia uwezo wa kutengeneza GPA kubwa.

Kwa ujumla tu katika mazingira ya mfumo wa elimu ya Tanzania wa leo hii, hii mada yako wengi wataiona ni kituko japo there is very important suggestions in it.
 
INAWEZEKANA ILA VIJANA WABADIRI MTAZAMO WAO NA FIKIRA ZAO..waache maisha ya omba omba na mizinga..
 
Mkuu mwanakijiji hoja yako ni nzuri ila ni impractical kwa Tanzania. Zamani miaka ya 80 kurudi nyuma wanafunzi wengi wa chuo kikuu, nikiongelea chuo kikuu kwa wakati huo unanielewa (yaani UDSM) walikuwa wana muda wa kufanya kazi za ziada na baadhi yao walikuwa wanafanya kazi. Kilichokuja kuharibu ni baada ya migomo na watawala kutukanwa. Ikaonekana kuwa wanafunzi wa chuo kikuu wana muda mwingi wa ziada ndiyo unaowafanya kufanya mambo ya kipuuzi kama migomo, n.k. Mkakati ukawa dawa ni kuwa keep busy na shule, wataalam wa mitaala wakaanzisha kitu kinachomuweza busy mwanafunzi kuanzia saa moja asubuhi mpaka saa mbili usiku. Anachofikiria ni chakula na darasani tu kama yupo serious na elimu.

wakaanzisha mfumo wa semester kutoka term system, wakaongeza idadi ya kozi, unakuta mtu ana kozi mpaka nane kwa semester na zote hizo anatakiwa kuhudhuria, lecture, seminar/tutorials, katika course assessment anakuwa na homework plus tests. Hii inamfanya mwanafunzi 24hrs a day kufikiria jinsi ya kupangua issue moja ya elimu baada ya ingine, je saa ngapi atapata muda wa kufanya part time job?.

Kingine ni suala la uchumi, kutokana na hali kuwa ngumu waajiri hawaajiri tena, maana kama kuna mtu kamaliza masomo miaka miwili iliyopita na bado hajapata kazi unatarajia aliyeko shuleni atafanikiwa?. Nakumbuka mimi enzi zetu unakuta mtu bado hajamaliza hata mitihani tayari ana offer tatu au nne za kazi mpaka anachanganyikiwa lakini si sikuhizi, tena kibaya zaidi waajiri wameanzisha mchezo wa kuangalia GPA (Grand Points Average) ili mtu awe shortlisted for an interviews, the higher the GPA the higher the chance of being called for the interviews, sasa mtu akiangalia kufocus katika part time kutampunguzia uwezo wa kutengeneza GPA kubwa.

Kwa ujumla tu katika mazingira ya mfumo wa elimu ya Tanzania wa leo hii, hii mada yako wengi wataiona ni kituko japo there is very important suggestions in it.

mkuu imefikia hatua tusiwe watu wakukata tamaa kwa kila kitu.
haya mambo yanazungumzika na yanaweza kupangwa yakafanyika, ni system tu tunaibadilisha kukidhi maitaji yetu, hata serikali ya magamba wanaweza ili sio issue ya kushindikana kabisa
 
INAWEZEKANA ILA VIJANA WABADIRI MTAZAMO WAO NA FIKIRA ZAO..waache maisha ya omba omba na mizinga..

i hope huna maana wasipewe msaada na familia zao na serikali ?
sidhani kama mzee mwanakijiji ana maana wawe full time employed in ajira ya kupata uzoefu wa maisha/kazi na
hela ya pipi/mkate maana hata nchi zinazofanya hivyo bado wanafunzi ni tegemezi kwa kiasi furani ila sio 100%
kama tanzania, lakini pia inaleta ukuaji bora yaani kujenga hali ya kuwajibika toka utotoni
 
Sio tu katika miaka ya 70 na 80 vijana walikuwa wanafanya kazi za ajira, bali pia walikuwa wanajitolea hadi vijijini wanachimba barabara, wanajenga zahanati, wanasafisha vyanzo vya maji ya kula, nk. Kadri ubadhirifu wa mali ya umma na ufisadi vilivyozidi, ndivyo na moyo wa wananchi kujitolea ulizidi kudhoofika, na ndivyo fikira za kwamba 'serikali ina pesa ndio inapaswa kufanya kila kitu' zilivyozidi kutawala. Utamaduni wo wote ule (uwe chanya au hasi) unaochipua na wakati mwingine kukomaa katika jamii ni muhimu uangaliwe katika muktadha mpana zaidi.
Nyongeza tu ya hoja nyepesi: tukisema wanafunzi wa vyuo vikuu wafanye kazi kama hizo na hata kuwa mabaa meidi - huo umati wa wanaomaliza darasa la saba si wote watakuwa vibaka na ma-cd. Hilo utalielezaje?:confused2:
 
Kazi zitatoka wapi iwapo wahitimu wa drs 12, 14, na vyuo hawana kazi.
 
INAWEZEKANA ILA VIJANA WABADIRI MTAZAMO WAO NA FIKIRA ZAO..waache maisha ya omba omba na mizinga..

umesema vema kabisa.Nikiangalia aina ya kazi alizotaja MMKJJ - sijui kama vijana wa siku hizi watataka kujihusisha nazo.Bado kuna fikra hasi kuhusu kazi kama hizo.Watanzania kwa ujumla au waafrika tuseme, wanachagua kazi na kuona kazi kama hizo ni za wasio na elimu yoyote! Inabidi kuanzia mahali hata hivyo. Wanafunzi toka shule za msingi wajengewe fikra za kuthamini kazi yoyote inayompa mtu kipato bila kujali elimu.Utegemezi utapungua kama kila mtu ataona fursa kwenye kazi yoyote,Huenda isiishie kwenye vyuo tu.Kuna kazi za usafi maeneo mengi ya miji yetu.Huenda wasomi wakaweza kuleta fikra mpya katika utendaji na ufanisi wa kazi zile zisizoonekana kuhitaji elimu ambazo ufanywaji wake umekuwa wa kulipua lipua mno.

Na kwa wasichana ambao siku za karibuni wamejivunia sifa ya kupenda vya mteremko kwa kujishushia heshima na kujitweza kwa wanaume pengine kazi hizi zitawarejeshea heshima.Ukitizama wasichana wengi wa vyuoni, inasikitisha aina ya maisha wanayoishi.Wapo wanaoishi maisha ya uchangudoa ati wajipatie vipato vya kukogana na kushindana kwa mavazi, mapambo na hata magari! AIBU JAMANI WANAWAKE WENZETU!
 
Nakubaliana nawe kwenye hoja ya pili lakini hii ya Kwanza siyo kweli.
Mkuu mwanakijiji hoja yako ni nzuri ila ni impractical kwa Tanzania. Zamani miaka ya 80 kurudi nyuma wanafunzi wengi wa chuo kikuu, nikiongelea chuo kikuu kwa wakati huo unanielewa (yaani UDSM) walikuwa wana muda wa kufanya kazi za ziada na baadhi yao walikuwa wanafanya kazi. Kilichokuja kuharibu ni baada ya migomo na watawala kutukanwa. Ikaonekana kuwa wanafunzi wa chuo kikuu wana muda mwingi wa ziada ndiyo unaowafanya kufanya mambo ya kipuuzi kama migomo, n.k. Mkakati ukawa dawa ni kuwa keep busy na shule, wataalam wa mitaala wakaanzisha kitu kinachomuweza busy mwanafunzi kuanzia saa moja asubuhi mpaka saa mbili usiku. Anachofikiria ni chakula na darasani tu kama yupo serious na elimu.

wakaanzisha mfumo wa semester kutoka term system, wakaongeza idadi ya kozi, unakuta mtu ana kozi mpaka nane kwa semester na zote hizo anatakiwa kuhudhuria, lecture, seminar/tutorials, katika course assessment anakuwa na homework plus tests. Hii inamfanya mwanafunzi 24hrs a day kufikiria jinsi ya kupangua issue moja ya elimu baada ya ingine, je saa ngapi atapata muda wa kufanya part time job?.

Kingine ni suala la uchumi, kutokana na hali kuwa ngumu waajiri hawaajiri tena, maana kama kuna mtu kamaliza masomo miaka miwili iliyopita na bado hajapata kazi unatarajia aliyeko shuleni atafanikiwa?. Nakumbuka mimi enzi zetu unakuta mtu bado hajamaliza hata mitihani tayari ana offer tatu au nne za kazi mpaka anachanganyikiwa lakini si sikuhizi, tena kibaya zaidi waajiri wameanzisha mchezo wa kuangalia GPA (Grand Points Average) ili mtu awe shortlisted for an interviews, the higher the GPA the higher the chance of being called for the interviews, sasa mtu akiangalia kufocus katika part time kutampunguzia uwezo wa kutengeneza GPA kubwa.

Kwa ujumla tu katika mazingira ya mfumo wa elimu ya Tanzania wa leo hii, hii mada yako wengi wataiona ni kituko japo there is very important suggestions in it.
 
Na kwa wasichana ambao siku za karibuni wamejivunia sifa ya kupenda vya mteremko kwa kujishushia heshima na kujitweza kwa wanaume pengine kazi hizi zitawarejeshea heshima.Ukitizama wasichana wengi wa vyuoni, inasikitisha aina ya maisha wanayoishi.Wapo wanaoishi maisha ya uchangudoa ati wajipatie vipato vya kukogana na kushindana kwa mavazi, mapambo na hata magari! AIBU JAMANI WANAWAKE WENZETU!

Kweli kabisa; nilikuwa nafikiria hicho vile vile; kwamba yaweza ikawapa uhuru mabinti zetu kuweza kuishi maisha ambayo yanaendana na utu wao. Nimependa hili.
 
Mkjj hii hoja ni nzito na inahitaji ifanyiwe kazi maana si tu kuondoa utegemezi bali hata zile fikra za wakati wa uhuru zilizodumu mpaka leo kwamba msomi lazima afanye kazi ofisini. Inachekesha pale unakuta jitu zima linamtukana baa medi kisa kwa kujiona limeshushiwa hadhi wakati linakaa mjin i kwa dada yake bila kazi yeyote ile. Kuna mijitu pale TZ iko kwenye NGO's ina vitambi vikubwa vikubwa na kutembelea magari makubwa makubwa lakini haijui kwamba hela hiyo wanayotanulia imechangwa na wakata majani, bartenders, waosha vyoo na wengi wao wakiwa wanafunzi tena wengine in high schools.

To me hii scheme kama ilivyopendekezwa ndiyo huko zipitishiwe hata hela za the so called mikopo. Well we can argue about time, lakini inawezekanaje nchi zilizoendelea watu wanasoma, wanafanya kazi, wanacheza michezo na bado wanaenda vacations?
 
This is a bit off-topic, Watu wako SUA pale hawajawahi kushika jembe wala kuji-involve na maswala yeyote ya kilimo na hawatawahi kushika jembe wla ku-operate jembe. Sasa kwa nini mlipakodi amlipie mtu kama huyu kusomea kilimo?
 
C;moon eti nilikuwa najiuliza tumefikaje hapa, nagundua kumbe hatujawahi hata kuwepo huko kwenye other side of the wall.
 
Kazi zitatoka wapi iwapo wahitimu wa drs 12, 14, na vyuo hawana kazi.

Mkuu Kichuguu,
Kwa mujibu wa maelezo ya Mzee mwanakijiji na uzoefu wangu huku ughaibuni ni kwamba kazi zinapatikana ndani ya chuo kwa kugawana ama kuwapunguza kama si kuwa-lay off kabisa hao watu wasio wanafunzi walioajiriwa ndani ya vyuo kufanya kazi zilizo ndani ya uwezo wa wanafunzi kama vile uhudumu wa vyakula na vinywaji kwenye migahawa, lab assistants, tutorial assistants, utunzaji bustani na majengo, uhudumu maktaba na maduka ya vitabu chuoni n.k Mkjj kapendekeza na hao Sekondari Darasa la 12 na 14 wafikiriwe pia japo ni suala gumu sana hasa ukizingatia uchache income resources zilizopo na ufinyu wa muda (saa 11 alfjr mchaka mchaka; saa 12 asbh kujiandaa; saa moja Brekafast-Uji/Chai; saa 1asbh parade; saa 1:40asbh darasani; saa 5:20asb break; saa 6 mchn darasani kumalizia ngwe ya siku hadi saa 8:20mchn; saa 8:30 mch Lunch; Saa 10 jion Usafi wa mazingira hadi saa 11:30; Saa 12 jion dinner; saa 2 uck Prepo (kujisomea, homework wengine wanatongozana kwenye viunga vya dark corners-omba usishikwe na kiranja wa ulinzi n.k) na saa 4 na kuendelea watu wanarudi vitandani(speaking to my experience kule Govt boarding school pande za kaskazinI TZ)
Kwa wanafunzi wa chuo wengi wao hawana ratiba ngumu kama za hao drs la 12 na 14. Unakuta Mwanafunzi anaanza na kozi ya kwanza saa 2 asbh kozi ya pili saa 10 jion au anaweza akawa na kozi moja au hasiwe na kzoi kwenye siku fulani. Kwa mfano J'3, J'5 na Ijumaa yupo darasan J'4, J'5 na wikiendi akawa anazurura Kahumba Night club- watu wa SUA, Jolly Club, Bills, Maisha club ama Mlimani City -IFM/UDSM, au Mnadani na kushangaa jengo la Bunge-UDOM badla ya kulitumia hilo gap angalau kujishhugulisha na vibarua vitakavyomuingizia kipato ambacho kiasi fulani kinapunguza utegemezi wa familia au hata kuwalipia ada wadogo zao walio sekondati.
 
Hii inawezekana kabisa lakini kazi zenyewe ziko wapi?
Halafu hawa vjana wetu 'MASHAROBARO' kazi nyingine hawapendi kuzifanya. Laiti kama wangepitia JKT labda hili wazo lingewezekana.
 
Wanavyuo wanaweza pia kusambazwa shule za kata ili wafundishe kwa mshara, kwa ile mikoa ambayo vyuo hivi vipo. Wanafunzi wa sekondari wanasema kuwa wanafunzi waalimu hujituma zaidi (wakiwa field) kuliko walimu waajiriwa. Ni wazo zuri sana hili
 
Nakubalina na wewe MM
Ila kama alivyodokeza mmoja wetu hapo juu, mitaala ni lazima irekebishwe
ili kuwezesha mazingira ya hii kitu.
Niongezee vitu viwili
1. Mitaala ibadilishwe such that, mtu anaweza akasitisha masomo
kwa muda baada ya term au semester kama amekamata kazi
inayomlipa.

2. Kwenye hili la ajira za wanafunzi wa secondary, isiishie hapo tu
watoto kuanzia miaka hata kumi na tano waruhusiwe kufanya kazi
hii itawapatia on the job training and expertise, mfano halisi tunao
kwamba mafundi magari wengi hapa nchini ni watu ambao wameanza
kama maspaner boys lakini wanapata shule ya uhakika na kuwatoa kimaisha.

hii ni muhimu sababu, badala ya nchi kuzalisha watoto wa mitaani ambao
baadae watabadilika na kuwa vibaka wazoefu tutakuwa tunajenga jamii
ya wafanyakazi endelevu. Ila wasiruhusiwe kiholela tu kama ilivyo sasa
bali kuwe na policy ya kitaifa ama kimkoa itakayoweka muda wa mtoto
kufanya kazi, idadi ya watoto wanaoruhusiwa kufanya kazi kisheria,
na kila muwekezeji alazimishwe kisheria kuwa na serious training
program kwa watoto hawa n.k
 
Back
Top Bottom