Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Kuna kundi kubwa la watu ambao wanasubiri serikali iwapatie fedha za masomo n.k na wazazi wao wakati wana uwezo wa kufanya kazi. Kwa muda mrefu mfumo ulioundwa na serikali ya CCM unazuia na kufanya iwe ngumu sana kwa wanafunzi kufanya kazi. Matokeo yake, walinzi kwenye vyuo wanaajiriwa nje, wasafisha madarasa na vyoo ni watu wa nje, wakata majani ni watu wa nje wakati kuna nguvu kazi ambayo ipo tu.
Tumetengeneza mfumo wa kundi tegemezi ambalo linachukua tu kutoka kwenye jamii lakini halirudishi. Wengi wa hawa wanapata nafasi ya kufanya kazi kidogo kama sehemu ya kutimizwa matakwa ya elimu yao (research, internships n.k). Je, umefika wakati wa kutengeneza mfumo wa wanafunzi kuchangia elimu kwa kuwapatia nafasi za kazi humo humo mashuleni na kuweka kiwango cha chini cha mishahara ya wanafunzi (iwe tofauti na kima cha chini cha mtu wa kawaida).
Kwa mfano, badala ya kuwapatia posho bila kufanyia kazi kwanini posho za wanafunzi nchini zisiingizwe kama sehemu ya mapato yao wanayofanyia kazi?
je wanafunzi watakuwa tayari kusafisha vyoo, kufagia, kukata majani, kulisha wanyama, kufanya kazi za uwaiter/bartender n.k ili wajipatie kipato cha matumizi?
Je, tunaweza kuweka utaratibu hata wanafunzi wa sekondari nao waruhusiwe kufanya kazi na kujipatia kipato badala ya kutegemea fedha za posho toka kwa familia, wadau na wapambe?
Tumetengeneza mfumo wa kundi tegemezi ambalo linachukua tu kutoka kwenye jamii lakini halirudishi. Wengi wa hawa wanapata nafasi ya kufanya kazi kidogo kama sehemu ya kutimizwa matakwa ya elimu yao (research, internships n.k). Je, umefika wakati wa kutengeneza mfumo wa wanafunzi kuchangia elimu kwa kuwapatia nafasi za kazi humo humo mashuleni na kuweka kiwango cha chini cha mishahara ya wanafunzi (iwe tofauti na kima cha chini cha mtu wa kawaida).
Kwa mfano, badala ya kuwapatia posho bila kufanyia kazi kwanini posho za wanafunzi nchini zisiingizwe kama sehemu ya mapato yao wanayofanyia kazi?
je wanafunzi watakuwa tayari kusafisha vyoo, kufagia, kukata majani, kulisha wanyama, kufanya kazi za uwaiter/bartender n.k ili wajipatie kipato cha matumizi?
Je, tunaweza kuweka utaratibu hata wanafunzi wa sekondari nao waruhusiwe kufanya kazi na kujipatia kipato badala ya kutegemea fedha za posho toka kwa familia, wadau na wapambe?