Wanafunzi masnitch wapewa onyo ST. Joseph

May 5, 2017
94
32
Kikundi cha kukamilisha harakati za pale kati kilichojipa jina kali wametoa onyo kwa KIBARAKA yoyote na KIMBELEMBELE MUOGA yoyote atakayesogeza miguu yake St Joseph kesho wakati wenzao watakapogoma.
Ni mwaka mmoja tangu serikali ya wanafunzi wa St. Joseph ya kuanzia February 2016 hadi February 2017 ilipoandika waraka unaoanisha matatizo yao na kupelekea mgomo wao ambao ulifikia siku ya tatu na Waziri wetu mahiri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia kufika chuoni hapo na kumaliza mgogoro uliojitokeza kwa kuwasihi wanafunzi waendelee na shughuli za taaluma huku yeye na mamlaka zilizo chini yake zikiendelea kuyatatua matatizo hayo kwa namna ya MAAGIZO kwa Chuo. Ninachokusudia kuandika hapa ni kwa namna gani wahindi hawa wamekuwa wakifanya wanayowajua wao na kushindwa kutekeleza maagizo yote halali kutoka TCU na Wizarani.Waziri alitekeleza ahadi lakini wahindi ambao ndio watekelezaji wameonyesha jeuri na dharau ambayo imefikia kumsimamisha masomo Rais wa sasa wa wanafunzi baada ya kumuandikia Waziri na Waziri Mkuu akiomba wawasaidie wanafunzi anaowaongoza ili waraka wao ushughulikiwe kikamilifu.Waziri na Waziri Mkuu hawakufanya ajizi wakamjibu lakini badala ya kutatua matatizo wanaongeza matatizo na sasa wanachokitafuta wahindi hawa wachache watakipata hivi punde. Nawasihi mpitie post zangu muelewe mlolongo ulivyokuwa mpaka Rais akasimamishwa masomo na sasa kinachofuata ni kuwaonyesha wahindi hawa wachache(nitawataja)kuwa UZALENDO HAUPIMWI. Rais huyu aliyebambikizwa kesi na makanjanja hao aliandika kwenye barua yake sentensi kwamba mpaka sasa yapo matatizo mengi yaliyomo warakani hayajashughulikiwa na hakuna dalili ya kushughulikiwa. Kilichofuata ni kutengenezewa kesi kuwa ameghushi taarifa kwa madhumuni ya kukitia hasara Chuo .Wahindi hao walitumia kipengele 4.17 cha makosa na 20.8 cha adhabu kutimiza azma yao. (NIMEAMBATANISHA soft copy ya waraka na by law za Chuo).Sasa hapa nawaletea ukweli wa nini katika waraka kimeguswa na kimefanyika na kufikia wapi. Kumbuka kutatua tatizo ni kulimaliza ndani ya muda ulioamriwa kwa hiyo mengi hawajatatua na uzi huu utaondoa shaka kuwa Rais huyu alikurupuka:<br /><br />UONGOZI MBOVU<br />Ilielezewa vyema:Uongozi usio na viwango vinavyotajwa na Sheria ya Vyuo vikuu.Agizo likawa watolewe na wawekwe wenye sifa.Utekelezaji ukawa alitolewa Vice Principal Pratheep na kuwekwa mwenye sifa. Chuo hakikuwa na Deputy Vice Chancellors.Amewekwa mmoja.Wakuu wa vitivo wengi hawana sifa zilizoainishwa na sheria ya vyuo vikuu.Status:Vice Chancellor ni Dr. Bhaskara Raju...sio Professor..sio Associate Professor..sio Assistant Professor.Lakini Sheria ya vyuo vikuu inataka asipokuwa huko kote basi awe senior academician yaani awe mjumbe wa academy yoyote rasmi nchini na awe senior katika rank za academy hiyo.Huyu Bhaskara Raju hayupo hata huko! Ukibisha mtafute Prof. Kikula au Prof. Mgaya uwaulize kama kwenye TANZANIA SCIENCE ACADEMY wana mjumbe anaitwa Bhaskara Raju?Huyu Bhaskara ndiyo yuleyule niliyesema humu ni porn addict..ameshiriki kuamuru kutengenezewa kesi wanafunzi na wengine wamedisco na sasa kafika kwa Rais kufanya uhaini uleule.Huyu alishasema kauli ileile iliyomfanya Mwalimu Nyerere kumfungia mtu kukanyaga Africa kama msamaha wake. Bhaskara alishasema mwaka 2015 wakati wa mgomo kule Arusha "serikali yenu(ya Tz) tumeiweka mkononi" kwa kujiamini.Alikuwa anawakodia baadhi ya watumishi wa ngazi za juu serikalini hoteli na kuwalipia safari za ndege enzi hizo rushwa imezoeleka. Huyu ameshiriki kukuza ubaguzi wa rangi hapa chuoni maana anasema hawezi kuongea na wanafunzi wanamsumbua. Huyu anasigina haki za walimu wa wanafunzi wetu kwa kuwapangia muda mrefu wa kukaa chuoni bila hata OC. Huyu anafanya biashara ya kugawa sapu kwa wanafunzi(anatakatisha kufelisha wanafunzi) kwa visingizio ameagizwa na TCU ya Prof. Mageni na kwamba hataeleweka wanafunzi wengi wasipofeli. Huyuhuyu anamtisha Vice Principal Administration Prof. Saburi kwa kile anachokiita Prof huyu mzalendo anawaharibia soko.Na huwa hazungumzi kifichoni...anapofanya uhaini wake na kiburi chake anafanya kwa kebehi nyingi. Sijui katumwa na nani kuvuruga uendeshaji wa mambo ya taaluma ya watoto wetu wahandisi WAZALENDO watarajiwa?Watoto wanaolipa milioni 3 kupata dhahabu na wanakutana na kizuizi cha kanjanja huyu anayetaka wazipate kwa taabu. Yupo kigogo wao ambaye baadhi ya maofisa wa juu serikalini akiwemo mmoja katika Wizara ya Elimu.. Dr. M***ambo na mmoja wa ERB Eng.Msa***a wanashuhudia kuwa ni mtembeza rushwa na mla bata na vibinti. Kazi yake huyu ni kutumia ada za watoto wetu kujitanua na kutembeza rushwa. This corrupt fellow anaitwa Dr.T.A.X.Ananth na ndiye Mwenyekiti wa Bodi ya Chuo.Wahindi wanamwita Mr. President .Alizoea mazoea mabaya na sasa kakutana na hali ngumu ya mazoea yake ya rushwa. Uongozi ulio chini ya viwango,uliozoea rushwa na unaovuruga uzalendo wa vijana hawa kumbe bado upo. Wao wakafanya siasa kumtumbua yule aliyetolewa mfano kwenye waraka halafu majipu yenyewe wameyaacha. Nadhani Rais wetu mpendwa Dr. John Pombe Joseph Magufuli alishawahi kuonyesha demo kwa makanjanja ya kihindi kama haya kule Lindi. Nyang'anya PASSPORT.. Nyang'anya VISA... Rudisha hawa kwao. Hiyo ndiyo dawa sahihi kwa LIJIPU hili.Hatujaishia hapo. Yupo kijana wa kihindi mtiifu kwa majipu haya naye anaitwa JAISON JACOB ambaye ndiye DEAN kwa vitendo na ASSISTANT DEAN 2 kwa cheo. Hapo St. Joseph kuna CHIEF DEAN ambaye ni MEJA MSTAAFU MATHEW NGULUNGULU na ASSISTANT DEAN 1 KANALI MSTAAFU ISAYA MWAIPOPO. Hawa wazee ni vivuli tu wa bwana mdogo JAISON JACOB ambaye ni kibaraka cha hao wahindi wawili wakubwa.Ana tabia ya kupindisha kila hali ili kuwatetea mabwana wake ili kukandamiza serikali ya wanafunzi.Hili halijaisha bado. Kwa hiyo lile agizo la Serikali kuu kwamba kuwe na Ofisi yenye meno ya Dean of Students lilipuuzwa. Kwani nani aliyetekeleza agizo la kufukuzwa Bachubila? Ni JAISON JACOB.Huu ukiukwaji wa kifungu namba 49 cha sheria ya vyuo vikuu hautakiwi kupuuzwa na serikali kuu. Oneni wenyewe jinsi tatizo moja lilivyokuzwa kwa upuuzi wa wahindi hasa CHANCELLOR ambaye ni Padre mhindi aishiye India kushindwa kutekeleza amri halali ya serikali kuu. Wapo! <br /><br />MAKTABA ISIYO NA MAZINGIRA RAFIKI. <br />Malalamiko yalikuwa kwamba maktaba hii ina taratibu zinazolea urasimu, maktaba haina vitabu vya kutosha, maktaba inafungwa saa 12.Kilichobadilika ni kuondoa urasimu mmoja tu wa kutoruhusu wanafunzi kujichagulia vitabu na maktaba kufungwa saa 2 usiku.Wiki iliyopita tunaambiwa Waziri wa Elimu wa serikali ya wanafunzi iliyopita,kijana mzalendo hasahasa, aliandika ujumbe kwenye group chats za whatsapp akielezea jinsi mhindi anayesimamia uendeshaji wa maktaba hiyo mida ya jioni anavyoingia akiwa ananuka pombe na sigara na kuingilia mchakato wa wanafunzi kutumia kompyuta za maktaba.Ana tabia ya akikukuta unasikilza hotuba,documentary,lectures basi anakughasi kukuambia usome ya kozi yako tu! Kwake hiyo ndiyo Elimu.Sishangai kuambiwa kuwa Waziri huyu kijana mstaafu aliamua kuwasihi wenzake wamtumbue na waupinge ujinga popote ulipo.Huyu msimamizi ni mjinga kwa sababu hajui maana ya elimu kwa Tanzania na hajui hata dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2025.Majipu maktaba...Wapo!<br /><br />MAPROFESA NA PHD HOLDERS. <br />Vijana walilalamika kuwa pamoja na ada nyingi wanayoilipa,hakuna Profesa katika kitivo chochote.Serikali ikaagiza waajiriwe Maprofesa na maDokta wa kutosha na uwiano uwe mtaalam mmoja kwa kila wahadhiri wanne(1:4).Wakasema, vijana hawa,kuna wahadhiri wengi mno kutoka India kiasi kwamba akili zao zinachoka mno kuzoea tamaduni zao za ajabu za kufuatiliana maisha!Agizo likawa ratio iwe kwa kila wahadhiri wanne wa kizalendo kuwe na mmoja tu wa kihindi.Lakini ratio ni 1:2 na mpaka sasa katika wahadhiri 84++ waliopo kuna Profesa Mneney,Prof mmoja wa Mechanical,mmoja wa mwaka wa kwanza na mmoja wa ualimu.Piga mwenyewe ratio na utapata 1:21 wakati waliagizwa 1:4.Je,Bachubila kakosea kusema hakuna dalili za utatuzi wa dhati?Wahindi hawa ni waghushi nyaraka.Katika ripoti yao ya utekelezaji maagizo wakasema wamerudisha wahindi 26 kwao lakini katika orodha hiyo wamo waliokuwa wameshaondoka,yupo mmoja ambaye bado anafundisha na yuko kitivo cha uhandisi umeme.Na wamepeleka ripoti hiyo TCU. Bachubila kaghushi taarifa? Wahindi wahuni waghushi taarifa... Wapo! Wanaodharau maagizo ya serikali kuu kuhusu elimu.... Wapo! <br />Hakuna sera ya utafiti,hakuna watafiti, wanafunzi hawafundishwi mbinu za utafiti.Uhuni tupu!<br /><br />ADA KUBWA, MICHANGO MINGI. <br />Vijana hawa wakasema kuwa ada wanayoilipa ni kubwa na michango ni mingi bado. Waziri Ndalichako akasema suala la ada wanafunzi waongee na Chuo na pia Chuo kikaagizwa kufuta michango! Wakaleta utaratibu mkali wa kulipa ada na kusimamisha wanafunzi 81 kwa kutomaliza ada.Wakarudisha ada ya mtihani kinyemela. Vijana wakamlilia Bachubila kuhusu utapeli huu. Kumbe mpaka utapeli? <br /><br />KUKANDAMIZWA KWA HAKI ZA WANAFUNZI NA UBAGUZI. <br />Vijana walilalamika kuwa serikali ya wanafunzi haiheshimiwi, haipewi mazingira rafiki! Kwa kifupi wahindi walibainika kutotambua TANGAZO LA SERIKALI NAMBA 178.Katiba iliyopo ya serikali ya wanafunzi imetungwa na Senate ya Chuo! Uhuni! Agizo likawa serikali ya wanafunzi iachwe ijiendeshe. Bado wahindi wakaingilia mchakato wa bajeti na mpaka sasa inafanya kazi bila bajeti na inatumia matakwa ya yule mhindi kijana kibaraka JAISON JACOB.Wahindi wakaingilia mchakato wa kutengeneza katiba na wakafeli na sasa hawajaweka nia ya kuipeleka ikapitishwe na Bodi ya Chuo.Wahindi wanataka eti safari zote na barua zote za serikali ya wanafunzi zipitie kwa Dean! Wahindi hawataki kuipa serikali ya wanafunzi nafasi ya kupendekeza marekebisho ya sheria ndogondogo ambazo ni kandamizi(nimeambatanisha by laws hizo). Wahindi hawataki kumuachia Rais wa serikali ya wanafunzi mamlaka ya kuteua wanafunzi anaoona wanafaa kushika nyadhifa za uongozi.Wanatumia kigezo chao wenyewe cha GPA kumzuia kuteua viongozi.Wanataka Kiongozi wa kuteuliwa asiwe na sapu na GPA chini ya 3.5.Hii ni kinyume na Tangazo namba 178 la serikali kuu. Majipu! <br /><br />KUKOSEKANA KWA MAZINGIRA RAFIKI YA KUJISOMEA. <br />Vijana walilalamika kwamba wanasomea vyumbani mwao na kwenye bwalo la chakula. Kote hakuna hali nzuri ya kujisomea.Vijana walitaka hela zao ziache kuhongahonga na kufanyia starehe na vijengwe vimbweta. Vimbweta bado! Hata upembuzi yakinifu bado! Wako busy kula za sapu sasa!Maagizo yalikuwa waweke mazingira rafiki! <br /><br />MAABARA ZISIZOKIDHI VIWANGO NA WATAALAM WA MAABARA WACHACHE. <br />Vijana walilalamika kuhusu maabara duni katika vitivo vyote.TCU ikajiridhisha na ikatoa maagizo makali yaliyofikia kuwaelekeza hata nafasi ya maabara iweje!Wamegusa maabara ya Kemia,wamegusa maabara moja tu ya uhandisi ujenzi, wamegusa maabara ya uhandisi mekanika,wamegusa workshop na nyingine hakuna dalili na zilizoguswa zote bado zina mapungufu ya kitaalam mapya ikiwemo vifaa vya kizamani, chakavu na vichache!Wataalam wa maabara bado ni walewale na walioongezwa ndo hao wanakutana na mazingira magumu ya kazi. <br /><br />Hiyo ni simplified version ya volume ya mududu wanayoendeleza wahindi hawa wachache wanaosimamia uendeshaji wa St. Joseph.Vijana katika waraka wao wa kwanza walitoa mapendekezo na Mimi natoa yangu Leo:<br /><br />KUHUSU UONGOZI MBOVU; <br />Serikali ya JMT ione uhujumu unaofanywa na wahindi hawa:DR.T.A.X.ANANTH,DR.BHASKARA RAJU,JAISON JACOB na MR.RANJITH,na iwachukulie hatua kali madhubuti.Alinyang'anywa vitambulisho vyake.Hawa wameshasimamia ubovu mwingi na kuulinda kwa rushwa,vitisho na uonevu. Hawa warudi kwao. Hakuna namna. Warudi kwao na Pro Chancellor wa Chuo hiki Mhadhama Polycarp Pengo atafutwe na ahimizwe kutumia Sera Katoliki ya Elimu ya juu ili kuasisi Uongozi mpya wenye viwango na ufanisi kuliko huu wa matapeli hawa.Huyu na Padre Dr. Emmanuel Raj wa India ndio wamiliki wa Chuo hiki.Lazima wachukue hatua. Ama sivyo tuwe tayari kwa migogoro kila kukicha na baadae kuingia migogoro ya kidiplomasia.Uongozi ndiyo msimamizi na mtekelezaji wa maagizo ya serikali kuu yanayolenga kuleta elimu bora.Hawa ndiyo tatizo na ndiyo wachonganishi wa wanafunzi na serikali yao ya JMT. Ndiyo jipu kuu. Tumbueni hili leo na maagizo yenu yatatafutiwa namna ya kutekelezwa na sio namna ya kujitetea.<br /><br />KWENU TCU. <br />Nyinyi ni tegemeo la wanafunzi hawa. Mwokoeni Rais wao, simamieni utekelezaji wa maagizo yenu kwa ukali na uzalendo bila kuchoka na Tanzania itawatukuza.Prof Mageni,Dr.Mollel,Dr.Matimbo,Dr.Damean,kumbukeni waliowatangulia walitumbuliwa kwa kusitasita mno kuyatumbua majipu ya St. Joseph.Siwatishi.Nawaaminia.Fanyeni yenu na inapobidi kitawaleni hicho Chuo kwa muda. <br /><br />KWAKO PROF NDALICHAKO. <br />Umejitosheleza.Tafiti zako zinaishi maana moja umeshaitumia tayari kuamua kuhusu suala la kusoma sayansi mpaka kidato cha 4.Intellectual anafanya yale ambayo mawazo yake yanamshawishi kufanya kwa nia ya kuyaheshimu mawazo yake. Hiki Chuo sio cha kukushinda.Uongozi wake sio wa kukudharau kiasi hicho! Fanya maamuzi ya kizalendo na ya lazima kutindua mfumo mbovu wa uongozi huu uliochoka. <br /><br />KWAKO WAZIRI MKUU MH. MAJALIWA <br />Unaaminika pasipo shaka.Umemjibu Rais huyu na kesho yake akafukuzwa. Ulifika Ilboru kutumbua enzi zile ukiwa Naibu Waziri wa TAMISEMI-Elimu. Wahindi hawa usisubiri intelijensia tena.Vuka mipaka ya intelijensia, wape nafasi vijana wa St. Joseph kwa kuwatembelea na kutumbua majipu haya bila haya. <br /><br />KWAKO MTUKUFU RAIS DR. JOHN POMBE JOSEPH MAGUFULI. <br />Ulimnyang'anya vitambulisho yule tapeli kule Lindi. Wapo matapeli hao hapo waliozoea hongo na mtelezo wa ganda la ndizi. Wapo! Warudi kwao kwa kudharau mamlaka yako, kwa kusema serikali yako inashughulikia waraka usio rasmi na wamejipanga kukata rufaa TCU.Ongea na Kardinali ambaye ni Pro Chancellor ili muafikiane ama kufanya mageuzi au Wahindi wote kwao na wanafunzi wabebwe na serikali kama wenzao wa Arusha na Songea lijulikane moja. Kama kuna Kiongozi aliyeleta sura ya uongozi iliyosahaulika(ya walking the talk) basi ni wewe Mtukufu Rais. Hii ni ukweli mtupu.<br /><br />KWENU WANAFUNZI WA ST. JOSEPH <br />Acheni ushirikisho,acheni ueducation na u engineering,acheni utimu Gadaffi na utimu Barongo! Wote nyinyi ni wahanga wa uhuni unaofanywa na hao wahindi wachache.Kuweni wamoja katika yote muyatoe hayo majipu ili mbaki na jina safi popote mtakapokwenda. <br /><br />KAULI MBIU YA LEO NI,"UKITUPIMA UZALENDO TUTAKUONYESHA NGUVU YA UZALENDO"<br /><br />Wenu mtiifu,<br />CITY HUNTER.<br />Naambatanisha waraka na by laws <br />
screenshot_2017-05-18-19-06-26-png.511183
screenshot_2017-05-18-19-06-42-png.511184
screenshot_2017-05-18-16-23-47-png.511185
screenshot_2017-05-18-16-23-55-png.511186
 

Attachments

  • AL+SHABAAB+.pdf
    154.5 KB · Views: 89
Kikundi cha kukamilisha harakati za pale kati kilichojipa jina kali wametoa onyo kwa KIBARAKA yoyote na KIMBELEMBELE MUOGA yoyote atakayesogeza miguu yake St Joseph kesho wakati wenzao watakapogoma.
Acha basi hizo kutisha wenzako, kila mtu amekuja chuo kwa malengo yake, kama wewe una agenda hiyo huyo ni wewe usilamishe mwenzako kwa kuwatisha, hii ndio democrasia tunayoililia kila siku kwa kutishana hivi!?
 
Acha basi hizo kutisha wenzako, kila mtu amekuja chuo kwa malengo yake, kama wewe una agenda hiyo huyo ni wewe usilamishe mwenzako kwa kuwatisha, hii ndio democrasia tunayoililia kila siku kwa kutishana hivi!?
Ndo maana umeambiwa usije kama unaogopa! Hujatishwa! Umepewa uchague kati ya kumpigania Rais wako anayepigania haki zako na kutokuja lakini ukisnitch lazima wenzako wasikuelewe. Kwa hiyo acha woga lakini pia acha kimbelembele cha kujikuta unataka kukwamisha wenzako.
 
kweli kuna wanafunzi 'wapumbavu'. Akili za hao jamaa (wanachuo) wanaojiita alshaba hazifikii hata Robo ya akili/mbinu tulizokua tukitumia Kibiti boys form 5 & 6 enzi hizo katika kuandaa migomo na kufanikiwa kwa kiwango kikubwa kabisa hadi kufikia hatua ya Kumng'oa mkuu wa shule. Intelijensia ya 'wanachuo' hao ni ziro
 
Ndo maana umeambiwa usije kama unaogopa! Hujatishwa! Umepewa uchague kati ya kumpigania Rais wako anayepigania haki zako na kutokuja lakini ukisnitch lazima wenzako wasikuelewe. Kwa hiyo acha woga lakini pia acha kimbelembele cha kujikuta unataka kukwamisha wenzako.
Unalazimisha wenzako wasije class hiyo attandency utawaongezea wewe?, goma kivyako buana
 
Ndo maana umeambiwa usije kama unaogopa! Hujatishwa! Umepewa uchague kati ya kumpigania Rais wako anayepigania haki zako na kutokuja lakini ukisnitch lazima wenzako wasikuelewe. Kwa hiyo acha woga lakini pia acha kimbelembele cha kujikuta unataka kukwamisha wenzako.
c lazima wote muwe na mawazo sawa fala ww
 
kweli kuna wanafunzi 'wapumbavu'. Akili za hao jamaa (wanachuo) wanaojiita alshaba hazifikii hata Robo ya akili/mbinu tulizokua tukitumia Kibiti boys form 5 & 6 enzi hizo katika kuandaa migomo na kufanikiwa kwa kiwango kikubwa kabisa hadi kufikia hatua ya Kumng'oa mkuu wa shule. Intelijensia ya 'wanachuo' hao ni ziro
 
Sasa hao wanaxhotaka Ni nn!?msikiti chuoni au huyo kiongozi wao kurudi!!?
Ushauri Mdogo nawapa kama mnasoma hapa,kamanaona hapo st Joseph Amna msikiti amieni morogoro kwenye chuo cha dini yenu!!
 
Mkigoma ni kwa hasara yenu wenyewe

Anyetaka kugoma mwache agome

"why to waste u'r time in riot's
Can you afford to loss 6 moths of u'r life time ???"

Ukiwa unagoma fikilia tena kwamba the most scarcity resource in the world is not money is time

After all vision zetu haziendani na hatufanani so kwa anaye taka kugoma mwache agome kwa sababu kwa kufuata mkumbo utaloss lifetime yako
 
Gomeni Bana Haki Haipatikani Kwa Maneno Tu Hakuna Kitu Kinachowaogopesha Wahindi Kama Mgomo Hadi Nyuso Zao Hubadilika Rangi Na Hii Itapeleka Alert Kwa Waziri Husika
 
Back
Top Bottom