TANMO
JF-Expert Member
- Apr 12, 2008
- 11,515
- 11,277
Hii thread imenipa simanzi,
R.I.P wapendwa wetu waliotutangulia...
Last edited by a moderator:
queenkami umenigusa na huu ujumbe,yaan nimejikuta natafakari mambo mengi,siku mm cheusie roho itakapoacha mwili sijui nan atakuja jf kuwajulisha,ila roho yangu haitatulia nife bila kuambiwa R.I.P CHEUSIE na wana jf.Lazima nikifa wana jf waniambie R.I.P hivyo jamani nan anataka kukutana na cheusie mlimani city this weekend??sharti atakayekuja kama ni mkaka aje na mkewe?
queenkami umenikumbusha kuna memba mmoja anaitwa HOYANGA aliwahi kuja humu jamvini na kulalamika kuwa anaumwa sana hivyo anahisi kuwa atarest in peace siku sio nyingi, kama unavyoifaham jf kuna waliompa pole na kumshauri aende kwa madaktari bingwa, kuna waliomdhihaki na kumcheka n.k.... Toka siku ile sijawahi tena kumwona yule memba humu jamvini na ni mda mrefu sana umepita kama miezi 6 au 8 hivi... Hatujui labda alizidiwa na kutangulia mbele ya haki kweli( siombei iwe hivyo) au vipi......kufahamiana/kujuana ni jambo jema na la msingi sana.
yaani acha tu
NYANI N,what more do you want,waswahili tunasema mtende umeotea kibarazaniitakuwa bingo kwangu,kujuana na rais wa wabeba box..? Mwaka si ndio huu jamani
Namkumbuka Kandambilimbili(RIP)!
Huenda siku moja atarudi atujulishe kama huko alipo kuna JF au kitu kinachofanana nayo!
gOOSH!...Pole sana.RIP Baruthi (baba mkwe).
Too bad!Humu ndani wengi tumekutana na tumejuana, sasa kwa wengine sijui. Kuna mtu anaitwa MWANAHAKI amealzwa sana pale Tumaini hospitali. Leo hii amefanyiwa Leo amefanyiwa SKIN GRFT SURGERY hapo KCMS. TUmuweke kwenye maombi na wale wote mlioko MOSHI ebu kamsalimieni kama mnapata muda.
Mwenye kupenda kwenda huko anaweza nitext ili nimpatie namba ya simu. Namba yangu 0655 447788. Tujuliane hali kwenye shida
MUNGU AWABARIKI SANA.CD
gOOSH!...Pole sana.
I knew this guy very much!...alikuwa mhasibu professionally, so alipita ofisini kwangu mara kadha kwa kazi moja mbili!
Hoja zake zilikuwa zimesimama sana, na alikuwa akitumia utaalamu wake kusupport hoja!
Anyway, naamini somewhere inlife we gonna see these friends!
[/QUO
Apumzike kwa amani ya bwana!
red: mawazo yako si sahihi hata kidogo! Hata jambazi akifa watu wa ukoo wake wanasikitika!... Wewe ni mtumishi mkuu, na hata wanaokulaumu, huwa wanaku'admire sana kwa kazi yako!PAW akitutoka naamini taarifa zitafika kwenu hakika, na wengine sherehe... Ama kwa hakika inatia huzuni kubwa kwa wenzetu waliotutangulia mbele za haki. Mungu awapumzishe sehemu salama Amin JF ni zaidi ya familia.
r.i.p chetuntu,queen umeongea la maana sana.kuna haja ya kutafuta mtu humu anijue kiukweli
queenkami umenikumbusha kuna memba mmoja anaitwa HOYANGA aliwahi kuja humu jamvini na kulalamika kuwa anaumwa sana hivyo anahisi kuwa atarest in peace siku sio nyingi, kama unavyoifaham jf kuna waliompa pole na kumshauri aende kwa madaktari bingwa, kuna waliomdhihaki na kumcheka n.k.... Toka siku ile sijawahi tena kumwona yule memba humu jamvini na ni mda mrefu sana umepita kama miezi 6 au 8 hivi... Hatujui labda alizidiwa na kutangulia mbele ya haki kweli( siombei iwe hivyo) au vipi......kufahamiana/kujuana ni jambo jema na la msingi sana.
Ingawaje humu ndani kuna memba wengi wanaojuana.
Hii Thread sijaipenda, sababu ya kutokuipenda imenikumbusha member wa JF aliyefariki 17 November 2011lakini ID yake ya hapa JF sikuwahi kuijua alikuwa anafanya siri. Jina lake la Ukweli ni SALIM HASSAN, Marehemu alianguka ghafla wakati anafanya mazoezi ya kukimbia asubuhi, aliitiwa Ambulance na kumpeleka Steve Biko Hospital Pretoria, Marehemu alikuwa kwenye COMA kwa week, baada ya week alifariki na mwili wa marehemu ulisafirishwa nyumbani Tanzania na kuzikwa kwao Zanzibar. Marehemu alikuwa Mfanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania nchini South Africa as Driver. Marehemu aliacha Mke na Mtoto mmoja wa kike nchini South Africa, RIP.
View attachment 44968
View attachment 44968
View attachment 44969
Mimi huwa namkumbuka sana yule mwenzetu aliyejiita Mpenzi wa Islam. Huyu alinigusa sana kwa jinsi alivyokuwa mpole na kutumia lugha ya kistaarabu katika majadiliano katika jukwaa la dini. Pamoja na baadhi ya wachangiaji walikuwa wakitumia matusi na kashfa nzito nzito dhidi ya dini ya Kiislam, Mpenzi wa Islam hata siku moja hakukashifu, kumtukana mtu/dini au kutumia lugha ambazo si za kistaarabu bali alijibu kwa kujaribu kuwaelewesha wachangiaji hao. Nilipenda sana kusoma michango yake na hadi nikamuomba urafiki hapa jamvini. Nilipenda sana kukutana naye na tayari nilishapanga kumtafuta pindi nafasi ingeruhusu lakini kabla ya kufanikiwa kufanya hivyo akafariki. Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu na wengine wote waliowahi kuwa wanachama wa jamvi hili mahali pema peponi~AMEN.
JF Imeeanza mda mrefu saaana..... Saana tena.... It is bound to happen kua wengi hatuko nao tena hapa; Ni kweli kua yawezekana wengine ni members ambao tayari twajuana katika jamii.... BUT with JF it is different.... for the simple reason mtu aishi vile atakavo. Nafikiri sometimes the inner self ya mtu ipo true JF (coz watu wapo comfy hawajulikani) kuliko hata mtaaani.
Malengo ya huu uzi.... nimeyapenda.... Hatujui has ni ipi ID the person behind is deceased.... BUT ile tu kua twawaombea heri na kwa Mungu wapumzike kwa Amani (kama zimetoka rohoni mwetu.... NAAMINI Mungu ni Mkumba na anapokea sala na maombi yetu). Naomba nikupe pole kwa kumpoteza huyo rafikiyo... na pole kwa kukumbuka pia, ila ni vizuri ujue kua some BEST MEMORIES are so painful; But still we reminisce... Pray.... and hope that we will meet again....
Salim Hassan Naamini alikua ni Muislam... Kwa mktadha huo naomba niombe;...
"Allahuma, ghufil'lahu, wal'hamhu, wasa'knahu, fil'janah" - (Salim Hassan); "Innah Lilah' wa innah Lilah' innah lillah Rajyun"
"Alhamdullih rabil ar'Amin"
Nilimjua kuwa Marehemu ni member wa JF alikuwa analalamika kuwa amepigwa BAN na nilipomuuliza kuwa anatumia ID gani akaniambia hawezi kuniambia, ingawa nilitamani kuijua ID yake kwani nilimwambia ID yangu ya hapa JF lakini akakataa kuniambia ID yake. Kwa hiyo sikuweza kumlazimisha, nilijaribu kutaka kuijua lakini sikuweza kufanikiwa mda mwingi alikuwa ana browse kwenye simu yake. Kwa hiyo nilishindwa kuijua.
ingekua jambo zuri sema mie niko mbali na dar.
Humu ndani wengi tumekutana na tumejuana, sasa kwa wengine sijui. Kuna mtu anaitwa MWANAHAKI amealzwa sana pale Tumaini hospitali. Leo hii amefanyiwa Leo amefanyiwa SKIN GRFT SURGERY hapo KCMS. TUmuweke kwenye maombi na wale wote mlioko MOSHI ebu kamsalimieni kama mnapata muda.
Mwenye kupenda kwenda huko anaweza nitext ili nimpatie namba ya simu. Namba yangu 0655 447788. Tujuliane hali kwenye shida
MUNGU AWABARIKI SANA.
CD