Wana Kagera Njooni Hapa Tutete, Tujadili, Tuzungumze, Tufanye Maamuzi, na Tuchuke Hatua!

Mtazamo wako nimeupenda, inawezekana:
but under this perspective we need also to review our regional administration system as the step ahead to see if we can re-build our status and patriotism.
 
Mkuu huu uzi ni mzuri ila ujue ubinafsi ndo uliotuponza tukafika hapa tulipo.

Naomba huu uzi tutumie lugha ambazo wengi wanazifahamu yaani kiswahili na kiingereza.

Naamini kuna wengi ambao sio Wahaya ambao wanaupenda mkoa wa Kagera sasa tukiendelea kutumia kihaya ndo tutazidi kuwatenga. Tanzania ni yetu sote na tuna wajibu wa kuijenga kwa kushirikiana

Naamini hata hao wa Shinyanga sio wote waliosaidia mabadiliko ni wenyeji wa huko. Mfano mimi ni Mhaya lakini naishi Mtwara, naamini wale makabila mengine ambayo watu wake wanafanya kazi zao huko kagera wanaweza kuwa na michango yenye afya zaidi kuliko watu kama sisi tulio mbali.

Kitu ambacho huwa kinatuponza sie wa kagera ni ujuaji na umimi. Tukirekebisha hayo, naamini tutapiga hatua haraka
 
Ombeni JF waweke Jukwaa la wahaya kwani mnatuboa ni vilugha vyenu. Lugha ya Taifa ni Kiswahili, andikeni kwa kiswahili ili na sisi tuwape mawazo kama huyo mwana jamvi aliyewaambia nyie ni wavivu.

Kweli mko nyuma kimaendeleo kwenye mkoa wenu, inabidi mfanye kazi ya ziada na muwe wamoja. Mnayo nafasi ya kuwa na wasomi wengi na watu wengi wenye nafasi serikalini, sisemi kwamba wawapendelee ila watumie akili zao kwa manufaa ya mkoa wenu pia. Watumie pesa zao kwenye uwekezaji mjini bukoba na si kujenga tu huku dar na miji mingine. Mna ardhi yenye rutuba, samaki, maji ya ziwa na nafasi ya kufanya biashara kwenye nchi jirani.
Msipoangalia, mtatoka kwenye usomi na kuanza kufanya kazi majumbani kwa watu. Wakora waitu.
 
Waitu Mulimu??
Nimefurahi sana kuona kuna watu wanajipanga kutafuta namna ya kukomboa mkoa wetu. Kusema kweli hali ya Mkoa wetu ni mbaya na hapo hujazungumzia maisha ya mtu mmoja mmoja.
Hali halisi ni mbaya sana na ni wakati huu sasa kuachana na dhuruma na woga tuliotiwa na wazee wetu, waoga wa Magamba. Kwa pamoja tujipange kuukomboa mkoa wetu.
M4C lazima itanyanyue kwa pamoja na kuakikisha tunaijenga Kagera mpya. Kwa watakao kuwa na nafasi kesho tunakutana kuanza mipango maridhawa ya kukomboa mkoa wetu.
 
Fimbo ya mbali haiui nyoka. Twende nyumbani tukawaelimishe. 2015, lazima kieleweke. Mi niko mbioni kurudi nikatoe elimu kwa jamii yangu.
 
Asante sana kwa kutuwekea mada mahsusi kwa ustawi wa mkoa wetu pendwa-Kagera. Naomba nichangie hapa:

Kuna tatifi mbalimbali zilikwisha fanyika kuhusiana na tatizo hili. Fuatilia hapa: Reduced cost of tissue culture banana can help control spread of Banana Bacterial Wilt in Great Lakes region na Farmer Capacity Building in Tissue Culture Banana Cultivation labda walakini uko katika uwezo wa mtu wa Morogoro kumfundisha mzaliwa wa Dar es Salaam kuogelea Baharini!

Ericus, asante kwa hiyo link uliyoitoa lakini kama zilivyokuwa tafiti na eventually papers zinazotokana na hizo tafiti unakuta zina mapungufu kuanzia eneo (area) utafiti ulikopafanyika pamoja na wahusika (population0 na jinsi ya kuwachagua.

Mwisho ni repoti itakanayo na utafiti wenyewe. Hiyo lugha iliyotumika katika link hiyo ni too scientific ambayo kwayo uilewe na upate kutumia kinachoelezwa umo unatakiwa either unayo literature ya mambo ya kilimo au una akili sana.

Sasa baba, mama, dada, kaka, babu zetu walioko kule hata kama wamekwenda shule wengi watakuwa ni wa kiwango cha kati. They are not agricultural technicians nor to be professionals to be able to understand those technical jargons let alone to interprete them on practical footing. Nakumbuka dawa fulani ya kuua wadudu kwenye migoma miaka ya mwisho wa 70 na mwanzoni mwa 80 iliyoletwa na wakulima walinza kuitumia short of agricultural technicians guidance na mwisho iliishia kuua naona vimelea rafiki kwenye ustawi wa migomba na migomba illishia kunyauka.

Ni mfano mdogo na hapo sijasema jinsi theodan ilivyooishia kuua watu badala ya vimelea vya mibuni. Sasa kinachohitajika ni wataalamu wa kilimo tena wanaolewa mazingira ya kule waende mashambani wafanye utafiti na area of study iwe kule Kagera na wakipata jibu labda dawa fulani basi waanze with pilot areas of excellence sio Mkoa wote kuwekwa kwenye majaribio.

Dawa ikifanya kazi then majority should be practically be demonstrated how to properly apply. Bila proper scientific guidance itabaki kuwa vioja na umaskini utaongezeka na mwisho hamna mkoa.

Mbunge wangu wa Muleba Kaskazini kila akikumbana na queries from peasants kuhusu suluhisho la ugonjwa amekuwa anatoa suluhisho ambazo ni costly, unscientific and incosistent. Mara ya kwanza alisema mgomaba ulioambukizwa ukatwe toka kwenye shina na vichipukizi vyake, vichimbiwe shimo, vimwagiwe mafuta ya taa na kuchomwa then kufukiwa.

It turned out to be abortive as the problem never healed. Akaja na kongoa na kutupa mbali nyikani (omwirungu) kusikokuwa na migomba lakini akasahau kuwa similar attack ilainzia kwa mihogo, viazi viatmu kabla haijagusa moyo (ndizi).) Juzi kaja na mpya kuwa watu wanunue dawa ya kuondoa madoa (jike) na wanunue bomba na kupiga migomba iliyoshambuliwa. kwanza hiyo dawa gari na haijulikani kama utafiti ulifnywa.

Anyway, Ericus, ni kwamba tunahitaji wataalamu wa kushauri na kukaa mashambani ili waelekeze na kuspport juhudi za wakulima wetu
 
Ndugu,

bakuza, Bigaraone, Chaimaharage, evoddy, Gagnija, Hagga, Jaji, james chapacha, Kagalala, Kaitampunu, kanyagio, Kibera, Lonestriker, Mkomamanga, MPIGA ZEZE, MUGUNDA, naivasha, Ngeleshi, PrN-kazi, Qixima mQiqa, RUBERTS, Rwamarungu, Rweza, sangija, Seneta,mukama talemwa,Speedy, timbilimu, Tukundane, Yakuza,rugumisa,GALIMA,BigTime,Kakalende,PrN-kazi, Alexism+, kilikiliani,kanyagio,BUSHAIJABWE, Libaba, Smarty, Baba Collins,Eddy M, BUBE, Tata, KASHOROBANA na wengine nyote mnaoipendea mema na maendeleo Kagera

Hapo chini ni mabadiliko yanayoendelea kutokea nchini. Yameninyong'onyesha na kunifedhehesha sana nilipojaribu kulinganisha Shinyanga na Kagera.

Nawaomba mje hapa tufanye mjadala mpana utakaoishia katika maamuzi na kuchukuliwa hatua kivitendo juu ya nini kifanyike toka sasa mpaka 2015 ili nasi walau tuweze kuwemo kwenye basi la Mabadiliko na Ukombozi wa Tanganyika
Niwazo zuri sana ambalo hata mimi nililiwaza siku nyingi na nikaanzisha group humu JF ila emyaga ekakanya nikashindwa kuliweka active!Kagera development - JamiiForums | The Home of Great Thinkers Nilitamani kitu kama hicho sasa naona tunaweza kuanzia hapo!!
 
Mkulu ruttashobolwa
asante sana kwa kunitakia nami kutembea kwenye VX. Nasikia sifa ya kwanza kuupata urais lazima upende kuwa rais! Binafsi napenda kubaki mkulima lkn endelevu. Kagera tumesomesha na tunao vijana wazuri tu tatizo hawajitokezi. Waambieni waje tutawaunga mkono. Ata wewe pia njoo utapata nguvu yetu wapenda maendeleo ya Kagera.

Omutwale tukuwe olabasa?
 
Last edited by a moderator:
Ni kweli kuna ujuaji mwingi sana within few na hauwezi kuondolewa hivihivi lazima kuna mzizi wake. Wakati makabila mengine elimu ilikoazia iliwapa unyenyekevu, umoja na ujasiri wa kupambana na maisha kwa mfano mchaga na ujasiriamali naona kwa kiasi kikubwa wanakagera iliwapa kile wanachokiita academic arrogance.

Badala ya kuangalia input na humbleness ya mtu yule aliweza kupiga sana kelele na kujinadi na kile asichokuwa nacho akaonekana wa maana. Kuna nepotism ambayo bado inatatutafuna na Watanzania wanaichanganya na tribal segregation. Si kweli kuna umimi na ubinafsi wa kifamilia kuliko ukabila kwani tayari wanakagera wana tofauti.

Lakini hili si tatizo sana maana linaweza kukemewa na kuisha tatizo is how to convince people whose stomachs and pockets are empty to turn over the new leaf. It's like squaring the circle.

Na ndio mtaji ambao wanasiasa wanautumia kuendelea kuwatumia wananchi kwa faida yao. Maana ukishakuwa na mfuko mtupu hata watoto na vijukuu wataishia kutokusoma au kuishia shule mithili ya zile za kata. Hivyo wakati tunakuwa na mjadala kama huu lazima tuangalie mambo ya msingi kama elimu, ajira hasa ya kilimo.

Sifa kama iliyokuwepo zamani ya kuwa wanataaluma toka Kagera ipo. Tutawapata tena kina Professor Justinian Rweyemamu watoke tena Ihungo? Tutapata tena kina Dr.Kyaruzi, Cardinal Rugambwa, Askofu Kibira na wengine amidts current educational system?
 
.

WATU WENYE NJAA SIO RAHISI KUCHAGUA UPINZANI, WATADAGANYIKA KIRAHISI KWA WALI NA KOFIA. TATIZO LILILO LA MSINGI NI UCHUMI WA KAGERA ULIODUMAA.

KUNAWEZA KUWAPO SBB NYINGI ZA KUENDELEA KUSHUKA KWA UCHUMI KATIKA ENEO HILO (mnawazidi DODOMA na SINGIDA TU) .Mimi naona Uvivu uliokithiri na kutojituma ndio sababu kubwa.Hakuna chakula,migomba haikubali (awali mlizoea kutifua udongo kidogo tu na kuisimika aridhini, JEMBE HAMJUI KUSHIKA, MNANYOFOA MAGUGU SHAMBANI MKIWA MMEKAA,KUSOGEA HATUA NYINGINE MNAJIVUTA).

Wakati wa kulima mahindi na mtama kama zao la chakula umefika. jifunzeni kukamata jembe au mnasubiri matrekta ya kilimo kwanza? Kahawa haina soko tena( mikahawa yenyewe ilikuwa kama miti ya miembe,haifanyiwi chochote mnasubiria msimu tu.Na hakukuwa na jitihada ya kupanda mipya) samaki wanapelekwa nje tu.Kuna wakati nilisikia vanila inakubali sana huko, ila kwa kuwa inahitaji sana matunzo watu wavivu mkashindwa.

Mtu mvivu sio rahisi kupenda au kukubali mabadiliko na hatimaye akawa na mawazo ya kukabili changamoto mpya kama kuhama au kuchagua chama kingine cha siasa, anaona uvivu. mnapenda sana kula bata ndugu.hampendi kazi ngumu.komaeni,pigeni kazi, enzi za ulangila kwishinei.Wavivu kiasi kwamba hadi mambo yenu yaleeeeee ya SHULE yanawashinda siku hizi.

Hapo kaka umenena...yaan uvivu kutojituma na kupenda kuchagua kazi laini ndo imeturudisha nyuma..ebu fikiria mwanamke wa kihaya mwbie hata atembeze ndiz mjin au afanye umachinga hawawezi...kazi ni kujifanya wanachagua kazi na kutojituma kabisa..kazi ni majungu na kutegemea migomba ambayo sa hizi imeharibika..subili itakapo tangazwa mkoa unaongoza kwa njaa! We have to wake up!!
 
"People of the world, unite". Ndg zangu wana Kagera salaam. Nimefurahi kwa michango ya mawazo ni mizuri. Ila nawaombeni hakuna haja ya kulaumu hapa tunatakiwa kuchukua hatua na kuwa na mkakati.

Hatua ni pamoja na hii ya kuanza kujadiliana na kuonesha haja au basi umuhimu wa kuwa na mabadiliko. Mabadiliko haya naamini lazima yaguse nyanja zote vinginevyo tutakuwa tunajidanganya. Issue isiwe mabadiliko ya kisiasa tu, bali kwa kuanzia na mabadiliko ya kisiasa sawa kama Dr. Nkrumah alivyonena, "Seek first the political kingdom and others will be added unto you".

Hivyo tunatakiwa tutafakari jinsi ya kufanya mapinduzi ya kisiasa, kiuchumi, kijamii, kielimu, n.k. Pia, tunatakiwa kuwa na mkakati wa pamoja na mikakati midogo midogo. Haya yote yanawezekana tukiainisha madhaifu, matatizo, fursa na uwezo wetu sisi na watu wetu wa Kagera walio Kagera na kwingineko popote duniani.

Kama ndugu yangu Ta Omutwale ulivyotutambua basi tuendelee kutambuana na kujenga ushirikiano madhubuti. Naamini tukishirikiana tutaweza. Naamini kila mtu anao watu wake anaowasiliana nao na kushauriana nao juu ya mstakhabari wa mkoa wa Kagera. Hivyo shime tuanze sasa kujadili tufanye nini na wala siyo kulaumu au kutoa visingizio vyovyote.

Chamsingi tunahitaji mabadiliko. Sasa tufanyeje? Karibuni kwa tafakari na michango.
 
Wachangiaji wote naomba kuwafahamisha kuwa huu ni mjadala endelevu ambao kikomo chake kitafikiwa kwa kuweka maazimio na kugawana majukumu. Lazima tufanye mambo kitofauti kama hatutaki kupata matokeo yaleyale. Najitolea kuufuatilia mjadala huu na kuandika maazimio. Naomba msaada wenu juu ya timeframe; lini ufungwe na kutangaza maazimio na kugawa majukumu?
 
Omutwale. Tuko pamoja. Niliwahi kuandika ktk sredi moja siku za nyuma kwamba Kagera tusipo changamkia mageuzi,tusimlaumu yeyote tutakapo jikuta pembezoni ya utawala wa nchi.
 
Siku zote mabadiliko yanaanza na mimi na wewe,tukiamua kuwa siriaz bila kurudi nyuma na kutumia mitandao mbalimbali tutaukomboa mkoa wetu,bila ivyo itabaki historia
 
Katule lugaba'katule ekikaka,leo nimechelewa kuingia lkn nimeumia sana kukosa mjadala huu,uchaguzi uliopta nilikuwa nkenge,nilisikitishwa na jinsi jimbo lilivyo kwapuliwa kidhaifu mno!!ninacho waomba tujaribu kufanya utafiti mapema tuone nijinsi gani yakuwapanga vija kabla ya 2015.Nimeona kuna mtandao unaitwa bukoba wadau,jaribu kuufanyia utafiti tuone kama unaweza kutumika kuikomboa kagera.KASSINGE OMUTWALE
 
Kuna ndugu yangu mmoj ameishi Amerika miaka walau isyopungua 10 na nilikutana naye briefly kama sikosei mwaka 2010 na alikuwa na mkakati ambao alitaka kuutekeleza kwa kuanzia vijijini akisema kuwa ukienda mashambani wazee wetu waliweka streets (ebiongorelo).

Akasema kwa hiyo walikuwa so strategic bila kujua and at that material period when most of them had not seen inside the classroom but had a scope to put in place something that has lived.

Hivyo alitaka zile plots ambazo kila familia inamiliki ziwe formalised kwa maana ya registration and then title deeds that could enable them to get loans and use their formalised assets (land) as collatoral security.

Sijui kama alifanikiwa. It was good idea kwa hiyo namwalika kama yumo humu jamvini ashushe nondo au azipeleke kwa Ta Omutwale inaweza kuwa grains of salts n the boiling port. Kama sikosei anatoka Kamachumu, Buzima au Bushaka
 
Ahsante Mkuu Ericus hayo ndio mawazo ya busara, sasa ili tuwe na mkakati mzuri lazima tuwe base, zamani tulikuwa na vyama vya ushirika mahaili pa kutolea mawazo, ushirika yaanai coops zilikufa!!! Kwa hiyo inabidi tuanzishe kitu fulani kama Kagera Development Fund au chama chetu kama SACCOS.

Hicho chama kiwe na wanachama hai na tutafute jinsi ya kukutana ili tuunde aina ya umoja from JF!! Kwa sasa kuna vyama vingi katika sehemu mbali mbali kwa ajili ya malengo fulani kama misiba kusaidiana etc etc!! Na watu wahamasishwe waelewe ukombozi wa Kagera ni wana Kagera wenyewe wachague serikali bora isiyo ya wezi!! Tusiogope kila kitu kina mwanzo, wana JF from Kagera na wale watakao tuunga mkono kwa hili tuanzishwe umoja fulani very strong tuwe comited kwa ajili ya kuboost maendeleo ya mkoa wetu!!! Jamani toeni mawazo tunaanzia wapi?????

Wataalamu wa IT ma web master mnaweze kutengeneza Kagera link au folum ya pekee kwa ajili ya hilo jambo, au mtu ajitolee blog yake itumike kwa kazi hiyo!!!! Mwami Mutwale, Ta Muganyizi na abandi abali interested nimugamba mutai aliekyo????
 
Chadema walituangusha kutosimamia na kuangalia mtu ambae anagombea ubunge anamtazamo gani,wakachukua dj wakamsimamisha agombee ubunge uko nkenge mwisho wa kampeni akaondoa jina akamuachia nafasi Mushamu atambe nkenge peke yake,ila yote ii ni kwasababu tulimpoteza mtu ambae alikuwa mpiganaji Julius Ndyanabo Mungu amuweke pema,viongozi wa chadema geukia uko ISHOZI,ISHUNJU,GERA,BWANJA,KANYIGO,BUYANGO,BUGANDIKA,KYAKA,BUNAZI,KAKUNYU,MUTUKULA,NK

Nimeipenda sana hii, Nakaa na kufikiria, hivi ukijiita msomi alafu hatuoni impact za usomi wako tunaaminije kuwa umeelimika? wana kagera haya ni maajabu na ni aibu kubwa sana!wasomi wa hii nchi walianzia Kilimanjaro na Kagera!na sababu ziko wazi iweje leo Mkoa wa kagera umekwama, sifa za kijinga zinatufanya tubweteke, mimi ni mzaliwa wa Kanyigo, nimeshuhudia utawala wa mbunge Rwegasira, nikamuona Kamara, na sasa ni mshama! Je kuna nini kimefanyika hadi sasa chini ya utawala wa hawa wenzetu? HATA KAJA! DARAJA AMBALO HALIZI KM2 LIMESHINDIKANA, MVUA IKINYESHA INABIDI WATU WA KANYIGO YANI KKIGARAMA, KIKUKWE, NSHUMBA KASHENYE NA KUENDELEA WAPITE ISHOZI THEN WAPANDE MTUMBWI! MATESO GANI HAYA|! KOSA NI KUWEKA VIONGOZI WABOVU, MAHIRI WA KUGAWA KANGA NA KOFIA! TULIPOKOSEA TUNAPAELEWA SASA NI WAKATI WA KUJIREKEBISHA!NI WAKATI WA KUWEKA DAMU CHNAGA ZENYE KULETA HAMASA NA MABADILIKO YA KWELI! UNADHANI ALIYEKUHONGA PESA KAPATA WAPI NA JE ATARUDISHAJE? HUU NI MUDA MUAFAKA WA KUTAFAKARI JINSI YA KUREKEBISHA MKOA WETU NA MJI WETU AMBAO UNAONEKANA KAMA MAKUMBUSHO!
 
Back
Top Bottom