Wana Kagera Njooni Hapa Tutete, Tujadili, Tuzungumze, Tufanye Maamuzi, na Tuchuke Hatua!

Mkuu huu uzi ni mzuri ila ujue ubinafsi ndo uliotuponza tukafika hapa tulipo.
Naomba huu uzi tutumie lugha ambazo wengi wanazifahamu yaani kiswahili na kiingereza.
Naamini kuna wengi ambao sio Wahaya ambao wanaupenda mkoa wa Kagera sasa tukiendelea kutumia kihaya ndo tutazidi kuwatenga. Tanzania ni yetu sote na tuna wajibu wa kuijenga kwa kushirikiana
Naamini hata hao wa Shinyanga sio wote waliosaidia mabadiliko ni wenyeji wa huko. Mfano mimi ni Mhaya lakini naishi Mtwara, naamini wale makabila mengine ambayo watu wake wanafanya kazi zao huko kagera wanaweza kuwa na michango yenye afya zaidi kuliko watu kama sisi tulio mbali.

Kitu ambacho huwa kinatuponza sie wa kagera ni ujuaji na umimi. Tukirekebisha hayo, naamini tutapiga hatua haraka
Ni kweli mkuu umeeleweka vizuri maendeleo ya Kagera si lazima wawe Wahaya peke yao kuchangia hata watu wenye interest hasa vested interest wanaweza kuchangia!!! Kuhusu lugha hata mimi nilijisahau familia yangu ni kubwa na si wote wanaongea kihaya, from my wife my kids and others, ahsante kwa kutufungua. Ubarikiwe!!!

 
Ndugu,

bakuza, Bigaraone, Chaimaharage, evoddy, Gagnija, Hagga, Jaji, james chapacha, Kagalala, Kaitampunu, kanyagio, Kibera, Lonestriker, Mkomamanga, MPIGA ZEZE, MUGUNDA, naivasha, Ngeleshi, PrN-kazi, Qixima mQiqa, RUBERTS, Rwamarungu, Rweza, sangija, Seneta,mukama talemwa,Speedy, timbilimu, Tukundane, Yakuza,rugumisa,GALIMA,BigTime,Kakalende,PrN-kazi, Alexism+, kilikiliani,kanyagio,BUSHAIJABWE, Libaba, Smarty, Baba Collins,Eddy M, BUBE, Tata, KASHOROBANA na wengine nyote mnaoipendea mema na maendeleo Kagera

Hapo chini ni mabadiliko yanayoendelea kutokea nchini. Yameninyong'onyesha na kunifedhehesha sana nilipojaribu kulinganisha Shinyanga na Kagera.

Nawaomba mje hapa tufanye mjadala mpana utakaoishia katika maamuzi na kuchukuliwa hatua kivitendo juu ya nini kifanyike toka sasa mpaka 2015 ili nasi walau tuweze kuwemo kwenye basi la Mabadiliko na Ukombozi wa Tanganyika

Nimeipenda sana hii, Nakaa na kufikiria, hivi ukijiita msomi alafu hatuoni impact za usomi wako tunaaminije kuwa umeelimika? wana kagera haya ni maajabu na ni aibu kubwa sana!wasomi wa hii nchi walianzia Kilimanjaro na Kagera!na sababu ziko wazi iweje leo Mkoa wa kagera umekwama, sifa za kijinga zinatufanya tubweteke, mimi ni mzaliwa wa Kanyigo, nimeshuhudia utawala wa mbunge Rwegasira, nikamuona Kamara, na sasa ni mshama! Je kuna nini kimefanyika hadi sasa chini ya utawala wa hawa wenzetu? HATA KAJA! DARAJA AMBALO HALIZI KM2 LIMESHINDIKANA, MVUA IKINYESHA INABIDI WATU WA KANYIGO YANI KKIGARAMA, KIKUKWE, NSHUMBA KASHENYE NA KUENDELEA WAPITE ISHOZI THEN WAPANDE MTUMBWI! MATESO GANI HAYA|! KOSA NI KUWEKA VIONGOZI WABOVU, MAHIRI WA KUGAWA KANGA NA KOFIA! TULIPOKOSEA TUNAPAELEWA SASA NI WAKATI WA KUJIREKEBISHA!NI WAKATI WA KUWEKA DAMU CHNAGA ZENYE KULETA HAMASA NA MABADILIKO YA KWELI! UNADHANI ALIYEKUHONGA PESA KAPATA WAPI NA JE ATARUDISHAJE? HUU NI MUDA MUAFAKA WA KUTAFAKARI JINSI YA KUREKEBISHA MKOA WETU NA MJI WETU AMBAO UNAONEKANA KAMA MAKUMBUSHO!
 
Nani anaweza kunitegulia sababu inayofumbua mafumbo haya:

Mkoa wa Kegera
Mkoa wa Kilimanjaro
Tunalima migomba
Wanalima migomba
Migomba yetu iko mahututi
Migomba yao ina uhai

Tunalima kahawa
Wanalima kahawa
Bei anayopewa mkulima wa kahawa Kagera imemkatisha tama mpaka ameamua kung’oa mibuni
Bei ya mkulima wa Kilimanjaro imemhasisha kuongeza idadi ya mibuni mipya kila mara
Kahawa ya Kagera imeathiriwa na bei katika “soko la dunia”
Kahawa ya Kilimanjaro imeshamiri kwa bei za mnada wa Moshi



Kwa mawazo yangu nadhani Kagera tumekuwa wajinga na mbumbumbu wa kuelewa, serikali zilizopita zote ziliwekeza saana Mosh yaani Kilimanjalo kuanzia enzi za kina Eiufoo, Cleopha Msuya former PM hadi sasa!! Wakuu wa serikali waliona sisi Kagera hatuna pressure za maendeleo, ukitilia maanani makatibu wakuu wengi wa serikali wizarani walikuwa wahaya sijui waliogopa kupeleka development projects Kagera kulinda ajira zao au walilizika kujijenga pale walipokuwa!!! Hata vyama vyetu vya ushirika watu hawakuchachamaa ili kuondoa wabadhilifu kuweka watu wazuri wenye maono ya maendeleo, chama cha CCM kilishika hatamu ikawa basi matokeo yake ndio hayo!!! Tunahitaji new breed of leaders kwa ajili ya ukombozi wa Kagera yetu, viongozi bogus wanatakiwa kuondolewa, CCM damu wamekwamisha maendeleo ya Mkoa wetu tuupendao!!!

 
Kuna mchangiaji alishauri kuwa tutengeneze framework; ni kweli itatuongoza kujua tunaanzia wapi na tunaishia wapi. Nitajaribu kuomba Regional Profile ya Kagera ili tuiweke hapa itupatie sura halisi ya Mkoa wetu. Na labda huo unaweza kuwa msingi wa kuendesha majadiliano. Tatizo linalozidi kukomaa ni kwamba mijadala ya mitandaoni inaibua mambo mazuri na inatoa suluhisho linaloonekana kuwa sahihi, kisha mambo yote yanaishia kuitwa”mawazo mazuri” huku yakikosa utekelezwaji.

Pili, mnaonaje tukiwaomba viongozi wa vyama vya wanafunzi toka Elimu ya Juu (UDSM, MUHAS, ARDHI, KAIRUKI, DIT, KIU, SAUT, MIU, MZUMBE, TUMAINI, ST. JOHN, MANDELA, na kwingineko) wanaotoka Kagera waje kushiriki nasi toka mwanzo wa mjadala huu hapa? Mwenye mawasiliano nao atuwekee hapa na tutachangia gharama za kupiga simu na kutuma SMS. Hawa ni wadau muhimu sana kuongeza kasi ya mabadiliko ya fikra. Na kama tayari wapo hapa si vibaya wakijitambulisha. Kwenye suala hili tupunguze “usiri wa majina” yetu halisi maana hata aibu zetu hazifichiki! Wachagga wanaziona, wasukuma wanaziona, na tena wanakyusa, wahehe, na wajita imekuwa ndiyo jingle ya kutufanyia utani wenye ukweli. Nawapeni moyo, hakuna haja ya kuendelea kutumia majina bandia


Ahsante Mkuu Ericus hayo ndio mawazo ya busara, sasa ili tuwe na mkakati mzuri lazima tuwe base, zamani tulikuwa na vyama vya ushirika mahaili pa kutolea mawazo, ushirika yaanai coops zilikufa!!! Kwa hiyo inabidi tuanzishe kitu fulani kama Kagera Development Fund au chama chetu kama SACCOS.

Hicho chama kiwe na wanachama hai na tutafute jinsi ya kukutana ili tuunde aina ya umoja from JF!! Kwa sasa kuna vyama vingi katika sehemu mbali mbali kwa ajili ya malengo fulani kama misiba kusaidiana etc etc!! Na watu wahamasishwe waelewe ukombozi wa Kagera ni wana Kagera wenyewe wachague serikali bora isiyo ya wezi!! Tusiogope kila kitu kina mwanzo, wana JF from Kagera na wale watakao tuunga mkono kwa hili tuanzishwe umoja fulani very strong tuwe comited kwa ajili ya kuboost maendeleo ya mkoa wetu!!! Jamani toeni mawazo tunaanzia wapi?????

Wataalamu wa IT ma web master mnaweze kutengeneza Kagera link au folum ya pekee kwa ajili ya hilo jambo, au mtu ajitolee blog yake itumike kwa kazi hiyo!!!! Mwami Mutwale, Ta Muganyizi na abandi abali interested nimugamba mutai aliekyo????
 
Kagera ni mkoa uliosheheni ilmu na una wasomi wengi na wengi walishika vyeo mbalimbali katika Serikali na hata Kimataifa kama UN na taasisi zake. Kilichokosekana na msukumo wa kuwaunganisha kuwa kitu kimoja kuinua uchumi wa Mkoa wenu.

nawatakia kila la kheir kama mumegundua siri hiyo. Mola atawabarik sana.
Wakora.

Lakin napenda kuchukua nafasi hii kuwakaribisha kwenye harusi ya Kijana wangu (Huyu ni yatima nimemlea toka akiwa miaka minne mpaka leo miaka 24) kijana Shumbushi Rweikiza ambaye atafunga ndoa na Bi Dhamira Kokujama Mutunzi. Ndoa itafanyika msikiti mkuu wa Kamachumu, siku ya ijumaa taarih 6th July 2012 baada ya swala ya ijumaa.

Na baadae tafrija fupi ijumaa mosi hapo hapo Kamachumu. Familia yangu (mke na watoto wote) ipo huko kwa maandalizi na mimi inshallah nitatuwa huko taarih 5 July.

Wote nawakaribisha.
 
Katule lugaba'katule ekikaka,leo nimechelewa kuingia lkn nimeumia sana kukosa mjadala huu,uchaguzi uliopta nilikuwa nkenge,nilisikitishwa na jinsi jimbo lilivyo kwapuliwa kidhaifu mno!!ninacho waomba tujaribu kufanya utafiti mapema tuone nijinsi gani yakuwapanga vija kabla ya 2015.Nimeona kuna mtandao unaitwa bukoba wadau,jaribu kuufanyia utafiti tuone kama unaweza kutumika kuikomboa kagera.KASSINGE OMUTWALE
Mkuu James ahasante tafadhari weka hapa huo mtandao wa Bukoba Wadau ili kama ikiwezekana pia utumike kwa malengo yanayoanzishwa!!!
Mukulu Omutwale tafadhari endelea na huu mjadala tuone tutafikia wapi ili tuwe na muafaka mzuri kwenye haya malengo ya kuleta maendeleo Kagera!!!

 
Naunga mkono aliyesema njaa ndio sababu ya ku 'fall in love'na magamba, migomba imekauka bei ya kahawa chini bei ya saamaki chini, ukichanganya na ushamba wa kuchagua kiongozi kwa kufuata u prof wake au utajiri wake,,, elimu haijawakomboa baddo.
 
TAARIFA YA MAENDELEO YA MJADALA: LEO TAREHE 26/06/2012 KUNA MKUTANO WA KIMKAKATI DAR
....ili tuwe na mkakati mzuri lazima tuwe base, zamani tulikuwa na vyama vya ushirika mahaili pa kutolea mawazo, ushirika yaanai coops zilikufa!!! Kwa hiyo inabidi tuanzishe kitu fulani kama Kagera Development Fund au chama chetu kama SACCOS. Hicho chama kiwe na wanachama hai na tutafute jinsi ya kukutana ili tuunde aina ya umoja ........ tuanzishwe umoja fulani very strong tuwe comited kwa ajili ya kuboost maendeleo ya mkoa wetu!!! Jamani toeni mawazo tunaanzia wapi?????

Kulingana na taarifa zinazozidi kumiminika, leo kuna watu makini wanakutana huko Dar kuanza rasmi hii movement ya kuukomboa Mkoa wa Kagera. Leo asubuhi nilipata simu ya mualiko lakini baada ya kuwaambia niko BK wakashindwa kunijulisha saa na mahali wanapokutana. Labda Rweza atusaidie!

..... Kwa pamoja tujipange kuukomboa mkoa wetu.... Kwa watakao kuwa na nafasi kesho tunakutana kuanza mipango maridhawa ya kukomboa mkoa wetu.
 
TAARIFA YA MAENDELEO YA MJADALA: LEO TAREHE 26/06/2012 KUNA MKUTANO WA KIMKAKATI DAR


Kulingana na taarifa zinazozidi kumiminika, leo kuna watu makini wanakutana huko Dar kuanza rasmi hii movement ya kuukomboa Mkoa wa Kagera. Leo asubuhi nilipata simu ya mualiko lakini baada ya kuwaambia niko BK wakashindwa kunijulisha saa na mahali wanapokutana. Labda Rweza atusaidie!

mi niko Dar hiyo taarifa ya kukutana na mahali pa kukutania sijaipata; au kuna watu special ndo wanaanza kukutana kwa maandalizi ya awali?????
 
Kuna mchangiaji alishauri kuwa tutengeneze framework; ni kweli itatuongoza kujua tunaanzia wapi na tunaishia wapi. Nitajaribu kuomba Regional Profile ya Kagera ili tuiweke hapa itupatie sura halisi ya Mkoa wetu. Na labda huo unaweza kuwa msingi wa kuendesha majadiliano. Tatizo linalozidi kukomaa ni kwamba mijadala ya mitandaoni inaibua mambo mazuri na inatoa suluhisho linaloonekana kuwa sahihi, kisha mambo yote yanaishia kuitwa”mawazo mazuri” huku yakikosa utekelezwaji.

Pili, mnaonaje tukiwaomba viongozi wa vyama vya wanafunzi toka Elimu ya Juu (UDSM, MUHAS, ARDHI, KAIRUKI, DIT, KIU, SAUT, MIU, MZUMBE, TUMAINI, ST. JOHN, MANDELA, na kwingineko) wanaotoka Kagera waje kushiriki nasi toka mwanzo wa mjadala huu hapa? Mwenye mawasiliano nao atuwekee hapa na tutachangia gharama za kupiga simu na kutuma SMS. Hawa ni wadau muhimu sana kuongeza kasi ya mabadiliko ya fikra. Na kama tayari wapo hapa si vibaya wakijitambulisha. Kwenye suala hili tupunguze “usiri wa majina” yetu halisi maana hata aibu zetu hazifichiki! Wachagga wanaziona, wasukuma wanaziona, na tena wanakyusa, wahehe, na wajita imekuwa ndiyo jingle ya kutufanyia utani wenye ukweli. Nawapeni moyo, hakuna haja ya kuendelea kutumia majina bandia
Mkuu hilo nalo neno la busara, vijana jitokezeni wenye nia nzuri na Kagera tupate the way forward!!!!!

 
TAARIFA YA MAENDELEO YA MJADALA: LEO TAREHE 26/06/2012 KUNA MKUTANO WA KIMKAKATI DAR


Kulingana na taarifa zinazozidi kumiminika, leo kuna watu makini wanakutana huko Dar kuanza rasmi hii movement ya kuukomboa Mkoa wa Kagera. Leo asubuhi nilipata simu ya mualiko lakini baada ya kuwaambia niko BK wakashindwa kunijulisha saa na mahali wanapokutana. Labda Rweza atusaidie!
Big up bakulu na baada ya mkutano mtujulishe maazimio mliyofikia sote tuweze kuchangia, wengine tuko Arusha na kwingineko!!!

 
Watu wenyewe hao' nshomil'e ndo utakuta mahakinu , majaji, makamishna wa polisi mikoani n.k. serikalini wao wanatumiwa tu lakini ukifika pale mji wao mkuu Bukoba' pako hoi taabani huwezi amini,ujanja wa bure !

Tatizo lako ni kutokufikiria zaidi.Ingawa unachosema ni kweli lakini tatizo ni kubwa zaidi ya unavorahisha mambo.
 
Wakuu tunawategemea mje na updates, wakuu msiwasahau hata kina Mhe Maghufuli ....Au nimekosea Chato sio Kagera???

Mh. Maghufuli aliona Kagera tunakuwa kikwazo kwa kasi yake ya maendeleo akahamishia tarafa yake ya CHATO kwenda mkoa mpya wa Geita na kuipandisha hadhi chato kuwa Makao Makuu ya Mkoa. Huu ndiyo mfano mzuri wa matokeo ya jinsi tulivyochoka mpaka wenye akili wanajitenga na mkoa na bado watu wanaona mambo mswano! Mtumishi Wetu unaanza kutonesha vidonda sasa.
 
Back
Top Bottom