Sajenti
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 3,651
- 412
Nasikitika kuwafahamisha kuwa nimepata msiba leo alfajiri mke wangu kipenzi amenitoka. Kimsingi mazishi yamefanyika leo saa 10 kwenye makaburi ya changanyikeni...wife ameniachia watoto wawili wa kike 11 & 8...msiba uko makongo juu kwa wale wanaotokea mwenge/mlimani city unapanda dalax2 ya makongo juu unateremkia mwisho zinzpoishia dalax2 uliza eneo linaitwa kizota. Kwa wanaotokea ubungo kupitia chuo kikuu panda dalax2 za changanyikeni teremkia kituo cha bondeni ( chuo cha takwimu) then ulizia kitongoji cha kizota. Hata wenye usafiri binafsi utaratibu ni huo huo. Tunafanya hitma ya marehemu leo saa 10 alasiri karibuni tujumuike sote. Namba yangu ni 0765 068886.