Mvaa Tai
JF-Expert Member
- Aug 11, 2009
- 6,159
- 4,443
Habari za asubuhi wana Jamvi, mimi ni mmoja kati ya watu walio omba kuuziwa viwanja vya mradi wa Gezaulole Kigamboni, nilichukua form nane moja ya kwangu nyingine ya mke wangu na hizi zingine za wadogo wangu ambao ni watu wazima na hawana makazi, niliamini tutapata japo viwanja viwili vitatu. Lakini cha ajabu orodha imebandikwa rasmi kinyemela pale Manispaa ya Temeke ikionyesha watu wanao stahili kuuziwa hivyo viwanja, sisi hatuja bahatika hata kiwanja kimoja. Kwa haraka haraka nimegundua ili kupata hivyo viwanja inabidi uwe na bahati sana au uwe na jina kubwa kama ambavyo yanasomeka pale Temeke. Baadhi ya watu waliobahatika kupata hivyo viwanja ni.
1.Khalfani Kikwete amepata haki ya kuuziwa kiwanja cha ujazo wa chini(Kikubwa)
2.H. Ghasia amepata haki ya kuuziwa kiwanja cha ujazo wa chini(Kikubwa)
3.M. Mwandosya amepata haki ya kuuziwa kiwanja ila hawaja-specify aina ya kiwanja anachotaka.
Hawa ni watu wachache tu kati ya orodha ndefu ambayo kutokana na moyo wangu kuumizwa sana sikuendelea kuisoma.
Inaniuma sana kati ya form nane hakuna mwenye sifa za kuuziwa kiwanja na serikali? kwasababu tuliambiwa kiwanja kimoja tutashindanishwa watu watatu. Na kama ushindani ulikuwa mkubwa inakuwaje mtu amepata kuuziwa kiwanja ambacho bado specifications zake zinafanyiwa kazi?
Source: Ubao wa matangazo manispaa ya Temeke
1.Khalfani Kikwete amepata haki ya kuuziwa kiwanja cha ujazo wa chini(Kikubwa)
2.H. Ghasia amepata haki ya kuuziwa kiwanja cha ujazo wa chini(Kikubwa)
3.M. Mwandosya amepata haki ya kuuziwa kiwanja ila hawaja-specify aina ya kiwanja anachotaka.
Hawa ni watu wachache tu kati ya orodha ndefu ambayo kutokana na moyo wangu kuumizwa sana sikuendelea kuisoma.
Inaniuma sana kati ya form nane hakuna mwenye sifa za kuuziwa kiwanja na serikali? kwasababu tuliambiwa kiwanja kimoja tutashindanishwa watu watatu. Na kama ushindani ulikuwa mkubwa inakuwaje mtu amepata kuuziwa kiwanja ambacho bado specifications zake zinafanyiwa kazi?
Source: Ubao wa matangazo manispaa ya Temeke