Katika utafiti nilioufanya kuanzia Julai 31 hadi sasa nimegundua makundi matatu ya walimu waliokataa kuunga mkono mgomo na sababu zao. KUNDI la kwanza ni la walimu walioajiriwa Februari 2012. Hawa wanaogopa kugoma kwa sababu wengi wao bado hawana uzoefu na bado si wanachama wa CWT. KUNDI la pili ni la wale wanaokaribia kustaafu. Hawa wanahofia kupoteza mafao ya kustaafu(pension) endapo serikali itawafukuza waliogoma. KUNDI la tatu ni la wale wanaopandishwa vyeo kiholela. Hawa wanatafuta kupanda madaraja hivyo mishahara ya kuongezeka.