Walimu waliokalia madaftari kwa kunyang'anywa viti wapatiwa viti na meza

Nyendo

JF-Expert Member
Jun 4, 2017
1,194
4,114
Baada ya kuripotiwa kwa taarifa ya walimu wa shule ya msingi Nyansalala iliyopo kata ya Bukondo Halmashauri ya wilaya ya Geita kufanya kazi wakiwa wamekaa chini kwa madai ya kunyang’anywa madawati waliyokuwa wanatumia kama mbadala wa meza na viti Mkuu wa wa wilaya ya Geita Cornel Magembe amefika shuleni hapo na kusema kuwa changamoto iliyokuwepo tayari imetatuliwa na Shule hiyo imepokea viti Nane na meza nane kwaajili ya walimu wa Shule hiyo.

Akizungumza na Kurasa Mkuu wa wilaya ya Geita Cornel Magembe amesema kilichotokea kati ya mkuu wa shule na Afisa mtendaji wa kijiji ni kutoelewana lakini tayari shule hiyo imepokea viti na meza kwaajili ya matumizi ya walimu wa shule hiyo.

“Changamoto iliyotokea nikutoelewana tu siku hiyo iliaminika kuwa viti vilivyokuwa vimetengenezwa kwaajili ya walimu vilikuwa ndo vinaletwa wakati viti vile vinakuja kutoka kwa fundi walimu nao wakaelekezwa kwamba watoe zile meza walizokuwa wanatumia ili wapeleke kwa wanafunzi kwasababu wanafunzi walikuwa na upungufu wa madawati kwaiyo mpaka sasa tunavyozungumza viti na meza vililetwa siku hiyo na walimu wapo wanavitumia” -CORNEL MAGEMBE-Mkuu wa wilaya ya Geita.
 
“Changamoto iliyotokea nikutoelewana tu siku hiyo iliaminika kuwa viti vilivyokuwa vimetengenezwa kwaajili ya walimu vilikuwa ndo vinaletwa wakati viti vile vinakuja kutoka kwa fundi walimu nao wakaelekezwa kwamba watoe zile meza walizokuwa wanatumia ili wapeleke kwa wanafunzi kwasababu wanafunzi walikuwa na upungufu wa madawati kwaiyo mpaka sasa tunavyozungumza viti na meza vililetwa siku hiyo na walimu wapo wanavitumia” -CORNEL MAGEMBE-Mkuu wa wilaya ya Geita.
Mtendaji wa kijiji ndiyo boss wa HoS
 
Baada ya kuripotiwa kwa taarifa ya walimu wa shule ya msingi Nyansalala iliyopo kata ya Bukondo Halmashauri ya wilaya ya Geita kufanya kazi wakiwa wamekaa chini kwa madai ya kunyang’anywa madawati waliyokuwa wanatumia kama mbadala wa meza na viti Mkuu wa wa wilaya ya Geita Cornel Magembe amefika shuleni hapo na kusema kuwa changamoto iliyokuwepo tayari imetatuliwa na Shule hiyo imepokea viti Nane na meza nane kwaajili ya walimu wa Shule hiyo.

Akizungumza na Kurasa Mkuu wa wilaya ya Geita Cornel Magembe amesema kilichotokea kati ya mkuu wa shule na Afisa mtendaji wa kijiji ni kutoelewana lakini tayari shule hiyo imepokea viti na meza kwaajili ya matumizi ya walimu wa shule hiyo.

“Changamoto iliyotokea nikutoelewana tu siku hiyo iliaminika kuwa viti vilivyokuwa vimetengenezwa kwaajili ya walimu vilikuwa ndo vinaletwa wakati viti vile vinakuja kutoka kwa fundi walimu nao wakaelekezwa kwamba watoe zile meza walizokuwa wanatumia ili wapeleke kwa wanafunzi kwasababu wanafunzi walikuwa na upungufu wa madawati kwaiyo mpaka sasa tunavyozungumza viti na meza vililetwa siku hiyo na walimu wapo wanavitumia” -CORNEL MAGEMBE-Mkuu wa wilaya ya Geita.
Siku waliyonyang'anywa madawati mliwapiga picha wamekaa juu ya madaftari, leo mmewapa viti na meza hakuna picha. Huu ni uongo hakuna viti wala meza.
 
Kwa hiyo LIKUD unataka Tanzania hii hata wale tunaojikaza ili watoto wetu waende shule na bus za njano tuwalete huku ambako walimu wanakalia madaftari na vitabu huku watoto wakikaa chini kwenye vumbi?
IMG_20240128_110741.jpg


Acha utani masta tafuta hela
 
Back
Top Bottom