Walimu wa shule za awali na shule za msingi pamoja na wazazi kwa ujumla

Madame S

JF-Expert Member
Mar 4, 2015
17,172
34,311
Nawasalimia

Kuna jambo leo limeniumiza mno moyo na kichwa changu kwa mawazo

Kisa kipo hivi

Leo kwetu huku ni mvua tangu jana usiku, kulipokucha nilimwandaa mwanangu kwenda shule, sio mbali na eneo tunaloishi. Baada ya kuona muda unaenda mtoto harudi ndio nikakumbuka mvua imesababisha nikajiandaa kumfuata hapo shuleni kwao, nilipofika nikakuta wapo maskini na mwalimu wao wanasubiri wazazi waje wawachukue, nikakuta ugomvi mtoto mmoja ambae namjua amemuuma kwa meno mwenzie huku akililia chupa ya maji ya mwanangu. Ni kama mwalimu wao amezizoea vurugu hivo alikuwa ametulia tuli kitini anachat

Nilipoingia na kuukuta ugomvi ule nikaamulia kwa kuwapokonya ile chupa, mtoto alieumwa na mwenzie akawa analia, tukasalimiana na mwalimu pale nikawa nambembeleza mtoto anayelia akinionesha alipoumwa nikamuuliza nani kakuuma akanionesha moyo wangu ulipasuka kwa woga na presha yule mtoto wazazi wake hawako vizuri kiafya namaanisha ni waathirika na inasemekana na mtoto wao huyo pia ameukwaa.

Nilichokifanya nikamuita mwalimu pembeni, nikamuuliza unaijua hali halisi ya huyu mtoto? mwalimu akakataa, nikamuuliza alivyoletwa huyu mtoto mliambiwa chohote kuhusu afya yake pia akakataa ikabidi nimueleze hali halisi.

Walimu mnaofundisha hizi shule za awali jamani muwe makini, tunajua mnachoka na vurugu za hao kina junior na dada zao ila muwe macho masaa yote nimeogopa nawaza ingekuwa mwanangu ameumwa vile japo sijaona kama kamchubua lakini tahadhari ni bora zaidi ingekuaje? na wazazi ni bora ukamuita mwalimu pembeni ukamueleza hali yako ajue namna ya kuishi na huyo mtoto na kuwasaidia wenzie, hiki kitu leo kimenifikirisha sana nimejaribu kuwaza ni shule ngapi watoto wa hivi wapo, alichonambia mwalimu pia ni wazazi hatuwi wazi

Tusaidiane kuwa wazi na kulinda wengine, watoto wana michezo chungu nzima hujui bahati mbaya itatokea upande gani
 
Wazazi wakiathirika haimaanishi mtoto naye kaathirika..kupigana watoto shuleni ni jambo lankawaida kama vifo wodini..Mara my nyingi walimu na manesi wamekuawa wamezoea hizo hali ndo maana wanachukulia easy...Same ata wewe nyumbani siyo kila jambo analofanya mtoto utafeact the same
 
nawasalimia

kuna jambo leo limeniumiza mno moyo na kichwa changu kwa mawazo

kisa kipo hivi

leo kwetu huku ni mvua tangu jana usiku, kulipokucha nilimwandaa mwanangu kwenda shule, sio mbali na eneo tunaloishi. Baada ya kuona muda unaenda mtoto harud ndio nikakumbuka mvua imesababisha nikajiandaa kumfuata hapo shuleni kwao, nilipofika nikakuta wapo maskini na mwalim wao wanasubiri wazazi waje wawachukue, nikakuta ugomvi mtoto mmoja ambae namjua amemuuma kwa meno mwenzie huku akililia chupa ya maji ya mwanangu. Ni kama mwalim wao amezizoea vurugu hivo alikua ametulia tuli kitini anachat

Nilipoingia na kuukuta ugomvi ule nikaamulia kwa kuwapokonya ile chupa, mtoto alieumwa na mwenzie akawa analia, tukasalimian na mwalim pale nikawa nambembeleza mtoto anayelia aknionyesha alipoumwa nikamuuliza nan kakuuma akanionyesha moyo wangu ulipasuka kwa woga na presha yule mtoto wazazi wake hawako vizuri kiafya namaanisha ni waathirika na inasemekana na mtoto wao huyo pia ameukwaa nilichokifanya

nikamuita mwalim pembeni, nikamuuliza unaijua hali halisi ya huyu mtoto? mwalim akakataa, nikamuuliza alivyoletwa huyu mtoto mliambiwa chohote kuhusu afya yake pia akakataa ikabidi nimueleze hali halisi.

Walim mnaofundisha hizi shule za awali jaman muwe makini, tunajua mnachoka na vurugu za hao kina junior na dada zao ila mue macho masaa yote nimeogopa nawaza ingekua mwanangu ameumwa vile japo sjaona kama kamchubua lakini tahadhar n bora zaidi ingekuaje? na wazaz ni bora ukamuita mwalim pembeni ukamueleza hali yako ajue namna ya kuishi na huyo mtoto na kuwasaidia wenzie, hiki kitu leo kimenifikirisha sana nimejaribu kuwaza n shule ngap watoto wahivi wapo, alichonambia mwalim pia n wazaz hatuwi wazi

tusaidiane kua wazi na kulinda wengine, watoto wana michezo chungu nzima hujui bahati mbaya itatokea upande gani
Jambo la msingi sana hili liloliongelea. Bahati mbaya who cares?
 
Wazazi wakiathirika haimaanishi mtoto naye kaathirika..kupigana watoto shuleni ni jambo lankawaida kama vifo wodini..Mara my nyingi walimu na manesi wamekuawa wamezoea hizo hali ndo maana wanachukulia easy...Same ata wewe nyumbani siyo kila jambo analofanya mtoto utafeact the same
mkuu kwa hiki ninachokiandika hapa nina uhakika 95% huyo mtoto hayuko sawa mana hata hao wazaz wao husema wakat mwengine ningekua simfaham hata isingenifikirisha
 
Daah kweli kabisa inahitajika tuwe makini..
Kwa upande wangu mi niko makini sana kuanzia kumsimamia mtoto wakati wowote.

Makosa madogo madogo kama hayo hutokea endapo mwalimu nikishindwa kuwa miliki watoto.

Hii iliwahi nitokea japo haitokuja tokea tena.. mtoto mtundu sana katika kucheza alijigonga akaumia kichwani japo sio kivile.
Ila mzazi wake aliongea kidogo ila alinifundisha kitu "" wakati mtoto wangu anaumia wewe ulikua wapi""

Tangu hapo mi kesi za watoto hazijawahi nisumbua ,
Changamoto nyingine iliyokuja nikuta ni kipindi fulani uliibuka ugonjwa wa vipele daah sasa ishu ikawa wazazi hawaelewi an lawama tuu.
As if hawaelewi kuwa haya mambo ya kuambukiza nikisema nifunge kituo wanagoma daah

Watoto ni wa kuwa nao makini sana na mzazi anapofika lazima atoe information zote za mtoto husika an sio unapokea mtoto kiholela end of day yakija kutokea unaweza pata kesi kubwa sana
 
Daah kweli kabisa inahitajika tuwe makini..
Kwa upande wangu mi niko makini sana kuanzia kumsimamia mtoto wakati wowote.

Makosa madogo madogo kama hayo hutokea endapo mwalimu nikishindwa kuwa miliki watoto.

Hii iliwahi nitokea japo haitokuja tokea tena.. mtoto mtundu sana katika kucheza alijigonga akaumia kichwani japo sio kivile.
Ila mzazi wake aliongea kidogo ila alinifundisha kitu "" wakati mtoto wangu anaumia wewe ulikua wapi""

Tangu hapo mi kesi za watoto hazijawahi nisumbua ,
Changamoto nyingine iliyokuja nikuta ni kipindi fulani uliibuka ugonjwa wa vipele daah sasa ishu ikawa wazazi hawaelewi an lawama tuu.
As if hawaelewi kuwa haya mambo ya kuambukiza nikisema nifunge kituo wanagoma daah

Watoto ni wa kuwa nao makini sana na mzazi anapofika lazima atoe information zote za mtoto husika an sio unapokea mtoto kiholela end of day yakija kutokea unaweza pata kesi kubwa sana
hawa kwenye form ya kujiunga hakuna hata sehem ya kuandika afya ya mwanao ipoje ni kujaza tu details zako na mtoto, walim mna kazi ngumu lakini kua makini pia n jukumu lenu tunasaidiana wewe shule mimi nyumbani
 
walimu wana kazi ngumu sana, yaani wamulie hata ugomvi wa watoto kwa salary ya laki nne, mimi ni mwalimu wa masomo darasani tabia za mtoto ni yeye na mzazi wake
mkuu, wewe ni baba au mama wa mtoto wa mtu, siku moja atakua huyo mtoto tapeleka mwanae shule pengine yakawa haya mtakuja mlaum nani?? mimi sikatai mtoto tabia zake mzaz ndio anahusika kwa namna zote ila akiwa shule ni jukumu lako, sasa kuna watoto wanapigana mpaka kuumizana kutoana dam utasemaje??
 
hawa kwenye form ya kujiunga hakuna hata sehem ya kuandika afya ya mwanao ipoje ni kujaza tu details zako na mtoto, walim mna kazi ngumu lakini kua makini pia n jukumu lenu tunasaidiana wewe shule mimi nyumbani
Ndo hivyo maana mda mwingi mi ndio nakaa mda mrefu na mtoto kuliko mzazi..
 
Kuna watoto ni kama wana mashetani,yaani kuchangamana na wenzao hawawezi dakika mbili mara kamasukuma mwenzake,mara kamuuma,mara anapora vitu vya mwenzake.

Chanzo ni malenzi ya kishenzi ya wazazi wao.
 
Kuna watoto ni kama wana mashetani,yaani kuchangamana na wenzao hawawezi dakika mbili mara kamasukuma mwenzake,mara kamuuma,mara anapora vitu vya mwenzake.

Chanzo ni malenzi ya kishenzi ya wazazi wao.
No, tatizo ni mrundikano darasani. Una madawati 10 -15 una watoto 90! Utafanya nini wawe katika utulivu? Sekondari wanadai kila darasa meza na viti viwe 40/40 ila una students mpaka 70, unawatulizaje?
 
Back
Top Bottom