Walimu wa Parakuyo Kilindi mkoani Tanga wauza Mali zao kujihamisha

Nguva Jike

JF-Expert Member
Jan 22, 2018
856
1,006
Habari za mchana.

Kwa masikitiko makubwa walimu waliohamishwa kwenda katika shule tofauti za wilaya ya Kilindi wameuza vitu vyao vingi Ili wajihamishe wenyewe.

Hali hiyo imejitokeza baada ya jitihada zao za kupewa stahiki zao kushindwa kutekelezwa na mwajiri wao(DED-Kilindi) ambae a pia aliwaahidi kuwapa magari ya halmashauri Ili waweze kuhamisha vitu vyao.

Mpaka kufikia January pamoja na kukumbushia wapewe gari walipewa majibu kuwa mafuta hakuna.Ikumbukwe kuwa walimu wa Parakuyo Kilindi Tanga walihamishwa kutokana na shule hiyo kuwa ya Handeni baada ya mgogoro wa kimipaka kumalizwa.

Walimu hao wamenaswa wakisema Wana msongo wa mawazo huku wengine wakisema wanaidai Halmashauri ya Kilindi madai ya tangu 2016.Inasemekana kuna hatua wanataka kuchukua japo hawakusema ni hatua gani na mpaka Sasa wanaishi madarasani.So sad Kilindi.
 
Habari za mchana.

Kwa masikitiko makubwa walimu waliohamishwa kwenda katika shule tofauti za wilaya ya Kilindi wameuza vitu vyao vingi Ili wajihamishe wenyewe.

Hali hiyo imejitokeza baada ya jitihada zao za kupewa stahiki zao kushindwa kutekelezwa na mwajiri wao(DED-Kilindi) ambae a pia aliwaahidi kuwapa magari ya halmashauri Ili waweze kuhamisha vitu vyao.

Mpaka kufikia January pamoja na kukumbushia wapewe gari walipewa majibu kuwa mafuta hakuna.Ikumbukwe kuwa walimu wa Parakuyo Kilindi Tanga walihamishwa kutokana na shule hiyo kuwa ya Handeni baada ya mgogoro wa kimipaka kumalizwa.

Walimu hao wamenaswa wakisema Wana msongo wa mawazo huku wengine wakisema wanaidai Halmashauri ya Kilindi madai ya tangu 2016.Inasemekana kuna hatua wanataka kuchukua japo hawakusema ni hatua gani.So sad Kilindi.
Kwa hiyo wanachohitaji haswa ni kipi mkuu? Walipwe madai ya tangu 2016 au walipwe fedha za uhamisho?
 
Kwa hiyo wanachohitaji haswa ni kipi mkuu? Walipwe madai ya tangu 2016 au walipwe fedha za uhamisho?
Kilindi wilaya ile haitendi haki rushwa ya kutosha Halmashauri kila mtu wengi wao mungu watu mtu anahamishwa zaidi ya mara kumi Kuna nini hapo?
 
Kwa hiyo wanachohitaji haswa ni kipi mkuu? Walipwe madai ya tangu 2016 au walipwe fedha za uhamisho?
Wawalipe walimu waliohamishwa kwa dharura wa pale Parakuyo kwanini wanawaacha mpaka wanauza mali zao kwa kushindwa kuwalipa hata gari pia wanasema hawana mafuta huu ni ukatili dhidi ya watumishi.
 
Ona dhulma hii mtu anahamishwa ila hapewi kitu ilishanikuta hii ...Lakini uchaguzi na kampeni pesa zinatolewa kwa mda .


Hakika dhulma ni mbaya sana jaalia mtu anasononeka kwa sababu ya ujinga wako ,kupata stahiki ni haki yao kwa nn watu wanakuwa wakatili?
 
Back
Top Bottom