Mtoto Wa Mbale
JF-Expert Member
- May 15, 2011
- 457
- 300
akihutubia mkutano wa hadhara.
Heeeeeh! Mbona watoto wa shule za msingi? Hawa nao ni wapiga kura???
akihutubia mkutano wa hadhara.
Kwa kweli kwa uvumilivu namsifu sana Nape. Sasa sijui hao watoto alikuwa anawahutubia nini.akihutubia mkutano wa hadhara.
Samahani mtoa mada hapa jf hamna wakereketwa ila kuna great thinkers hao wakereketwa wako ccm
Nepi asipo angalia hiki chama kita mfanya awe mwehu kabisa maana naona sasa hivi kama vile anaeigiza lakini anako kwenda ikosiku sasa hawa watoto na kujivua magamba kwao kuna wahusu nini maana watoto wenye hapo walipo wanajaa mbaya kabia hapo walipo wanasubiri hata agawe pipi kama navyofanyaga mwenyekiti wa CCM....akihutubia mkutano wa hadhara.
Mwakyembe Kimya kumbe alikuwa anataka uwaziri shenzi kabisa...Waliitwa wapiganaji ndani ya CCM na wakawa ndio tumaini la CCM katika uvuaji magamba, je imetokea nini ? Mbona hawako Igunga kwenye uwanja wa mapambano na badala yake walioitwa mafisadi ndio wanatamba ? Naomba maoni ya wakereketwa humu ndani wanisaidie kulitatua hili fumbo, imekuaje hadi hawa wapiganaji hatuwasikii tena ?
View attachment 38028
Je wametupa silaha chini au yenyewe ndio magamba na sasa yamevuliwa ?
Lakini hata Lowassa na Chenge anayekijua vizuri Kisukuma hawako kule. Binafsi nakwazwa mno na mtu kufanyiwa kampeni badala ya yeye mwenyewe kufanya. Hii naifananisha na mtu kuchangiwa ili afanye harusi yake mwenyewe. Dalali kafunikwa kabisa na hawa ma-celebrity wa siasa za nchi hii.
Dawa ya mchawi mpe mtoto akulelea, mtoto atakuwa salama, ho wapiganaji uchwara wamezibwa midomo kwa kupewa uwaziri, unaibu na kelele zote kwisha, Ole sendeka na Kilango nao wananyenyekea huenda wakapata chochote , hii inaonyesha wazi kuwa wapiga kelele ndani ya CCM ni njaa tu,uchu wa madaraka hawana lolote.
Tanzania itakombolewa na umma wa watanzania kwa nguvu ya umma,walafi wa madaraka hawatatusaidia lolote.bahati nzuri Mungu humaliza mchezo wote hapahapa duniani na watu wakishuhudia,mfano Libya,aliyewaita wananchi Panya ndo kageuka panya buku sijui anakaa mapangoni kama Saddam. Mwisho wa CCM tutaushuhudia kwa macho yetu wenyewe.
You might think that you have made 'funny' writing but in reality you have made yourself laughable...who doesn't know the significance of this election in Igunga to both Chadema na CCM? Who doesn't know that it is a close call and ccm is using all that it has got to win?? Nzi can't be the representation of the opposition that chadema is giving to CCM in Igunga.CCM ina jeshi kubwa, kwa nn watumie bunduki kumuua nzi ? walio enda igunga wanatosha kuwapakata CDM na kuwafanya watakavyo
Waliitwa wapiganaji ndani ya CCM na wakawa ndio tumaini la CCM katika uvuaji magamba, je imetokea nini ? Mbona hawako Igunga kwenye uwanja wa mapambano na badala yake walioitwa mafisadi ndio wanatamba ? Naomba maoni ya wakereketwa humu ndani wanisaidie kulitatua hili fumbo, imekuaje hadi hawa wapiganaji hatuwasikii tena ?
View attachment 38028
Je wametupa silaha chini au yenyewe ndio magamba na sasa yamevuliwa ?
Acha kutoa utetezi wa kitoto, itakuwaje imani yao ya kisiasa ikawa tofauti na imani ya chama chao na kama unachosema ni kweli huko CCM wanafanya nini ? Huo utakuwa ni ulafi kwa kujali matumbo yao au unafiki kwa kutokuwa na msimamo unaoeleweka, period.Hawa hawakwenda kwa kua itapingana na itikadi yao ya kutaka ccm iwe safi zaidi...yaani ccm kumkumbatia RA pale igunga inapingana na imani yao kisiasa...
Grow up man, uamuzi wa kutokwenda Igunga haukuwa wao na kama kulikuwa na busara yoyote ile ni ya NEC ya CCM iliyowawekea mkwara wasikanyage Igunga wasije wakamkorofisha Rostamu, period. Huo msimamo wa kujifunika blanketi moja na hao unaodai ni mafisadi ni msimamo wa aina gani ?Walichoamua ni uamuzi wa busara kama hujui siasa inaweza kuonekana ni vinginevyo ila ni uamuzi ambao unawafanya wasionekane hawana msimamo au wanapinga msimamo wao wa kisiasa...
Rubbish with a capital R ! Utakuwaje mtaji wao wa kisiasa ndani ya chama - chama kipi, hiki kinachompigia magoti Rostamu ? Ukishakua mshabiki wa CCM hata uwezo wako wa kufikiri ni kama vile umechakachuliwa. Vipi katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama aliyesimama jukwaa moja na Rostamu ? Vipi mweka hazina wa CCM Mwigulu Nchemba ambaye pia ni mratibu wa kampeni kusimama jukwaa moja na Rostamu ? Mkama anadai katumwa na mwenyekiti wa CCM Jakaya Mrisho Kikwete ambaye pia ndiye Raisi ikiwa na maana kwamba amemwakilisha katika kusimama na Rostamu. Labda useme kuwa hao wote niliowataja hawajidhalilishi kisiasa kwa kuwa ufisadi ni jadi yao na kama ni hivyo, Sitta, Mwakyembe, Nape, Sendeka, Kilango na wewe Mharakati mnafanya nini huko chama cha mafisadi ? Naomba jibu.kumbuka mtaji wao kisiasa ndani ya chama na kwa jamii unatokana na hii dhana ya kupinga ufisadi sasa kusimama jukwaa moja na RA wangejidhalilisha kisiasa.
Hawa hawakwenda kwa kua itapingana na itikadi yao ya kutaka ccm iwe safi zaidi...yaani ccm kumkumbatia RA pale igunga inapingana na imani yao kisiasa... Walichoamua ni uamuzi wa busara kama hujui siasa inaweza kuonekana ni vinginevyo ila ni uamuzi ambao unawafanya wasionekane hawana msimamo au wanapinga msimamo wao wa kisiasa...kumbuka mtaji wao kisiasa ndani ya chama na kwa jamii unatokana na hii dhana ya kupinga ufisadi sasa kusimama jukwaa moja na RA wangejidhalilisha kisiasa.
Yaani mkuu ni vichekesho, sijui wapiganaji gani huwa wanauogopa uwanja wa Vita, yaani hii Igunga imewaondolea kabisa japo kale kaheshima kidogo walikojenga kwa baadhi ya watanzania. RA kweli kidume huko CCM hauna sijui Nape, Mwakyembe Sitta, Killango wote wamefyata kimyaaaaaaaaa!!!!