Wale tuliomaliza darasa la 7 mwaka 2000 kurudi nyuma tujikumbushe ilivyokua siku matokeo ya la 7 yanatangazwa

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Mar 29, 2012
10,233
22,316
Wakuu leo nikiwa natafakari mambo mbalimbali ya maisha nikakumbuka maisha ya shule y msingi. Zilikuwa nyakati za furaha ila pia nikahuzunika nilipowakumbuka classmates waliokuwa vizuri sana kitaaluma ila hawakubahatika kusonga mbele na kidato cha kwanza. Zilikuwa nyakati mbaya sana kwa uhaba wa shule za sekondari.

Ni nyakati ambazo kwenye darasa la wanafunzi 100 wanachaguliwa wanafunzi chini ya 10 kuendelea na elimu ya sekondari. Ninaweza sema kwa wakati ule nchi ilikuwa maskini sana hadi raia. Ni wazazi wachache walioweza kumudu gharama za private schools.

Binafsi niliambiwa na mzazi ukifeli utaenda gereji. Siku ya kutangazwa Matokeo ya mtihani wa darasa la saba ilikuwa ni siku adhimu sana iliyoteka hisia za wananchi wote. Hiyo siku kwa wengi ilikuwa kama siku ya hukumu. Jina lako lisipoonekana ubaoni basi inahesabika UMEFELI kitu ambacho kilikuwa kibaya mno. Hakukuwa na mambo ya Internet. Matokeo yalikuwa yanabandikwa kwenye ofisi za halmashauri na CCM. Yaani kuna watakaocheka na kulia.

Nakumbuka hiyo siku matokeo ya mtihani yametoka ya mwaka 1999 tulienda ofisi za manispaa Arusha tukiwa na classmates wengine kibao.

Tumefika tu nikawa wa kwanza kuona jina langu nimechaguliwa kwenda shule flani maarufu hapa nchini. Baadhi ya marafiki nao walikuwa wamechaguliwa ila kuna baadhi hawakuona majina yao. Ikawa furaha kwetu ila huzuni kuu kwa baadhi. Nakumbuka wakati tunarudi nyumbani tulipofika maeneo ya B.O.T ikabidi turudi tena manispaa kucheki upya majina baada ya wenzetu waliokuwa hawajachaguliwa kudhani hawakuangalia vizuri. Ilikuwa kimbembe.

Lakini maisha ni kitendawili. Wale marafiki zetu ambao hawakuchaguliwa kuna baadhi walijiingiza kwenye mambo ya utalii na wana makampuni yao huku wakipiga noti ndefu hatari.

Kuna wengine walipata bahati kwenda private schools na sasa hivi baadhi ni ma-Dr huko UDSM na vyuo vingine. Karibu group langu lote liko vizuri.

Shukrani kwa serikali ya CCM kuleta shule za kata zinazotoa fursa kwa vijana wote kupambania ndoto zao.

Zingekuwepo miaka ile kuna watu wengi sana wangefika mbali kielimu.
 
Nakumbuka siku hii kaka yangu alikuwa anasoma Form VI Azania ile anarudi kitaa na furaha tele, ananiambia, dogo umetokea gazetini top 10 ya jiji la Daslam.

Kesho yake kabla ya kufika ubao wa manispaa pale Taifa, nikawa nawaza na mimi naenda kuwa Aza boy tuu, mara paap Kibaha hii hapa. The rest is history….
 
Nime-like huu Uzi kwa sababu umebeba hisia nyingi sana kwangu.

Kimsingi matokeo yalikuwa yanabandikwa ila waliochaguliwa kwenda sekondari tulikuwa tunafuatilia kwenye magazeti.

Mimi nilifuatilia magazeti yote bila kuona jina
langu.

Nikaja kuona kwenye gazeti la daily news. Limebakia kuwa gazeti langu pendwa hadi leo kwa sababu ya hili tukio.
 
Nime-like huu Uzi kwa sababu umebeba hisia nyingi sana kwangu.

Kimsingi matokeo yalikuwa yanabandikwa ila waliochaguliwa kwenda sekondari tulikuwa tunafuatilia kwenye magazeti.

Mimi nilifuatilia magazeti yote bila kuona jina
langu.

Nikaja kuona kwenye gazeti la daily news. Limebakia kuwa gazeti langu pendwa hadi leo kwa sababu ya hili tukio.
Ilikuwa sio poa enzi hizo. Kuna shule hasa za vijijini zilikuwa hazitoi hata mwanafunzi mmoja
 
Nakumbuka siku hii kaka yangu alikuwa anasoma Form VI Azania ile anarudi kitaa na furaha tele, ananiambia, dogo umetokea gazetini top 10 ya jiji la Daslam.

Kesho yake kabla ya kufika ubao wa manispaa pale Taifa, nikawa nawaza na mimi naenda kuwa Aza boy tuu, mara paap Kibaha hii hapa. The rest is history….
Kwa Dar nadhani Azania ilikuwa maarufu zaidi.
 
Nilimaliza 1998 matokeo tulikua yakitoka tunaenda Bomani Mwanga na ni Alhamisi siku ya soko.Na hapo tumetokea Usangi kwa miguu tunapitia Shighatini,Male huko mnashuka kwa ngondi.
Tukafika pale tukakuta watu kibao wanaangalia yale matoke na sisi ni wadogo inabidi upambane uangalie majina yamebanfikwa kwenye notice board.
Bahati nikaliona Jina Langu. Bi mkubwa akanipa ofa ya wali maharage hotelini na nikaanza kununuliwa vifaa sokoni.
Form Four mwaka 2002 enzi hizo matokeo yanatoka kwenye magazeti.Ina maana kila siku gazeti linatoa shule na inabidi ununue kila siku mpaka uone shule yako.
Nililipata gazeti la Nipashe nikaona nimefaulu na sasa ikawa kusubiria selection.Nazo zinatoka kwenye gazeti kila siku mpaka uone umepata post ama la.
 
Nilimaliza 1998 matokeo tulikua yakitoka tunaenda Bomani Mwanga na ni Alhamisi siku ya soko.Na hapo tumetokea Usangi kwa miguu tunapitia Shighatini,Male huko mnashuka kwa ngondi.
Tukafika pale tukakuta watu kibao wanaangalia yale matoke na sisi ni wadogo inabidi upambane uangalie majina yamebanfikwa kwenye notice board.
Bahati nikaliona Jina Langu. Bi mkubwa akanipa ofa ya wali maharage hotelini na nikaanza kununuliwa vifaa sokoni.
Form Four mwaka 2002 enzi hizo matokeo yanatoka kwenye magazeti.Ina maana kila siku gazeti linatoa shule na inabidi ununue kila siku mpaka uone shule yako.
Nililipata gazeti la Nipashe nikaona nimefaulu na sasa ikawa kusubiria selection.Nazo zinatoka kwenye gazeti kila siku mpaka uone umepata post ama la.
Kumbe tumetoka mbali!
 
Nilimaliza 1998 matokeo tulikua yakitoka tunaenda Bomani Mwanga na ni Alhamisi siku ya soko.Na hapo tumetokea Usangi kwa miguu tunapitia Shighatini,Male huko mnashuka kwa ngondi.
Tukafika pale tukakuta watu kibao wanaangalia yale matoke na sisi ni wadogo inabidi upambane uangalie majina yamebanfikwa kwenye notice board.
Bahati nikaliona Jina Langu. Bi mkubwa akanipa ofa ya wali maharage hotelini na nikaanza kununuliwa vifaa sokoni.
Form Four mwaka 2002 enzi hizo matokeo yanatoka kwenye magazeti.Ina maana kila siku gazeti linatoa shule na inabidi ununue kila siku mpaka uone shule yako.
Nililipata gazeti la Nipashe nikaona nimefaulu na sasa ikawa kusubiria selection.Nazo zinatoka kwenye gazeti kila siku mpaka uone umepata post ama la.
Haha tumetoka mbali sana!
 
Elimu ya 2000 kurudi nyuma ilikuwa tough sana. Yani darasa lenye wanafunzi 45 wanachaguliwa wawili au watatu tu na hapo umekaza ile ile.
Siku hizi shule za CCM, mtu mpaka anamaliza std 7 hata jina lake kulisoma ni shida lakini nae anafaulu.
 
Back
Top Bottom