don-oba
JF-Expert Member
- Dec 8, 2011
- 1,387
- 677
Baada ya kukaa muda mrefu bila boom, sasa kuna taarifa kwamba kuanzia j'moc zoezi la kusaini litaanza. Nikiwa km mwanafunzi na mwajiriwa wa chuo hiki nimesononeshwa sana kwa jinsi uongozi wa chuo na SAUTSO walivyoshiriki kushughulikia hili suala la boom. Jana nimeongea na Daniel Naftel waziri wamikopo UDSM akaniambia suala la kuwahi kupata mkopo inategemeana na ushapu wa chuo husika. Wenyewe wamefungua juzi na tayari wamepata jana. Chuo kinaendeshwa kidikteta kana kwamba wanafunzi wanajawa na woga kudai haki zao. Hakuja jambo lililokera wengi kama kupiga penalty ya laki moja kwa wale waliochelewa kulipa ada mapema. SAUT ina slogan yake " BUILDING THE CITY OF GOD" huyo mungu wanayemzungumzia ni yupi?. Uongozi wa chuo na SAUTSO wameshindwa kushughulikia adha ya wanafunzi wanaoishi hostel za jirani. Wanafunzi wanalipa kuanzia laki 8 hadi mil 1.5 kwa chumba kimoja kwa mwaka! Sawa hii ni biashara huria ila chuo kushirikiana na uongozi wa mkoa wanaweza kukaa meza moja na wamiliki wa hostel kudhibiti hii hali. Pesa za matibabu ni uozo mwingine, kila mwanafunzi ni lazima alipe laki moja. Wengine tuna bima za afya, kuna uwezekano wa kumaliza chuo bila kutibiwa hapo SAUT dispensary na haurudishiwi pesa. Wanafunzi wa SAUT badirikeni muwe km wenzenu wa vyuo vingine nchini. Chuo kikuu ni ma hali ambapo chemichemi ya hekima na fikra pevu huzalishwa. Je sisi tukinyamaza, kule mtaani watafanya nini?. Tuwe wa kwanza kutetea haki na mabadiriko endelevu ktk nchi yetu tukianzia hapa chuoni kwetu. Wakati mwingine binadamu bila kumshtua kutoka usingizini atadamka muda umeishakwenda. Mimi nimepitia vyuo mbalimbali, ndani na nje ya nchi. Hii ni mara yangu ya kwanza kuona wanafunzi hawana ule muamsho wa kichuo kikuu, nadhani naeleweka. Sina nia mbaya katika hili kama wachache wao watakavyofikiria ila nina nia ya kuwaomba wanafunzi wa SAUT kukiweka chuo ktk mstari mnyoofu, hapa tutakuwa tumemsaidia REV DR. CHARLES H. KITIMA. Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki SAUT!.