Walaka wangu kwa wana - saut!.

don-oba

JF-Expert Member
Dec 8, 2011
1,387
677
Baada ya kukaa muda mrefu bila boom, sasa kuna taarifa kwamba kuanzia j'moc zoezi la kusaini litaanza. Nikiwa km mwanafunzi na mwajiriwa wa chuo hiki nimesononeshwa sana kwa jinsi uongozi wa chuo na SAUTSO walivyoshiriki kushughulikia hili suala la boom. Jana nimeongea na Daniel Naftel waziri wamikopo UDSM akaniambia suala la kuwahi kupata mkopo inategemeana na ushapu wa chuo husika. Wenyewe wamefungua juzi na tayari wamepata jana. Chuo kinaendeshwa kidikteta kana kwamba wanafunzi wanajawa na woga kudai haki zao. Hakuja jambo lililokera wengi kama kupiga penalty ya laki moja kwa wale waliochelewa kulipa ada mapema. SAUT ina slogan yake " BUILDING THE CITY OF GOD" huyo mungu wanayemzungumzia ni yupi?. Uongozi wa chuo na SAUTSO wameshindwa kushughulikia adha ya wanafunzi wanaoishi hostel za jirani. Wanafunzi wanalipa kuanzia laki 8 hadi mil 1.5 kwa chumba kimoja kwa mwaka! Sawa hii ni biashara huria ila chuo kushirikiana na uongozi wa mkoa wanaweza kukaa meza moja na wamiliki wa hostel kudhibiti hii hali. Pesa za matibabu ni uozo mwingine, kila mwanafunzi ni lazima alipe laki moja. Wengine tuna bima za afya, kuna uwezekano wa kumaliza chuo bila kutibiwa hapo SAUT dispensary na haurudishiwi pesa. Wanafunzi wa SAUT badirikeni muwe km wenzenu wa vyuo vingine nchini. Chuo kikuu ni ma hali ambapo chemichemi ya hekima na fikra pevu huzalishwa. Je sisi tukinyamaza, kule mtaani watafanya nini?. Tuwe wa kwanza kutetea haki na mabadiriko endelevu ktk nchi yetu tukianzia hapa chuoni kwetu. Wakati mwingine binadamu bila kumshtua kutoka usingizini atadamka muda umeishakwenda. Mimi nimepitia vyuo mbalimbali, ndani na nje ya nchi. Hii ni mara yangu ya kwanza kuona wanafunzi hawana ule muamsho wa kichuo kikuu, nadhani naeleweka. Sina nia mbaya katika hili kama wachache wao watakavyofikiria ila nina nia ya kuwaomba wanafunzi wa SAUT kukiweka chuo ktk mstari mnyoofu, hapa tutakuwa tumemsaidia REV DR. CHARLES H. KITIMA. Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki SAUT!.
 
Yaani wewe ni mwanafunzi wa chuo?!!!!!

Hii hainiingii akilini. Elimu yetu ikoje jamani? Mwanafunzi wa chuo anaandika kiswahili kichefuchefu namna hii!!

Mod nisaidieni mimi sichelewi kuchefuka na waharibifu wa lugha. Huyu ni mara yake ya kwanza kuona wanafunzi hawana mwamsho wa kichuokikuu na mimi ni mara yangu ya kwanza kuona mwanafunzi ameanza darasa la kwanza mpk sasa yupo chuo cha elimu ya juu na hawezi kuandika WARAKA
 
Yaani wewe ni mwanafunzi wa chuo?!!!!!

Hii hainiingii akilini. Elimu yetu ikoje jamani? Mwanafunzi wa chuo anaandika kiswahili kichefuchefu namna hii!!

Mod nisaidieni mimi sichelewi kuchefuka na waharibifu wa lugha. Huyu ni mara yake ya kwanza kuona wanafunzi hawana mwamsho wa kichuokikuu na mimi ni mara yangu ya kwanza kuona mwanafunzi ameanza darasa la kwanza mpk sasa yupo chuo cha elimu ya juu na hawezi kuandika WARAKA

mkuu ni makosa ya kimatamshi tu, yameathiri andiko langu. Si lugha niliyoifanyia mtihani tangu primary. Usikashfu elimu yangu mkuu, kweli unataka tupimane uelewa wangu na wako?.
 
Yaani wewe ni mwanafunzi wa chuo?!!!!!

Hii hainiingii akilini. Elimu yetu ikoje jamani? Mwanafunzi wa chuo anaandika kiswahili kichefuchefu namna hii!!

Mod nisaidieni mimi sichelewi kuchefuka na waharibifu wa lugha. Huyu ni mara yake ya kwanza kuona wanafunzi hawana mwamsho wa kichuokikuu na mimi ni mara yangu ya kwanza kuona mwanafunzi ameanza darasa la kwanza mpk sasa yupo chuo cha elimu ya juu na hawezi kuandika WARAKA

Vp elimu yako mkuu? Kwani kakwambia anasoma shahada ya kiswahili? Mimi chuoni nilifundishwa na mwalimu kutoka Bulgaria alikuwa hajui hata salaamu ya kiswahili.
 
hahah, mie cna shaka na solidarity ya wana saut, ILA "nahc migomo itaanza siku yesu ataporudi".....chuo kimejaa WAOGA tu....Hamna hata mmoja anayetaka kuwa "kondoo wa sadaka" ili kuamsha ile "internal awareness" juu ya haki na wajibu wa kila mwanachuo ya KUDAI HAKI......
NI KWELI tunajua mnalelewa kiseminary..
NI KWELI tunajua mnaongozwa kibabe...
NA NI KWELI tunajua serikali yenu ya wanafunzi imejaa woga kiasi cha kushindwa kuhoja masuala ya msingi...,.
Ni lini mtajifunza mambo toka kwa wenzenu hasa wa UD.!?!!!
NA MTATESEKA SANA MPAKA MKOME..!!!!!!
 
mkuu ni makosa ya kimatamshi tu, yameathiri andiko langu. Si lugha niliyoifanyia mtihani tangu primary. Usikashfu elimu yangu mkuu, kweli unataka tupimane uelewa wangu na wako?.

Sina haja ya kukashifu elimu yako, tayari mwenyewe umeshaikashifu.

Halafu kesho usiwe na majibu ya kuungaunga, matamshi yataathiri vipi uandikaji wako ikiwa unajua unachoandika.

Unataka tupime uelewa wangu kwa kutumia kipimo gani?
 
Vp elimu yako mkuu? Kwani kakwambia anasoma shahada ya kiswahili? Mimi chuoni nilifundishwa na mwalimu kutoka Bulgaria alikuwa hajui hata salaamu ya kiswahili.

One of them. Sikusema asomee kiswahili kukijua, ni lugha yake. Shida ya universities nowadays ni sehemu za kuoneshea mitindo ya nguo na laptop. Huyo mbulgaria angeweza kujifunza kiswahili na kuongea kwa ufasaha ikiwa ana ubongo tofauti na wako.
 
Vp elimu yako mkuu? Kwani kakwambia anasoma shahada ya kiswahili? Mimi chuoni nilifundishwa na mwalimu kutoka Bulgaria alikuwa hajui hata salaamu ya kiswahili.

Kwani hao wenzake anaowashangaa walimwambia wameenda SAUT kusomea migomo?

Elimu yangu ni ya nadharia. Unasemaje...?
 
One of them. Sikusema asomee kiswahili kukijua, ni lugha yake. Shida ya universities nowadays ni sehemu za kuoneshea mitindo ya nguo na laptop. Huyo mbulgaria angeweza kujifunza kiswahili na kuongea kwa ufasaha ikiwa ana ubongo tofauti na wako.

Ndiyo wale wale! UDOM hawasomi wabongo pekee kwa taarifa yako. Vipi `u jump` into conclusion kuwa Kiswahili ni lugha yake? Watu wa aina yenu mnaboa sana, badala ya kujadili mada mnajifanya kukosoa lugha. ******** wakubwa!
 
One of them. Sikusema asomee kiswahili kukijua, ni lugha yake. Shida ya universities nowadays ni sehemu za kuoneshea mitindo ya nguo na laptop. Huyo mbulgaria angeweza kujifunza kiswahili na kuongea kwa ufasaha ikiwa ana ubongo tofauti na wako.

Mkuu mbona una wivu hivyo, kisa umeshndwa kuvaa vizuri na kununua laptop ndio imekua nongwa pole sana, jipange na wewe ununue laptop na uvae vizuri
 
Sina haja ya kukashifu elimu yako, tayari mwenyewe umeshaikashifu.

Halafu kesho usiwe na majibu ya kuungaunga, matamshi yataathiri vipi uandikaji wako ikiwa unajua unachoandika.

Unataka tupime uelewa wangu kwa kutumia kipimo gani?
Mwalimu wangu alinifundisha hivi "the most profound statements are often said in SILENCE".
 
Back
Top Bottom