Wakuu wapya wa wilaya kusaidia kukabiliana na nguvu ya CDM nchini-Dk Benson Bana

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu Dar es Salaam, Dk Benson Bana amesema uteuzi wa wakuu wa wilaya umelenga kuiimarisha CCM kutokana na vijana kupewa nafasi zaidi.

Alisema hizo ni dalili kwamba CCM wameona nguvu kubwa ya upinzani na sasa wameanza kujiimarisha kwa kuwatumia vijana na wakuu hao wa wilaya jambo ambalo ni jema sana kwa CCM.

“Wamehofia kuwa wanaweza kwenda Chadema ndio maana wameamua kuwapa nafasi vijana, hiyo ni changamoto ambayo wameifanyia kazi” alisema Dk Bana.

Source:Mwananchi Ijumaa
 
Ushenzi type huu, kwa hiyo kwa akili zake ni kwamba vijana woooooote walioko CCM wamepewa nafasi hizo na kwa hiyo nchi nzima hakuna atakayehama? Wapo maelfu ambao hawajachaguliwa ambao hata kesho wanaweza wakahama.
Foolish remarks from a foolish mind.
 
Amethibitisha kuwa ukuu wa wilaya ni nafasi ya kupeana wana ccm kwenda kueneza sera na ufisadi wa chama chao kwa gharama za kodi zetu. Mzee Warioba harakisha mchakato wa kukusanya maoni ya katiba mpya ili tuifutilie mbali hii nafasi. Kumbe ndio maana akina Kilango walikomalia wakuu wa wilaya kusimamia zoezi la kukusanya maoni kwa kuwa ni makada wao. Nchi haitakalika kama watataka kuchakachua katiba.
 
Tusubiri tutaona kama kuna jipya maana hao wakuu wa wilaya ni kama wafanyakazi hewa kwani hawana kazi ya kufanya mbele ya jamii.
 
Nchi hii vyeo vimekua kama pipi. Watu wanapeana tuuu.

Binafsi nimesha post thread nyingi kupinga hiki cheo cha ukuu wa wilaya, hata kabla ya hii list mpya kutoka..

Kwenye katiba mpya tutoe haya madaraka ya kishkaji. Tanzania tuna_waste hela nyingi kuwalipa mishahara na malupulupu watu ambao hata leo hii ukiwatoa, hawana faida yoyote kwa maslahi ya nchi. wapo pale kufanikisha malengo ya wanasiasa.

Wakuu wa wilaya ni viongozi wa CCM, kwa nini wasilipwe mshahara na utawala wa CCM???? Hizo hela zinazotumika kuwalipa mishahara, tungekuwa na fly overs kila kona ya nchi hii.

Tanzania tuna wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, meya wa halmashauri na wa jiji, mkurugenzi wa manispaa na wa jiji n.k. Yani vyeo kibao, lakini wanafanya same work.

Hii system tumeenda nayo kwa miaka 50 tumeshindwa sasa. Ebu tuwe kama China au marekani. Tupunguze idadi ya mikoa iwe ndogo. Afu wakuu wa mikoa wachaguliwe na wananchi. Hawa wakuu wa mikoa wawe na madaraka ya mikoa yao. Kuweka vipaumbele na mikakati..
Sio kusubiri waziri anayeishi Dar kuja kupanga maendeleo ya mkoa. Mkoa wenyewe uwe na sera zake without interfere from center government.
 
huyu jamaa naye anajipendekeza labda iko siku atateuliwa mbunge viti maalum apigwe na uwaziri. Jamaa huyu kaanzia s/msingi hadi university cha ajabu haonyeshi kipaji bali kupayukapayuka tu senseless aka trivial issues. Atakoma na vile kale ka mradi ka RIDET kalikomaa baada ya wafadhili kushitukia hela yao kukusanya maoni ya sisiem wanapendwa aslimia ngapi na watashinda ngapi, kwishini. Ukiwa msomi kama huyu inabidi tumbo li lilokuzaa liwe declared a lost one. Anaboa hata hizo media zinazotafuta opinion toka kwake zijiangalie credibility zao
 
Amethibitisha kuwa ukuu wa wilaya ni nafasi ya kupeana wana ccm kwenda kueneza sera na ufisadi wa chama chao kwa gharama za kodi zetu. Mzee Warioba harakisha mchakato wa kukusanya maoni ya katiba mpya ili tuifutilie mbali hii nafasi. Kumbe ndio maana akina Kilango walikomalia wakuu wa wilaya kusimamia zoezi la kukusanya maoni kwa kuwa ni makada wao. Nchi haitakalika kama watataka kuchakachua katiba.

sure kabisa, naunga mkono hoja 100%.
 
Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu Dar es Salaam, Dk Benson Bana amesema uteuzi wa wakuu wa wilaya umelenga kuiimarisha CCM kutokana na vijana kupewa nafasi zaidi.

Alisema hizo ni dalili kwamba CCM wameona nguvu kubwa ya upinzani na sasa wameanza kujiimarisha kwa kuwatumia vijana na wakuu hao wa wilaya jambo ambalo ni jema sana kwa CCM.

"Wamehofia kuwa wanaweza kwenda Chadema ndio maana wameamua kuwapa nafasi vijana, hiyo ni changamoto ambayo wameifanyia kazi" alisema Dk Bana.

Source:Mwananchi Ijumaa

Mkuu wa Wilaya analipwa mshahara na serikali kuu; anapewa gari, posho na dereva kutoka serikalini kwenda kukiimarisha chama tawala!
 
kumbe haya majamaa yapo kwa maslahi ya sisiemu! kwa mantiki hii itabidi walipwe mishahara na chama na sio serikali! kwanza hakuna faida yoyote ya uwepo wa MaDC! ni wezi tu!
Bana kaa ukitambua hii sio tz tunayoitaka sisi! 2015 tutakuonyesha!!!
 
Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu Dar es Salaam, Dk Benson Bana amesema uteuzi wa wakuu wa wilaya umelenga kuiimarisha CCM kutokana na vijana kupewa nafasi zaidi.

Alisema hizo ni dalili kwamba CCM wameona nguvu kubwa ya upinzani na sasa wameanza kujiimarisha kwa kuwatumia vijana na wakuu hao wa wilaya jambo ambalo ni jema sana kwa CCM.

"Wamehofia kuwa wanaweza kwenda Chadema ndio maana wameamua kuwapa nafasi vijana, hiyo ni changamoto ambayo wameifanyia kazi" alisema Dk Bana.

Source:Mwananchi Ijumaa

Hii ndo habari yote???? Weka yote mkuu tuisome na sisi maana line spacing and understanding are sometimes interlaced
 
Vijana gani? Hao ambao walishakuwa wabunge, manaibu waziri na makada wa muda mrefu! Unapokuwa Dr jiangalie unasema nini. Tena wananiudhi waandishi wa habari maana ni kama vile wameelezwa wamhoji yeye! Kila kitu Dr Bana as if he is so authoritative!
 
Msomi mjinga huyo. Kumbe unaweza kusoma na ukabaki kuwa mjinga? Niliwahi kumsikiliza kwenye kipima joto siku moja haki ya nani mzee hana uelewa kabisa. Naomba niandaliwe mdahalo na huyu msomi uchwara nimtoe knock out! Niwape pole walisomeshwa na huyu mchumia tumbo! Deus Kibamba kama ulifundishwa na huyu pole sana!! Hivi hahitaji ushauri nasaha huyu?!
 
Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu Dar es Salaam, Dk Benson Bana amesema uteuzi wa wakuu wa wilaya umelenga kuiimarisha CCM kutokana na vijana kupewa nafasi zaidi.

Alisema hizo ni dalili kwamba CCM wameona nguvu kubwa ya upinzani na sasa wameanza kujiimarisha kwa kuwatumia vijana na wakuu hao wa wilaya jambo ambalo ni jema sana kwa CCM.

“Wamehofia kuwa wanaweza kwenda Chadema ndio maana wameamua kuwapa nafasi vijana, hiyo ni changamoto ambayo wameifanyia kazi” alisema Dk Bana.

Source:Mwananchi Ijumaa

Huyu Dk Bana anawatia aibu waadhiri wenzake,hizi ni akili na mawazo ya watu wazima wa vijiweni waliokosa elimu kabisa,hivi yeye anafikiria Watanzania wanafuata upepo kwa kua chama fulani kina viongozi vijana basi ngoja twende huko?sasa kiongozi kijana kama Nepi ana tija gani kwa maendeleo ya Mtanzania?au kubwabwaja kusiko na tija(propaganda) nako kuna badili maisha ya Mtanzania?C.C.M imechokwa kwa kua imeshindwa kuleta maendeleo kwa Watanzania,si kua eti kwa kua wana viongozi vijana au wazee,hayo ni mawazo ya kilimbukeni!ndio maana Watanzania wengi waliofunguka kiakili wameamua kupata mbadala wa c.c.m
 
Huyu Bana ni mshauri na rafiki mkubwa wa JK kwa hiyo huu ndiyo ushauri aliompa kilaza mwenzake jinsi ya kutumia kodi zetu kukiokoa chama chao cha kifisadi. Sawa tumekusikia kilaza Bana na uhuni wako. Lakini kama Mungu aishivyo kamwe CCM haitaepuka hasira za walalahoi wa nchi hii, wao wana pesa na dola sisi tuna Mungu.
 
Sidhani kama huyu dkt. bana ana upeo wa kueleweka. ipo cku...

Ulitarajia nini kwa Bana zaidi ya kujikomba kwa wakubwa? Ukuu wa wilaya ni mzigo kwa Taifa tunapaswa kuufuta kwenye katiba mpya DAS na Mkurugenzi wanatosha kabisa kwenye uwajibikaji wa kazi za wilaya kila siku.
 
Back
Top Bottom