Wakongwe: Uliangalia wapi Fainali ya Kombe la Dunia 1994 kati ya Brazil VS Italia

ulimwengu usio na stress
Ulimwengu usio na stress na usio na hizi raha za dunia. Ukaamua kuja kupata raha na stress, huwa haziachani, endless circle.
Jambo la muhimu wewe zingatia raha, stress zipe ''airtime'' ndogo na ukubali kuwa ni sehemu ya maisha.
Na zile stress za kujitakia, hizo ziepuka pambana na zile za lazima tu ili upime ''strain power'' yako.
 
Wakongwe habari!
Nimepata kumbukumbu za Fainali za Kombe la Dunia mwaka 1994, wakati huo nilikuwa nipo shule ya Msingi.
Mechi za mashindano haya nilizingalia Jet Club (ilikuwa ndani ya eneo la Uwanja wa ndege wa Julius Nyerere International Airport wakati ule ulijulikana kama Uwanja wa ndege wa Dar es Salaam - Dar es Salaam International Airport.
Watu wengi waliokuwa wakiishi Kipawa na Kiwalani hapa ndio eneo la kwenda kuangalia mpira hasa kwa wale ambao walikuwa na ndugu ama marafiki wanaofanya kazi uwanja wa ndege.
Miaka ile uwanja wa ndege haukuwa na uzio wa ukuta kama ilivyo sasa.
Fainali ilipigwa Rose Bowl, katika jiji la Pasadena, California
Mechi ilichezwa kwa dakika 120 mpaka kwenye mikwaju ya penati. Brazil ikishinda kwa 3 na Italia kupata penati 2


Uliangalia mechi ya fainali ukiwa wapi?
Magomeni kwa marehemu sheikh Yahaya
 
Ulimwengu usio na stress na usio na hizi raha za dunia. Ukaamua kuja kupata raha na stress, huwa haziachani, endless circle.
Jambo la muhimu wewe zingatia raha, stress zipe ''airtime'' ndogo na ukubali kuwa ni sehemu ya maisha.
Na zile stress za kujitakia, hizo ziepuka pambana na zile za lazima tu ili upime ''strain power'' yako.
Nimekuelewa mkubwa🙏
 
Niliangalia kwenye Kibanda-Umiza kwa Binamu yangu Deo Matengelele Visiga Kibaha. Kulikuwa na Mzee anakuja na tv na antena yake na kuonyesha mpira pale kupitia ITV.

Mashindano yale kiujumla yalikuwa bora hata kwa Cameroon ya mkongwe wa miaka 42 Roger Milla. Kulikuwa na bingwa wa kufunga magoli ya kichwa...mtu mweusi mmoja wa Sweden akiitwa Darlin.

Vya kale ni dhahabu kwakweli...
 
Niliangalia kwenye Kibanda-Umiza kwa Binamu yangu Deo Matengelele Visiga Kibaha. Kulikuwa na Mzee anakuja na tv na antena yake na kuonyesha mpira pale kupitia ITV.

Mashindano yale kiujumla yalikuwa bora hata kwa Cameroon ya mkongwe wa miaka 42 Roger Milla. Kulikuwa na bingwa wa kufunga magoli ya kichwa...mtu mweusi mmoja wa Sweden akiitwa Darlin.

Vya kale ni dhahabu kwakweli...
Yeah Martin Dahlin pande la mtu hivi.
 
Wakongwe habari!
Nimepata kumbukumbu za Fainali za Kombe la Dunia mwaka 1994, wakati huo nilikuwa nipo shule ya Msingi.
Mechi za mashindano haya nilizingalia Jet Club (ilikuwa ndani ya eneo la Uwanja wa ndege wa Julius Nyerere International Airport wakati ule ulijulikana kama Uwanja wa ndege wa Dar es Salaam - Dar es Salaam International Airport.
Watu wengi waliokuwa wakiishi Kipawa na Kiwalani hapa ndio eneo la kwenda kuangalia mpira hasa kwa wale ambao walikuwa na ndugu ama marafiki wanaofanya kazi uwanja wa ndege.
Miaka ile uwanja wa ndege haukuwa na uzio wa ukuta kama ilivyo sasa.
Fainali ilipigwa Rose Bowl, katika jiji la Pasadena, California
Mechi ilichezwa kwa dakika 120 mpaka kwenye mikwaju ya penati. Brazil ikishinda kwa 3 na Italia kupata penati 2


Uliangalia mechi ya fainali ukiwa wapi?
niliangalia kwa jirani kituo itv, nlikuwa form 5
 
Back
Top Bottom