Wakongwe habari!
Nimepata kumbukumbu za Fainali za Kombe la Dunia mwaka 1994, wakati huo nilikuwa nipo shule ya Msingi.
Mechi za mashindano haya nilizingalia Jet Club (ilikuwa ndani ya eneo la Uwanja wa ndege wa Julius Nyerere International Airport wakati ule ulijulikana kama Uwanja wa ndege wa Dar es Salaam - Dar es Salaam International Airport.
Watu wengi waliokuwa wakiishi Kipawa na Kiwalani hapa ndio eneo la kwenda kuangalia mpira hasa kwa wale ambao walikuwa na ndugu ama marafiki wanaofanya kazi uwanja wa ndege.
Miaka ile uwanja wa ndege haukuwa na uzio wa ukuta kama ilivyo sasa.
Fainali ilipigwa Rose Bowl, katika jiji la Pasadena, California
Mechi ilichezwa kwa dakika 120 mpaka kwenye mikwaju ya penati. Brazil ikishinda kwa 3 na Italia kupata penati 2
Uliangalia mechi ya fainali ukiwa wapi?
Nimepata kumbukumbu za Fainali za Kombe la Dunia mwaka 1994, wakati huo nilikuwa nipo shule ya Msingi.
Mechi za mashindano haya nilizingalia Jet Club (ilikuwa ndani ya eneo la Uwanja wa ndege wa Julius Nyerere International Airport wakati ule ulijulikana kama Uwanja wa ndege wa Dar es Salaam - Dar es Salaam International Airport.
Watu wengi waliokuwa wakiishi Kipawa na Kiwalani hapa ndio eneo la kwenda kuangalia mpira hasa kwa wale ambao walikuwa na ndugu ama marafiki wanaofanya kazi uwanja wa ndege.
Miaka ile uwanja wa ndege haukuwa na uzio wa ukuta kama ilivyo sasa.
Fainali ilipigwa Rose Bowl, katika jiji la Pasadena, California
Mechi ilichezwa kwa dakika 120 mpaka kwenye mikwaju ya penati. Brazil ikishinda kwa 3 na Italia kupata penati 2
Uliangalia mechi ya fainali ukiwa wapi?