Wake zetu na Ma-house girls, Kulikoni?

Wana-jf sina uhakika kama hili lilishawahi kuzungumzwa hapa au la. Lakini nimeona si vibaya tukalijadili na kuchangia mawazo. Ndugu yangu mmoja hakumaliza wikiendi yake vizuri jana. Kisa ni kuwa mke wake amechachamaa anataka house girl aondoke haraka. Kwa maelezo ya huyo ndugu yangu ni kuwa jumamosi ya juzi binti wa kazi aliomba ruhusa kwa mother house kwenda kusuka nywele tangu alipoondoka saa 4 asubuhi akarudi saa 11 jioni. Mother house alipomuuliza binti kulikoni kachelewa vile akadai kuwa msusi alikuwa na kazi nyingi na wateja wa kusuka walikuwa wengi so alilazimika kusubiri. Mother house hataki anasema binti ameshakuwa na kiburi so akiondoka anarudi muda anaotaka. Jamaa amejaribu kumsihi mkewe amsamehe huyo binti kwa kuwa kwanza hana uhakika wa kupata h/girl mwingine kwa haraka na ukizingatia wana watoto wadogo wa kati ya miaka 5 na 2. Mother house amepamba moto kwa nini jamaa anapinga binti kuondolewa au yeye ndio anayempa kiburi may be kashamuonja so kanogewa hataki aondoke. Kwa kweli jamaa kila akifikiria busara ya kumfukuza binti ukizingatia yeye na mkewe wote ni wafanyakazi haelewei kilichompata mkewe. Na kibaya zaidi mother house kampigia simu mpaka mama yake mzazi ( mama wa mother house) kuwa yeye muda wowote atarudi kwao kwa kuwa jamaa anapinga binti wa kazi kuondolewa kwa kuwa eti huenda anampenda sana h/girl kuliko kusikiliza ushauri wa mkewe. Ndani ya nyumba hakuna amani kisa msichana wa kazi.. Jamani hii vipi? FL, Nyamayao, Pretty na wadada/wamama wengine ndivyo mlivyo au??
Observation zangu kuhusu hilo ni kuwa
1. Kina mama wengi hasa wanaojiweza kwa kisingizio cha uchovu wa kazi humuachia kazi karibu zote nyumbani na wanasahau kuwa hawa ma house maid ni binadamu na wanahitaji kupumzika na kusocialize hivyo kazi zao karibu wengi ni masaa 18 kwa siku
2. Kina mama humuachia hata shughuli za chumbani.
3. Mara nyingi kwenye ndoa hasa kwa zile zimedumu muda na mama akiwa na uwezo basi hufanya/husema mambo ambayo yanamhusu mume ambayo ni negative mbele ya house girl
Tatizo linakuja unapo appreciate [hata kama hakuna mahusiano ya kimapenzi] na kumsifu au kumtetea mbele ya mama kasheshe huanza [mama hutambua inadequacy yake lakini hapendi kukubali]. Wakati mwingine kina mama bila kujua wanawafanya waume zao watembee na hawa wasaidizi [mwanamume ingawa tuna musuli lakini ni viume dhaifu sana].
Siku moja kwa utani niliwahi kumuuliza memsap 'sasa huyu mfanyakazi ananipikia, ananifulia,anatandika kitanda ninacho lala, anatunza watoto pamoja na nyumba Sasa wewe mpenz unafanya nini??? jee huoni kuwa huyu house girl ananitunza kuliko inavyopasa?? Eeh bwana majibu aliyonipa hayafai kuyaeleza hapa na huyo mfanyakazi aliachishwa kazi baada ya muda tuu Lakini uzuri ni kwamba ingawa ilikuwa utani lakini aliichukulia kama wake up call na hivi sasa ingawa tuna mfanyakazi lakini naye anachacharika hapo nyumbani kiasi kwamba week ends inabidi nimsaidie baadhi ya shughuli.
 
Jamani huyu house girl alipewa adhabu kali mno!!,just tu kuchelewa ndio anakosa kazi?,just imagine hata sie maofisini tungekuwa tunachelewa tunatimuliwa kazi ingekuaje?,twende mbele turudi nyuma,huyu mtoto mpaka kuwa kwako anafanya kazi ni shida/matatizo ndio yanamfanya awe hapo,sasa kumfukuza kisa kachelewa tunakuwa somehow hatujamtendea haki!!!!
 
Jamani huyu house girl alipewa adhabu kali mno!!,just tu kuchelewa ndio anakosa kazi?,just imagine hata sie maofisini tungekuwa tunachelewa tunatimuliwa kazi ingekuaje?,twende mbele turudi nyuma,huyu mtoto mpaka kuwa kwako anafanya kazi ni shida/matatizo ndio yanamfanya awe hapo,sasa kumfukuza kisa kachelewa tunakuwa somehow hatujamtendea haki!!!!

Hapo inaonekana si bure kuna kibifu kilikuwa kishaanza kitambo tu, haiwezekani mama house apandishe kwa issue moja tu.

Waswahili wanasema kosa moja haliachishi mke.
 
Jamani huyu house girl alipewa adhabu kali mno!!,just tu kuchelewa ndio anakosa kazi?,just imagine hata sie maofisini tungekuwa tunachelewa tunatimuliwa kazi ingekuaje?,twende mbele turudi nyuma,huyu mtoto mpaka kuwa kwako anafanya kazi ni shida/matatizo ndio yanamfanya awe hapo,sasa kumfukuza kisa kachelewa tunakuwa somehow hatujamtendea haki!!!!


Thanks Sugar...you have read my mind kwa kweli! That and over reaction.

Na mi nadhani pia sualala housegal kumwachia mama peke yake haifai kwa sababu kwanza HG ni binadamu kama wengine na anastahili heshima kwa kiasi chake.

Sasa kuna ubaya gani kama mimi baba mwenye nyumba nikatoa mawazo yangu hasa kwa mtu anayeshinda na watoto wangu na to be honest anayewajua kuliko hata mimi? nimwache afukuzwe eti nitaonekana nakula mzigo il hali sio kweli? ku wapi kujiamini kwetu?
 
........Huyo mama ana lake jambo, msichana kuchelewa kusuka sio sababu ya yeye kumfukuza kazi. Kuna uwezekano amehisi kitu kati ya mumewe na huyo binti wa kazi, hivyo kuchelewa imekuwa sababu tu.
Kama vp mwambie atafute house boy awe mlezi wa watoto na usafi ndani ya nyumba.
 
Jamani hii issue ya hgirls na motherhouse ina vipengele vingi. Kuna wengine ni wazuri na wasikivu, lakini wengi wanaotoka huko vijijini wakifika mijini wanajiona wamefika. Huwa hawapendelei tena kurudi huko kwa vile husuka mbinu za ku survive.

Na nyinyi akina fatherhouse mukiona amependeza tu hamuwachi kum'Mahita' (unakumbuka kesi ya Mahita na yule house girl?) ndio maana mukitoa comments za sifa tu kuna kengele ya tahadhari huwa inalia.
 
Thanks Sugar...you have read my mind kwa kweli! That and over reaction.

Na mi nadhani pia sualala housegal kumwachia mama peke yake haifai kwa sababu kwanza HG ni binadamu kama wengine na anastahili heshima kwa kiasi chake.

Sasa kuna ubaya gani kama mimi baba mwenye nyumba nikatoa mawazo yangu hasa kwa mtu anayeshinda na watoto wangu na to be honest anayewajua kuliko hata mimi? nimwache afukuzwe eti nitaonekana nakula mzigo il hali sio kweli? ku wapi kujiamini kwetu?

Naungana na wewe mkuu.
Binafsi naona kama wanawake wanakuwa na mtazamo hasi juu ya H/G ambazo hazistahili kuwepo. Nawaona HG kama wafanyakazi wengine wanavyostahili staha. tumesikia HG wakinyanyaswa kuanzia pengine mshahara, socialization na hata mambo mengine mengi tu. mfano kutengwa kula na wanafamilia wengine, wakati huo huo ndo wao wanaandaa hivyo vyakula!!!
HG nao wanahitaji mazingira mazuri ya kazi na pia ni matatizo yanawafanya waje kuhangaika kufanya kazi ngumu wanazozifanya kwa ujira mdogo wa sh 10,000 - 20,00 ambazo kimsingi haziwasaidii kitu. Na zaidi ya yote ndo hao wanawatunza vizuri watoto (kuwalisha, kuwaandaa kwenda shule nk). Madhara ya kutowaheshimu kama binadamu ni makubwa sana kwa familia hasa kwa watoto wetu!! Ukiwa na HG mbaya hata watoto wanakosa raha japo wapo nyumbani kwao na wanapewa vitu vizuri tu na wazazi wao.
Kufukuza fukuza hovyo HG kunapelekea watoto kulelewa na HG kibao ambao wengine malezi yao kifamilia huwa si mazuri na inaweza kuwaambukiza wanao.
Binafsi sihafiki mke wangu aibuke asubuhi/jioni na kumfukuza HG!. Lazma aniambie kosa lake na tukubaliane hatua za kuchukuliwa baada ya kupima uzito wa kosa. Kama wewe mwanamke unahisia fulani juu ya HG, fanya utafiti then fanya uamuzi badala ya kumnyanyasa HG. Siye maofsini tunalalama watu wanafukuzwa hovyo hovyo lakini sisi wale wale majumbani tunawafukuza HG zaidi ya hovyo hovyo.
 
Kwa kawaida mtu akioa au kuolewa nia ni kupata msaidizi. Hata hivyo, kwa hali tunayoenda sasa imeakuwa kama "fashion" kwa kwa wake zetu hata kama hana kazi (mama wa nyumbani) kutafuta "binti wa kazi" na yeye awe anashinda mitaani tu akirudi kila kitu akute tayari kama ambavyo mumewe anavyotegemea kwake.

Tatizo linakuja pale ambapo mwanamke anapoleta "binti wa kazi" akitaka afanye kila kitu wakati huo huo huyo mke ana wivu kupita kiasi na mumewe.

Wapo wananawake wanathibutu kumwambua "hausigeli" afue mpka nguo za ndani za kwake na za mumewe na pia atandike kitanda wanacholalia na mumwe wakati yeye amenyoosha miguu...inapofikia kwenye kiwango cha juu zaidi mke anakuwa mvivu na muda wote anataka hausigeli awepo nyumbani.

Hili lipo kwenye familia nyingi, mama anaenda kumtafuta binti wa kazi kupitia "ma shosti" lakini baadae mume unaletewa "invoice" tu ya kulipa mshahara wa binti wa kazi na kwa wanawake wengi mume japo ndo unalipa mshahara(kama mama han kazi) bado huitakiwi kuhoji utendaji kazi wa huyo binti wala kumtetea pindi mama akikasirika.

Lakini cha ajabu, ikitokea siku Mke ameshindwa kutimiza wajibu wake, huwa anamsukumia binti wa ndani ili kama utaanza kumkemea na yeye atakupa "support".

Kwa ujumla wanawake huwa hawapendani hata kidogo, na ndo maana matatizo mengi kwenye familia yanahusihwa na "wifi, mama mkwe, dada nk".

Kanuni ya jumla ambayo inaweza kuzuia matatizo ni kumfanya mke awajibike kwa majukumu yake na sio kusingizia hausigeli....ukiruhusu hilo kila siku atakuambia "dada ndo kafanya hivi...si mimi.," akisema hiyo, atamwita mbele yako na kumkemea na pengine kumwadhibu utadhani yeye hausiki kabisa au yeye na wewe ndo baba mwenye nyumba na binti wa kazi ndo mke!...
 
Just imagine kule ofsini mkeo ni muhudumu wa ofisi na analambwa na Bosi, eti akirudi nyumbani ana kukaripia kwa nini unatembea na takataka au mwanamke asie na hadhi kama H/G.....where is the difference??? kumbe hajui hata mke wa Bosi nae akisikia mumewe anatembea na mhudumu wa ofisi atamthaminisha mkeo kwa viwango vile vie vya chini pengine kuliko H/G.
 
Halafu kina mamam muelewe kuwa mahgls na binadamu kama nyie nao wana hamu kama nyie. KSasa unafukiri kwa kuwa tu anakaaa na wewe asiwe na mahusiano miaka yote? Akipita barabarani akapendwa an haki ya kuwa na mtu wake. tena sio vibaya akapewa ruhusa hatat ikibidi kulala na hatimae arudi.. mkiwabana sana ndio mana wanawaibia waume zenu,.. wakiombwa hawakatai kwa sababu wanakuwa wamebanwa sana na hamu. Jaribu kufikiria na hilo kwa je huyu dada haja zake vipi mpe uhuru akipata mtu cha msingi ni kupanga na kuomba ruhusa basi.. Nao ni binadamu kama nyie. Sasa sio anakuwa na mtu eti unamchapa... why?
 
hii ishu ya mamsaps na hg ni ngumu sana na wamama wengi act irrationally na unapojaribu wakati wa conflict kuthink rationally wanakugeuzia kibao unampenda hg. mi siku hizi siingilii kabisa ugomvi wao na akitaka kuwafukuza i just remind her nani atafanya makazi ya nyumbani, kutunza mtoto usafi etc. akiwaza hilo zigo mwenyewe anapoa
 
Naweza kudiscuss nae issue, atatoa opinions. But decisions zote about hgeli ni juu yangu. badala ya ku-discuss jinsi gani ya kuboresha penzi letu na kujiongezea maendeleo, we cant waste our precious time to discuss hgeli, mtu ambaye anaweza akakuamsha alfajiri kukuambia naondoka zangu! Hata talaka ina notice!

"We can't waste our precious time to discuss hgeli." Really, Dada King'asti? Hgeli huyuhuyu tunaemwamini na kumuachia our precious chidren, tunawaamini watutayarishie maakuli yetu ya kila siku? Wakina mama wanawaamini na kuwàacha nyumbani na waume zao? Lakini unadhani sio muhimu kudiscuss issues zao ndani ya familia?
 
Jamani huyu house girl alipewa adhabu kali mno!!,just tu kuchelewa ndio anakosa kazi?,just imagine hata sie maofisini tungekuwa tunachelewa tunatimuliwa kazi ingekuaje?,twende mbele turudi nyuma,huyu mtoto mpaka kuwa kwako anafanya kazi ni shida/matatizo ndio yanamfanya awe hapo,sasa kumfukuza kisa kachelewa tunakuwa somehow hatujamtendea haki!!!!

kuna mambo mengi hapo...tatizo linaweza kuwa ni la hausgel..mama mwenye nyumba au huyo baba mwenye nyumba!
 
Hapo kuna yafuatayo; 1.Mama ni mvivu na kutokuwepo kwa dada kwake ilikua mzigo. 2. Dada kwa kufahamu mama yupo Aliona ni fursa muafaka kwake kupunguza sumu mwilini(namaanisha genye)..ndio naye si ntu. 3. Mama anaogopa dada akianza kwenda saloon ataibua urembo wake uliojoficha kutokana na kukosa hayo macarolite...mama anaogopa hatoweza kumudu upinzani huo. Mwisho: Ni mara chache kukuta Mama yuko na mapenzi ya kweli na dada ashkum si matusi anamuona kama mbwa tu...baba akimtetea unabambikizwa Kesi .
 
Nafikiria tofauti. Mkeo atakuamini iwapo wewe mwenyewe ni mwaminifu. Sasa jamani, housegirl ni msaidizi wa mama. baba, unapokataa asiondoke maana yake nini? mimi sihitaji permission ya mume ku-fire house girl(though wangu ana ruhusa ya kutoka every sunday, asije nchukulia l'azizi wangu eh!)

We tukikuacha uendelee na mawazo haya utakuja kiwa Genius.
 
hapo sidhani kama kuna haja ya kuumiza kichwa kiasi hicho,kama maza huose anakomaa binti aondoke baba mji ni suala ka kumuuliza mkewe amhakikishie binti mwingine wa kaz before huyo kuondoka ili kuepusha misuguano mingine isiyo na tija
 
Kuna vitu havihitaji rocket science kufanyia maamuzi. Unaangalia tu unaamua tupa kule.
Kama nyumbani kwako mnafanyabconference ya siku 7 kumjadili hgal, kwangu hakuna nafasi hiyo. Pole kwa kukustua, we operate kama kampuni ya kigeni, i tell u.
"We can't waste our precious time to discuss hgeli." Really, Dada King'asti? Hgeli huyuhuyu tunaemwamini na kumuachia our precious chidren, tunawaamini watutayarishie maakuli yetu ya kila siku? Wakina mama wanawaamini na kuwàacha nyumbani na waume zao? Lakini unadhani sio muhimu kudiscuss issues zao ndani ya familia?
 
mwacheni amfukuze abaki hapo home na wanaye wakati anatafuta mdada mwingine.
 
Wife wangu anamuachia house girl kupika,kunitengea chakula na nguo zangu kufua anafua yeye,nikimwambia haya majukumu yako anadai yeye anachoka,nimepanga kumzingua one day nasubiri wakati tunkula najifanya kuuliza chakula kapika nani? Akisema dada wa kazi hapohapo nampa zawadi ya elfu tano akanywe soda.najua atamaindi kwa sana,ujumbe utafika kuwa asimuachie house girl kila kitu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom