Wakatoliki watakiwa kuisoma Katiba pendekezwa

Seif al Islam

JF-Expert Member
Nov 14, 2011
2,156
638
WAKRISTO wa dhehebu la Katoliki nchini wametakiwa kuisoma kwa makini Katiba inayopendekezwa kabla ya kupiga kura ya maoni ili kufanya chaguo sahihi.

Hayo yalisemwa juzi na Paroko wa Parokia ya Bikira Maria Mama wa Huruma (BMMH) Mbezi Tangibovu jijini Dar es Salaam, Andrew Mwakibindu wakati akiongoza ibada ya pili kanisani hapo.

Katiba mahubiri yake, paroko huyo aliwaasa waamini wa dhehebu hilo popote walipo kuacha kusikiliza maneno ya wengine kuhusu katiba inayopendekezwa watumie muda wao kusoma ili wapigie kura kitu wanachokielewa.

"Nawashauri kuisoma sana katiba inayopendekezwa msisikilize kelele za watu mwende mkachague kitu mnchokielewa… ya Mungu mpeni Mungu na yaliyo ya Kaisari mpeni Kaisari.

"Msiache kuisoma katiba inayopendekezwa kwa sababu ile ni mali ya watanzania wote bila kujali chama cha mtu wala dini yake," alisisitiza paroko Mwakibindu na kuwataka kuliombea amani taifa hili.

Aliwataka waamini hao kutii sheria za nchi ikiwemo kulipa kodi na kutimiza wajibu wao katika kanisa wa kulipa zaka, fungu la 10 na kumrejeshea Mungu sadaka iliyonona ili wapokee baraka za Mungu.

Chanzo:Tanzania Daima
 
siyo wakatoliki watu wote tunaisoma vema ili kufanya maamuzi sahihi hakuna mtu anayeweza kutupotosha kwa kujifanya yeye ni wakala wa siasa.
 

Aliwataka waamini hao kutii sheria za nchi ikiwemo(kutokuandamana) kulipa kodi na kutimiza wajibu wao katika kanisa wa kulipa zaka, fungu la 10 na kumrejeshea Mungu sadaka iliyonona ili wapokee baraka za Mungu.

Chanzo:Tanzania Daima
Mwenye masikio na asikie.

 
siyo wakatoliki watu wote tunaisoma vema ili kufanya maamuzi sahihi hakuna mtu anayeweza kutupotosha kwa kujifanya yeye ni wakala wa siasa.

Mkuu sisi Wakatoriki tunafuata waraka waliotusomea kanisani kuwa atutambui mbunge la katiba na mambo yake yote kama tunavyomkataa ibirisi
 
mimi ni mkristo na nimishaisoma yote na kuielewa kura yangu ni hapana.

Ibara ya 21waiondoe kwanza, mtu unapewa haki kwa mkono wa kulia baadae unapokonywa kwa mkono wa kushoto. huu ni ujinga sana.

Kwa mfano: wakulima wameambiwa kuwa, wana hakiya kupata ardhi kwa ajili ya kilimo chao ila sasa tatizo ni hili, usipopata hiyo ardhi huna haki ys kwenda kushtaki popote na mahakama zote zimezuiwa kupokea, kusikiliza na kutoa maamuzi yoyot juu ya sura hii ya pili.

hivyo hivyo, wafugaji, huduma za afya, elimu, maji nk.

hizi nazo wamesema kuwa wananchi wanayohaki kupata elimu bora, maji safi na salama, maeneo ya kulishia mifugo na huduma bora za afya, ila usipopewa hivi vitu hutashitaki popopte.

Ibara hii inaturudisha tulipo sasa kwani serikali inakimbia uwajibikaji kwa wananchi na kuruhusu hata pesa zilizotengwa kwa huduma hizi ziendelee kuliwa kama sasa na mchwa wa Halmashauri na idara zingine.

PIA: kamati ya uteuzi wa TUME YA UCHAGUZI wamo akina SPIKA NA NAIBU WAKE hii haikubaliki, TUME ya warioba iliweka vile kwa kuzingatia mfumo wa serikali tatu na kwamba Hawatatokana na vyama vya siasa, sasa kwa mfumo wao huu wa serikali mbili kuwaacha SPIKA NA NAIBU wake eti wawe wateuzi wa wajumbe wa TUME HURU ya uchaguzi haikubaliki.
 
WAKRISTO wa dhehebu la Katoliki nchini wametakiwa kuisoma kwa makini Katiba inayopendekezwa kabla ya kupiga kura ya maoni ili kufanya chaguo sahihi.

Hayo yalisemwa juzi na Paroko wa Parokia ya Bikira Maria Mama wa Huruma (BMMH) Mbezi Tangibovu jijini Dar es Salaam, Andrew Mwakibindu wakati akiongoza ibada ya pili kanisani hapo.

Katiba mahubiri yake, paroko huyo aliwaasa waamini wa dhehebu hilo popote walipo kuacha kusikiliza maneno ya wengine kuhusu katiba inayopendekezwa watumie muda wao kusoma ili wapigie kura kitu wanachokielewa.

"Nawashauri kuisoma sana katiba inayopendekezwa msisikilize kelele za watu mwende mkachague kitu mnchokielewa… ya Mungu mpeni Mungu na yaliyo ya Kaisari mpeni Kaisari.

"Msiache kuisoma katiba inayopendekezwa kwa sababu ile ni mali ya watanzania wote bila kujali chama cha mtu wala dini yake," alisisitiza paroko Mwakibindu na kuwataka kuliombea amani taifa hili.

Aliwataka waamini hao kutii sheria za nchi ikiwemo kulipa kodi na kutimiza wajibu wao katika kanisa wa kulipa zaka, fungu la 10 na kumrejeshea Mungu sadaka iliyonona ili wapokee baraka za Mungu.

Chanzo:Tanzania Daima

father,mi ni mkatoliki damu.kura yangu ni HAPANA
 
Back
Top Bottom