Wakamatwa kwa kujitangaza kutoa huduma ya internet ya Starlink Instagram

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,446
7,822
Kamanda Murilo leo ametangaza kukamata watu wawili, mtanzania na mchina kwa kuingiza vifaa na kutangaza kutoa huduma ya internet ya starlink. Polisi wamesema wameuza vifaa hivyo bila kuidhinishwa na TCRA.

Naona kama mitandao yetu wanaipiga pini starlink by fire, by force 😅 Kwanini Serikali wasimalize mchakato kama wananchi ndio wanahitaji.

Murilo_Starlink.png


=========

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa kushirikiana na kikosi kazi maalum cha kuzuia na kupambana na matumizi ya makosa ya kimtandao limewakamata Claudian Makaranga (28) mkazi Kawe na Hongliang Yang (35) Mchina, mkazi wa Kigamboni, kwa tuhuma za kuingiza vifaa vya mawasiliano ya intaneti nchini bila kufuata utaratibu wa kisheria vyenye jina la STARLINK KIT/DEVICE.

Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda maalum SACP Jumanne Muliro anasema Watuhumiwa hao wamekuwa wakijitangaza kuuza vifaa na kutoa huduma ya internet nchini kupitia mtandao ya kijamii wa Instagram kwa akaunti yenye jina la STARLINK.

Baadhi ya vifaa vilivyoingizwa nchini imebanika vilishauzwa na kutumika katika baadhi ya maeneo ya Dar es Salaam kitendo ambacho ni kosa na kinyume na sheria kwani havijaidhinishwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).

EATV
 
Kwani ukipata kifaa unaaccess hata kama nchi imezuia?

Kama ipo hivyo, hayo makatazo, mazuio na ukamataji(ambao nao unatangazwa🤨) ni viungo katika tangazo moja kuuuuuuuuuuuuubwa la 'black market' ya starlink.

Ukitumia akili utaiona hiyo 'grand scheme of it'. Akili tu mtu wangu. Bora tu wahalalishe tusipoteze mapato.
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum linawashikilia Claudian Makaranga (28) Mkazi wa Kawe, Kinondoni na Raia wa China Hongliang Yang (35), Mkazi wa Kigamboni, kwa tuhuma za kuingiza Nchini vifaa vya Mawasiliano ya Intaneti vyenye jina la STARLINK KIT/DEVICE bila kufuata utaratibu wa Kisheria

Februari 26, 2024 Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye, kupitia Mtandao wa X (Twitter) alisema Kampuni ya Starlink inayotoa Huduma za Intaneti kwa kutumia 'Satelaiti' inakamilisha hatua za mwisho ili kupata vibali vya kutoa Huduma nchini

Aliongeza kuwa Starlink ikishatimiza taratibu zote itaanza kutoa huduma na kwamba Serikali inasubiri wakamilishe tu taratibu hizo
 
Kamanda Murilo leo ametangaza kukamata watu wawili, mtanzania na mchina kwa kuingiza vifaa na kutangaza kutoa huduma ya internet ya starlink. Polisi wamesema wameuza vifaa hivyo bila kuidhinishwa na TCRA...
Ndio maana Tanzania na hata katika nchi nyingine nyingi za ki-Afrika hakuna Ugunduzi wala Uvumbuzi mpya wa kisayansi unaofanyika kutokana na kuwapo kwa tawala mbaya ambazo haziweki mazingira mazuri na wezeshi ya watu kuweza kufanya kazi zao kwa uhuru.
 
Kwani ukipata kifaa unaaccess hata kama nchi imezuia?

Kama ipo hivyo, hayo makatazo, mazuio na ukamataji(ambao nao unatangazwa🤨) ni viungo katika tangazo moja kuuuuuuuuuuuuubwa la 'black market' ya starlink.

Ukitumia akili utaiona hiyo 'grand scheme of it'. Akili tu mtu wangu. Bora tu wahalalishe tusipoteze mapato.
Zina operates kama vile Dish za TV na za Internet ambazo tayari zipo hapa Tanzania , Changamoto Kifurushi kikiisha lazima ukinunue nje ya Tanzania Kwani STARLINK awana Sales/Support Offices kama vile zile za DSTV wenye makao yao makuu nchini South Africa.Hiyo ndo Changamoto. Kenya wapo.
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa kushirikiana na kikosi kazi maalum cha kuzuia na kupambana na matumizi ya makosa ya kimtandao limewakamata Claudian Makaranga (28) mkazi Kawe na Hongliang Yang (35) Mchina, mkazi wa Kigamboni, kwa tuhuma za kuingiza vifaa vya mawasiliano ya intaneti nchini bila kufuata utaratibu wa kisheria vyenye jina la STARLINK KIT/DEVICE.

Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda maalum SACP Jumanne Muliro anasema Watuhumiwa hao wamekuwa wakijitangaza kuuza vifaa na kutoa huduma ya internet nchini kupitia mtandao ya kijamii wa Instagram kwa akaunti yenye jina la STARLINK.

Baadhi ya vifaa vilivyoingizwa nchini imebanika vilishauzwa na kutumika katika baadhi ya maeneo ya Dar es Salaam kitendo ambacho ni kosa na kinyume na sheria kwani havijaidhinishwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).

Source EATV
GJRp8pJW8AAqUe0.jpeg
 
Back
Top Bottom