Wajuzi wa Muungano naomba ufafanuzi katika hili

Termux

JF-Expert Member
Oct 7, 2017
406
980
Maoni yenu wadau, Wajuzi wa muungano mimi hapa sijaelewa naomba ufafanuzi kidogo, Tanzania ni muunganiko wa
( tanganyika na zanzibar ) iweje zanzibar wana .... arafu tanganyika wapo empty, huu muungano ulikuwaje???????

Maana hapa inakuwa Tanzania na zanzibar inainyonya tanganyika katika huu muungano.

#UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
*Nyimbo ya taifa
*Jeshi
*Raisi
*Katiba
*Bunge
*Mahakama

#ZANZIBAR
*Nyimbo ya taifa
*Jeshi
*Raisi
*Katiba
*Bunge
*Mahakama

#TANGANYIKA FEDERATION
?
?
?
?
?
?

Muhimu serikari Tatu maana hapa kuna upendeleo. Kwanini tanganyika awana chochote. Naitaji kifahamu ili, wajuzi wa muungano naombeni muongozo kidogo, wanasheria au kikatiba hii imekaaje

#KUNA HUU UZI NAONA UMEKAA KMYA SANA AMBAO ULIWEKWA NA SALIZAH
###################

Shikamoo Babu. Babu nimesoma katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 ibara ya 2A inasema "Zanzibar ni miongoni mwa nchi mbili zinazounda jamhuri ya muungano wa Tanzania". Kweli naiona Zanzibar ipo kama nchi maana ina Rais wake, katiba na bendera yake. Nchi ya pili ambayo ni sehemu ya muungano hapa namaanisha Tanganyika Iko wapi? Rais wake ni nani?, na yenyewe inatekelezea wapi mambo yasiyo ya muungano? Je huu ni muungano wa Tanganyika na Zanzibar au Tanzania na Zanzibar?

Babu kwa nini Urais siyo jambo la muungano lakini Umakamu wa Rais ni jambo la muungano? Kwa nini elimu ya msingi si jambo la muungano lakini elimu ya juu ni jambo la muungano? Kwa ni mambo ya sheria ni jambo la muungano lakini kuna mahakama kuu ya Tanzania na mahakama kuu ya Zanzibar? Kwa nini kuna mwanasheria mkuu wa Tanzania na mwanasheria mkuu wa Zanzibar? Kwa nini kuna jaji mkuu wa Tanzania na jaji mkuu wa Zanzibar? Ukiangalia yale mambo 22 ya muungano yaliyotajwa kwenye katiba utagundua zipo kwa nini nyingi sana ambazo zina majibu tata..

Je Babu umewahi kujiuliza kuwa kwa katiba tuliyonayo na mfumo wa sasa kuna uwezekano Jamhuri ya muungano wa Tanzania ikawa na Rais, waziri mkuu, mkuu wa majeshi, mkuu wa jeshi la polisi, mkuu wa usalama wa Taifa, makatibu wakuu na idadi kubwa ya mawaziri wote kutoka Zanzibar? ambayo ni sehemu moja ya muungano. Lakini kwa katiba na mfumo huu huu haitatokea hata siku moja viongozi katika nyazifa nilizotaja hapo juu watoke Tanganyika. Kwa sababu hakuna nchi inayoitwa Tanganyika katika uso wa dunia. Ilikufa kifo cha mende mnamo mwaka 1964, mwaka ambao Zanzibar si tu iliachwa kuendeleza uhai wake kama nchi bali ilibatizwa na kupewa baraka za kuungana rasmi na Tanzania. Jambo ambalo ni gumu sana kulielewa.

Babu nimechoka kukariri dhana ya huu MUUNGANO nataka kuuelewa sasa ili niwe na majibu ya kuja kuwapa wajukuu zangu.

Babu nadhani sura ya muungano huu wa sasa kwa mfano rahisi ni sawa na kusema hivi "Kuna majirani wawili ( Tanganyika na Zanzibar ) wakubaliane kuvunja mazizi na kuchanganya mifugo yao na kuipeleka kwa mjumbe ( Tanzania ) ili kurahisisha uchungaji na kufanya ufugaji wenye tija lakini baada ya muungano huo wanaweka muongozo wa usimamiaji wa mifungo hiyo ( katiba ) ambayo cha kushangaza inampa mjumbe ( Tanzania ) na jirani mmoja ( Zanzibar) nguvu ya kisheria ya kuanzisha tena zizi lake na kuendeleza shuguli za ufugaji kama zamani kisha inamnyang'anya haki hiyo jirani mwingine ( Tanganyika ) na kumpoteza kabisa katika uso wa dunia.

Babu ukisoma katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania ibara ya 47 (3) "Mtu atateuliwa kugombea kiti cha makamu wa Rais kwa kufuata kanuni kwamba endapo Rais wa Jamhuri ya muungano atatoka sehemu moja ya muungano, basi makamu wa Rais atakuwa ni mtu anayetoka sehemu ya pili ya Muungano. Kwa Ibara hii inamaanisha kuna sehemu mbili za muungano ambazo ni Tanganyika na Zanzibar. Lakini Zanzibar ni nchi na Tanganyika haijulikani ilipo. Ipo kasoro mahali na kama ukitaka kuiona kasoro hiyo ifufuliwe Tanganyika leo ipewe mamlaka ya ki nchi kama Zanzibar.

Katika ibara hiyo hiyo 47 ( 5 ) inasema nanukuu " Chama chochote hakitazuiwa kumpendekeza mtu yeyote kuwa mgombea kiti cha Makamu wa Rais kwa sababu tu kwamba mtu huyo kwa wakati huo ameshika kiti cha Rais wa Zanzibar au kiti cha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano." mwisho wa kunukuu. Maana yake ni kwamba kama Tanganyika ingekuwa hai pia ingekuwa na haki ya viongozi wake kuteuliwa kugombea nafasi ya makamu wa Rais kama ilivyo Zanzibar. Na kifungu ibara hiyo ingesomeka hivi "Chama chochote hakitazuiwa kumpendekeza mtu yeyote kuwa mgombea kiti cha Makamu wa Rais kwa sababu tu kwamba mtu huyo kwa wakati huo ameshika kiti cha Rais wa Zanzibar au Tanganyika au kiti cha Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano". Nadhani sasa angalau unapata mantiki ya andiko langu.

Babu yangu nadhani nitakuwa sahihi nikisema sura ya muungano inachelewesha maendeleo ya nchi yetu na inazorotesha uwajibikaji. Kwa sasa ni ngumu Tanzania kupanga mkakati wa maendeleo bila kuifikiria Zanzibar au hata bila kuiuliza Zanzibar ili kupata maoni yake juu ya jambo hilo. Kwa ikitokea serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania imefanya maamuzi mabaya juu ya jambo lolote siyo rahisi au haiwezekani kabisa Rais, jaji mkuu au mwanasheria mkuu wa Zanzibar kuhoji au kukosoa jambo hilo. Kinadharia ni kwamba muungano unazungumza lugha moja lakini kimatendo na kiuhalisia ni kinyume kabisa. Tumefikishwa hapo na muundo wa muungano ambao kwa mawazo yangu naona hauko sahihi na unastahili marekebisho ili kuuboresha.

Babu yangu nafikiria kimtazamo kuifufua Tanganyika inaonekana ni ngumu kwa sababu ni kama jinamizi linalotembea nyuma ya kivuli cha Tanzania na kuiua Zanzibar ni ngumu zaidi kwa sababu siyo tu inatembea ubavuni mwa Tanzania bali imeshasimika mizizi imara sana kwenye ardhi iitwayo muungano. Lakini ukweli na uhalisia ni kwamba ni swala la muda tu ambapo Tanganyika aidha itasogea upande wa pili wa ubavu wa Tanzania ama itachukua nafasi ya Tanzania na kuanza kutembea mkabala na Zanzibar wakati Tanzania ikirudi nyuma na kuwa kama mchungaji aongozaye mifugo yake kwenda malishoni. Sababu hilo ndilo lengo mama muungano.

Babu naomba nimalizie Kwa kusema nimegundua kundi kubwa la watu wa bara ( watanganyika ) hawakuwa na bado hawaoni ni fahari sana kutaka Tanganyika ifufuliwe kwa sababu walikuwa na bado wana nia njema na umoja au muungano kama unavyojitanabaisha, pia walikuwa na bado wana mapenzi na imani kubwa na Jamhuri ya muungano. Lakini hata kama unapenda safari ya baharini, na unaiamini meli na nahodha anayeiongoza meli hiyo. Lakini ukiona bahari ina dalili za kuchafuka au nahodha anaonesha dalili za kushindwa kuiongoza meli hiyo huo ndiyo wakati sahihi wa kuanza kujiuliza maswali juu ya uhakika wa safari na kama majibu unayopata yanakupa wasiwasi, basi huo ndiyo wakati mzuri pia wa kuanza kufanya maandalizi ya kuchukua tahadhali na kuandaa zana za uokoaji endapo tu kama una asilimia nyingi za kuamini maafa yatatokea huko mbeleni. Na siyo dhambi kuyafanya hayo kwa kujihakikishia usalama wako pamoja na ndugu na majirani zako mnaosafiri nao au kubadili uelekeo wa safari kabisa.

....Mimi Salizah
 
Maoni yenu wadau, Wajuzi wa muungano mimi hapa sijaelewa naomba ufafanuzi kidogo, Tanzania ni muunganiko wa
( tanganyika na zanzibar ) iweje zanzibar wana .... arafu tanganyika wapo empty, huu muungano ulikuwaje???????

Maana hapa inakuwa Tanzania na zanzibar inainyonya tanganyika katika huu muungano.

#UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
*Nyimbo ya taifa
*Jeshi
*Raisi
*Katiba
*Bunge
*Mahakama

#ZANZIBAR
*Nyimbo ya taifa
*Jeshi
*Raisi
*Katiba
*Bunge
*Mahakama

#TANGANYIKA FEDERATION
?
?
?
?
?
?

Muhimu serikari Tatu maana hapa kuna upendeleo. Kwanini tanganyika awana chochote. Naitaji kifahamu ili, wajuzi wa muungano naombeni muongozo kidogo, wanasheria au kikatiba hii imekaaje

#KUNA HUU UZI NAONA UMEKAA KMYA SANA AMBAO ULIWEKWA NA SALIZAH
###################

Shikamoo Babu. Babu nimesoma katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 ibara ya 2A inasema "Zanzibar ni miongoni mwa nchi mbili zinazounda jamhuri ya muungano wa Tanzania". Kweli naiona Zanzibar ipo kama nchi maana ina Rais wake, katiba na bendera yake. Nchi ya pili ambayo ni sehemu ya muungano hapa namaanisha Tanganyika Iko wapi? Rais wake ni nani?, na yenyewe inatekelezea wapi mambo yasiyo ya muungano? Je huu ni muungano wa Tanganyika na Zanzibar au Tanzania na Zanzibar?

Babu kwa nini Urais siyo jambo la muungano lakini Umakamu wa Rais ni jambo la muungano? Kwa nini elimu ya msingi si jambo la muungano lakini elimu ya juu ni jambo la muungano? Kwa ni mambo ya sheria ni jambo la muungano lakini kuna mahakama kuu ya Tanzania na mahakama kuu ya Zanzibar? Kwa nini kuna mwanasheria mkuu wa Tanzania na mwanasheria mkuu wa Zanzibar? Kwa nini kuna jaji mkuu wa Tanzania na jaji mkuu wa Zanzibar? Ukiangalia yale mambo 22 ya muungano yaliyotajwa kwenye katiba utagundua zipo kwa nini nyingi sana ambazo zina majibu tata..

Je Babu umewahi kujiuliza kuwa kwa katiba tuliyonayo na mfumo wa sasa kuna uwezekano Jamhuri ya muungano wa Tanzania ikawa na Rais, waziri mkuu, mkuu wa majeshi, mkuu wa jeshi la polisi, mkuu wa usalama wa Taifa, makatibu wakuu na idadi kubwa ya mawaziri wote kutoka Zanzibar? ambayo ni sehemu moja ya muungano. Lakini kwa katiba na mfumo huu huu haitatokea hata siku moja viongozi katika nyazifa nilizotaja hapo juu watoke Tanganyika. Kwa sababu hakuna nchi inayoitwa Tanganyika katika uso wa dunia. Ilikufa kifo cha mende mnamo mwaka 1964, mwaka ambao Zanzibar si tu iliachwa kuendeleza uhai wake kama nchi bali ilibatizwa na kupewa baraka za kuungana rasmi na Tanzania. Jambo ambalo ni gumu sana kulielewa.

Babu nimechoka kukariri dhana ya huu MUUNGANO nataka kuuelewa sasa ili niwe na majibu ya kuja kuwapa wajukuu zangu.

Babu nadhani sura ya muungano huu wa sasa kwa mfano rahisi ni sawa na kusema hivi "Kuna majirani wawili ( Tanganyika na Zanzibar ) wakubaliane kuvunja mazizi na kuchanganya mifugo yao na kuipeleka kwa mjumbe ( Tanzania ) ili kurahisisha uchungaji na kufanya ufugaji wenye tija lakini baada ya muungano huo wanaweka muongozo wa usimamiaji wa mifungo hiyo ( katiba ) ambayo cha kushangaza inampa mjumbe ( Tanzania ) na jirani mmoja ( Zanzibar) nguvu ya kisheria ya kuanzisha tena zizi lake na kuendeleza shuguli za ufugaji kama zamani kisha inamnyang'anya haki hiyo jirani mwingine ( Tanganyika ) na kumpoteza kabisa katika uso wa dunia.

Babu ukisoma katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania ibara ya 47 (3) "Mtu atateuliwa kugombea kiti cha makamu wa Rais kwa kufuata kanuni kwamba endapo Rais wa Jamhuri ya muungano atatoka sehemu moja ya muungano, basi makamu wa Rais atakuwa ni mtu anayetoka sehemu ya pili ya Muungano. Kwa Ibara hii inamaanisha kuna sehemu mbili za muungano ambazo ni Tanganyika na Zanzibar. Lakini Zanzibar ni nchi na Tanganyika haijulikani ilipo. Ipo kasoro mahali na kama ukitaka kuiona kasoro hiyo ifufuliwe Tanganyika leo ipewe mamlaka ya ki nchi kama Zanzibar.

Katika ibara hiyo hiyo 47 ( 5 ) inasema nanukuu " Chama chochote hakitazuiwa kumpendekeza mtu yeyote kuwa mgombea kiti cha Makamu wa Rais kwa sababu tu kwamba mtu huyo kwa wakati huo ameshika kiti cha Rais wa Zanzibar au kiti cha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano." mwisho wa kunukuu. Maana yake ni kwamba kama Tanganyika ingekuwa hai pia ingekuwa na haki ya viongozi wake kuteuliwa kugombea nafasi ya makamu wa Rais kama ilivyo Zanzibar. Na kifungu ibara hiyo ingesomeka hivi "Chama chochote hakitazuiwa kumpendekeza mtu yeyote kuwa mgombea kiti cha Makamu wa Rais kwa sababu tu kwamba mtu huyo kwa wakati huo ameshika kiti cha Rais wa Zanzibar au Tanganyika au kiti cha Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano". Nadhani sasa angalau unapata mantiki ya andiko langu.

Babu yangu nadhani nitakuwa sahihi nikisema sura ya muungano inachelewesha maendeleo ya nchi yetu na inazorotesha uwajibikaji. Kwa sasa ni ngumu Tanzania kupanga mkakati wa maendeleo bila kuifikiria Zanzibar au hata bila kuiuliza Zanzibar ili kupata maoni yake juu ya jambo hilo. Kwa ikitokea serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania imefanya maamuzi mabaya juu ya jambo lolote siyo rahisi au haiwezekani kabisa Rais, jaji mkuu au mwanasheria mkuu wa Zanzibar kuhoji au kukosoa jambo hilo. Kinadharia ni kwamba muungano unazungumza lugha moja lakini kimatendo na kiuhalisia ni kinyume kabisa. Tumefikishwa hapo na muundo wa muungano ambao kwa mawazo yangu naona hauko sahihi na unastahili marekebisho ili kuuboresha.

Babu yangu nafikiria kimtazamo kuifufua Tanganyika inaonekana ni ngumu kwa sababu ni kama jinamizi linalotembea nyuma ya kivuli cha Tanzania na kuiua Zanzibar ni ngumu zaidi kwa sababu siyo tu inatembea ubavuni mwa Tanzania bali imeshasimika mizizi imara sana kwenye ardhi iitwayo muungano. Lakini ukweli na uhalisia ni kwamba ni swala la muda tu ambapo Tanganyika aidha itasogea upande wa pili wa ubavu wa Tanzania ama itachukua nafasi ya Tanzania na kuanza kutembea mkabala na Zanzibar wakati Tanzania ikirudi nyuma na kuwa kama mchungaji aongozaye mifugo yake kwenda malishoni. Sababu hilo ndilo lengo mama muungano.

Babu naomba nimalizie Kwa kusema nimegundua kundi kubwa la watu wa bara ( watanganyika ) hawakuwa na bado hawaoni ni fahari sana kutaka Tanganyika ifufuliwe kwa sababu walikuwa na bado wana nia njema na umoja au muungano kama unavyojitanabaisha, pia walikuwa na bado wana mapenzi na imani kubwa na Jamhuri ya muungano. Lakini hata kama unapenda safari ya baharini, na unaiamini meli na nahodha anayeiongoza meli hiyo. Lakini ukiona bahari ina dalili za kuchafuka au nahodha anaonesha dalili za kushindwa kuiongoza meli hiyo huo ndiyo wakati sahihi wa kuanza kujiuliza maswali juu ya uhakika wa safari na kama majibu unayopata yanakupa wasiwasi, basi huo ndiyo wakati mzuri pia wa kuanza kufanya maandalizi ya kuchukua tahadhali na kuandaa zana za uokoaji endapo tu kama una asilimia nyingi za kuamini maafa yatatokea huko mbeleni. Na siyo dhambi kuyafanya hayo kwa kujihakikishia usalama wako pamoja na ndugu na majirani zako mnaosafiri nao au kubadili uelekeo wa safari kabisa.

....Mimi Salizah
Muungano ninaoufahamu mimi!;
Niuwe duka langu na ww uuwe duka lako Tuwe na duka.1 la muungano!
Ukate nusu ya duka lako na mimi nusu ya duka lako tuunganishe hizi nusu.2 Tuwe na duka la muungano!
Hii ww umebakia na duka lako!; ila langu ndio la liwe muungano, na unashiriki kikamilifu dukani!
Hii Haikubaliki hata akiwa mkeo au mwanao
 
Muungano ninaoufahamu mimi!;
Niuwe duka langu na ww uuwe duka lako Tuwe na duka.1 la muungano!
Ukate nusu ya duka lako na mimi nusu ya duka lako tuunganishe hizi nusu.2 Tuwe na duka la muungano!
Hii ww umebakia na duka lako!; ila langu ndio la liwe muungano, na unashiriki kikamilifu dukani!
Hii Haikubaliki hata akiwa mkeo au mwanao
Hapa kuna kitu hakipo sawa, wana tanganyika tunatakiwa tuwe kama zanzibar.
 
Maoni yenu wadau, Wajuzi wa muungano mimi hapa sijaelewa naomba ufafanuzi kidogo, Tanzania ni muunganiko wa
( tanganyika na zanzibar ) iweje zanzibar wana .... arafu tanganyika wapo empty, huu muungano ulikuwaje???????

....Mimi Salizah
asante
P
 
Back
Top Bottom