Kakati
Senior Member
- Apr 11, 2009
- 167
- 47
Jamiiforums,
Hivi mtu akitaka kutoa maoni yake kwa tume ya katiba online atatakiwa afanyeje? Tume ya Warioba ina website kwa ajili hiyo?
Mimi kuna jambo linanipa shida sana. Leo mtu kaenda kujiandikisha ili apate kitambulisho cha taifa. Yule mwandishi akamwambia apeleke barua ya mjumbe wake wa nyumba kumi bila hivyo hawezi kumwandika hata kama ana vitambulisho gani! Ugonvi ulikuwa mkubwa.
Mimi natafuta njia ya kufikisha pendekezo la kumaliza tatizo hilo kwa njia ya katiba. Ninapendekeza katika katiba mpya kuwekwe kifungu kinachozuia watu kunyimwa huduma fulani hadi watambulishwe na kiongozi aliyepatika kutoka chama fulani. Hawa watu wanaoitwa wajumbe si viongozi wa kuchaguliwa na wananchi. Kiongozi wa chini kabisa kiutawala wa nchi hii ni Mwenyekiti wa Mtaa au Kitongoji (mijini/vijijini).
Kama tukitaka wajumbe wawe ni chombo cha kuwatambua watu kwa karibu zaidi badala ya viongozi wa mitaa au vijiji na vitongoji, basi tuweke utaratibu wa watu hawa kuchaguliwa na watu wa vyama vyote ndani ya eneo husika kama inavyofanyika kwa wenyeviti wa mitaa.
Najua CCM wanafurahia hali ya kutokuwa na kiongozi rasmi wa serikali katika ngazi ndogo badala yake wanaweka kiongozi wa CCM na wanataka watu wanaendelea na utamaduni wa zamani wa kutumia balozi/mjumbe wa shina ambaye hapo zamani alikuwa na kofia ya chama na serikali. Wanajaribu kuwafanya waTanzania wasitofautishe kati ya CCM na Serikali lakini. Hii haitusaidii na kuna wakati/mahali inaleta vurugu.
Tuondoe habari ya mjumbe au tuifanye ya kuchaguliwa na watu wote. Mwenye mawao tofauti au anayejua jinsi gani naweza kuwasilisha hoja hii anisaidie.
Hivi mtu akitaka kutoa maoni yake kwa tume ya katiba online atatakiwa afanyeje? Tume ya Warioba ina website kwa ajili hiyo?
Mimi kuna jambo linanipa shida sana. Leo mtu kaenda kujiandikisha ili apate kitambulisho cha taifa. Yule mwandishi akamwambia apeleke barua ya mjumbe wake wa nyumba kumi bila hivyo hawezi kumwandika hata kama ana vitambulisho gani! Ugonvi ulikuwa mkubwa.
Mimi natafuta njia ya kufikisha pendekezo la kumaliza tatizo hilo kwa njia ya katiba. Ninapendekeza katika katiba mpya kuwekwe kifungu kinachozuia watu kunyimwa huduma fulani hadi watambulishwe na kiongozi aliyepatika kutoka chama fulani. Hawa watu wanaoitwa wajumbe si viongozi wa kuchaguliwa na wananchi. Kiongozi wa chini kabisa kiutawala wa nchi hii ni Mwenyekiti wa Mtaa au Kitongoji (mijini/vijijini).
Kama tukitaka wajumbe wawe ni chombo cha kuwatambua watu kwa karibu zaidi badala ya viongozi wa mitaa au vijiji na vitongoji, basi tuweke utaratibu wa watu hawa kuchaguliwa na watu wa vyama vyote ndani ya eneo husika kama inavyofanyika kwa wenyeviti wa mitaa.
Najua CCM wanafurahia hali ya kutokuwa na kiongozi rasmi wa serikali katika ngazi ndogo badala yake wanaweka kiongozi wa CCM na wanataka watu wanaendelea na utamaduni wa zamani wa kutumia balozi/mjumbe wa shina ambaye hapo zamani alikuwa na kofia ya chama na serikali. Wanajaribu kuwafanya waTanzania wasitofautishe kati ya CCM na Serikali lakini. Hii haitusaidii na kuna wakati/mahali inaleta vurugu.
Tuondoe habari ya mjumbe au tuifanye ya kuchaguliwa na watu wote. Mwenye mawao tofauti au anayejua jinsi gani naweza kuwasilisha hoja hii anisaidie.