Wajumbe 7 mbumbumbu wa bunge la katiba

mwanawao

JF-Expert Member
Aug 18, 2010
3,142
5,634
Watanzania walio wengi tulitegemea wajumbe walioko katika bunge la katiba ni watu makini na wenye uwezo mkubwa wa kuchambua mambo. Katika hali isiyo ya kawaida jana wakati wa kupiga kura ya kumchagua mwenyeketi kura saba ziliharibika. Huwezi kutegemea watu ambao wanategemewa kuja na katiba ambayo ni msingi wa Taifa hata kupiga kura tu kunawashinda? Je, kujenga hoja ya kutetea maslahi ya Taifa wataweza?

Mara nyingi tunategemea kura kuharibika sehemu ambazo kuna jamii isiyojua kusoma wala kuandika ndo huwa wanafanya madudu ya namna hiyo, na hatuwalaumu kwa sababu uwezo wao hauwaruhusu kufanya mambo juu ya uwezo wao. Ila kwa hawa wanaokula kodi zetu kila siku wakati uwezo wao ni mdogo haikubaliki.

Ni vyema hao waliofanya hayo madudu wajipime kama wanastahili kuendelea kukaa katika bunge hilo. Otherwise kwa hiari yao waondoke tu badala ya kuendelea kula kodi ya Watanzania. Maana hamna sababu ya Taifa kuendelea kuharibu hela kwa watu ambao ni mizigo.
 
Mkuu hapo umechemsha kwani si lazima upige kura.
Wajumbe wayo haki ya kumchagua wamtakaye ila hawalazimishwi kuchagua au kupiga kura kama hawaoni wamtakaye.
Inawezekana hao wajumbe saba hawakuona chaguo lao kati ya wagombea na hivo kutumia haki yao ya kutochagua ndo maana kura zao zinahesabiwa zimeharibika.
 
Huo nao ni ujinga mwingine maana kama wengi wameshapitisha watu wawili kugombea haiwezekani kati ya hao wawili ukakosa angalau anayeelekea kufaa kuongoza.
 
Huo nao ni ujinga mwingine maana kama wengi wameshapitisha watu wawili kugombea haiwezekani kati ya hao wawili ukakosa angalau anayeelekea kufaa kuongoza.

Mkuu sipingani nawewe ila ni vizuri mtu ukasimamia unachokiamini. Sio vizuri kufata mkumbo lazima uwe na maamuzi yako mwenyewe.
Ni haki kama kati ya walioteuliwa huna unayemwona kufaa uongozi basi huna haja ya kupiga kura. Dhamira ikikataa huna haja ya kulazimisha.
Ni haki na wala si upumbavu kutopiga kura.
 
Huo nao ni ujinga mwingine maana kama wengi wameshapitisha watu wawili kugombea haiwezekani kati ya hao wawili ukakosa angalau anayeelekea kufaa kuongoza.
ndoo maana wanalazimisha kura za wazi:wink2:
 
Mkuu sipingani nawewe ila ni vizuri mtu ukasimamia unachokiamini. Sio vizuri kufata mkumbo lazima uwe na maamuzi yako mwenyewe.
Ni haki kama kati ya walioteuliwa huna unayemwona kufaa uongozi basi huna haja ya kupiga kura. Dhamira ikikataa huna haja ya kulazimisha.
Ni haki na wala si upumbavu kutopiga kura.

Mkuu hata kwenye chaguzi kubwa nchini siyo kwamba tunakubaliana na wale wote wanaopigiwa kura. Mara nyingine unakuta hawafai lakini inabidi mtu kupiga kura tu angalau kwa yule ambaye anafaa kidogo ili kuokoa jahazi kuliko apatikane mbovu kabisa. Maana usipopiga kura wapo ambao watapiga kura na wanaweza kumpigia yule ambaye hafai kabisa na likawa tatizo kubwa zaidi.

Tutakuwa tunakosea sana pale tutakaposusa kupiga kura kwa sababu tu waliowekwa ni wabovu, maana kama kura kupigwa itapigwa tu. Na kama watakuwepo wengi wa style hii ya kususa ina maana atapatikana kiongozi mbovu kabisa wa kuiwakilisha jamii. Na huo mwisho ndo utakuwa mbaya zaidi.

RAI yangu watu tusiwe tunasusia upigaji kura ni afadhali nusu shari kuliko shari kamili.
 
Mkuu, nenda kaisikilize vizuri tena ile hotuba, hizo kura 7 zilipigwa kabisa though ziliharibika, kuharibika maana yake wapiga kura hawakuonesha wamemchagua nani!? Hapo ndipo inapokuja hoja ya mleta uzi, kama hawa ndio wanaotutengenezea katiba while kupiga kura tu hawajui, hivi si ni balaa hilo!? Wonders shall never end in this country!
Mkuu hapo umechemsha kwani si lazima upige kura.
Wajumbe wayo haki ya kumchagua wamtakaye ila hawalazimishwi kuchagua au kupiga kura kama hawaoni wamtakaye.
Inawezekana hao wajumbe saba hawakuona chaguo lao kati ya wagombea na hivo kutumia haki yao ya kutochagua ndo maana kura zao zinahesabiwa zimeharibika.
 
Mkuu, nenda kaisikilize vizuri tena ile hotuba, hizo kura 7 zilipigwa kabisa though ziliharibika, kuharibika maana yake wapiga kura hawakuonesha wamemchagua nani!? Hapo ndipo inapokuja hoja ya mleta uzi, kama hawa ndio wanaotutengenezea katiba while kupiga kura tu hawajui, hivi si ni balaa hilo!? Wonders shall never end in this country!

Mkuu afadhali wewe umenipata vizuri. Yaani hili ni tatizo kubwa ajabu ni kwa sababu tu watu hawajalitazama kwa undani. Ni aibu kubwa mno!!!!
 
Mkuu mimi nina wasiwasi na hili lililotokea,siamini kama limetokea kwa bahati mbaya ila ni makusudi/kimkakati kwa ajili ya kulitumia hapo baadaye kujenga hoja ya kwa nini kuna umhimu wa kuiruhusu kura ya wazi iweze kufanya kazi.
 
Kuna tetesi "SIMIYU YETU" mzimu wa CHADEMA unamtesa mpaka mjengoni kwa hiyo alijikuta kipindi cha kura akiandika CHADEMA badala ya kuchagua kati ya hao wagombea wawili na hivyo kuharibu kura moja.
 
Mkuu hapo umechemsha kwani si lazima upige kura.
Wajumbe wayo haki ya kumchagua wamtakaye ila hawalazimishwi kuchagua au kupiga kura kama hawaoni wamtakaye.
Inawezekana hao wajumbe saba hawakuona chaguo lao kati ya wagombea na hivo kutumia haki yao ya kutochagua ndo maana kura zao zinahesabiwa zimeharibika.

Na hapo ndipo umuhimu wa kura ya SIRI unavyojitokeza. Vinginevyo hao wajumbe 7 wangeunga mkono jambo ambalo hawaliamini.
 
Kuna tetesi "SIMIYU YETU" mzimu wa CHADEMA unamtesa mpaka mjengoni kwa hiyo alijikuta kipindi cha kura akiandika CHADEMA badala ya kuchagua kati ya hao wagombea wawili na hivyo kuharibu kura moja.

Mkuu umenisaidia kumtaja m1, tuwataje wote, wa pili atakuwa Lusinde, majimarefu, Lakairo, Capt. Komba
 
Naona wale jamaa saba mburula hata kwenye kura umakamu mwenyeketi wametoka kapa tena..
 
Hapa tatizo sio kutokupiga kura bali in kura kuharibika. Ukweli ni kwamba wale wajumbe saba walioharibu kura ni mbumbu mno. Ni heri ingejulikana kwamba hawakupiga kura kuliko kuharibu.
 
Mkuu, nenda kaisikilize vizuri tena ile hotuba, hizo kura 7 zilipigwa kabisa though ziliharibika, kuharibika maana yake wapiga kura hawakuonesha wamemchagua nani!? Hapo ndipo inapokuja hoja ya mleta uzi, kama hawa ndio wanaotutengenezea katiba while kupiga kura tu hawajui, hivi si ni balaa hilo!? Wonders shall never end in this country!

Mmojawapo atakuwa Paul Makonda
 
Hapa tatizo sio kutokupiga kura bali in kura kuharibika. Ukweli ni kwamba wale wajumbe saba walioharibu kura ni mbumbu mno. Ni heri ingejulikana kwamba hawakupiga kura kuliko kuharibu.

mimi ninauhakika mmoja wa walioharibu kura ni mtikila. sasa mtikila ni mbumbumbu? kwa mfano kuna mtu amejiapisha hatawahi kumpigia kiumbe yeyote anayetoka CCM kura. Sasa Hashimu Rungwe lionekana kabisa alikuwa anasindikiza. sasa kuonesha kwamba sijaridhika na wagombea wote nafanyaje? nachora zombi kwenye karatasi ya kura. nakuwa nimefikisha ujumbe na sijaumiza dhamiri yangu kukubaliana na jambo ambalo haliniridhishi. Na umuhimu wa kura ya siri ndipo unapoonekana hapa.
 
Back
Top Bottom