safuher
JF-Expert Member
- Feb 11, 2019
- 11,170
- 15,851
Habarini za kutwa wadau,natumai muwazima wa afya tele.kwanza kabisa naruhusu mapovu kwa wale wote ambao wataona mimi ni jasusi ama ni kafiri ambae natumia mgongo wa uislamu kuwatukana mashekhe lakini hapa situkani nazungumza hali halisi.
Katika watu ambao wanaonekana na sura ya ushekhe katika madhhabu ya kiislamu ponda huwezi kumkosa,na amekuwa ni mtu ambae anasauti kwa waislamu wengi pale anaposema jambo fulani basi watu huliitikia jambo hilo.
Lakini jambo ambalo nataka niwajuze watu kwa ufupi ni kwamba huyu anayeitwa shekhe ponda iissa ponda ni muislamu wa kawaida tu ambae amekuwa mzungumzaji mzuri na wala hakupaswa kuvikwa vazi la ushekhe na etii asimame kusemea maslahi ya waislamu.hili mtukane mpasuke habari ndo hiyo.
Ponda sio mwanazuoni ambae anaweza kutegemewa katika baadhi ya mambo ya kiislamu,lakini tu amekuwa mwanaharakati musialmu,mzungumzaji mzuri na hapo ndo akapewa ushekhe kwa sababu ukiwa na hayo mambo katika uislamu utaonekana shekhe tu.
Nakupa mfano wa wasomi ambao tunaweza kusema ni wasomi wamekaa wakasoma usialmu,mfano ni SHEKHE KUNDECHA huyu bwana ni msomi wa dini kinyume na ponda japo kuwa na yeye ni mwanaharakati.mfano tu.
Sasa bwana ponda huyu ndigu zangu waislamu mnatakiwa kuwa makini nae kwa sababu anafanya na kusema mambo ambayo hata uislmau wenyewe una mkataa kama vile kuwatia hamasa waislamu kuandamana eti kudai baadhi ya mambo alafu katika maandamano hayo unakuta waislamu wanapigwa na kuwagwa damu,hivi anajua thamani ya damu katika uislamu?
Uislamu unaruhusu hata kumkufuru Mungu ikiwa tu umeambiwa kama hautokufuru unakufa,uislamu unakuruhusu kukufuru kwa ajili ya kulinda hishma ya damu yako.lakini mtu kama ponda lini aliwahi kukemea mambo ya maandamano kutokana na hasara za watu kuumia na kufa?
Alafu katika mambo mbali mbali ya kijamii huyu bwana amekuwa anatoa matamko ambayo huwenda yakaashiria na kupelekea hali mbaya,huyu bwana ni hodari wa kudai usawa katika serikali kwamba waislamu nao wawe wemgi huko sijui atapata faida gani.
Juzi juzi kumetokea tokeo ya UDOM huko ambako naye katoa tamko ambalo ukiliskiliza linaitupia lawama fulani na sio ajabu baadae akaja juu tena huyu ponda kuhusu hili sakata na kuwatia hamasa waislamu.
Ponda ni mtu wa kupuuzwa,anawapotezea muda sana waislamu na kuwatia katika mlango wa chuki baina ya waislamu na serikali jambo ambalo litazidi kuwafanya waislamu kuzidi kuishi kwa dhiki kuliko mwanzo.
Ponda hana uelewa wa kujua kwamba jambo hili akilifanya madhara yake ni makubwa kuliko faida na hivyo liepukwe,ponda haelewi hilo,anachojua yeye kila jambo kuja nalo juu tuu.
KUNDECHA ALILIZUNGUMZIA SUALA LA MSIKITI PALE UDOM MBELE YA RAIS ikulu na likasikika lakini ponda naye amekuja majuzi kulisemea,anatafuta nini huyu?
Ponda ni mwanasiasa aliyejificha katika mlango wa dini na ndiyo maana huwezi kumkuta anafanya harakati za kufundisha waislamu mambo ya dini yao,yeye na serikali tu alafu matokeo yake faida chache na hasara ni kubwa miongoni mwa hasara hizo ni uislamu kuonekana dini ya fujo fujo tu.
Ponda ni muislamu ambaye hatakiwi kuitwa mwnazuoni,ni muislamu mwanasiasa tu ambaye hana tofauti na watu wengine kama akina lissu au mbowe,lakini tu yeye hulenga katika mambo ya dini.
Huyu ponda anapenda sana huko serikalini kuwe na usawa kati ya wakristo na waislamu,zanzibar ambako kuna waislamu tupu serikalini kimefanyika nini ambacho yeye ponda kasimama akakisifia kwa wingi wa waislamu hao?
Povu ruksa
Katika watu ambao wanaonekana na sura ya ushekhe katika madhhabu ya kiislamu ponda huwezi kumkosa,na amekuwa ni mtu ambae anasauti kwa waislamu wengi pale anaposema jambo fulani basi watu huliitikia jambo hilo.
Lakini jambo ambalo nataka niwajuze watu kwa ufupi ni kwamba huyu anayeitwa shekhe ponda iissa ponda ni muislamu wa kawaida tu ambae amekuwa mzungumzaji mzuri na wala hakupaswa kuvikwa vazi la ushekhe na etii asimame kusemea maslahi ya waislamu.hili mtukane mpasuke habari ndo hiyo.
Ponda sio mwanazuoni ambae anaweza kutegemewa katika baadhi ya mambo ya kiislamu,lakini tu amekuwa mwanaharakati musialmu,mzungumzaji mzuri na hapo ndo akapewa ushekhe kwa sababu ukiwa na hayo mambo katika uislamu utaonekana shekhe tu.
Nakupa mfano wa wasomi ambao tunaweza kusema ni wasomi wamekaa wakasoma usialmu,mfano ni SHEKHE KUNDECHA huyu bwana ni msomi wa dini kinyume na ponda japo kuwa na yeye ni mwanaharakati.mfano tu.
Sasa bwana ponda huyu ndigu zangu waislamu mnatakiwa kuwa makini nae kwa sababu anafanya na kusema mambo ambayo hata uislmau wenyewe una mkataa kama vile kuwatia hamasa waislamu kuandamana eti kudai baadhi ya mambo alafu katika maandamano hayo unakuta waislamu wanapigwa na kuwagwa damu,hivi anajua thamani ya damu katika uislamu?
Uislamu unaruhusu hata kumkufuru Mungu ikiwa tu umeambiwa kama hautokufuru unakufa,uislamu unakuruhusu kukufuru kwa ajili ya kulinda hishma ya damu yako.lakini mtu kama ponda lini aliwahi kukemea mambo ya maandamano kutokana na hasara za watu kuumia na kufa?
Alafu katika mambo mbali mbali ya kijamii huyu bwana amekuwa anatoa matamko ambayo huwenda yakaashiria na kupelekea hali mbaya,huyu bwana ni hodari wa kudai usawa katika serikali kwamba waislamu nao wawe wemgi huko sijui atapata faida gani.
Juzi juzi kumetokea tokeo ya UDOM huko ambako naye katoa tamko ambalo ukiliskiliza linaitupia lawama fulani na sio ajabu baadae akaja juu tena huyu ponda kuhusu hili sakata na kuwatia hamasa waislamu.
Ponda ni mtu wa kupuuzwa,anawapotezea muda sana waislamu na kuwatia katika mlango wa chuki baina ya waislamu na serikali jambo ambalo litazidi kuwafanya waislamu kuzidi kuishi kwa dhiki kuliko mwanzo.
Ponda hana uelewa wa kujua kwamba jambo hili akilifanya madhara yake ni makubwa kuliko faida na hivyo liepukwe,ponda haelewi hilo,anachojua yeye kila jambo kuja nalo juu tuu.
KUNDECHA ALILIZUNGUMZIA SUALA LA MSIKITI PALE UDOM MBELE YA RAIS ikulu na likasikika lakini ponda naye amekuja majuzi kulisemea,anatafuta nini huyu?
Ponda ni mwanasiasa aliyejificha katika mlango wa dini na ndiyo maana huwezi kumkuta anafanya harakati za kufundisha waislamu mambo ya dini yao,yeye na serikali tu alafu matokeo yake faida chache na hasara ni kubwa miongoni mwa hasara hizo ni uislamu kuonekana dini ya fujo fujo tu.
Ponda ni muislamu ambaye hatakiwi kuitwa mwnazuoni,ni muislamu mwanasiasa tu ambaye hana tofauti na watu wengine kama akina lissu au mbowe,lakini tu yeye hulenga katika mambo ya dini.
Huyu ponda anapenda sana huko serikalini kuwe na usawa kati ya wakristo na waislamu,zanzibar ambako kuna waislamu tupu serikalini kimefanyika nini ambacho yeye ponda kasimama akakisifia kwa wingi wa waislamu hao?
Povu ruksa