The Analyst
JF-Expert Member
- Feb 26, 2011
- 464
- 246
Katika kusoma threads nyingi za Jukwaa la Siasa nimegundua tabia za wafuasi wa vyama hivi hasimu zinafanana sana, hasa ktk uhafidhina wao. Kuna wafuasi wa CCM ambao daima hawaoni chochote cha msingi katika thread yoyote inayojaribu kukusoa serikali yao ama kupinga ufisadi wao. Cha ajabu eti hata baadhi ya wafuasi wa CDM nao hawataki kuambiwa chochote kuhusu mambo yasiyokuwa mazuri katika upande wao. Wanataka kusifiwa na kuungwa mkono tu, muda wote pasipo kutafakari hoja za msingi japo zinatoka kwa mahasimu wao.
Picha ninayoipata hapa ni kwamba CDM watakapokuwa madarakani itakuwa vigumu sana kuwakosoa kwa kuwa nao wata-behave kama CCM tu.
Ingetokea tukapata kiongozi mmoja anayeipenda nchi kama nilivyo mimi ili awe dikteta (kwa mtazamo wa wana-demokrasia) lakini atumie muda mwingi atakaong'ang'ania madarakani kuijenga nchi ili walau tuweze kuwafikia wenzetu waliopiga hatua katika maendeleo.
Hizi chaguzi za kuiga sometimes ndo zinatufikisha hapa. JK alipendwa sana lakini uwezo wake wa kuongoza 0% ya matarajio. Nani anajua Mbowe (kama atataka na kupata) atakuwa vipi akiingia madarakani?
Wachina wamekwepa mtego huu wa Magharibi na sasa mambo yao super!
Yote haya yananitoka kwa kuwa nimegundua; wafuasi wa vyama hivi ni kama mapacha. Tofauti yao ni ndogo tu, kwamba mmoja anataka madaraka ambayo mwenzake anaogopa kuyapoteza.
Picha ninayoipata hapa ni kwamba CDM watakapokuwa madarakani itakuwa vigumu sana kuwakosoa kwa kuwa nao wata-behave kama CCM tu.
Ingetokea tukapata kiongozi mmoja anayeipenda nchi kama nilivyo mimi ili awe dikteta (kwa mtazamo wa wana-demokrasia) lakini atumie muda mwingi atakaong'ang'ania madarakani kuijenga nchi ili walau tuweze kuwafikia wenzetu waliopiga hatua katika maendeleo.
Hizi chaguzi za kuiga sometimes ndo zinatufikisha hapa. JK alipendwa sana lakini uwezo wake wa kuongoza 0% ya matarajio. Nani anajua Mbowe (kama atataka na kupata) atakuwa vipi akiingia madarakani?
Wachina wamekwepa mtego huu wa Magharibi na sasa mambo yao super!
Yote haya yananitoka kwa kuwa nimegundua; wafuasi wa vyama hivi ni kama mapacha. Tofauti yao ni ndogo tu, kwamba mmoja anataka madaraka ambayo mwenzake anaogopa kuyapoteza.