Mwana wa Mungu
JF-Expert Member
- Aug 14, 2008
- 1,003
- 83
Wakubwa, sisi wengine hatupo hapo bongo kwa sasa, kutokana na kazi zetu. Nilikuwa naomba kuuliza, hivi bunge la tz linakaa lini? na kama tayari, WABUNGE WANALIONGELEAJE SUALA LA TZ KUTUMIA MAJI YA ZIWA VICTORIA, kutokana na msimamo wa Misri? tunataka kuwasikia wabunge wakiongea hili. na tunataka waliongelee bungeni. nimesoma baadhi ya threads humu, nimeona inauma. kwamba watz singinda, shinyanga, Dodoma na maeneo mengine ya Arusha etc, wanakunywa maji ya topa, wakati kulikuwa na uwezekano wa kuwavutia maji wakanywa, wakauza wakamwagilia hadi kwenye vitalu vya mashamba yao.....hivi anayetunza ziwa victoria ni nani? ni Misri au tz, hivi ziwa victoria liko Misri?hivi mbona wanatuchezea hivi? rais wetu yuko wapi, na ajitokeze basi kuliongelea hili, tunamtaka aliongelee, au ndo kama wengine wanavyosema, anawaabudu hao watoto wa mamdogo....kwa hili asipoangalia, litagawa wengi. ujumbe kwa vyama vya upinzani, tunaoma chukueni hili kama silaha nzito juu ya kikwete kwenye kampeni za uchaguzi mwaka huu, mtwangeni nayo hadi atoe maelezo kuhusu msimamo wake, kwasababu kama yeye anaenda kwenye birthday za kina Gadafi, si wote tz tunamfagilia huyu gaidi wa Libya, pamoja na rafiki zake wa Sudan na misri. la sivyo, aachie ngazi, kuna wengi tu tunaweza kuongoza nchi na kutetea maslahi ya nchi. period. inaudhi sana.