Wabunge wa chadema ni wazalendo

Somi

JF-Expert Member
Feb 7, 2009
3,605
4,361
Pongezi nyingi ziwaendee wabunge wa chadema wakiongozwa na mh Mbowe pale walipotoka nje wakati mwenyekiti wa ccm anahutubia.Wametekeleza kidemokrasia msimamo wa chama na kupeleka kilio cha mamilioni ya watanzania waliotaka mabadiliko ya kuondokana na umasikini lakini kauli yao ikaporwa na nec.Wangeamua kubaki bungeni na kusema ndiyo mzee kwa miaka mitano huku wakipata ela za kutosha lakini wakatanguliza mbele maslahi ya watanzania,pamoja na kwamba tumewachagua wakashugulikie shida za majimbo yetu pia tumewatuma wakatete maslahi ya taifa kama katiba mpya na tume huru ya uchaguzi.Wabune wa ccm ambao juzi walizomea kama wahuni wa mitaani wanajali maslahi yao sio ya wananchi wa tanzania ndio maana wengi wao waliiba kura kwa kusaidiwa na nec na wengine wakashindwa.
 
Back
Top Bottom