Wabunge wa CCM kuweni wazalendo japo kidogo!

Rich Dad

JF-Expert Member
Dec 15, 2010
748
133
Jana wakati wabunge wa Chadema wakisusia kikao kilichokuwa na nia ya kutoa tafsiri ya kambi rasmi ya upinzania bungeni, sikutaka kuamini kile nilichokuwa nakisikia kutoka kwa wabunge waliobaki ( kwa uwingi wao CCM). Kutoa lugha chafu za kejeli kwa wenzao waliokuwa wanatoka sikuona hata chembe ya busara waliyonayo.
Yaani kumbe nimegundua ni watu waliozoea mipasho, upashkuna, na maneno ya vijembe vya kwenye taarabu na Kanga.

Kweli hawa ni watu watanzania tunaowategemea watajadili mijadala yenye maslahi kwa taifa?? MMh inatia mashaka mno.

Ushauri wangu;
Binadamu ameumbwa na mdomo mmoja, na masikio mawili. Mungu alikuwa na makusudi yake kuweka masikio mawili, sikia zaidi kabla ya kurusha maneno. Nashauri bunge liweke kozi maalumu zitakazowaandaa wabunge wote kuwafanya watambue kwamba bunge sio sehemu ya vita ya kutumia nguvu, hoja zenye maana na ushawishi ndio nguvu pekee itakayokuwezesha kumu-win mpinzani wako.

Kozi za soft skills pia zinahitajika kwa wabunge i.e. presentation skills, persuasive skills, interpersonal skills n.k
 
hakuna cha kushaangaa hapo mzeee, mipasho kwa ccm ni kawaida mnoo. kwanza nikukumbushe kuwa ccm ni chama pekee kinachomiliki kundi la taarabu TOT, Pia mwenyekiti wao ndo kawaambukiza mipasho ulitegemea kamata au mrema angesema nini wakati wanaume wanatoka bungeni?
 
hakuna cha kushaangaa hapo mzeee, mipasho kwa ccm ni kawaida mnoo. kwanza nikukumbushe kuwa ccm ni chama pekee kinachomiliki kundi la taarabu TOT, Pia mwenyekiti wao ndo kawaambukiza mipasho ulitegemea kamata au mrema angesema nini wakati wanaume wanatoka bungeni?
Duh kuna mama mmoja nilisikia anamung'una maneno ya kiingereza cha kuungaunga kuwatupia wanaume. Alikuwa anajaribu kuongea kiingereza kwa lafudhi ya kikwere.
 
Hawa jamaa mbona wanapotosha?
Ni wabunge wa UPINZANI ndio walilalamika au ni WANANCHI pamoja na WANAHARAKATI?
sasa kwa nini CCM wanapotosha tena Bungeni?
wana mdanganya nani hawa wenye MAGAMBA?
 
Achana na hao watu wameshamaliza wamenunua mafenicha ya mamilioni huku hata wazazi wao wanakaa kwenye nyumba zisizoeleweka, saa hizi wanasubiri posho tu za maanna makinda!
 
Halafu wanapewa MIKOPO mingine, kuna mmoja kalalamika kuwa MAKATO yamezidi, BUnge liwafikirie jinsi ya kuamishia MAKATO sehemu nyingine!
 
Wapo wabunge walilalamika, magazetu yapo, katafute, mie nawajua, halafu wakazikimbilia fasta kuzichukua.
 
WABUNGE wamewalaumu watu wanaohoji kwa nini wamekopeshwa Sh milioni 90 kununua vyombo vya usafiri na wanaowashutumu kwa kununua magari ya kifahari.

Mbunge wa Same Mashariki (CCM), Anne Kilango Malecela, amesema bungeni mjini Dodoma kuwa, kuna watu wamekuwa wakipotosha kuhusu malengo ya mikopo hiyo na akawashangaa wabunge wa kambi ya upinzani kwa kujiweka kando kama vile mikopo hiyo haiwahusu.

Malecela amesema, usafiri ni jambo la msingi kwa Mbunge ili aweze kuwahudumia wapiga kura wake hivyo wana haki ya kukopeshwa. Ametoa mfano wa jimbo lake kuwa lina kata 15, 10 kati ya hizo ni eneo lenye milima mirefu, na tano ni eneo tambarare.

“Naomba wananchi wote mliotuchagua muelewe kuwa hii ni mikopo, tunakatwa kwenye mishahara mwisho wa mwezi” amesema Mbunge huyo wakati anachangia Azimio la Bunge la kurekebisha Mfuko wa Kutoa Mikopo kwa Wabunge na kuunda Mfuko wa Mikopo kwa Watumishi wa Serikali Kuu.

Mbunge wa Nzega (CCM) Dk. Hamisi Kigwangala, anashangaa kwa nini watu wanalalamika kwamba wabunge wamekopeshwa na kwamba, kwa sababu za kisiasa, jambo hilo limekuwa likipotoshwa.

Mbunge amewataka wapinzani waache kuwapotosha Watanzania na akadai kuwa hali ikiendelea hivi, taifa halitafikia malengo yake ya kukuza uchumi.

Mbunge wa Ukonga (CCM), Eugen Mwaiposa, amesema bungeni kuwa kauli za kupotosha kuhusu mkopo huo zimewafedhehesha. “Ile ni mikopo ambayo tunakatwa katika mishahara yetu” amesema Mbunge huyo wakati anachangia azimio hilo.

Mwaiposa amesema, Serikali pia inapaswa kuangalia utaratibu mwingine ili wabunge wasikatwe bima katika mikopo ya magari.

Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Stella Manyanya, amesema, wananchi wamekuwa wanahoji kwa nini wabunge wamenunua magari ya kifahari ikiwa ni pamoja na Toyota Land Cruiser badala ya gari kama Suzuki.

Source: Habari Leo

Surprising Careers With High Earning Potential

These occupations have the potential to pay more than you might think.

Pop quiz: who makes a fatter annual income?

Nuclear techs or elevator repairmen? How about power plant operators or funeral directors? Urban planners or high school art teachers?

The correct answers may surprise you.

•Elevator repairmen ($67,950) edge out nuclear technicians ($66,700) in annual income.
•Funeral directors ($60,390) beat power plant operators ($60,270).
•High school art teachers ($68,230) make more than urban planners ($64,680).

USA wage by yahoo.com
 
WABUNGE wamewalaumu watu wanaohoji kwa nini wamekopeshwa Sh milioni 90 kununua vyombo vya usafiri na wanaowashutumu kwa kununua magari ya kifahari.

Mbunge wa Same Mashariki (CCM), Anne Kilango Malecela, amesema bungeni mjini Dodoma kuwa, kuna watu wamekuwa wakipotosha kuhusu malengo ya mikopo hiyo na akawashangaa wabunge wa kambi ya upinzani kwa kujiweka kando kama vile mikopo hiyo haiwahusu.

Malecela amesema, usafiri ni jambo la msingi kwa Mbunge ili aweze kuwahudumia wapiga kura wake hivyo wana haki ya kukopeshwa. Ametoa mfano wa jimbo lake kuwa lina kata 15, 10 kati ya hizo ni eneo lenye milima mirefu, na tano ni eneo tambarare.

“Naomba wananchi wote mliotuchagua muelewe kuwa hii ni mikopo, tunakatwa kwenye mishahara mwisho wa mwezi” amesema Mbunge huyo wakati anachangia Azimio la Bunge la kurekebisha Mfuko wa Kutoa Mikopo kwa Wabunge na kuunda Mfuko wa Mikopo kwa Watumishi wa Serikali Kuu.

Mbunge wa Nzega (CCM) Dk. Hamisi Kigwangala, anashangaa kwa nini watu wanalalamika kwamba wabunge wamekopeshwa na kwamba, kwa sababu za kisiasa, jambo hilo limekuwa likipotoshwa.

Mbunge amewataka wapinzani waache kuwapotosha Watanzania na akadai kuwa hali ikiendelea hivi, taifa halitafikia malengo yake ya kukuza uchumi.

Mbunge wa Ukonga (CCM), Eugen Mwaiposa, amesema bungeni kuwa kauli za kupotosha kuhusu mkopo huo zimewafedhehesha. “Ile ni mikopo ambayo tunakatwa katika mishahara yetu” amesema Mbunge huyo wakati anachangia azimio hilo.

Mwaiposa amesema, Serikali pia inapaswa kuangalia utaratibu mwingine ili wabunge wasikatwe bima katika mikopo ya magari.

Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Stella Manyanya, amesema, wananchi wamekuwa wanahoji kwa nini wabunge wamenunua magari ya kifahari ikiwa ni pamoja na Toyota Land Cruiser badala ya gari kama Suzuki.

Source: Habari Leo

Surprising Careers With High Earning Potential

These occupations have the potential to pay more than you might think.

Pop quiz: who makes a fatter annual income?

Nuclear techs or elevator repairmen? How about power plant operators or funeral directors? Urban planners or high school art teachers?

The correct answers may surprise you.

•Elevator repairmen ($67,950) edge out nuclear technicians ($66,700) in annual income.
•Funeral directors ($60,390) beat power plant operators ($60,270).
•High school art teachers ($68,230) make more than urban planners ($64,680).

USA wage by yahoo.com

wabunge wa chadema wamekaa kimya, kwako unaitafsiri vipi?
 
Niliweka post moja hapa juzi kwamba CCM ni sawa na gari chakavu au kuukuu linalotoa moshi mwingi barabarani, na mafundi kila wanapofanya tune up ndo moshi unazidi kuongezeka hadi kufeli emission test. Hivyo ni bora kupelekwa recycling dep.

Mishahara na malupulupu ya viongozi na wawakilishi wa wananchi haviwiani na hali ya maisha ya watanzania wanaowatumikia. Ni aibu kwa wawakilishi wa CCM kuendelea kutetea hali hiyo inayowanyonya walipa kodi.

Nchi zilizoendelea walimu, na wataalamu mbalimbali wanalipwa zaidi kuliko wanasiasa na ndio wengi wa wanasiana wanafanya zaidi kwa kujitolea. Tanzania walimu na wataalamu wanakimbilia siasa kwa vile mishahara hawalipwi kadiri ya taaluma yao.

Katu hatutaondokana na hili hadi mapinduzi ya kweli ya kijamii yataweza letwa na chama kingine chenye itikadi tofauti na chama kikuukuu cha ccm.
 
Wabunge wasiwafanye watanzania wajinga ,kwani katika hali ya kawaida mshahara unao weza kulipa mkopo wa milioni tisini kwa miaka mitano ni mshahara mkubwa sana ambao mafisadi tu wanalipwa.
 
Unafiki wa Chadema na Wabunge wao! Hivi Wabunge wa Chadema hawakuchukua 90 milioni? Kama wanaweza kutoka nje ya ukumbi kwa nini wamelamba 90 m nakutulia!!! Sauti ya Wabunge wa Chadema mbona haitoki hapa kwenye 90 milion?
 
WABUNGE wamewalaumu watu wanaohoji kwa nini wamekopeshwa Sh milioni 90 kununua vyombo vya usafiri na wanaowashutumu kwa kununua magari ya kifahari.

Mbunge wa Same Mashariki (CCM), Anne Kilango Malecela, amesema bungeni mjini Dodoma kuwa, kuna watu wamekuwa wakipotosha kuhusu malengo ya mikopo hiyo na akawashangaa wabunge wa kambi ya upinzani kwa kujiweka kando kama vile mikopo hiyo haiwahusu.

Malecela amesema, usafiri ni jambo la msingi kwa Mbunge ili aweze kuwahudumia wapiga kura wake hivyo wana haki ya kukopeshwa. Ametoa mfano wa jimbo lake kuwa lina kata 15, 10 kati ya hizo ni eneo lenye milima mirefu, na tano ni eneo tambarare.

"Naomba wananchi wote mliotuchagua muelewe kuwa hii ni mikopo, tunakatwa kwenye mishahara mwisho wa mwezi" amesema Mbunge huyo wakati anachangia Azimio la Bunge la kurekebisha Mfuko wa Kutoa Mikopo kwa Wabunge na kuunda Mfuko wa Mikopo kwa Watumishi wa Serikali Kuu.

Mbunge wa Nzega (CCM) Dk. Hamisi Kigwangala, anashangaa kwa nini watu wanalalamika kwamba wabunge wamekopeshwa na kwamba, kwa sababu za kisiasa, jambo hilo limekuwa likipotoshwa.

Mbunge amewataka wapinzani waache kuwapotosha Watanzania na akadai kuwa hali ikiendelea hivi, taifa halitafikia malengo yake ya kukuza uchumi.

Mbunge wa Ukonga (CCM), Eugen Mwaiposa, amesema bungeni kuwa kauli za kupotosha kuhusu mkopo huo zimewafedhehesha. "Ile ni mikopo ambayo tunakatwa katika mishahara yetu" amesema Mbunge huyo wakati anachangia azimio hilo.

Mwaiposa amesema, Serikali pia inapaswa kuangalia utaratibu mwingine ili wabunge wasikatwe bima katika mikopo ya magari.

Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Stella Manyanya, amesema, wananchi wamekuwa wanahoji kwa nini wabunge wamenunua magari ya kifahari ikiwa ni pamoja na Toyota Land Cruiser badala ya gari kama Suzuki.

Source: Habari Leo

Surprising Careers With High Earning Potential

These occupations have the potential to pay more than you might think.

Pop quiz: who makes a fatter annual income?

Nuclear techs or elevator repairmen? How about power plant operators or funeral directors? Urban planners or high school art teachers?

The correct answers may surprise you.

•Elevator repairmen ($67,950) edge out nuclear technicians ($66,700) in annual income.
•Funeral directors ($60,390) beat power plant operators ($60,270).
•High school art teachers ($68,230) make more than urban planners ($64,680).

USA wage by yahoo.com

Duh, kuna kukuza uchumi wa taifa hapa?
 
WABUNGE wamewalaumu watu wanaohoji kwa nini wamekopeshwa Sh milioni 90 kununua vyombo vya usafiri na wanaowashutumu kwa kununua magari ya kifahari.

Mbunge wa Same Mashariki (CCM), Anne Kilango Malecela, amesema bungeni mjini Dodoma kuwa, kuna watu wamekuwa wakipotosha kuhusu malengo ya mikopo hiyo na akawashangaa wabunge wa kambi ya upinzani kwa kujiweka kando kama vile mikopo hiyo haiwahusu.

Malecela amesema, usafiri ni jambo la msingi kwa Mbunge ili aweze kuwahudumia wapiga kura wake hivyo wana haki ya kukopeshwa. Ametoa mfano wa jimbo lake kuwa lina kata 15, 10 kati ya hizo ni eneo lenye milima mirefu, na tano ni eneo tambarare.

“Naomba wananchi wote mliotuchagua muelewe kuwa hii ni mikopo, tunakatwa kwenye mishahara mwisho wa mwezi” amesema Mbunge huyo wakati anachangia Azimio la Bunge la kurekebisha Mfuko wa Kutoa Mikopo kwa Wabunge na kuunda Mfuko wa Mikopo kwa Watumishi wa Serikali Kuu.

Mbunge wa Nzega (CCM) Dk. Hamisi Kigwangala, anashangaa kwa nini watu wanalalamika kwamba wabunge wamekopeshwa na kwamba, kwa sababu za kisiasa, jambo hilo limekuwa likipotoshwa.

Mbunge amewataka wapinzani waache kuwapotosha Watanzania na akadai kuwa hali ikiendelea hivi, taifa halitafikia malengo yake ya kukuza uchumi.

Mbunge wa Ukonga (CCM), Eugen Mwaiposa, amesema bungeni kuwa kauli za kupotosha kuhusu mkopo huo zimewafedhehesha. “Ile ni mikopo ambayo tunakatwa katika mishahara yetu” amesema Mbunge huyo wakati anachangia azimio hilo.

Mwaiposa amesema, Serikali pia inapaswa kuangalia utaratibu mwingine ili wabunge wasikatwe bima katika mikopo ya magari.

Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Stella Manyanya, amesema, wananchi wamekuwa wanahoji kwa nini wabunge wamenunua magari ya kifahari ikiwa ni pamoja na Toyota Land Cruiser badala ya gari kama Suzuki.

Source: Habari Leo

Surprising Careers With High Earning Potential

These occupations have the potential to pay more than you might think.

Pop quiz: who makes a fatter annual income?

Nuclear techs or elevator repairmen? How about power plant operators or funeral directors? Urban planners or high school art teachers?

The correct answers may surprise you.

•Elevator repairmen ($67,950) edge out nuclear technicians ($66,700) in annual income.
•Funeral directors ($60,390) beat power plant operators ($60,270).
•High school art teachers ($68,230) make more than urban planners ($64,680).

USA wage by yahoo.com

Duh, kuna kukuza uchumi wa taifa hapa?
 
WABUNGE wamewalaumu watu wanaohoji kwa nini wamekopeshwa Sh milioni 90 kununua vyombo vya usafiri na wanaowashutumu kwa kununua magari ya kifahari.

Mbunge wa Same Mashariki (CCM), Anne Kilango Malecela, amesema bungeni mjini Dodoma kuwa, kuna watu wamekuwa wakipotosha kuhusu malengo ya mikopo hiyo na akawashangaa wabunge wa kambi ya upinzani kwa kujiweka kando kama vile mikopo hiyo haiwahusu.

Malecela amesema, usafiri ni jambo la msingi kwa Mbunge ili aweze kuwahudumia wapiga kura wake hivyo wana haki ya kukopeshwa. Ametoa mfano wa jimbo lake kuwa lina kata 15, 10 kati ya hizo ni eneo lenye milima mirefu, na tano ni eneo tambarare.

"Naomba wananchi wote mliotuchagua muelewe kuwa hii ni mikopo, tunakatwa kwenye mishahara mwisho wa mwezi" amesema Mbunge huyo wakati anachangia Azimio la Bunge la kurekebisha Mfuko wa Kutoa Mikopo kwa Wabunge na kuunda Mfuko wa Mikopo kwa Watumishi wa Serikali Kuu.

Mbunge wa Nzega (CCM) Dk. Hamisi Kigwangala, anashangaa kwa nini watu wanalalamika kwamba wabunge wamekopeshwa na kwamba, kwa sababu za kisiasa, jambo hilo limekuwa likipotoshwa.

Mbunge amewataka wapinzani waache kuwapotosha Watanzania na akadai kuwa hali ikiendelea hivi, taifa halitafikia malengo yake ya kukuza uchumi.

Mbunge wa Ukonga (CCM), Eugen Mwaiposa, amesema bungeni kuwa kauli za kupotosha kuhusu mkopo huo zimewafedhehesha. "Ile ni mikopo ambayo tunakatwa katika mishahara yetu" amesema Mbunge huyo wakati anachangia azimio hilo.

Mwaiposa amesema, Serikali pia inapaswa kuangalia utaratibu mwingine ili wabunge wasikatwe bima katika mikopo ya magari.

Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Stella Manyanya, amesema, wananchi wamekuwa wanahoji kwa nini wabunge wamenunua magari ya kifahari ikiwa ni pamoja na Toyota Land Cruiser badala ya gari kama Suzuki.

Source: Habari Leo

Surprising Careers With High Earning Potential

These occupations have the potential to pay more than you might think.

Pop quiz: who makes a fatter annual income?

Nuclear techs or elevator repairmen? How about power plant operators or funeral directors? Urban planners or high school art teachers?

The correct answers may surprise you.

•Elevator repairmen ($67,950) edge out nuclear technicians ($66,700) in annual income.
•Funeral directors ($60,390) beat power plant operators ($60,270).
•High school art teachers ($68,230) make more than urban planners ($64,680).

USA wage by yahoo.com



Ingekuwa ni bora ukaonyesha upande wa pili, wale wa CHADEMA wanaopinga mashangingi!
 
Wabunge wasiwafanye watanzania wajinga ,kwani katika hali ya kawaida mshahara unao weza kulipa mkopo wa milioni tisini kwa miaka mitano ni mshahara mkubwa sana ambao mafisadi tu wanalipwa.


Hawalipi zote hizo bali kuna msamaha karibu nusu ya hizo!
 
Back
Top Bottom